Hayati Dkt. Magufuli aliletwa duniani mahsusi na Mungu ili kuleta masomo fulani tujifunze

Hayati Dkt. Magufuli aliletwa duniani mahsusi na Mungu ili kuleta masomo fulani tujifunze

Somo la nane.
Uongo ukisemwa na mtu yeyote hata akiwa Rais, hauwezi kubadirika kuwa ni Ukweli. JPM alitulazimisha tuaminii Uongo wake kuwa ameiletea Tanzania Maendeleo ya kuwa na Uchumi wa Kati kiwango cha kuifanya TZ iwe Donar Country. Lakini baada ya Rais Samia kngia mdaraakani imegundulika nchi imeporomoka sana kiuchumi, iko hoi kiuchumi, ambapo kwa sasa inatapatapa kwa kutoza Tozo kwa Wananchi wake walio masikini ili kuiendesha Serikali ya Tanzania.
Kwahiyo kabla hajafariki kuna mradi uliokwama?
 
Uko sahihi kabisa, Hata Shetani alipo hasi Sheria ya Mungu, Robo tatu ya Malaika wa mbinguni, walimuunga Mkono shetani!! mpaka leo hao Malaika, wanamtumikia shetani kuzimu! ndo vijini makata, subihani, nk. ndo km ewe sasa!

uko radhi umfuate Kuzimu huyo bwana kuba wako!! km Jiwe ungekuwa mpango wa Mungu usinge haribiwa na kiumbe yeyote!!! eti km atrial fibrillation!! mwee!! Kumbuka tumeimba sana, kuwakumbusha kuwa ''Mpango wa Mungu Lazima utimie''

Tena akaongezea yeye ni Mwamba Hatikisiki, nani atatikisa kilichowekwa na Mungu km Nyarusare? walionijribu waliungua moto! uliza popote wana nijua! Mtu aliye teuliwa na Mungu!! kamwe hawezi kuwa km kifo cha Jiwe! kwanza cha hovyo!! no popularity!!

Si unaona alivo kwenda south, na kikwete!! weee!! Jk aliamusha hamasa, na alikuwa kivutio kwa wa-south, utadhani ndo rais, kuliko hicho kituko chenu, jiwe!! hatushangai shetani kupendwa hata wachawi wana muhusudu shetani!

na asikudanganye mtu shetani ni mzuri hasa Malaika wa nuru, hata akija hapo utadhani ni malaika! wachache sana tunajua sura ya shetani halisi!
Yesu alikufa kifo cha fedheha lakini hakuwa na dhambi. Kwahiyo kifo siyo kigezo cha kwamba mtu hayuko na Mungu.
 
Ongeza na hii
1. Alitudanganya kuwa kila mmoja atapewa noah kumbe ilikuwa utapeli na ule mchanga akaamua kuuchia baada ya kuona alichemka.

2. Maprof walikuwa wanafanya kazi kwa kumuogopa ndo mana hata takwimu zao zilikuwa za kumfurahisha tu ukiwa kinyume chake unashughulikiwa.

3. Alitudanganya kila kitu tunajenga kwa pesa ya ndani huku nyuma akikopa mapesa kibao na sasa kamuachia msululu wa madeni samia

3. Nchi iliongozwa kisanii na uongo uongo. Sasa hivi samia is suffering uongo wa jpm. Angalia machinga sasa hivi wanavyompa headache samia na issue ya corono ambayo jpm alitupiga fix baadae ikamfagia yeye mwenyewe.

