Hayati Magufuli anashambuliwa kila kona. Siyo kesi, ila mambo yaende; yasipoenda wananchi watawazomea kila kona

Hayati Magufuli anashambuliwa kila kona. Siyo kesi, ila mambo yaende; yasipoenda wananchi watawazomea kila kona

Spidi aliyokuwa nayo Marehemu Magufuli ya kufanya mambo yaende na kufanyika kwa kasi inayoonekana wazi kwa kila mtu, ni challenge kwa waliopo iwe serikalini au bungeni au Mahakamani kuifikia baada ya kifo chake

Matarajio ya wananchi ni kuwa spidi itakuwa kubwa kuliko ile au itabaki ile ile.

Sasa hivi Marehemu anapondwa sana kuwa ohh alikuwa dikteta mara ohh alikuwa fisadi mara ohh staili yake haifai

Hakuna shida; cha msingi wananchi wanataka mambo yaende. Tukaneni matusi yote ila mwisho wa siku wananchi watalinganisha output yenu watukanaji na ya Magufuli kwenye kugusa maisha ya wananchi wanyonge

Marehemu Magufuli kila kona anakuwa attacked siyo kesi ila mambo yaende yasipoenda wananchi watawazomea kila kona Kila mtakakopita wadhalilisha Magufuli. Mtazomewa na kuambiwa Magufuli angekuwa hai hili lingefanyika na watawazomea.
The tax collection was not FAIR it was ROBBERY thus why
 
Kwa hiyo CAG ni msemaji pia waTraffic kuhusiana na foleni na misongamano ya magari kwenye stendi za nchi hii? Kwenye ukaguzi wake wa mahesabu? Hakuna stendi ngumu kuingia na kutoka kama ya Makumbusho.Sijaona kwenye ripoti ya mheshimiwa msemaji wa Traffic CAG.Mwakani aweke kwenye ripoti yake
Basi uliza kwann CAG anakagua ndege wakati yeye sio injinia?
 
Na hao ndio population kubwa ya Tanzania zaidi ya asilimia 80 na ndio wanyonge wenyewe waliompigia kura na ndio alijitahidi kuwapelekea miradi mingi na elimu bure nk

Ndio aliosimama nao.Lisu alisimama na wanaoielewa akaambulia kura milioni moja

Magufuli akasimama na wasiojielewa wenye elimu duni na uelewa duni na machinga na ma ntilie nk.

Nakubaliana na wewe alisimama na wengi wa chini hakusimama na wachaje wa juu au middle class
Ungejua moja ya sababu iliyofanya usimuone leo ni pamoja na kuhujumu uchaguzi nafikiri ungefyata kabisa wala usingeongea huu upumbavu unaouongea humu.

Magufuli katika uhai wake hakutaka uchaguzi wowote wa maana na akatuteulia viongozi nchi nzima toka kwenye vitongoji hadi yeye rais lakini imemgharimu vilivyo hakuna rais atakayekaa arudie huu upumbavu na atakayethubutu tu mchezo utarudiwa.

Eti alitabiri kifo cha vyama kabla ya 2020 akaacha kutabiri kifo chake sasa mjanja nani, kafa kiofisa na tai shingoni..alifikiri kuzungukwa na bodyguards kibao ni dawa lkn watu siku hizi ni mwendo wa Hi-Tech that goes beyond the physical security detail. Ulikuwa wapi kuzikwa naye?
 
muulize mtaakamu yeyote wa uhalifu duniani atakuambia unapunguzwa haumalizwi!

Magufuli alijitahidi sana kuupunguxa
Sema alijitahidi kupika data

Ndiyo maana hata riport ya prof assad ambayo ilikuwa inaonesha ubadhirifu wa fedha za umma aliikata ilikuficha madudu yake
 
umeme kila kijiji zilikuwa nyimbo? Barabara bora za lami.uswahilini na vijijini zilikuwa nyimbo?

Vituo vya afya kila eneo zilikuwa nyimbo?Miradi ya maji kila kona zilikuwa nyimbo?
Adabu sekta ya umma kuhudumia wanyonge zilikuwa nyimbo?

U salute you Magufuli wherever you are .Ume set record ambayo itachukua miaka mingi kuivunja kwa yeyote atakayeshika serikali
Ongezea na kufungia media
 
Rudi kwenye msingi wa hoja yako Chief!

“Lawama ziende kwa aliezika mchakato wa Katiba Mpya!”

Hayo mengine hayanihusu!
Kama unafikiri kuna aliyezika mchakato wa katiba tofauti na unayemtetea utakuwa sayari nyingine. Jiulize alizuiliwa na nani kuufufua? Au kwa uelewa wako unaamini marehemu hakuwa na mamlaka hayo? R.I.P marehemu.
 
