Hayati Magufuli alidhibiti ukatwaji wa umeme au mazingira yalimbeba?

Hayati Magufuli alidhibiti ukatwaji wa umeme au mazingira yalimbeba?

Mbona unaleta ubishi wa kimtaa kama mgonjwa wa fistura ya kichwa andika hoja PUNGUZA mahaba ya huyo mwehu wenu aliyefariki andika hoja mbwa wee
Hivi enzi ya kinyerezi yule mzee alisema mgao utakuwa historia
 
Hivi enzi ya kinyerezi yule mzee alisema mgao utakuwa historia
Suala la umeme Tanzania linatatizwa na migongano ya kifalsafa kuhusu umeme. Kuna wanaoamini kwamba umeme ni huduma na kuna wale wanaoamini kuwa umeme ni biashara. Wale wanaoamini kwamba umeme ni huduma kwa umma wao huwa wanajifanya kuzalisha na kusambaza umeme hakuna gharama kubwa inayotumika.

wapo wanaomini kuwa umeme ni biashara. Hawa nao hutumia njia za panya kuzipata fursa za kuiuzia Tanesco umeme ili watajirike bila ya kujali kama wanakidhi matakwa ya Uzalishaji na usambazaji wa umeme!!
 
Na ukijua hivo ni vema kwamba kila mtu atalala yooohh sasa yeye aliishi utadhani ana ahadi ya kuishi milele kutesa watu kuuwa pambafff sana alale tena
Hivi dhambi ni kutesa watu na kuuwa tu?
 
Hizo zingine ni dhambi pia lakini dhambi ya kutoa uhai wa mtu ni kufuru dhidi ya uumbaji wa MUNGU.
Kwa imani yangu ni kwamba kuna dhambi kubwa na ndogo, kuuwa ni miongoni mwa dhambi kubwa hivyo zipo dhambi zengine kubwa. Ila hapa naona imeshikiliwa dhambi ya kuuwa tu hali inayofanya kama wasiouwa wote peponi kumbe kuna dhambi zengine ambazo pia ni kubwa.
 
Vyanzo vya maji kwa ajili ya Mabwawa makubwa matatu ya kuzalishia umeme, yaani Bwawa la Mtera, Kidatu, na Kihanzi, vyote kwa asilimia tisini (90%) vinategemena na sehemu kubwa vinatokana na vyanzo vile vile. Kwa mfano sehemu kubwa ya maji yanayojaza bwawa la Mtera na Kidatu chanzo chake ni kile kile.

Kwa miaka miwili mfululizo kumekuwa na ukame mkubwa sana kwenye maeneo yanayotoa maji kwa ajili ya mabwawa ya Mtera na Kidatu. Wiki hii nilikuwa Mtera na kwa kweli hali ni mbaya sana kiasi kwamba inawezekana upungufu wa maji mtera umeweka historia kwa miaka ya hivi karibuni.

Sasa kama sehemu kubwa ya umeme wetu tunategemea umeme unaozalishwa kwa maji, na ukame ndiyo huu umeshika kasi, tunategemea muujuzi gani utakaotuzalishia umeme?

Enzi za Magufuli kulikuwa hakuna mgao mkubwa wa umeme, lakini jee pia kulikuwa kuna ukame kama ulioko sasa? Mara hii tumeshasahau ni kwa nini Enzi za Kikwete wafugaji walihamishwa toka hifadhi ya bonde oevu Ihefu?
Sehemu kubwa ya umeme wetu haitegemei umeme unaozalishwa na maji. Rekebisha hapo kwanza
Tunategemea sana gesi (65%)
Tulishatoka kutegemea maji muda mrefu sana, Sasa hivi tunategemea gesi sana

Hoja kubwa kwako ilipaswa iwe jinsi umeme unavyosambazwa. Ndio maana waziri amekuja na hiyo mikakati ya kubadilisha njia za usambazaji. Bandiko lako lilipaswa kuegemea hapo.
 
Sehemu kubwa ya umeme wetu haitegemei umeme unaozalishwa na maji. Rekebisha hapo kwanza
Tunategemea sana gesi (65%)
Tulishatoka kutegemea maji muda mrefu sana, Sasa hivi tunategemea gesi sana

Hoja kubwa kwako ilipaswa iwe jinsi umeme unavyosambazwa. Ndio maana waziri amekuja na hiyo mikakati ya kubadilisha njia za usambazaji. Bandiko lako lilipaswa kuegemea hapo.
Acha kuleta nadharia zugishi hapa (Consipirancy theories), hoja hapa ni kwamb umeme wa bei nafuu unaotegemewa kila siku na Tanesco ni wa maji na Gesi na mafuta ni umeme wa gharama kwa Tanesco kwa sababu mbali mbali za kiuzalishaji.

Kama upungufu wa umeme wa maji hauna taathira kwenye usambazaji wa umeme kwa matumizi ya kila siku, ni kwa nini Tanesco kila siku wanalalamikia upungufu wa maji kwenye mabwawa yetu kama ndiyo chanzo cha mgao wa umeme?
 
Vyanzo vya maji kwa ajili ya Mabwawa makubwa matatu ya kuzalishia umeme, yaani Bwawa la Mtera, Kidatu, na Kihanzi, vyote kwa asilimia tisini (90%) vinategemena na sehemu kubwa vinatokana na vyanzo vile vile. Kwa mfano sehemu kubwa ya maji yanayojaza bwawa la Mtera na Kidatu chanzo chake ni kile kile.