3. Maduka kariakoo yalifungwa yote kisa uchumi imeharibika
Kwahiyo saivi utapata Noah siyo baada ya yeye kufariki
 
Mzee JPM alikuwa bora kwa utendaji wa kazi na ufuatiliaji wa maelekezo aliyotoa kuona yametekelezwa, lakini kwenye eneo la HAKI ZA BINADAMU, alikuwa "Sufuri" kabisa. Ukishafeli kwenye eneo hili, basi hata kama ungejenga miradi gani utabaki kuwa Sufuri. Kwa wale Wakristo Kuna aya inasema: "hata nikiwa na Imani ya kuhamisha milima, kama sina UPENDO ,si kitu Mimi". JPM kwenye eneo la HAKI ZA BINADAMU alikuwa zero kabisa. Chaguzi zikawa zinatolewa matamko tu namtaka fulani mniletee BADALA ya sanduku la kura liamue nani awe nani. Wakurugenzi wakaamriwa wapitishe wagombea wa chama chake tu kwa kuwa anawalipa yeye, mafuta ya magari anawapa. Wafuasi wa vyama vingine wakawa muhanga wa mateso, kupigwa, kubambikwa kesi na kufungwa. Hali hii imemwondoa JPM kwenye ubora na kuwa Rais wa hovyo kupindukia, rejea ule MFANO, hata nikiwa na Imani ya kuhamisha milima, kama sina UPENDO si kitu mimi. Chama chake pia hakitakiwi kiendelee na U-hovyo wa aina hii unaoligawa Taifa na kuvunja mshikamano.
Kwahiyo kuwa na upendo na watu ni kufanya Unyonyaji
 
JPM alikuwa fundi sanaa hasa katika uongozi wake. Kwanza aliweza kuweka mambo wazi nyanja zotee.

1. Kimaendeleo hasa linapo kuja swalia za ripoti mbali mbali mfano.Madini kwakweli kupitia Mzee JPM nliweza kujua karibia kila kitu kilicho kuwa kinaendelea katika madini.
Lihali sasa naona giza tu hata taarifa za habari kutoka Channel na redio mbali mbali kukosa mvuto.

2. Aliweza kututia moyo sanaa hasa kwenye swala la kunitegemea na kutuamisha kuwa sisi ni matajiri basi hata kama ni uwongo basi sisi tulijihisi tunaweza na kila mtu alipata mhamko wa kuchapa kazi.JPM best of the Best.

3. Aliweza kukipa hadhi kiti cha uraisi na kueshimika kwa Jinsi alivyo jiweka na mdomaana mnaweza sema alijifanya Mungu mtu lakini kwakweli uraisi ulitua mahala sahihi.

4. Wale matajiri na wakwepa kodi mzee JPM alilala nao mbele mpaka wakakiona cha moto hadi wengine wamepotea kwenye ramani mpaka sasa wameshindwa kusimama tena.
5.Bila majungu nidham serikalini ilirudi kwa sehem kubwa tena sanaa.Si mahospitali nasehem zingine za kijamii.

6. Hakusafiri kwenda popote nje ya Bara la Africa na kulinda maslahi ya nchi yake kwa kuleta maendeleo kitu ambacho mabeberu walikonda sanaa.


Any way zipo zababu nyingi tuu nzuri na pia tunapaswa kujua Binadamu hatukosi kasoro katika maisha yetu ya kila siku.

ILA JPM MPAKA SASA KILA SEHEM HUKAI DAK KADHAA BILA KUTAMKWA JINA LAKE.

HAKIKA TUNA KAZI SANAA YA KUMSAHAU HASA KIZAZI HIKI CHA KWETU.
Umeniwakilisha vyema mkuu asante sana.
 
Ongezea na

1. Miradi ya tija kwenye jamii, zamani ilikuwa ni ndoto kuona lami uswahilini lkn wkt wa JPM tumeona.

2. Umeme, zamani tuliamini umeme hauwezi kuwa wa uhakika nchini kwetu kwani ni maskini nchi hii so tukawa tunaona umeme kukatika katika ni haki yake lkn baada ya JPM kuchukua madaraka umeme kukatika ikawa historia.

3. Miradi mikubwa ya historia, zamani viongozi wetu walishindwa kufanya miradi mikubwa wakisema kuwa nchi yetu ni maskini haiwezi kufanya miradi inayofanyika nchi zilizoendelea lkn wkt wa JPM tuliona ikifanyika mfano electrical SGR, ujenzi wa moja kati ya mabwawa makubwa kabisa ya umeme Africa na duniani JNHPP, flyovers na interchanges, Airports, Ports, ununuzi wa ndege kubwa, ujenzi wa meli kubwa kubwa, masoko n.k kiasi cha kwamba leo hii imeshakuwa fashion kwamba ili ukubalike na jamii lazima ufanye kama alivyokuwa anafanya JPM.

