Hayati Magufuli alikuwa kiongozi mbaya; aliua mifumo ya utawala bora akawadanganya Watanzania na vitu vidogo kama madaraja, stendi, ndege n.k

Sio unafiki au kutojua. Watu wanamjaji Magufuli kwa ujenzi wa madaraja na flyovers. Kila rais anajenga hayo mambo kama mpango endelevu wa nchi.

Ushenzi wa Magufuli ni mkubwa na unajulikana na wenye uelewa, wajinga kama kawaida hawajui mambo.
Kwamba watu walimpenda Magufuli kwa sababu ya madaraja na flyover? Kwahiyo hao watu hawamkubali sasa Rais Samia kwa sababu hajengi madaraja na flyover? Ina maana Magufuli aliposema "mtanikumbuka" alikusudia hayo madaraja na flyover?
 
Mungu yupo aisee kwa jinsi tulivyoishi maisha ya huzuni kipindi lile jamaa Lipo tuliteseka sana Mungu akaamua aturudishie furaha yetu
Hatuna option nyengine zaidi ya kuchagua kati ya mfumo wa kidikteta au serikali dhaifu.
 
Kwamba watu walimpenda Magufuli kwa sababu ya madaraja na flyover? Kwahiyo hao watu hawamkubali sasa Rais Samia kwa sababu hajengi madaraja na flyover? Ina maana Magufuli aliposema "mtanikumbuka" alikusudia hayo madaraja na flyover?
Na viongozi wazuri hawakumbukwi kwa miundombinu; akina Nyerere, Mandela, etc ni mifano mizuri.
 
Jibu hoja. Pamoja na kuua bunge ili liwe la kupiga mhuri yale anayotaka afanyike kama vile kutumia hela nje ya budget aliua aliua pia 1) mfumo wa haki kwa kuteua majaji bila kufuata vigezo kama kumpa mtu ujaji eti kwa sababu ameandika hukumu kiswahili 2) Uteuzi wa M-DED na ma-RAS kuweka makada wa CCM na kuathiri utendaji na uchaguzi wa mwaka 2019 na 2020 3) Kuanzisha miradi mikubwa inayohitaji pesa nyingi bila kuzungatia ilani ya uchaguzi ya CCM yenyewe ya mwaka 2015 4) kuwekeza hela nyingi nyumbani bila kuzungatia maslahi ya nchi.
Haya ni kwa uchache tu.


Sent from my Infinix X689F using JamiiForums mobile app
 
Ni kweli kabisa ila siku tukichinjana kwa wizi wenu ndio mtaelewa maana kuna wanajeshi wanafia nchi yao kujenga nyumba zao mpaka wakope wakati nyie mnatafuna tu keki peke yenu na wao wanaishia kuwalinda.ipo siku tutaelewana tu pale Dodoma.
 
Sasa unashauri tumfanye nini huyu Magufuli Ili asiendelee na hii tabia yake. Au aletwe kwanza mbele yako ajitetee (kusudi tufuate utawala bora na haki)! Unasemaje kuhusu hilo?
 
Kama nimeandika uongo au nimemsingkzia sema jamiiforum ni jukwaa huru.
Umemsingizia, hujui unachotaka na unacho kitetea. JPM si ameisha kufa Sasa unayasema hayo Ili ajisahihishe au aache? Mbona miaka ya utawala wake hukuonyesha Kwa vitendo kwamba hukubaliani na anayo yafanya? Inawezekana wewe ni wale waliokuwa washauri wake wakuu!
 
Eti good what?
Story za jaba na hot air.
 
Bora huyu mwenye vitu vidogo madara. Ndege elimu bure vituo bya afya sgr stend za mabasi nk kuliko huyu aayeuza nchi kwa wajomba zake waarabu.jinga kabisa mleta mada.
 
Sahizi kubwa tulilo nalo wananchi ni uporaji wa bandari yetu ba kumgawia mwarabu.

Kwa marehemu, kuhusiana na hili la bandari ni bunge batili alilotuachia. Marehemu amelala, haitusaidii kuendelea kumsakama, tupambane na hawa majuha wa sasa.
 