Yuko mtu anadanganywa na kadanganyika. Anafikiri hii nchi ikikwama watakao jibu ni wanao mdanganya. Kumbe watakuwa pembeni wakicheka na kutabasamu.

Hajui kwamba kajichafua na kuchafua anaofanya nao kazi. Sijui kazi atafanya na nani sasa? Unachafua mpaka Jeshi na vyombo vya Usalama kuwa havi kufanya kazi yake kikamilifu wakati ndio mbereko inayo kubeba kila uchao.

Chupi ikichanika kinyesi hutapakaa....naona mzee hali tete....
 
Ila mimi huwaga siwaelewi baadhi ya watu kwaio hao mawaziri nao wanakubali waonekana wezi for the sake ya kuhujumu legacy ya mtu aliyejipumzikia ?? Haya watu wanamchafua ili kiwe nini ?? Nisaidie kuwaza

Mawazo yako yameishia kuhujumu legancy basi. Wewe ndio wamekutuma uwasemee wamekubali. Angalia sura ya Kigwangala na ujiulize kwa nini kasema ana mwachhia Allah whalahi.
 
Achana na hao wamama wenye uelewa mdogo(ashakum si matusi),wewe msimamo wako ni upi juu ya uongozi wa the Late JPM?
Mimi kiimani yangu siruhusiwi kumsema marehemu kwa ubaya ngoja apambanae na amali zake kaburini...!!!
 
He is not being attacked,mfalme amevuliwa nguo,wananchi wamefunguliwa masikio na macho yao waweze kuona na kusikia yaliyokuwa nyuma ya pazia.

Mzee Magufuli alibana uhuru wa media kuripoti habari za uchunguzi,uhuru wa watu kujadilia mada hasi za utendaji wa wake na serikali yake. Mzee amekufa na suddenly tumepata uhuru wa kusikia kuona na kujadili taka ambazo zilifunikwa na sheria kandamizi za habari.
Very good. MUOSHA,HUOSHWA.
 
Mawazo yako yameishia kuhujumu legancy basi. Wewe ndio wamekutuma uwasemee wamekubali. Angalia sura ya Kigwangala na ujiulize kwa nini kasema ana mwachhia Allah whalahi.

Leo nakufundisha mdogo wangu, ukiona mtu anamtaja taja sana Mungu ndo ukae nae kwa makini sana wengi wao huwaga wanafiki.

Cha pili cha kujifunza CAG hatoi ripoti kama hajakuhoji na kujiridhisha na maelezo yako na huwasilisha kila kitu hivo mpaka ukiona mtu yupo hapo juu alishaulizwa lakini hakutoa maelezo yanayostahili moja ni juu ya hizo fedha na pili juu ya mchakato. (Funga katiba ibara ya 143 na 144).
 
Huyu alifurushwa kutoka TRA anaweza akatumiwa vilevile. Sisi tuliona siku ya tatu baada ya maziko hii ripoti kupokelewa na ilikuwa Jumapili.

Wapambe nuksi wakaanza kumchafua mwenda zake kwamba ingekuwa ni yeye angekuwa kanisani akihutubia kutoka madhabahuni. Mungu akawa amewasahaulisha na wakasahau mwendazake ilikuwa ni zake pia kuapisha jumapili.

Mareheme siku ya tatu kaburini watu walianza kumpakaza hii oil chafu kama mafuta.
Kama Taifa tumekosea mahali, viongozi wameshindwa kutuongoza tukaomboleza vizuri msiba huu kwa taratibu za kitanzania na kiafrika, tumenajisi maombolezo. Sasa ni swala la muda tutashuhudia mengi, wengine bado wanaomboleza wakimaliza nao watanena.Marais wa SADC waliasa tuwe na moyo mkuu katika kuomboleza.Naona mpasuka kichama mkubwa sana
 
Kama Taifa tumekosea mahali, viongozi wameshindwa kutuongoza tukaomboleza vizuri msiba huu kwa taratibu za kitanzania na kiafrika, tumenajisi maombolezo. Sasa ni swala la muda tutashuhudia mengi, wengine bado wanaomboleza wakimaliza nao watanena.Marais wa SADC waliasa tuwe na moyo mkuu katika kuomboleza.Naona mpasuka kichama mkubwa sana

Hawa ni watu walio shindwa kabla ya kuanza na hurumìa Taifa hili. Tunajihurumia watu wa Taifa hili lakini JPM mwenda zake alituasa sana kuhusu kumtegemea Mungu. Hivi kweli Mungu hata weza kututetea? Kazi hii tumkabizi yeye. Neno la Mungu lasema hivi.

Kumbukumbu la Torati 20:4
Kwa maana BWANA Mungu wenu(Wetu Watanzania), ndiye awaandaye kwenda kuwapigania juu ya adui zenu. Ilikuwaokoa ninyi.

