Hatma ya Muslim University of Morogoro na Maono ya Aga Khan kuwasaidia Waislamu kujenga Chuo Kikuu

Hatma ya Muslim University of Morogoro na Maono ya Aga Khan kuwasaidia Waislamu kujenga Chuo Kikuu

Wizra ya elimu haina ubaguzi wowote sema waislamu hawapendi kusoma. Kama kuna ubaguzi ni vipi wewe ulisoma, akina Kikwete, Prof Malima RIP, Prof Shivji na Waislamu wote kwa maelfu walio na degree!!

Acheni kuharibu nchi kwa ashiki zenu udini. Baada ya maisha hapa duniani huko ahera/peponi hakuna dini tena
Stux...
Kama nilivyokwisha kukueleza kuwa Waislam wamefikisha ushahidi wao serikalini.

Serikali ina hofu kubwa katika somo hili.

Haina majibu kwa nini ilizuia EAMWS kujenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968 wala haina majibu kwa nini waliinyima OIC kibali cha kujenga Chuo Kikuu Tanzania katika miaka ya 1970.

Halikadhalika haina majibu ya yaliyokuwa yakifanyika Wizara ya Elimu wala haina majibu ya yaliyokuwa yakifanyika NECTA.

Muhimu ni kuwa tunayajadili haya hadharani na yanafahamika.
 
Hii inabidi FaizaFoxy na adriz wajipe ilim vizuri zaidi.
Ukweli usemwe;
Mimi nilikuwa Muislam ila baadae niliamua kuokoka,kwahiyo nitazungumza vyema sana kuhusu Uislam na Elimu kama ifuatavyo;

Uislam unaichukulia Elimu Dunia kama elimu ya kikaffir bali wanawekeza nguvu kubwa sana kwenye elimu akhera.......Nakumbuka Baba yangu alikuwa akitoka kazini swali la kwanza ni kuwa "Ulienda chuo (Madrasa)?" Na kama sikwenda basi atanichapa sana ila kama sikwenda skuli basi huchukulia kawaida tu..........na wazazi wengi wa kiislam wanataka wana wao wakalili Alif,Bee,Tee badala ya A,B,C.......wakati huo watoto wa kikristo wanapoteza muda wao mwingi kwenye Tuition na ata kama ni dini hujifunza Sunday school,tofauti kabisa na uislam ambao kila siku ni Kuhudhuria madras

Waislamu wao kwa wao mtu akisoma sana wanaanza kumuonea wivu kuwa kakengeuka na anataka kuwa kaffir.......Mimi Kuna dada yangu alisoma mpaka chuo sasa ule mtaa mzima hakuna binti wa Rika lake ambaye aliwahi kusoma vile na wengi wao waliposwa mapema sana kwa kisingizio cha dini......walianza kumuandama eti kwanini haolewi na umri amefikisha wa kuolewa,Kuna imaam wa msikiti akataka amuowe kama mke mdogo,dada akagoma aiseeh!!! Kilinuka ikabidi atoke zenj aje bara na mpaka anamaliza chuo hakuwahi kurudi........Aliolewa na Muikristo.

Waislamu hawataki kutoa nguvu zao kwenye mambo ya elimu kama wafanyavyo kwenye Dini pamoja na ndoa.........Unaweza ukafaulu kwenda vidato vya juu kielimu lakini watakao kuunga mkono kimawazo au kiuchumi ni wachache lakini ukitaka kuoa au kuolewa utaungwa mkono na Jamii nzima..........Waislamu wenyewe hawataki kujenga Skuli au Hospitali zao wenyewe kama wafanyavyo Wakristo,lakini ukipitishwa mchango wa kujenga Msikiti au kumlipa mwalimu wa madras pesa uwa yapatikana muda huo huo

Elimu ndio kila kitu ndugu zangu Waislamu .....Jamii ya wajinga ni rahisi sana kuwadanganya na kuwatawala, ndio maana tulishindwa kumtoa Sultan wenyewe mpaka tukasaidiwa na John Okello(Muikristo mmoja anawaongoza wazenj milioni 3 kudai kupigana vita)..... .....leo hii mikoa maskini ya Waislam ndio maskini sana kuliko ata ya Wakristo
 
Mfumo wa elimu tangia ukoloni ulipindishwa kuwapa fursa wakiristo na kuwatenga waislamu. Huu ulikua ni mpango mmoja wa serikali ya kikoloni na kanisa katoliki. Hizi njama zilianza kutokea wajerumani na ukaendelezwa na waingereza na mpaka uhuru.
Kumbuka common factor ilikuwapo ni kanisa katika mipito yote serikali kuanzia wajerumani, waingereza na uhuru, kwa hiyo muendelezo wa hii njama haukuvurugwa katika mabadiliko yote ya serikali yaliotokea.

Taasisi za kiislamu hazikua na uhuru wa kutekeleza mipango yao hasa ya elimu wakati wa ukoloni. Baada ya uhuru wakaanzisha bidii kubwa kurekebisha mapungufu hayo ya elimu ndipo mwalimu Nyerere kuingilia na kudhoofisha taasisi za kiislamu na kuzima mipango yao yote ya kujiendeleza kielimu. Na hili limetia doa katika jina lake mwalimu sababu ni lazima alikua anajua kinachoendelea.

Muhimu sasa ihakikishwe kuwa fursa zinatolewa kwa haki na usawa. Na kanisa liwekwe mbali kabisa na shughuli za serikali.
Nusu ya Wakristo wa Ujerumani ni Protestants, Waingereza ni Waangelikana sasa waliwapendeleaje Wakatoliki?!
 
