Hayati Magufuli huwezi kusahaulika kwa miaka mingi sana kwa Meli kubwa Ziwa Victoria

Hayati Magufuli huwezi kusahaulika kwa miaka mingi sana kwa Meli kubwa Ziwa Victoria

Mwaka 1996 wakati ajali kubwa ikitokea Ziwa Victoria mimi nilikuwa Ukraine nikiwa nimemaliza mwaka wa kwanza wa lugha nikijitayarisha kuingia mwaka wa masomo. Nakumbuka namna sisi watanzania tulivyoanzisha mjadala juu ya ajali hiyo iliyoua ndugu na jamaa zetu wengi.

Mwaka huu itatimia miaka 27 tangu msiba ule utokee. Huwa tunalo tatizo la kutoa takwimu halisi za vifo haswa kwa malengo ya kisiasa yenye nia ya kujaribu kupunguza hasira za walengwa wa moja kwa moja wa ajali (victims). Ni hulka iliyoendelea kuwepo kwa muda mrefu. Ukisika wamekufa watu 10,000 basi tambua ni zaidi ya 30,000 wamepoteza maisha.

Sina uhakika kama hayati JPM alipoteza ndugu zake wa karibu katika msiba ule mzito. Lakini kwa maamuzi ya kutoangalia watasema nini wale wakosoaji wa kila jambo akaamua kwa ushujaa kuanza kujenga meli kubwa ili itumike katika Ziwa Victoria. Ni maamuzi ya kijasiri sana na ya kizalendo.

Kuwa tayari huku mtaani watu walalamike vyuma vimekaza lakini serikali yake ikiwa inafanya kazi yenye kuacha kitu chenye kuonekana maishani mwetu (tangible).

Serikali ya JPM licha ya lawama na upungufu wa hapa na pale lakini iliweza kwa kiasi kikubwa kupambana kuacha vitu vyenye kuonekana na vyenye kuweza kupigiwa hesabu vimenunuliwa kwa pesa kiasi gani.

Manunuzi ya ndege mpya na ukarabati wa viwanja kadhaa, ujenzi wa daraja la Busisi na haya ya hapa Dar, na mambo mengi yenye kuonekana na hivyo kuchangia katika mzunguko wa pesa kiuchumi na kuinua kiwango cha maisha cha watu hao hao.

Vilio vya wote waliofiwa na ndugu zao pale ziwani tarehe 21 May 1996 angalau vimefutwa machozi na uwepo wa Meli yenye kuweza kubeba watu 2700 na tani 400 za bidhaa mbalimbali.

Wale watoto waliokuwa yatima kwa sababu ya ajali ile katili, angalau wanacho chombo cha kusafiria wakiwa na amani moyoni.

Wale wajane walioishi miaka 27 wakiwaombea misa maalum wenza wao kila siku makanisani wanacho chombo cha kusafiria chenye kulingana na uzito wa kodi wanayolipa kila wanaponunua chochote mahali popote.

JPM kwa hii meli ya Ziwa Victoria mimi kama mtu mwenye asili ya kanda ya ziwa nitakuenzi daima. Ulale mahali pema peponi.

Huko usukumani Yes hawatamsahau kwa meli! Kila mtu atamkumbuka kivyake tusipangiane, kwani kabla hajazaliwa hakukua na meli Tanzania? Mv Liemba ilikuwepo kabla ya babu yako wala yake, so hamna jipya hapo labda kwako mtoto wa juzi!
 
Mwaka 1996 wakati ajali kubwa ikitokea Ziwa Victoria mimi nilikuwa Ukraine nikiwa nimemaliza mwaka wa kwanza wa lugha nikijitayarisha kuingia mwaka wa masomo. Nakumbuka namna sisi watanzania tulivyoanzisha mjadala juu ya ajali hiyo iliyoua ndugu na jamaa zetu wengi.

Mwaka huu itatimia miaka 27 tangu msiba ule utokee. Huwa tunalo tatizo la kutoa takwimu halisi za vifo haswa kwa malengo ya kisiasa yenye nia ya kujaribu kupunguza hasira za walengwa wa moja kwa moja wa ajali (victims). Ni hulka iliyoendelea kuwepo kwa muda mrefu. Ukisika wamekufa watu 10,000 basi tambua ni zaidi ya 30,000 wamepoteza maisha.

