Hayati Magufuli alikuwa na uelewa mdogo wa masuala ya dini, asilaumiwe

Hayati Magufuli alikuwa na uelewa mdogo wa masuala ya dini, asilaumiwe

HAYATTI MAGUFULI ALIKUWA NA UELEWA MDOGO WA MASUALA YA DINI, ASILAUMIWE.

Na, Robert Heriel.

Leo kijiweni kuna mada Moto ilikuwa ikiendelea inayohusu masuala ya UVAAJI WA BARAKOA, baadhi ya wachangiaji wa mada walimtumia zaidi Hayati Magufuli katika kutetea hoja zao kuwa hakuna ulazima wa kuvaa Barakoa, isipokuwa kumwomba Mungu pekee inatosha.

Vijana hawa niligundua wamepata elimu hiyo kutoka kwenye hotuba alizokuwa akizitoa Mzee wetu, Hayatti.

Hicho ndicho kimenifanya niandike andiko hili.

Kwanza nianze Kwa kusema kuwa, Hayati Magufuli kutokana na Hotuba zake alizokuwa akizitoa na matamshi yake, nachelea kusema Hakuwa na Uelewa, Elimu, ujuzi na maarifa ya mambo ya kiroho, Magufuli Hakuwa anaujua vizuri dini licha ya kuwa alikuwa akipenda Sana kumtaja mwenyezi MUNGU.

Na mtu yeyote ambaye anaufahamu mdogo, ujuzi hafifu, Uelewa Finyu na Elimu duni ya Kidini na Kiroho basi lazima mtu huyo awe Mpotoshaji.

Hii ni kusema Hayati alikuwa Mpotoshaji hasa wa masuala ya kiroho kwani Hakuwa na Uelewa mkubwa wa mambo hayo.

Sio ajabu ndio maana alikuwa akiwanyamba baadhi ya viongozi WA dini waliokuwa wakivaa Barakoa mpaka Kanisani. Tena alikuwa akiwadhihaki na kuwakejeli Jambo ambalo Kama angejua walau hata robo ya elimu ya Dini au mambo ya kiroho asingefanya hivyo.

Andiko hili limekusudia kuwaonya Wale wote waliokuwa wakimuamini Magufuli hasa kwenye kukataza matumizi ya Barakoa au Chanjo Kwa kutumia mgongo wa Kidini ati wamtegemee Mungu. Acheni Fikra hizo, huyo uliyemuamini Hakuwa na elimu ya Kidini wala kiroho.

Mungu hategemewi na wajinga, Mungu hategemewi na watu wasiomfahamu, wasiomjua, wasio na Uelewa naye, wasio na elimu yake, wasio na maarifa naye, Mungu hawezi kutegemewa na watu wa namna hiyo.

Neno la Mungu kasema; MJUE SANA MUNGU ILI UWE NA AMANI

Pia linaongeza kuwa Watu wangu wanaangamia Kwa kukosa Maarifa.

Kisha unaeleza pia, ya kaisari mpe kaisari; ya Mungu mpe Mungu.

Magufuli anaweza kuwa Bora kwenye Maeneo mengi tuu ambayo nilishawahi kuyaeleza lakini haimuondolei udhaifu wake wa kutokujua Elimu ya Kidini na Kiroho ambao huo ni udhaifu.

Hivyo Wale mnaofuata mafundisho yake na falsafa yake ya kutokuvaa Barakoa Kwa kutumia VIGEZO vya kiimani, VIGEZO vya Kidini mkae mkijua Mzee alikuwa anaelimu duni ya Kidini na Uelewa hafifu.

Hivyo msije mkaangamia Kwa kukosa Maarifa.

Pia nitoe onyo Kwa viongozi wengine wakisiasa, Kama huna elimu ya Jambo Fulani msipende kujifanya mnazielezea elimu msizozijua vyema, mnaathiri jamii.