Maku...

Waislam wa Tanzania na Tatizo la Udini Katika Wizara ya Elimu.

Ndugu Waziri,
Kwa muda mrefu sasa, kumekuwa na maswali mengi wakijiuliza Waislamu, moja likiwa inakuwaje katika maeneo yenye Waislamu wengi ambapo idadi ya wanafunzi Waislamu inakuwa zaidi ya asilimia 70, lakini wanapochaguliwa kwenda sekondari, idadi ya watoto wa Kiislamu huporomoka na kuwa chini ya asilimia 20.

Swali na kitendawili hiki kimekuwepo kwa muda mrefu bila kupatiwa majibu.

Hata lilipofikishwa Bungeni mwaka 1999 na aliyekuwa Mbunge wa Kigamboni, Mzee Kitwana Selemani Kondo, bado halikupatiwa jibu.

Akihoji juu hali hiyo, Mzee Kitwana Kondo alitoa mfano jinsi hali ilivyokuwa katika shule ya Pembamnazi iliyokuwa na Waislamu watupu na kwa miaka mingi mfululizo kulikuwa hakuna hata mtoto mmoja aliyekuwa akichaguliwa kwenda sekondari kutoka katika shule hiyo.

Aidha alisema kuwa, katika mkoa wa Dar es Salaam na Pwani, takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya watoto wa Kiislamu katika shule za msingi ilikuwa zaidi ya asilimia 70 lakini inapokuja kuchaguliwa kwenda sekondari, idadi ya Waislamu iliporomoka na kuwa chini ya asilimia 20.

Akizungumza Bungeni tarehe 2 Februari, 1999 alisema kuwa katika watoto waliofanya mtihani wa darasa la saba mwaka 1998, idadi ya Waislamu ilikuwa asilimia 71 na Wakristo 29%. Hata hivyo akasema, ilipotoka orodha ya waliochaguliwa kwenda sekondari, idadi ya Wakristo ikawa asilimia 79 (79%) na Waislamu 21%.

Je, hiyo ilikuwa na maana kuwa watoto wa Kiislamu kwa asili yao hawana akili?

Alitaka kujua Mzee Kitwana Kondo. Lakini hakuweza kupata jibu.

Mheshimiwa Waziri,
Ni wazi kuwa Waziri wa Elimu au Waziri Mkuu ambaye ndiye msimamizi wa mambo ya serikali Bungeni asingeweza kutoa majibu ya uhakika kwa sababu swali lilihitaji kufanyika uchunguzi huru wa kina na makini kwanza.

Mheshimiwa Waziri,
Mwaka 1987 aliyekuwa Waziri wa Elimu, Profesa Kighoma Ali Malima, aliweka utaratibu mpya wa ufanyaji wa mtihani wa darasa la saba ambapo namba zilitumika toka kufanya mtihani, kusahihisha na kuchagua wanafunzi wa kwenda kidato cha kwanza.

Namba zilivishwa majina baada ya taratibu zote hizo kukamilika. Mwaka huo idadi ya watoto wa Kiislamu waliokwenda kidato cha kwanza iliongezeka kwa asilimia 40 ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

Hata hivyo, mara aliondolewa Waziri Malima katika wizara hiyo na utaratibu wa zamani ukarejeshwa ambapo yalikuwa yakichaguliwa majina na idadi ya Waislamu ikaporomoka na kurudi chini ya asilimia 20.

Mheshimiwa Waziri,
Hali kama hii hapana shaka inazua maswali mengi ambayo yanahitaji majibu na majibu hayo hayawezi kupatikana bila ya kufanyika uchunguzi.

Labda tuongeze mifano ili kuliweka wazi zaidi jambo hili.

Mwaka 1983 mwanafunzi aliyekuwa akiitwa Kopa Abdallah akisoma katika shule ya msingi Kichangani, Kilosa, alikosa kuchaguliwa kwenda sekondari.

Yeye binafsi, wazazi wake na hata walimu wake hawakuamini matokeo yale kutokana na alivyokuwa akifanya vizuri kuliko wanafunzi wote.

Baadae ilikuja kugundulika kuwa nafasi yake alipewa mwanafunzi aliyekuwa akiitwa Antoni Samirani ambaye alikuwa na uwezo mdogo sana ikilinganiswa na Abdallah.

Kilichofanyika ni kuwa jina la Abdallah lilifichwa na baadae Antoni akapewa jina hilo kimya kimya na kwenda kusoma sekondari akitumia jina Abdallah wakati yeye ni Antoni.

Taarifa zinasema kuwa Kopa Abdallah alipogundua hakuweza kufanya kitu akaishia kuwa dereva.

Hali kama hiyo ilimkuta pia Adam Ramadhani aliyekuwa akisoma shule ya msingi Rutihinda jijini Dar es Salaam na kumaliza darasa la saba mwaka 1999. Yalipotoka matokeo ya mtihani wa darasa la saba na kuonekana kuwa Adam hakuchaguliwa, baba yake hakuamini kuwa mtoto wake anaweza kufeli kutokana na uwezo aliokuwa nao na zaidi akitizama walivyochaguliwa watoto ambao Adam alikuwa mwalimu wao shuleni na mitaani.

Katika kufuatilia suala hilo wizarani, ilikuwa aibu kwa wizara baada ya kuonekana kuwa walichaguliwa watoto wa Kikristo wenye alama za chini kabisa huku akiachwa Adam Ramadhani aliyekuwa na alama za juu kuliko wote.

