Ikiwa tumeingia mwezi wa 3 , ambao kwa mahesabu ya Tanzania na wanazuoni ni mwezi wa Mungu ( wenye akili wameelewa ) , tutajitahidi kuanzia leo na kuelekea mwisho kuwaletea makala za kusikitisha za uozo wa serikali ya awamu ya 5 na viongozi wake , wakiwemo waliokufa na walio hai , wakiwemo wenye madaraka hadi leo na wale ambao wako Benchi .
Tunachoahidi ni kuhakikisha kwamba kila hoja zetu zitakuwa na ushahidi uliotukuka bila longolongo yoyote , kikubwa twende na kanuni ileile ya kwamba AKUANZAE MMALIZE
Pichani ni Tito Magoti aliyetekwa na kunusurika kuuawa na utawala huo akipelekwa mahakamani , nusura yake ilitokana na makelele ya Watu kutaka apatikane akiwa hai , hii ni baada ya Mashuhuda kuona namna alivyotekwa tangu mapema kabisa , huyu aliponea tundu la sindano
View attachment 2933711
Ombi letu ni hili , kila mwenye ushahidi wa mambo yote machafu ya awamu ya 5 ajitokeze kuuleta , katika makala zetu hizi kabambe za Mwezi huu wa Mungu , HATUTAKUWA NA MSWALIE MTUME .
NITASEMA KWELI DAIMA FITNA KWANGU MWIKO