4. Thamani ya mwananchi, zamani mwananchi hasa wa hali duni alikuwa hathaminiki kabisa lkn baada ya JPM vyombo vya dola, wabunge na watumishi serikalini wakaijua thamani halisi ya mtanzania bila kujali ni tajiri au maskini.

5. Heshima ya Tanzania na Watanzania, zamani nchi yetu ilidharaulika sn hasa na nchi jirani, lkn miaka michache baada ya JPM nchi ikapanda thamani na kuwa mfano hapa Afrika kwa utekelezaji wa uchumi jumuishi (inclusive economy)

6. Shamba la bibi, zamani kabla ya JPM nchi yetu ilikuwa shamba la bibi lkn baada ya JPM kila mtu anajua kilichotokea.

7. Msimamo, JPM alikuwa kielelezo cha msimamo wa waafrika mbele ya wazungu kwamba tuna haki ya kupanga mambo yetu pasipo kuingiliwa na mtu yeyote.

Kuna mengi ya kumuelezea Magufuli ambapo kama nitaamua kuyaweka humu itakuwa ni kitabu, hivyo basi itoshe tu kusema kwamba JPM alikuwa moja kati ya viongozi bora zaidi kuwahi kutokea katika nchi hii japo kama mwanadamu hakukosa kasoro lkn kiukweli kabisa kasoro zake haziwezi kuficha mema mengi aliyoifanyia nchi hii.
Asante
 
Jamaaa alikuwa mbinafsi sana na roho mbaya sana wenzio aliwafungia akaounti zao za mshahara mfano mbowe ila yy aliendelee kupokea mshahara kwa jasho letu watz
Unamzungumzia huyu huyu mbowe aliyesema kuwa kavamiwa na watu wasiojulikana wakampiga kumbe ukweli alikuwa kalewa faru john yeye pamoja na kimada wake!?
 
Kama ni hivyo basi huyo mungu ni katili sana kuwaletea watu wake gaidi
 
Unamzungumzia huyu huyu mbowe aliyesema kuwa kavamiwa na watu wasiojulikana wakampiga kumbe ukweli alikuwa kalewa faru john yeye pamoja na kimada wake!?
Kuongea uongo na kumsingizia mtu ni Kati ya mambo mliyorithi kwa hayati ndio maana hatushangai pale baadhi yenu mliposema lisu alijipiga risasi mwenyewe za blankoo mna dhambi nyie watu Basi tu imagine mnasema mbowe ndio kahusika kumshambulia lisu Yani Basi tu mungu amewapa watanzania uvumilivu.
 
Hatutasahu sipriani musiba mwanaharakati wa rais alipoongea kwa kujiamini kwamba lisu alijipiga risasi za blankoo never shall we forget that Yani hata siasa mlizipeleka level za uhasama wa Hali ya juu mno na huu ndio urithi aliowaachia hayati maana kabla ya hapo jakaya alituachia upendo na mkapa alituachia siasa za kujenga hoja ndio maana mkapa alipenda Sana debating Ila mtu wenu aliposhika nchi akauwa mijadala ya mkapa na upendo wa jakaya wa kunywa juice na kina lissu ikulu akaleta siasa za visasi ubabe ukatili kusingiziana uongo na kukomoana.
 
Serikali ya Magufuli ilikuwa ni serikali ya propaganda ili kukamata akili za wajinga
 
1.Ni kweli alikuwa katiri kwa mabeberu na vibaraka wao

2.alikuwa dikiteta kwa mafisadi wote bila kujari cheo cha mtu

3.aligusa masirahi ya matajiri fake waliotumia kivuri cha serikali kuwakanyaga masikini

Ukweli ni kwamba hata kama aliiba kura nikwa misingi ya kumlinda masikini nae apate haki

Aliyo yaacha ni alama isiyofutika vizazi na vizazi vya kitanzania watayakuta mapinduzi makuu ya huyu mzalendo
Wewe ambaye hata kuandika tu Kiswahili ni shida, ndiyo utakuwa na uwezo wa kutambua kama kiongozi ni mzuri au mbaya? Bahati mbaya siku hizi hata elimu ya ngumbaru imefutwa, ulistahili kwenda huko.