Kwa miaka miwili mfululizo kumekuwa na ukame mkubwa sana kwenye maeneo yanayotoa maji kwa ajili ya mabwawa ya Mtera na Kidatu. Wiki hii nilikuwa Mtera na kwa kweli hali ni mbaya sana kiasi kwamba inawezekana upungufu wa maji mtera umeweka historia kwa miaka ya hivi karibuni.

Sasa kama sehemu kubwa ya umeme wetu tunategemea umeme unaozalishwa kwa maji, na ukame ndiyo huu umeshika kasi, tunategemea muujuzi gani utakaotuzalishia umeme?

Enzi za Magufuli kulikuwa hakuna mgao mkubwa wa umeme, lakini jee pia kulikuwa kuna ukame kama ulioko sasa? Mara hii tumeshasahau ni kwa nini Enzi za Kikwete wafugaji walihamishwa toka hifadhi ya bonde oevu Ihefu?
Acheni kuabudu shetani. Hata wakati wa dikteta Magufuli umeme ulikuwa unakatika. Tofauti pekee ni uwazi wa taarifa. Hata wewe Allen Kilewella kipindi cha dikteta usingeweza kuandika kitu kinahusu udhaifu wa serikali yake
 
Acheni kuabudu shetani. Hata wakati wa dikteta Magufuli umeme ulikuwa unakatika. Tofauti pekee ni uwazi wa taarifa. Hata wewe Allen Kilewella kipindi cha dikteta usingeweza kuandika kitu kinahusu udhaifu wa serikali yake
Tafuta mada zangu enzi za mwenda zake uone nilichokuwa naandika. Siyo wote tulipigishwa magoti wengine tulikubali kula mtama kwa maji badala ya nyama kwenye meza ya mfalme!!
 
Labda huyo kaingia JF baada ya kufa Jiwe.
Wewe dogo usinilinganishe na wenzio. Nenda uka click jina langu mwenyewe uone joining date yangu. Mimi nimeingia humu wakati wewe hata kuvaa boxer hujajua
 
Acha kuleta nadharia zugishi hapa (Consipirancy theories), hoja hapa ni kwamb umeme wa bei nafuu unaotegemewa kila siku na Tanesco ni wa maji na Gesi na mafuta ni umeme wa gharama kwa Tanesco kwa sababu mbali mbali za kiuzalishaji.

Kama upungufu wa umeme wa maji hauna taathira kwenye usambazaji wa umeme kwa matumizi ya kila siku, ni kwa nini Tanesco kila siku wanalalamikia upungufu wa maji kwenye mabwawa yetu kama ndiyo chanzo cha mgao wa umeme?
Sijui hujanielewa? Kwenye bandiko lako umesema tunategemea maji kwa kiwango kikubwa kuzalisha umeme, Mimi nimekurekebisha kuwa hatutegemei maji kwa kiwango kikubwa kuzalisha umeme bali tunategemea gesi.ndio nikakuambia umeme unaozalishwa nchini 65% unatokana na gesi

Hapo nimekuzubaisha wapi?
 
Acheni kuabudu shetani. Hata wakati wa dikteta Magufuli umeme ulikuwa unakatika. Tofauti pekee ni uwazi wa taarifa. Hata wewe Allen Kilewella kipindi cha dikteta usingeweza kuandika kitu kinahusu udhaifu wa serikali yake
Unajichanganya, waziri anasema umeme ulikuwa haukatiki sababu mitambo ilikuwa inalazimishwa kufanya kazi sana ndio sababu sasa hivi imechoka. Wewe unasema ulikuwa unakatika. Waziri ni muongo?
 
Hapo nimekuzubaisha wapi?
Gesi haitumiki muda wote kuzalishia umeme bali maji ndiyo yanategemewa kwa kuzalisha umeme. muda wote. Tanesco kila mara wanalalamikia gharama za umeme wa Gesi na mafuta. Amini usiamini maji ndiyo chanzo kikuu kinachotegemewa kwa kuzalisha umeme Tanzania.

Gesi ndiyo lakini lazima tujiulize kama gesi ndiyo inatumika kuzalisha asilimia 65 ya umeme wa Tanzania, ni kwa nini umeme wa maji usipokuwepo kunakuwa na katizo la umeme? Sibishani na wewe bali ni kwa manufaa ya mjadala!!
 
Gesi haitumiki muda wote kuzalishia umeme bali maji ndiyo yanategemewa kwa kuzalisha umeme. muda wote. Tanesco kila mara wanalalamikia gharama za umeme wa Gesi na mafuta. Amini usiamini maji ndiyo chanzo kikuu kinachotegemewa kwa kuzalisha umeme Tanzania.

Gesi ndiyo lakini lazima tujiulize kama gesi ndiyo inatumika kuzalisha asilimia 65 ya umeme wa Tanzania, ni kwa nini umeme wa maji usipokuwepo kunakuwa na katizo la umeme? Sibishani na wewe bali ni kwa manufaa ya mjadala!!
Sijui kwa nn unabisha hili la Tanesco kutegemea zaidi gesi kuzalisha umeme kuliko maji.

Maji yanazalisha umeme kwa 33%, yakipungua au kukiwa na ukame haimaanishi tatizo la umeme halitakuwepo. Kwa kuwa kutakua na upungufu kwenye uzalishaji.

Hata hivyo nimekueleza tatizo la mgao wa umeme kwa sasa halitokani sana na maji, linatokana na kuzidiwa na kuchoka kwa mitambo ya uzalisha Kama waziri anavyosema kila mara. Hapa tunapoongea kuna mgao wa umeme kwa baadhi ya mikoa, na sababu iliyotolewa ni hiyo kutengeneza mitambo
 
Back
Top Bottom