Robert Herieli
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro
Namba zako hazipatikani
 
Kwanza nianze Kwa kusema kuwa, Hayati Magufuli kutokana na Hotuba zake alizokuwa akizitoa na matamshi yake, nachelea kusema Hakuwa na Uelewa, Elimu, ujuzi na maarifa ya mambo ya kiroho, Magufuli Hakuwa anaujua vizuri dini licha ya kuwa alikuwa akipenda Sana kumtaja mwenyezi MUNGU.
.
.
.
Nimeishia hapo kusoma yan unaakili za kipumbavu sijapata ona
 
Huko pengine sina Uelewa Napo Sana

Ila kwenye dini Mara nyingi alikuwa akipotosha.

Viongozi wote wa dini waliozidisha unafiki waondolewe.

Kuna yule Mufti aliyesema Bwana Yesu asifiwe sijui Kwa nini Waislam hawamuondoi.
Hivi unajua Waislamu wanamtambua Yesu / Issa kama Nabii ?, Sasa kwa imani yake / zao kuna ubaya gani wa kumsifu Nabii ?

Yaani hizi Imani zilizokuja tabu tupu..., badala ya kutuunganisha naona zinatutenganisha..., na Ukizingatia hii ni karne ya 21, nadhani tunahitaji kuchunguzwa vijwani mwetu...
 
Rais Magufuli alijitofautisha sana na Marais waliopita naamini ata kwa wanaokuja, Nisime Rais Magufuli alitumia 90% ya ubongo wake kuamua masuala ya kitaifa kuliko Marais wengine. Rais Magufuli hakuwa mtu wa kumpelekea karatasi asome na asaini hapana! Alikuwa mtu anaesoma asopopata majibu yakulidhisha alikuwa anatafuta majibu kwa njia zake.

Kuhusu issue ya Corona sioni sehemu yoyote yakumlumu cos angekuwa amekosea basi 60% ya wananchi wa ili Taifa tungekuwa hatuko Duniani, Ugonjwa wa Corona ni ugonjwa uliombatana na propaganda na ndiyo maana alipiga stop farmigation kuwa haiui kirusi lakini wakati anasema mkamtungia mpaka wimbo kumcheka kupitia wakina Roma mpaka WHO walipokuja kisema kuwa kweli farmigation hakiui kirusi cha Covid, alikataa Lockdown ata barakao alisisitiza kama kuvaa vaa uliyotengeneza hapa nchini. Leo ukiniambia Rais Magufuli alifail kwenye issue ya Covid nitakuomba unipe ulinganifu nani alifauru zaidi yake?

World Bank juzi amewahakikishia bara la Ulaya muwa atahakikisha kufikia 60% ya waafrika watakuwa wamepata chanjo ya Covid, Rais magufuli hakukataa kabisa chanjo ila alisema lazima tujilidhishe hipi ni sahihi kwetu! Sio mtu analeta chanjo huku anakupa mkopo alafu anakuambia kama unataka hii hela lazima uchukue chanjo ya Covid..! Na ndiyo maana ata ilani ya chama 2020-2025 iliona ielekeze serikali kutenga bajeti ya kutosha kwaajili ya utafiti NIMR.

Hayati Rais Magufuli alikuwa akituambia wazi tuendelee kuchapa kazi ila tujifukize, tungwe tangawizi ikibidi na mazoezi na kweli mi binafsi nilipata hicho kitu kinaitwa Covid wimbi la kwanza na niliponea kwa Tangawizi na malimao + kitunguu swaumu na sikuwai kulala ata siku moja eti nisiende kibaruani
Sauti hii iskike mpaka oldonyo lengai.........bandiko bora sana
 
Kwanza nianze Kwa kusema kuwa, Hayati Magufuli kutokana na Hotuba zake alizokuwa akizitoa na matamshi yake, nachelea kusema Hakuwa na Uelewa, Elimu, ujuzi na maarifa ya mambo ya kiroho, Magufuli Hakuwa anaujua vizuri dini licha ya kuwa alikuwa akipenda Sana kumtaja mwenyezi MUNGU.
.
.
.
Nimeishia hapo kusoma yan unaakili za kipumbavu sijapata ona

Yeye mwenyewe aliwahi Kiri Jambo hilo sasa wewe utasema nini
 
Magufuli Yu hai Hadi leo. Imeshindikana kusahaulika japo ni marehem. Ni miezi 3 kuelekea minne..