Mheshimiwa Waziri,
Mifano kama hii ni mingi mno na ipo katika ngazi zote kwa maana kutoka elimu ya msingi kwenda sekondari, kutoka kidato cha nne kwenda kidato cha tano na kutoka kidato cha sita kwenda Chuo Kikuu.

Kwamba hata kutoka kidato cha nne kwenda kidato cha tano, wapo watu waliopata kushuhudia majina ya wanafunzi wa Kiislamu yakiwekwa pembeni japo walikuwa na sifa za kuchaguliwa.

Mheshimiwa Waziri,
Ukiacha hujuma katika kuwaacha wanafunzi Waislamu wenye sifa kuendelea na masomo, matatizo huanzia kwenye kuamua nani amefaulu na nani kafeli.

Tuhuma zilizopo ni kuwa wapo wanafunzi wanapewa madaraja ya juu wakati alama zao ni za chini na wapo wanaopewa madaraja ya chini wakati alama zao ni za juu.

Na hii ni kwa masomo yote.

Mheshimiwa Waziri,
Kumekuwa na utamaduni katika nchi hii wa kukataa ukweli.

Kufuatia uchunguzi uliofanywa na Kamati za Bunge, tumeshuhudia wizi na ufisadi wa kutisha ukifichuliwa Bungeni hivi karibuni hali iliyopelekea mpaka Mheshimiwa Rais kubadili Baraza lake la Mawaziri.

Sasa baada ya kuyasema yote hayo, tunasema kuwa Baraza la Mitihani la Tanzania, limekuwa likilalamikiwa kwa zaidi ya miaka 30, lakini malalamiko hayo yamekuwa yakipokewa kwa sikio la uziwi.

Imefikia mahali tunasema kuwa hatuna tena imani na Baraza hilo.

Mheshimiwa Waziri,
Ili kupata ukweli wa malalamiko na shutuma hizi, na ili kujibu lile swali juu ya watoto wa Kiislamu ambalo halikupata jibu Bungeni, tunaitaka serikali kufanya yafuatayo:

1. Tume huru iundwe kuchunguza Baraza la Mitihani la Tanzania na utendaji wake kazi kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita.

2. Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (NECTA) ajiuzulu mara moja ili kulinda heshima ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzaani na Baraza la Mitihani.

Watendaji wakuu wa kitengo cha mitihani na wanaohusika na mfumo wa Kumputa ya Baraza la Mitihani nao wawajibishwe mara moja.

3. Hatua za kisheria na kibinadamu zichukuliwe dhidi ya watumishi wa Baraza la Mitihani watakaothibitika kuhusika na kashfa hii.

4. Muundo wa Baraza la Mitihani uzingatie uwiano wa kidini, kitendo cha chombo nyeti kama hiki kujazana watu wa dini moja kunaliondolea Baraza la Mitihani sura ya kitaifa, kwani takwimu zinaonyesha Makatibu Wakuu Watendaji na Manaibu Katibu Wakuu wamekuwa Wakristo na Wenyeviti wa Baraza hilo ni Wakristo tangu lilipoanzishwa mwaka 1973, mpaka hii leo na takwimu tunazo.

Mheshimiwa Waziri,
Tunaomba ieleweke kuwa tunachotaka ni kupatikana haki na kufanyika uadilifu kwa watu wote.

Hatudai wala hatutaki upendeleo kwa Waislamu na wala hatutaki kuona mtu yeyote anaonewa au kuporwa haki yake, awe Mwislamu au mtu wa dini nyingine.

Tunachoamini ni kuwa kama Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi haina cha kuficha, basi itaunda Tume hiyo kwa haraka na kuhakikisha kuwa ni Tume ya kuaminika itakayofanya kazi yake kwa umakini, kwa kina na kwa uadilifu wa hali ya juu kabisa.

Lakini kama Wizara yako itaona kuwa haiwezi kuunda Tume ya uchunguzi, tunacho kuhakikishia ni kuwa sisi tutafanya kila liwezekanalo na kwa namna yoyote kuhakikisha kuwa Tume hiyo inaundwa.

Na ikigundulika kuwa kuna hujuma zinafanyika katika utendaji wa Baraza, basi itabidi uwajibikaji uanze kwenye Wizara kabla ya kuwawajibisha watendaji wa Baraza la Mitihani.

Ni imani yetu kuwa utayapokea madai ya Waislamu na kuyafanyia kazi kwa umakini na kwa haraka ili kujenga mustakbali mwema wa nchi hii na watu wake.

Tunaomba kuwasilisha,

Mwenyekiti,
Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu
Wala usihangaike sana katika hili, wewe angalia tu shule za mwisho kitaifa katika mitihani ya ngazi zote nyingi huwa zinatokea mikoa au kanda ipi.
 
Mohamad said najifunza mengi kwako likiwemo la uungwana na ustahimilivu. Lakini napata shida na hoja zako.