Sina uhakika kama hayati JPM alipoteza ndugu zake wa karibu katika msiba ule mzito. Lakini kwa maamuzi ya kutoangalia watasema nini wale wakosoaji wa kila jambo akaamua kwa ushujaa kuanza kujenga meli kubwa ili itumike katika Ziwa Victoria. Ni maamuzi ya kijasiri sana na ya kizalendo.

Kuwa tayari huku mtaani watu walalamike vyuma vimekaza lakini serikali yake ikiwa inafanya kazi yenye kuacha kitu chenye kuonekana maishani mwetu (tangible).

Serikali ya JPM licha ya lawama na upungufu wa hapa na pale lakini iliweza kwa kiasi kikubwa kupambana kuacha vitu vyenye kuonekana na vyenye kuweza kupigiwa hesabu vimenunuliwa kwa pesa kiasi gani.

Manunuzi ya ndege mpya na ukarabati wa viwanja kadhaa, ujenzi wa daraja la Busisi na haya ya hapa Dar, na mambo mengi yenye kuonekana na hivyo kuchangia katika mzunguko wa pesa kiuchumi na kuinua kiwango cha maisha cha watu hao hao.

Vilio vya wote waliofiwa na ndugu zao pale ziwani tarehe 21 May 1996 angalau vimefutwa machozi na uwepo wa Meli yenye kuweza kubeba watu 2700 na tani 400 za bidhaa mbalimbali.

Wale watoto waliokuwa yatima kwa sababu ya ajali ile katili, angalau wanacho chombo cha kusafiria wakiwa na amani moyoni.

Wale wajane walioishi miaka 27 wakiwaombea misa maalum wenza wao kila siku makanisani wanacho chombo cha kusafiria chenye kulingana na uzito wa kodi wanayolipa kila wanaponunua chochote mahali popote.

JPM kwa hii meli ya Ziwa Victoria mimi kama mtu mwenye asili ya kanda ya ziwa nitakuenzi daima. Ulale mahali pema peponi.
Magufuli ni rais aliofanya mambo makubwa kwa muda mchache hadi dunia ikashangaa. pumzika kwa amani Baba kazi ulioifanya imeonekana na MUNGU akusamehe makosa yako yote upumzike mbiguni kwa furaha na amani.Amina
 
Mwaka 1996 wakati ajali kubwa ikitokea Ziwa Victoria mimi nilikuwa Ukraine nikiwa nimemaliza mwaka wa kwanza wa lugha nikijitayarisha kuingia mwaka wa masomo. Nakumbuka namna sisi watanzania tulivyoanzisha mjadala juu ya ajali hiyo iliyoua ndugu na jamaa zetu wengi.

Mwaka huu itatimia miaka 27 tangu msiba ule utokee. Huwa tunalo tatizo la kutoa takwimu halisi za vifo haswa kwa malengo ya kisiasa yenye nia ya kujaribu kupunguza hasira za walengwa wa moja kwa moja wa ajali (victims). Ni hulka iliyoendelea kuwepo kwa muda mrefu. Ukisika wamekufa watu 10,000 basi tambua ni zaidi ya 30,000 wamepoteza maisha.

Sina uhakika kama hayati JPM alipoteza ndugu zake wa karibu katika msiba ule mzito. Lakini kwa maamuzi ya kutoangalia watasema nini wale wakosoaji wa kila jambo akaamua kwa ushujaa kuanza kujenga meli kubwa ili itumike katika Ziwa Victoria. Ni maamuzi ya kijasiri sana na ya kizalendo.

Kuwa tayari huku mtaani watu walalamike vyuma vimekaza lakini serikali yake ikiwa inafanya kazi yenye kuacha kitu chenye kuonekana maishani mwetu (tangible).

Serikali ya JPM licha ya lawama na upungufu wa hapa na pale lakini iliweza kwa kiasi kikubwa kupambana kuacha vitu vyenye kuonekana na vyenye kuweza kupigiwa hesabu vimenunuliwa kwa pesa kiasi gani.

Manunuzi ya ndege mpya na ukarabati wa viwanja kadhaa, ujenzi wa daraja la Busisi na haya ya hapa Dar, na mambo mengi yenye kuonekana na hivyo kuchangia katika mzunguko wa pesa kiuchumi na kuinua kiwango cha maisha cha watu hao hao.