Zaburi 44:5
Kwa nguvu zako(Mungu/Bwana Yesu) tutawaangusha watesi wetu;
Kwa jina lako(Bwana Yesu) tutawakanyaga watupingao.

Romani 8:31
Basi, tuseme nini juu ya haya? Mungu akiwa upande wetu, ni nani aliye juu yetu?

Maombi na Kufunga kwa Watanzania waliokuwa wana himizwa na mwenda zake hayata kuwa bure na kupotea kama machozi ya mamba majini.

Bwana Yesu tunakusihi kwa nguvu ya Jina lako mapenzi yako ya katimizwe katika Taifa hili. Kafara ya kifo cha mtumishi wako John Pombe Joseph Magufuli isiwe bure, isiwe ndio nafasi ya Jina lako kuzalilishwa/ kukejeliwa lakini iwe nafasi ya Utukufu na Ukuu wako kuonekana. Amen.
 
Utawala mpya unapaswa kupambana kuliondoa tabaka aliloliacha linakuwa kwa kasi la wanyonge kulitoa katika unyonge na kulipa maisha bora, hilo ndilo tabaka lake lililompenda sana
Mkuu kwa mtazamo wangu mimi, hatuna utawala mpya. Kiongozi aliopo alikuwepo wakati wa Magufuli. Sitarajii binafsi jipya Sana kutoka kwa huyu mama. Naame hivyo kwaajili ya Jambo Moja tu, hakuna Jambo ambalo mwenda zake , alilifanya ambalo halikuwa na Baraka za mama.

Lakini pia tunaposema mama aondoe tabaka la mwenda zake, tabaka hilo ni akina nani? Ukiangalia kimfumo wa kiuongozi hata Yeye pia ni tabaka lake, je unamaanisha aondoe wateuliwa wote wa Magufuli,? Ni Jambo gumu hakuna Kiongozi aliyewahi fanta hilo kwa mara Moja. Ninachomsihi mimi aache kufukua makaburi aliyochimba Yeye mwenyewe na mwendazake akiamini kuwa ni kumpaka matope mwenda zake.

Kama Yeye mpenda nchi mbona hakuwahi kujiuzulu kuonyesha kuwa utawala, Mwenda zake, hafanyi yapasayo.? Ikumbukwe dakika zamwisho alituaminisha kuwa mwenda zake Yuko salama. Huyu ni sehemu ya Tabaka la mwenda zake. Mwenda zake kuna aliyofanya mema Sana, kuna ambayo alifanya vibaya kabisa, tuchukue mema tusonge mbele, tusibaki kumjadili tunapoteza muda Sana, yana vuruga concentration ya utekelezaji wa Mambo ya msingi.
 
Spidi aliyokuwa nayo Marehemu Magufuli ya kufanya mambo yaende na kufanyika kwa kasi inayoonekana wazi kwa kila mtu, ni challenge kwa waliopo iwe serikalini au bungeni au Mahakamani kuifikia baada ya kifo chake

Matarajio ya wananchi ni kuwa spidi itakuwa kubwa kuliko ile au itabaki ile ile.

Sasa hivi Marehemu anapondwa sana kuwa ohh alikuwa dikteta mara ohh alikuwa fisadi mara ohh staili yake haifai

Hakuna shida; cha msingi wananchi wanataka mambo yaende. Tukaneni matusi yote ila mwisho wa siku wananchi watalinganisha output yenu watukanaji na ya Magufuli kwenye kugusa maisha ya wananchi wanyonge

Marehemu Magufuli kila kona anakuwa attacked siyo kesi ila mambo yaende yasipoenda wananchi watawazomea kila kona Kila mtakakopita wadhalilisha Magufuli. Mtazomewa na kuambiwa Magufuli angekuwa hai hili lingefanyika na watawazomea.
Kinachoshambuliwa ni upuuzi wa ccm na serikali yake.
 
Kipindi chake mambo yalikuwa hayaendi kabisa
 
Mwamba alitenga kabisa fungu la kupigiwa pambio na kutuzuga alikuwa anahakikisha kod zetu anatembea nazo barabarani ili kuwadanganya wanaoitwa wanyonge

Kweli Mungu kainusuru nchi yetu ila TUACHE UOGA MWAMBA ILITAKIWA AFURUSHWE MAPEMA
 
Alizuia criticism zote....ilibaki kumsifia au huwezi kusifia ukae kimya! Alifunga watu midomo. Sasa wacha apate share yake huko huko alipo.
Ni raha iliyoje kuondokewa na dhalim !
 

This man is true Hero of Africa
Not Pumbavu Mfu yule
 
Back
Top Bottom