Wewe ni mbaya zaidi yake! Mbona hukuwahi kumwambia alipokuwa hai unaanza kutusumbua leo akiwa hayupo? wewe uliye mzuri umetufanyia nini? Umeifanyia nini Tanzania so far? Mh Magufuli alishamaliza kazi yake aliyotumwa na sasa amepumzika! Ni wajibu wako wewe unayejiona mzuri kuliko yeye kufanya mazuri!

Acha marehemu wapumzike, usitupigie kelele!
 
Unaona unavyotukanwa usirudie tena kuongea upuuzi kama huu.
 
Sawa lakini ashakufa. Kwa nini usiachane naye mkuu? Hawezi kuja kujitetea kwa sababu yumo ardhini.
 
Hii ni kulingana na mtzamo wako tu,
Maybe katika maamuzi magumu ulikutwa na ukajenga chuki moyoni mwako.

Ila kuna shahidi mbalimbali kama ulivyosema wewe, Magufuli aliwini mioyo ya hao unaowaponda kuwa wanaupeo mdogo.

Kumbe nchi yetu hii ina percentage kubwa ya wenye upeo mdogo kiasi hiki. Hii ni ajabu, ila kheri yako wewe unaupeo mkubwa sana.

Unaposema kuwa aliua utawala bora, means mwanzoni kabla yake utawala bora ulikuwepo.
Wanasahau kwamba popote penye utawala bora au good governance kwa kizungu hayo yote ya barabara madaraja stendi masoko ya kisasa huja automatically.
Je hayo mambo madogo kwa wenye upeo mdogo kama tuflyover, tusoko twa kisasa, tudaraja na tubarabara kipind hicho mwanzoni tulishindwa vipi kuwepo?.

Huoni hata kasi yake ya kutujenga huto tujitu tunampa credit mwendazake?
 
Hii ni kulingana na mtzamo wako tu,
Maybe katika maamuzi magumu ulikutwa na ukajenga chuki moyoni mwako.

Ila kuna shahidi mbalimbali kama ulivyosema wewe, Magufuli aliwini mioyo ya hao unaowaponda kuwa wanaupeo mdogo.

Kumbe nchi yetu hii ina percentage kubwa ya wenye upeo mdogo kiasi hiki. Hii ni ajabu, ila kheri yako wewe unaupeo mkubwa sana.

Unaposema kuwa aliua utawala bora, means mwanzoni kabla yake utawala bora ulikuwepo.
Wanasahau kwamba popote penye utawala bora au good governance kwa kizungu hayo yote ya barabara madaraja stendi masoko ya kisasa huja automatically.
Je hayo mambo madogo kwa wenye upeo mdogo kama tuflyover, tusoko twa kisasa, tudaraja na tubarabara kipind hicho mwanzoni tulishindwa vipi kuwepo?.

Huoni hata kasi yake ya kutujenga huto tujitu tunampa credit mwendazake?

Alivyotackle lile janga la corona na kuihandle pressur, napo huoni kuwa alituwini sisi wenye upeo mdogo..

Wenye upeo mdogo wanakila sababu ya kukamatwa na mwendazake.
Wewe na utawala bora uliopo mmefanya nini zaidi ya lawama tu kila siku, mara migao ya maji, umeme, bei za vitu vinapanda tu, mnarudisha corona redioni..
Dharau ofisi za umma.. Na saizi wenye upeo mdogo mmeshindwa hata kuwajibu kuhusu bandari ili wasiwe na hofu na nchi yao... Ninyi hamjali kisa mnamamlaka.


Muacheni Magufuli, wewe unapambana hadi na marehemu hadi leo?
 
Magufuli ameshatangulia mbele ya haki. Na ubaya kama unavyosema ulikwenda na yeye alipokwenda. Hebu niambie, kama sasa hakuna mabaya yanayoendelea? Je tunaishi kwenye nchi ya maziwa na asali na unono usiokoma?
Tunapenda kukataa ukweli kwamba, kila siku inakuja na mazuri na mabaya yake. Muda ndio utaamua nani mbaya mbaya na nani mbaya mzuri. Kuwa kiongozi ili watu wakuchekee kwa kuruhusu kila mtu afanye anachotaka, mwisho wake ni kulia mwenyewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…