Vilio vya wote waliofiwa na ndugu zao pale ziwani tarehe 21 May 1996 angalau vimefutwa machozi na uwepo wa Meli yenye kuweza kubeba watu 2700 na tani 400 za bidhaa mbalimbali.

Wale watoto waliokuwa yatima kwa sababu ya ajali ile katili, angalau wanacho chombo cha kusafiria wakiwa na amani moyoni.

Wale wajane walioishi miaka 27 wakiwaombea misa maalum wenza wao kila siku makanisani wanacho chombo cha kusafiria chenye kulingana na uzito wa kodi wanayolipa kila wanaponunua chochote mahali popote.

JPM kwa hii meli ya Ziwa Victoria mimi kama mtu mwenye asili ya kanda ya ziwa nitakuenzi daima. Ulale mahali pema peponi.

Ni sawa kabisa, hata wajerumani tunawakumbuka na kuwaenzi sana sisi kama waTanzania kwa kutujengea miundombinu ya reli, MV Liemba ya ziwa Tanganyika nk.
 
Marais wangapi wenye uthubutu wa aina hiyo?. Uzalendo wa hali ya juu.

Kumsahau ni swala lako binafsi.

Kwamba ndio rais wa kwanza kusimamia fedha za umma kujenga miundombinu kadhaa akiwa madarakani au?
 
Kwamba ndio rais wa kwanza kusimamia fedha za umma kujenga miundombinu kadhaa akiwa madarakani au?
Rais wa kwanza kuamua kufuta machozi ya wahanga wa ajali ya May 1996 kwa kufanya maamuzi magumu ya kutengeneza meli mpya yenya ubora mkubwa.

Marais wote hujenga vitu vingi kwa mujibu wa maelekezo ya ilani ya CCM.
 
Ni sawa kabisa, hata wajerumani tunawakumbuka na kuwaenzi sana sisi kama waTanzania kwa kutujengea miundombinu ya reli, MV Liemba ya ziwa Tanganyika nk.
Mjerumani alijenga huku akiiba mali zetu JPM amejenga kwa kutumia pesa zile zile zinazopangiwa matumizi mengi pengine akipuuzia malalamiko ya wa chini yake.
 
Kwa hiyo unajustify mauaji aliyoyafanya jpm kwa kusema hata mkapa alifanya au siyo!!
Hakuna rais wa TZ mwenye mikono misafi kabisa. Nyerere miaka ile alifanya unyama pia.

Pale wizara ya mambo ya ndani kule nyuma karibu na ukuta unaopakana na YMCA, kulikuwa na nyumba ya mabati yenye rangi nyekundu, uliza waliokuwepo miaka ile mle ndani palikuwa ni maalum kwa shughuli zipi.
 
Hakuna rais wa TZ mwenye mikono misafi kabisa. Nyerere miaka ile alifanya unyama pia.

Pale wizara ya mambo ya ndani kule nyuma karibu na ukuta unaopakana na YMCA, kulikuwa na nyumba yenye bati lenye rangi nyekundu, uliza waliokuwepo miaka ile mle ndani palikuwa ni maalum kwa shughuli zipi.
Samia Hana mpango kabisa wa kuua .mtu ndo mana tunamuombe afie kwenye urais yaani atuongoze miaka mia ijayo
 
Wewe ndiye mwenye chuki dhidi ya viongozi wengine waliopita kama vile huyo unayemsifia alikuta nchi ni wonderland.
Kaacha meli ziwa victoria hapo sijaongelea masuala ya ndege zaidi ya kumi na mengi mengineyo.
 
Hakuna rais wa TZ mwenye mikono misafi kabisa. Nyerere miaka ile alifanya unyama pia.

Pale wizara ya mambo ya ndani kule nyuma karibu na ukuta unaopakana na YMCA, kulikuwa na nyumba ya mabati yenye rangi nyekundu, uliza waliokuwepo miaka ile mle ndani palikuwa ni maalum kwa shughuli zipi.
Duh we utakuwa TISS. Asante
 
Mwaka 1996 wakati ajali kubwa ikitokea Ziwa Victoria mimi nilikuwa Ukraine nikiwa nimemaliza mwaka wa kwanza wa lugha nikijitayarisha kuingia mwaka wa masomo. Nakumbuka namna sisi watanzania tulivyoanzisha mjadala juu ya ajali hiyo iliyoua ndugu na jamaa zetu wengi.