1. kila kitu kwako ni black and white. Kwako hii nchi ni ya wa Islam na wakristo. Ukweli ni kwamba zipo Imani nyingine pia ambazo zinawaumini Watanzania. Ambazo kwako siyo Muhimu.
2. katika hoja zako, hakuna mazuri ya Nyerere/Serikali kwa waislam.
3. waislam ndo wamenyanyasika kuliko raia wengine. Ukweli ni kwamba kwa miaka mingi sana, Elimu imekuwa changamoto kubwa sana hapa Tanzania, na wote tumekuwa wahanga wa hili. Mfano kwa miaka mingi, chuo kikuu kilikuwa UDSM. kuna Wilaya walikuwa wanafaulu/ wanachaguliwa wanafunzi si Zaidi ya 20 kwenda form one! Na kwa sababu hizi wilaya hazikuwa na shule za secondary walitegemea hisani ya wilaya nyingine. Hiki nacho ni kipengele, maana wengi walikosa fursa.
4. ndo maana humu wengi wanakushambulia kwa sababu mengi unayoyaongea, kiukweli uhalisia ni mdogo, maana sulba na changamoto za elimu tumezipitia wengi humu.
Personally, nilifaulu nikakosa shule. Nikaenda seminar. sijawahi Kulaumu popote.
5. wewe unaamini ndo mwenye uelewa wa historia kuliko wengine. Hapana, jitahidi kuwa accommodative na kujua kwamba you ain’t infallible. Wengi wanajua mengi usiyoyajua. Na si sahihi kutuaminisha kwamba uhuru wa tanganyika ulipiganiwa na waislam pekee.
6. kuna mdau hapo juu amekuuliza, ni changamoto Zipi za kielimu zinampata mtoto wa kisalmu,kwa sasa? Hukujibu. Ukweli ni kwamba changamoto za elimu ni za kitaifa. We are all suffering, from poor decisions by our politicians. Kwako hili hulioni.
7. mwisho St. Augustine University na MUM, sijui kipi kilianza, lakini tukilinganisha ubunifu na uwekezaji, majibu unayo.
8. Bado Naamini kuna waislam smart na wamefanya mambo makubwa nchi hii. Lakini, tunakwama na tutakwama tukitaka kuchanganya dini na maisha ya raia wetu ya kila siku.
9. Swali la kizushi kwako, unaamini Necta ikiongozwa na waislamu, fursa za waislamu kielimu zitabadilika?
Huu uzi ungefungiwa hapa
 
Nga...
Nyerere analaumiwa kwa kuivunja EAMWS na kuunda BAKWATA ili Waislam wasiwe na Chuo Kikuu kwani wakati ule EAMWS ilikuwa inajenga Chuo Kikuu.

Akamkamata Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir na kumfukuza Tanganyika asirejee tena.
Baada ya hapo mmejenga chuo kikuu kipi na hospital ipi ya maana?
 
Mzee maelezo uliyonukuu hayana ushahidi wowote kuthibitisha hujuma za kielimu dhidi ya Uislamu. Aidha hayajibu hoja iliyowasilishwa hapo juu
 
Mzee maelezo uliyonukuu hayana ushahidi wowote kuthibitisha hujuma za kielimu dhidi ya Uislamu. Aidha hayajibu hoja iliyowasilishwa hapo juu
Uzalendo...
Wanaostahili kutoa majibu kuwa hakuna ushahidi ni serikali ambayo Waislam wamefikisha malalamiko yao huko.

Serikali haitaki kulijadili tatizo hili kwani kwao huko ni kukubali kuwa lipo tatizo.

Hili linawatisha.

Waislam wanataka majibu kwa nini serikali iliipiga marufuku EAMWS wakati inajenga Chuo Kikuu?

Waislam wanataka majibu kwa nini OIC walijimwa kibali kujenga Chuo Kikuu?

Na mengi mengine.
Baada ya hapo mmejenga chuo kikuu kipi na hospital ipi ya maana?
Nyio...
Waislam hawapokei fedha kama za Memorandum of Understanding zinazotolewa na serikali kwa makanisa.
 
Uzalendo...
Wanaostahili kutoa majibu kuwa hakuna ushahidi ni serikali ambayo Waislam wamefikisha malalamiko yao huko.

Serikali haitaki kulijadili tatizo hili kwani kwao huko ni kukubali kuwa lipo tatizo.

Hili linawatisha.

Waislam wanataka majibu kwa nini serikali iliipiga marufuku EAMWS wakati inajenga Chuo Kikuu?

Waislam wanataka majibu kwa nini OIC walijimwa kibali kujenga Chuo Kikuu?

Na mengi mengine.
Nyio...
Waislam hawapokei fedha kama za Memorandum of Understanding zinazotolewa na serikali kwa makanisa.
Kwahiyo hata shule zetu bora ni fedha za zinazotolewa na serikali? Be serious
 
Kwahiyo hata shule zetu bora ni fedha za zinazotolewa na serikali? Be serious
Nyio...
Jinsi ulivyoniuliza hili swali tayari ushatoa jibu.

Zaidi umeniambia niwe "serious," yaani nisifanye maskhara.

Mimi ni "serious" sana kiasi kalamu yangu imefika mbali.

Kitabu changu kuhusu Abdul Sykes kinajadiliwa hapa JF toka 2008 na kimechapwa mara nne tunakwenda toleo la tano.

Nimekuwa Mwandishi Bora JF Jukwaa la Historia kwa miaka miwili mfululizo 2021 na 2022.

Nimefanikiwa kubadili historia nzima ya uhuru wa Tanganyika.

Nimesomesha hapa watu mambo ambayo hawakupata kuyajua.

Mimi ni mtu "serious."
 
Hapana, jitahidi kuwa accommodative na kujua kwamba you ain’t infallible.
Tatizo la Mohamed Said liko hapa


Swali la kizushi kwako, unaamini Necta ikiongozwa na waislamu, fursa za waislamu kielimu zitabadilika?

Kwa sasa inaongozwa na Muislam wala sijaona Waislam wakifanya vizuri kuliko wa dini nyingine. Waislam wanaojali ubora wa elimu wanapeleka watoto wao shule za Wakristu vyuo vya kanisa
 
Vv,

Hili jibu langu nimempa Makulanga.
Nawe linakufaa pia:

"Hakuna tatizo uzuri tumejadili.