Kwakawaida
Marehemu akisha ondoka basi tunamsahau na mabaya yake.

Lakini kwa huyu!! Utafikiri yupo ikulu bado. Huyu mtu hakika alikua chaguo la mungu kuiongaza Tanzania.
 
Hivi wote mnaoponda mnaijua dini kweli na mnaimani iliyotimilifu? Isiyopungua hata punje ya aladin
 
Marehemu alitumia muda wake mwingi kuwapumbaza watu. Na wajinga aliwaokota hasa. Aliwadanganya watu:

1) kuhusu makinikia. Kwa mwenye uelewa wa sekta hii, alichokuwa akiongea marehemu ilikiwa ni uwongo na ujinga wa hali ya juu

2) kuhusu gas. Eti imeuzwa kwa wachina, na wajinga wakaamini

3) kuhusu uchumi, eti tupo vizuri, wakati kwenye vigezo vyote tulianguka wakati wa utawala wake

4) kuhusu matajiri, eti wote ni mafisadi na majizi

5) kuhusu uwekezaji kwenye LNG, hakueleza jinsi alivyoharibu mpaka wawekezaji kuamua kuondoka na kwenda kuwekeza Mozambique. Aliwatumia maofisa mbalimbali kutaka warudi, wakamgomea, na kumweleza kuwa watafikiria kurudi baada ya miaka mitano

6) kuhusu Barrick, hakueleza ukweli jinsi alivyorudi na kuwapigia magoti, na kuwakubalia matakwa yao ikiwemo kutumia mahakama za kimataifa badala ya mahakama za ndani alizokuwa amezinajisi

7) kuhusu masuala ya kiimani, hakuwa na uelewa hata wa ABC. Hakujua jinsi Mungu alivyomwambia Nuhu atengeneze safina. Je, Nuhu asingetengeneza safina, badala yake asubirie muujiza wa Mungu, angepona? Wala hakujiuliza ni kwa nini Bwana wetu Yesu alivyoambiwa na shetani ajirushe toka juu, naye akagoma. Hakujiuliza, kwa nini Waisrael ili kujikomboa, Mungu aliwaambia waondoke usiku, watembee na fimbo zao mikononi. Kama wangeamua kukaa pale pale kwa Wamisri, wangepona? Hakujua kuwa Mungu ametuumba tufanye kazi ili kujiokoa, ili kupata mahitaji yetu ya kila siku, naye huweka baraka na miujiza katika zile jitihada zetu.
Ahsante sana Mkuu.
 
Magic is for those who believe...

The law of life is the law of beliefs...

A man become what he thinks about most of time...

What you think and feels is what you're attracting to...

Imani sehemu yake moyoni wala haina mafungamano na elimu Bali matendo ya kiimani (ibada) yanahitaji elimu msingi....
 
Kwanza nianze Kwa kusema kuwa, Hayati Magufuli kutokana na Hotuba zake alizokuwa akizitoa na matamshi yake, nachelea kusema Hakuwa na Uelewa, Elimu, ujuzi na maarifa ya mambo ya kiroho, Magufuli Hakuwa anaujua vizuri dini licha ya kuwa alikuwa akipenda Sana kumtaja mwenyezi MUNGU.
.
.
.
Nimeishia hapo kusoma yan unaakili za kipumbavu sijapata ona
Ni Kati ya waliopandikizwa ili kuua Legacy ya Magufuli na wanaotaka Hela za Mikopo ya huo ugonjwa wa Propaganda za Kiuchumi.Pumbavu Sana hawa wachumia tumbo
 
Mungu aliwapa sheria na kanuni za afya waisraeli (mambo ya walawi)

Aliwaambia wanawe kabla ya kula, kuoga kabla ya kuswali, wasile wala kuywa vitu kadhaaa.