Kujari, masirahi, katiri, kivuri - ndiyo nini?

Hata elimu ya msingi tu haikukusaidia kufahamu kuandika kwa Kiswahili? Au uliishia darasa la kwanza? Nilivyokuwa darasa la pili nilikuwa na uwezo wa kuandika vizuri zaidi kuliko ulivyoandika.

Tatizo ni elimu ndogo au akili kidogo?
 
Wewe ambaye hata kuandika tu Kiswahili ni shida, ndiyo utakuwa na uwezo wa kutambua kama kiongozi ni mzuri au mbaya? Bahati mbaya siku hizi hata elimu ya ngumbaru imefutwa, ulistahili kwenda huko.

Kujari, masirahi, katiri, kivuri - ndiyo nini?

Hata elimu ya msingi tu haikukusaidia kufahamu kuandika kwa Kiswahili? Au uliishia darasa la kwanza? Nilivyokuwa darasa la pili nilikuwa na uwezo wa kuandika vizuri zaidi kuliko ulivyoandika.

Tatizo ni elimu ndogo au akili kidogo?

Wewe ambaye hata kuandika tu Kiswahili ni shida, ndiyo utakuwa na uwezo wa kutambua kama kiongozi ni mzuri au mbaya? Bahati mbaya siku hizi hata elimu ya ngumbaru imefutwa, ulistahili kwenda huko.

Kujari, masirahi, katiri, kivuri - ndiyo nini?

Hata elimu ya msingi tu haikukusaidia kufahamu kuandika kwa Kiswahili? Au uliishia darasa la kwanza? Nilivyokuwa darasa la pili nilikuwa na uwezo wa kuandika vizuri zaidi kuliko ulivyoandika.

Tatizo ni elimu ndogo au akili kidogo?
Ujinga uko nao mwenyewe unaekalia makosa ya kiuandishi huku maana harisi ushaipata

Wapumbavu kama ww siku hizi hawapo kujitia msomi wa kushabikia ujinga tu
 
Mapungufu ya JPM ni machache mno kulinganisha na mazuri. Kwakuwa baya huonekana zaidi kwa akili finyu unaweza kudhani la kwanza ni kubwa kuliko the latter.

Anyways tusonge mbele ashaondoka kila mtu yuko safarini unaweza kuta hata we mwandishi umejaa uovu usio-neneka japo jicho linakupeleka kuona ya wengine.
JamiiForums1810231167.jpg
 
Kwahiyo kuwa na upendo na watu ni kufanya Unyonyaji
Ukishakuwa kiongozi unayependa chama chako tu na kuwaamuru Wakurugenzi wapitishe wagombea wa chama chako tu kwa kuwa anawalipa wewe, hali hiyo inakuondoa kabisa kwenye uongozi bora hata kama ungejenga miradi gani utabaki kuwa kiongozi wa hovyo. Kama sanduku la kura haliheshimiwi, ikabaki inahesabika amri na utashi wako nani awe nani, basi utabaki kuwa kiongozi wa hovyo tu. Hata ukiwa na Imani ya kuhamisha milima kama huna UPENDO, wewe ni bure tu.
 
Kuna watu walijilipa mamilioni ya pesa MH.waziri mkuu mpaka akasikitika hivi wamechukuliwa hatua gani? au mchakato wa KESI unaendelea? Enzi zake angemalizana nao Siku Ile Ile na ingekuwa fundisho
Wale wangekuwa segerea mda huu, na wale wa mafuta kigamboni ndo wangekuwa mfano... Nchi isharud ilikokuwa 2005-2015, tutegemee ufisadi wa kudondoka mtu, yaan wizara ya ilinzi et mama, duh, makamba nishati, asee kwel nchi inatafunwaaaaa, mama anasema anafoka kwa kalamu, amesahau kuwa hi Ni tz 2021
 
Back
Top Bottom