Umesoma hoja zangu nami nimesoma zako.

Nimeeleza historia ya Waislam jinsi walivyozuiwa kujenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968 kwa kupigwa marufuku EAMWS na kuunda BAKWATA na miaka ya 1970 kwa serikali kukataa OIC kujenga Chuo Kikuu Tanzania.

Nimeeleza matatizo ya ubaguzi katika Wizara ya Elimu na matatizo ndani ya Baraza la Mitihani.

Hii ni historia niliyotafiti na imechapwa katika kitabu na journals.

Vitabu na journals havichapi kazi za kuokoteza kwani huo ni uwanja wa wasomi."
Hayo matatizo bado yapo? Mbona hamjengi hicho chuo?
 
Rava...
Hizi si hadithi.
Soma utatambua.

EAMWS ilikuwa inajenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968 ikapigwa marufuku na serikali na BAKWATA ikaundwa.

Hii si hadithi ni historia ya Waislam wa Tanzania.
Huu upumbqvu wa kupigwa marufuku kujengwa chuo hapa tanzania umekuwa ni kilio kila mwaka hebu zeeka vizuri na wajukuu wako huna cha maana na mawazo ya kujenga kwa miaka ijayo wewe kilio chako chuo chuo
Amengia mwinyi kafanya kitu gani cha maana
Jakaya?
Na huyu s100 bado tu unalilia chuo sio kutoa ushauri kama taifa kwenda mbele zaidi wewe kulilia chuo tu ?
 
Tuwe wakweli ndugu zetu katika imani swala la elimu kwao ni kama dhambi hawajitambui na hawana bidii tumesoma nao wengi tu tena elimu ilee ya miaka ya nyuma unaona kabisa hawana juhudi hata ufuatiliaji nyumbani wazazi hawana muda zaidi ya kuhamasisha kwenda madrasa na kujifunza judo 😂😂😂 wajuzi wa kulalamika ila wanapewa feva nyingi na hawawezi zitumia
 
Nina marafiki wengi waislam na wengi elimu kubwa kubwa wamezipata taasisi zisizo za kiislam.

Baadhi wanakiri ni wazazi wao kufunguka tu ndio kuliwasadia , ukweli usemwe waislam hawatumii nguvu kuwekeza kwenye elimu ya kawaida kuliko dini.

Nimewahi kuona mashindano ya kuhifadhi quran yakiwa na promo kubwa au ufadhili wa safari za hija ila sijawahi kuona waislam hawa wakitoa ufadhili wa masomo kwa watoto wasio na uwezo kwenda kusoma shahada nchi za ughaibuni(kama rekodi ipo naomba iletwe hapa)

Waislam wote tuliokutana masomo ya juu na wengine nje ya nchi ukiwauliza hizi habari za kutumia almost masaa mengi madrasa watakuambia wazazi wao walikataa na kuamua kuwapeleka shule point yangi ni kwamba wanatakiwa wajifunze kubalance dini na mfumo wa maisha wa kisasa.

Leo hii waarabu kibao toka Saudia,Qatar, Yemen,Palestine n.k wanagombea fursa adhimu kwenda Ulaya na Amerika na wakifika huko wanaorudi makwao hawazidi 10%
 
Tuanze hapa tulipo hivi sasa kisha nitaweka tulipotokea baada ya uhuru:

TUJIKUMBUSHE

Waislam wa Tanzania na Tatizo la Udini Katika Wizara ya Elimu.

Ndugu Waziri,
Kwa muda mrefu sasa, kumekuwa na maswali mengi wakijiuliza Waislamu, moja likiwa inakuwaje katika maeneo yenye Waislamu wengi ambapo idadi ya wanafunzi Waislamu inakuwa zaidi ya asilimia 70, lakini wanapochaguliwa kwenda sekondari, idadi ya watoto wa Kiislamu huporomoka na kuwa chini ya asilimia 20.

Swali na kitendawili hiki kimekuwepo kwa muda mrefu bila kupatiwa majibu.

Hata lilipofikishwa Bungeni mwaka 1999 na aliyekuwa Mbunge wa Kigamboni, Mzee Kitwana Selemani Kondo, bado halikupatiwa jibu.

Akihoji juu hali hiyo, Mzee Kitwana Kondo alitoa mfano jinsi hali ilivyokuwa katika shule ya Pembamnazi iliyokuwa na Waislamu watupu na kwa miaka mingi mfululizo kulikuwa hakuna hata mtoto mmoja aliyekuwa akichaguliwa kwenda sekondari kutoka katika shule hiyo.

Aidha alisema kuwa, katika mkoa wa Dar es Salaam na Pwani, takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya watoto wa Kiislamu katika shule za msingi ilikuwa zaidi ya asilimia 70 lakini inapokuja kuchaguliwa kwenda sekondari, idadi ya Waislamu iliporomoka na kuwa chini ya asilimia 20.

Akizungumza Bungeni tarehe 2 Februari, 1999 alisema kuwa katika watoto waliofanya mtihani wa darasa la saba mwaka 1998, idadi ya Waislamu ilikuwa asilimia 71 na Wakristo 29%. Hata hivyo akasema, ilipotoka orodha ya waliochaguliwa kwenda sekondari, idadi ya Wakristo ikawa asilimia 79 (79%) na Waislamu 21%.

Je, hiyo ilikuwa na maana kuwa watoto wa Kiislamu kwa asili yao hawana akili?