Mwendazake alikuwa mjinga tu
Na hakuwahi kujua biblia vizuri
 
WABONGO SISI HATUWEZI ENDELEA KAMWE,KWHYO KAPU LA MABAYA LA MHE.MAGUFULI HALINA HATA MOJA JEMA?KWHYO NYIE MUNGU KUJUA ETI KWA ALYOYAFANYA ANAENDA MOTOTNI?KUMBUKA ALKUFA HKU AKIPAKWA MAFUT MATAKATIFU KABLA YA KIFO,UNJUA INAMAANISHA NN HIYO KW SISI WAKRISTO HUSUSAN WAROMA?MUNGU SI MWANADAMU,HAFANYI KAZI KWA KUONGOZWA NA BINADAMU NA HAITATOKEA,HATA KAMA ALKUA NA MABAYA UTAJUAJE KAMA ALTUBU KWA MUNGU WAKE?WEWE UKIFA LEO UMEJIANDAA?AU UNAZANI MTAISHI MILELE WATU MNAOMKASHFU MAGUFULI KAMA VILE HAMJAZALIWA?SHAME ON U AND ON UR BLACK ASSS..NYIE MNAOJUA DINI MPO WAPI?NA JE MSHAJHAKKSHIA UFALME WA MBINGU?MAKKUMA NYINYI
 
Askofu Mkuu wa Jimbo la Darces Salaam Yuda-Thadei Ruwa'ichi aliimiza waumini wavae barakoa Mwendazake akaenda St . Peter akasema hana imani , yalikuwa mambo ya ajabu sana kushindana na kiongozi wake wa kiroho Mwendazake alijifanya yeye ni kila kitu hakimu yeye, jaji. spika, mwanasheria mkuu, dpp kila kitu alikuwa yeye, mbaya zaidi akatundanganya hata papai lina corona
PAMOJA na UJANJA WoTE aliokua nao nakusali sana alikwepa kusimama na kudanganya watu kupitia kanisa .
Naye ni

Mwl Julius kambarage nyerere(mungu amrehemu)
 
Hivi unajua Waislamu wanamtambua Yesu / Issa kama Nabii ?, Sasa kwa imani yake / zao kuna ubaya gani wa kumsifu Nabii ?

Yaani hizi Imani zilizokuja tabu tupu..., badala ya kutuunganisha naona zinatutenganisha..., na Ukizingatia hii ni karne ya 21, nadhani tunahitaji kuchunguzwa vijwani mwetu...
Acha ujinga usimlinganishe Bwana Yesu NA huyo yesu faki sijui anaitwa issa. Huyo ni yesu wenu wa huko msikitini lakini Yesu aliye hai hawezi kuwa issa.
 
WABONGO SISI HATUWEZI ENDELEA KAMWE,KWHYO KAPU LA MABAYA LA MHE.MAGUFULI HALINA HATA MOJA JEMA?KWHYO NYIE MUNGU KUJUA ETI KWA ALYOYAFANYA ANAENDA MOTOTNI?KUMBUKA ALKUFA HKU AKIPAKWA MAFUT MATAKATIFU KABLA YA KIFO,UNJUA INAMAANISHA NN HIYO KW SISI WAKRISTO HUSUSAN WAROMA?MUNGU SI MWANADAMU,HAFANYI KAZI KWA KUONGOZWA NA BINADAMU NA HAITATOKEA,HATA KAMA ALKUA NA MABAYA UTAJUAJE KAMA ALTUBU KWA MUNGU WAKE?WEWE UKIFA LEO UMEJIANDAA?AU UNAZANI MTAISHI MILELE WATU MNAOMKASHFU MAGUFULI KAMA VILE HAMJAZALIWA?SHAME ON U AND ON UR BLACK ASSS..NYIE MNAOJUA DINI MPO WAPI?NA JE MSHAJHAKKSHIA UFALME WA MBINGU?MAKKUMA NYINYI
Hayo mafuta uliona akipokwa au unaleta hadithi za wanasiasa waongo hata tarehe ya kifo tunaambiwa siyo hiyo iliyotangazwa.Maisha ya mtu nimatendo na maneno yake nandivyo vitakavyomuhukumu
 
Back
Top Bottom