Alitaka kujua Mzee Kitwana Kondo. Lakini hakuweza kupata jibu.

Mheshimiwa Waziri,
Ni wazi kuwa Waziri wa Elimu au Waziri Mkuu ambaye ndiye msimamizi wa mambo ya serikali Bungeni asingeweza kutoa majibu ya uhakika kwa sababu swali lilihitaji kufanyika uchunguzi huru wa kina na makini kwanza.

Mheshimiwa Waziri,
Mwaka 1987 aliyekuwa Waziri wa Elimu, Profesa Kighoma Ali Malima, aliweka utaratibu mpya wa ufanyaji wa mtihani wa darasa la saba ambapo namba zilitumika toka kufanya mtihani, kusahihisha na kuchagua wanafunzi wa kwenda kidato cha kwanza.

Namba zilivishwa majina baada ya taratibu zote hizo kukamilika. Mwaka huo idadi ya watoto wa Kiislamu waliokwenda kidato cha kwanza iliongezeka kwa asilimia 40 ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

Hata hivyo, mara aliondolewa Waziri Malima katika wizara hiyo na utaratibu wa zamani ukarejeshwa ambapo yalikuwa yakichaguliwa majina na idadi ya Waislamu ikaporomoka na kurudi chini ya asilimia 20.

Mheshimiwa Waziri,
Hali kama hii hapana shaka inazua maswali mengi ambayo yanahitaji majibu na majibu hayo hayawezi kupatikana bila ya kufanyika uchunguzi.

Labda tuongeze mifano ili kuliweka wazi zaidi jambo hili.

Mwaka 1983 mwanafunzi aliyekuwa akiitwa Kopa Abdallah akisoma katika shule ya msingi Kichangani, Kilosa, alikosa kuchaguliwa kwenda sekondari.

Yeye binafsi, wazazi wake na hata walimu wake hawakuamini matokeo yale kutokana na alivyokuwa akifanya vizuri kuliko wanafunzi wote.

Baadae ilikuja kugundulika kuwa nafasi yake alipewa mwanafunzi aliyekuwa akiitwa Antoni Samirani ambaye alikuwa na uwezo mdogo sana ikilinganiswa na Abdallah.

Kilichofanyika ni kuwa jina la Abdallah lilifichwa na baadae Antoni akapewa jina hilo kimya kimya na kwenda kusoma sekondari akitumia jina Abdallah wakati yeye ni Antoni.

Taarifa zinasema kuwa Kopa Abdallah alipogundua hakuweza kufanya kitu akaishia kuwa dereva.

Hali kama hiyo ilimkuta pia Adam Ramadhani aliyekuwa akisoma shule ya msingi Rutihinda jijini Dar es Salaam na kumaliza darasa la saba mwaka 1999. Yalipotoka matokeo ya mtihani wa darasa la saba na kuonekana kuwa Adam hakuchaguliwa, baba yake hakuamini kuwa mtoto wake anaweza kufeli kutokana na uwezo aliokuwa nao na zaidi akitizama walivyochaguliwa watoto ambao Adam alikuwa mwalimu wao shuleni na mitaani.

Katika kufuatilia suala hilo wizarani, ilikuwa aibu kwa wizara baada ya kuonekana kuwa walichaguliwa watoto wa Kikristo wenye alama za chini kabisa huku akiachwa Adam Ramadhani aliyekuwa na alama za juu kuliko wote.

Mheshimiwa Waziri,
Mifano kama hii ni mingi mno na ipo katika ngazi zote kwa maana kutoka elimu ya msingi kwenda sekondari, kutoka kidato cha nne kwenda kidato cha tano na kutoka kidato cha sita kwenda Chuo Kikuu.

Kwamba hata kutoka kidato cha nne kwenda kidato cha tano, wapo watu waliopata kushuhudia majina ya wanafunzi wa Kiislamu yakiwekwa pembeni japo walikuwa na sifa za kuchaguliwa.

Mheshimiwa Waziri,
Ukiacha hujuma katika kuwaacha wanafunzi Waislamu wenye sifa kuendelea na masomo, matatizo huanzia kwenye kuamua nani amefaulu na nani kafeli.

Tuhuma zilizopo ni kuwa wapo wanafunzi wanapewa madaraja ya juu wakati alama zao ni za chini na wapo wanaopewa madaraja ya chini wakati alama zao ni za juu.

Na hii ni kwa masomo yote.

Mheshimiwa Waziri,
Kumekuwa na utamaduni katika nchi hii wa kukataa ukweli.

Kufuatia uchunguzi uliofanywa na Kamati za Bunge, tumeshuhudia wizi na ufisadi wa kutisha ukifichuliwa Bungeni hivi karibuni hali iliyopelekea mpaka Mheshimiwa Rais kubadili Baraza lake la Mawaziri.

Sasa baada ya kuyasema yote hayo, tunasema kuwa Baraza la Mitihani la Tanzania, limekuwa likilalamikiwa kwa zaidi ya miaka 30, lakini malalamiko hayo yamekuwa yakipokewa kwa sikio la uziwi.

Imefikia mahali tunasema kuwa hatuna tena imani na Baraza hilo.

Mheshimiwa Waziri,
Ili kupata ukweli wa malalamiko na shutuma hizi, na ili kujibu lile swali juu ya watoto wa Kiislamu ambalo halikupata jibu Bungeni, tunaitaka serikali kufanya yafuatayo:

1. Tume huru iundwe kuchunguza Baraza la Mitihani la Tanzania na utendaji wake kazi kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita.

2. Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (NECTA) ajiuzulu mara moja ili kulinda heshima ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzaani na Baraza la Mitihani.

Watendaji wakuu wa kitengo cha mitihani na wanaohusika na mfumo wa Kumputa ya Baraza la Mitihani nao wawajibishwe mara moja.

3. Hatua za kisheria na kibinadamu zichukuliwe dhidi ya watumishi wa Baraza la Mitihani watakaothibitika kuhusika na kashfa hii.

4. Muundo wa Baraza la Mitihani uzingatie uwiano wa kidini, kitendo cha chombo nyeti kama hiki kujazana watu wa dini moja kunaliondolea Baraza la Mitihani sura ya kitaifa, kwani takwimu zinaonyesha Makatibu Wakuu Watendaji na Manaibu Katibu Wakuu wamekuwa Wakristo na Wenyeviti wa Baraza hilo ni Wakristo tangu lilipoanzishwa mwaka 1973, mpaka hii leo na takwimu tunazo.

Mheshimiwa Waziri,
Tunaomba ieleweke kuwa tunachotaka ni kupatikana haki na kufanyika uadilifu kwa watu wote.

Hatudai wala hatutaki upendeleo kwa Waislamu na wala hatutaki kuona mtu yeyote anaonewa au kuporwa haki yake, awe Mwislamu au mtu wa dini nyingine.

Tunachoamini ni kuwa kama Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi haina cha kuficha, basi itaunda Tume hiyo kwa haraka na kuhakikisha kuwa ni Tume ya kuaminika itakayofanya kazi yake kwa umakini, kwa kina na kwa uadilifu wa hali ya juu kabisa.

Lakini kama Wizara yako itaona kuwa haiwezi kuunda Tume ya uchunguzi, tunacho kuhakikishia ni kuwa sisi tutafanya kila liwezekanalo na kwa namna yoyote kuhakikisha kuwa Tume hiyo inaundwa.

Na ikigundulika kuwa kuna hujuma zinafanyika katika utendaji wa Baraza, basi itabidi uwajibikaji uanze kwenye Wizara kabla ya kuwawajibisha watendaji wa Baraza la Mitihani.

Ni imani yetu kuwa utayapokea madai ya Waislamu na kuyafanyia kazi kwa umakini na kwa haraka ili kujenga mustakbali mwema wa nchi hii na watu wake.

Tunaomba kuwasilisha,

Mwenyekiti,
Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu

Sasa turudi nyuma wakati tumepata uhuru:


Ipyax,
Yametokea.
Serikali haiko tayari kutoa majibu.

Nina mengi naweza kukueleza muhimu ni wewe uwe tayari kusikiliza.

Marais Waislam hawakuchaguliwa kuchunguza watendaji Wakristo ndani ya serikali wana mchango gani katika matatizo haya yanayoelezwa na Waislam.

Endapo Rais Muislam ataingia madarakani na kuanza kuchunguza tatizo hili atakuwa anatengeneza tatizo kubwa zaidi linaloweza kuigawa nchi zaidi.

Hili la Waislam kuwekeza katika elimu hapa si mahali pake ila ningependa kukufahamisha kuwa baada ya kupatikana uhuru mwaka wa 1961 Mufti Sheikh Hassan bin Ameir alijiuzulu siasa na kuanzisha taasisi yake, "Daawat Islamiyya," yeye akiwa Mwenyekiti na Katibu wake Schneider Abdillah Plantan.

Sheikh Hassan bin Ameir akasema sababu ya yeye kujiuzulu siasa ni kuwaongoza Waislam katika kutafuta elimu kama alivyowaongoza katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

(Naamini inawezekana historia hii ninayokueleza ikakupa tabu kwani hujapata kuisoma popote kuwa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa mwanachama wa TANU na kapigania uhuru.

Schneider Plantan yeye ndiye aliyesimama mwaka wa 1950 kuutoa uongozi wa wazee katika TAA Rais ambae ni kaka yake, Thomas Plantan na Katibu Clement Mohamed Mtamila na kuingiza uongozi wa vijana Dr. Vedasto Kyaruzi kama President na Abdul Sykes Katibu).

Mwaka wa 1962 Sheikh Hassan bin Ameir akishirikiana na EAMWS wakaitisha Muslim Congress agenda kuu ikiwa elimu.

Hii Muislam Congress ndiyo iliyoweka mpango wa kujenga shule Tanganyika nzima na Chuo Kikuu na kazi ilianza mara moja.

Mwaka wa 1968 Rais Julius Nyerere akaweka jiwe la msingi kujenga Chuo Kikuu.

Miezi miezi michache baadae Rais Nyerere akaivunja EAMWS na kuunda BAKWATA.

Uwekezaji wa Waislam katika elimu na ujenzi wa Chuo Kikuu na shule ukakoma hapo.

Historia hii ni ndefu lakini naamini nimekujibu swali lako na umeelewa matatizo yanayowakabili Waislam.
Mh mzee Said nafikiri ni muhimu ukawa unajiridhisha haswa kwenye takwimu

Yaani waislamu 71% na wakristo 29% wapo shule moja. Matokeo yanakuja 71% wakristo wamechaguliwa na 29% waislamu wamechaguliwa.

Kabla hatujahukumu.

Totala number ya wanafunzi ilikua wangapi? Katika hii total waislamu wangapi na wakristo wangapi?

Waliofanya mtihani walikua wangapi? Katika hawa waliofanya, wakristo wangapi na waislamu wangapi?

Waliofaulu mtihani wangapi? Hapa waislamu wangapi na wakristo wangapi?

Waliofeli mtihani wangapi? Waislamu wangapi na wakristo wangapi?

Ambao hawakufanya mtihani wangapi? Wakristo wangapi na waislamu wangapi?

Hizi factors zote zizingatiwe. Haiwezekani mtu anakuletea namba tu hizo na wewe unaziwasilisha kwetu, hii siyo sawa.
 
Geza...
Hili ndilo kwanza nalisikia.
Mimi si Mzaramo mimi Mmanyema.

Wala sijapata kumchukia mtu katika maisha yangu.

Sikuumbwa hivyo.
Alhamdulilah.

Huna la kusema kuhusu waraka niliokuwekea la ubaguzi?

Unadhani ningekosa radhi ya waalimu wangu pale chuoni ningeweza kufanya haya ya kuandika vitabu, research papers na kuzungumza katika Vyuo Vikuu Afrika, Ulaya na Marekani?

Au hujui kuwa kitabu cha Abdul Sykes mtu wa kwanza kukipitia alikuwa mwalimu wangu wa historia Prof. Fredrick Kaijage?

Hii ni dalili ya mwanafunzi dhaifu aliyekuwa akipewa alama za chini na walimu wake?

Mimi nina radhi ya waalimu wangu wote walionisomesha kuanzia darasa la kwanza hadi Chuo Kikuu Dar-es-Salaam na Cardiff.

Nina radhi ya wazazi wangu.

Huwezi kunivunjia heshima yangu kwa maneno ya kipuuzi.

View attachment 2857222
Kulia: Dr. Ibrahim Msabaha, Prof. Emmanuel Bavu na Mohamed Said
View attachment 2857224
Kulia: Paul Sozigwa, Mohamed Said na Prof. Bavu Prof. Bavu alinitembelea nyumbani kwangu
Sema dingi umekula kitabu ila nashangaa huu upuuzi wa kuwachukia watu wasio waislamu umeanzia wapi!!... yaani pamoja na kuwa msomi mkubwa ila harakati zako ni kama za wale ambao hawakwenda hata chekechea. Udini wa kipumbavu sana.
 
Nina marafiki wengi waislam na wengi elimu kubwa kubwa wamezipata taasisi zisizo za kiislam.

Baadhi wanakiri ni wazazi wao kufunguka tu ndio kuliwasadia , ukweli usemwe waislam hawatumii nguvu kuwekeza kwenye elimu ya kawaida kuliko dini.

Nimewahi kuona mashindano ya kuhifadhi quran yakiwa na promo kubwa au ufadhili wa safari za hija ila sijawahi kuona waislam hawa wakitoa ufadhili wa masomo kwa watoto wasio na uwezo kwenda kusoma shahada nchi za ughaibuni(kama rekodi ipo naomba iletwe hapa)

Waislam wote tuliokutana masomo ya juu na wengine nje ya nchi ukiwauliza hizi habari za kutumia almost masaa mengi madrasa watakuambia wazazi wao walikataa na kuamua kuwapeleka shule point yangi ni kwamba wanatakiwa wajifunze kubalance dini na mfumo wa maisha wa kisasa.

Leo hii waarabu kibao toka Saudia,Qatar, Yemen,Palestine n.k wanagombea fursa adhimu kwenda Ulaya na Amerika na wakifika huko wanaorudi makwao hawazidi 10%
Wamekudanganya elimu ya madrasa ina vitu vingi ila sio ndefu kwa mfano ukisoma ukiwa darasa la kwanza yaani miaka 7 mpaka ukifika darasa la saba unakuwa mbali sana.

Hakuna sehemu ambayo waislamu wanapuuza elimu kwa hawaweki mkazo wapo wanaosoma na kufadhiliwa na taasisu ila haya mambo yakuwa chinu ya taasisi husika...Pia kusoma vyuo ambavyo sio vya kiislamu hakuna mtu kalazimishwa kusoma chuo cha kiislamu ni jukumu la mtu binafsi kusoma popote ....Vyuo ni biashara kama biashara nyingine wapo wanaoenda kusoma mpaka iran nawajua kibao ila wanakuwa chini ya taasisi kama ni mtu wa taasisi utapata fursa.

Hao wenzio wanakudanganya na hakuna ukweli yupe Ally hapi kasoma madarasa na wapo kibao,ukisoma ukiwa mdogo ukifa form four basi unakuwa unajua vingi sana wapo watota wana miaka 10 wanajua Qur an yote ....Hao wamekudanganya hakuna kitu kama hicho Qur an unasoma kutokana na akili yako wewe unaweza kuruka madarasa kibao kwa miaka 3 tu ,kama una kichwa kizuri unamaliza kila kitu..

Kwa vile elimu ya uislamu ni utekelezaji yaani mafunzo makubwa kama ndoa unaweza kusoma ukiwa form one yaani miaka 14,15 hata kuosha maiti ..Shariq zote unless otherwise utake kusoma upate degree ,masters na lazima uende nje ya
nchi kusoma kwa sana...

Kufundishwa kwa level ya chuo ni haki kwa vile ni ubobezi kama masomo mengine mbona programms za udaktari mpaka miaka minne ,kuna masters za miezi 18 wengine ni miaka 2 ..


Unachotaka ni hicho kama unataka kubobea kweny fani fulani.


Mdogo wangu yupo SUA yeye elimu ya madrasa mpaka kuwa mkubwa alisoma akiwa na miaka 5 mpaka anaanza form one kamaliza kitu ni shekhe anafundisha akiwa na miaka 15 tu.
 
Back
Top Bottom