Mwaka huu itatimia miaka 27 tangu msiba ule utokee. Huwa tunalo tatizo la kutoa takwimu halisi za vifo haswa kwa malengo ya kisiasa yenye nia ya kujaribu kupunguza hasira za walengwa wa moja kwa moja wa ajali (victims). Ni hulka iliyoendelea kuwepo kwa muda mrefu. Ukisika wamekufa watu 10,000 basi tambua ni zaidi ya 30,000 wamepoteza maisha.

Sina uhakika kama hayati JPM alipoteza ndugu zake wa karibu katika msiba ule mzito. Lakini kwa maamuzi ya kutoangalia watasema nini wale wakosoaji wa kila jambo akaamua kwa ushujaa kuanza kujenga meli kubwa ili itumike katika Ziwa Victoria. Ni maamuzi ya kijasiri sana na ya kizalendo.

Kuwa tayari huku mtaani watu walalamike vyuma vimekaza lakini serikali yake ikiwa inafanya kazi yenye kuacha kitu chenye kuonekana maishani mwetu (tangible).

Serikali ya JPM licha ya lawama na upungufu wa hapa na pale lakini iliweza kwa kiasi kikubwa kupambana kuacha vitu vyenye kuonekana na vyenye kuweza kupigiwa hesabu vimenunuliwa kwa pesa kiasi gani.

Manunuzi ya ndege mpya na ukarabati wa viwanja kadhaa, ujenzi wa daraja la Busisi na haya ya hapa Dar, na mambo mengi yenye kuonekana na hivyo kuchangia katika mzunguko wa pesa kiuchumi na kuinua kiwango cha maisha cha watu hao hao.

Vilio vya wote waliofiwa na ndugu zao pale ziwani tarehe 21 May 1996 angalau vimefutwa machozi na uwepo wa Meli yenye kuweza kubeba watu 2700 na tani 400 za bidhaa mbalimbali.

Wale watoto waliokuwa yatima kwa sababu ya ajali ile katili, angalau wanacho chombo cha kusafiria wakiwa na amani moyoni.

Wale wajane walioishi miaka 27 wakiwaombea misa maalum wenza wao kila siku makanisani wanacho chombo cha kusafiria chenye kulingana na uzito wa kodi wanayolipa kila wanaponunua chochote mahali popote.

JPM kwa hii meli ya Ziwa Victoria mimi kama mtu mwenye asili ya kanda ya ziwa nitakuenzi daima. Ulale mahali pema peponi.
Hitler alikuwepo kabla hujazaliwa! Idi Amin, Stalin na Saddam Hussein wanakumbukwa kila iitwayo kesho, sembuse Lucifer Magufuli wa juzi?!
Swali la kujiuliza ni je Hitler na Stalin, sadam, idi Amin nk wanakumbukwa kwa lipi, wema au ubaya?!

Lucifer Magufuli atakumbukwa sana kwa muda mrefu ujao ili taifa lisije kurudia makosa kama hayo milele!
 
Rais wa kwanza kuamua kufuta machozi ya wahanga wa ajali ya May 1996 kwa kufanya maamuzi magumu ya kutengeneza meli mpya yenya ubora mkubwa.

Marais wote hujenga vitu vingi kwa mujibu wa maelekezo ya ilani ya CCM.

Hata kusingekuwa na ilani unadhani miundombinu isingejengwa?
 
Mjerumani alijenga huku akiiba mali zetu JPM amejenga kwa kutumia pesa zile zile zinazopangiwa matumizi mengi pengine akipuuzia malalamiko ya wa chini yake.

Zile pesa zilizopelekwa China kuna tofauti gani na hizo za hao wakoloni? Na hao wajerumani waliiba nini sana nchi hii, mbona wameondoka zaidi ya miaka 100 na bado nchi hii ni masikini na mali walizoacha? Au walituibia na akili?
 
Zile pesa zilizopelekwa China kuna tofauti gani na hizo za hao wakoloni? Na hao wajerumani waliiba nini sana nchi hii, mbona wameondoka zaidi ya miaka 100 na bado nchi hii ni masikini na mali walizoacha? Au walituibia na akili?
Nchi hii ni maskini kwa sababu mimi na wewe tunapiga mdomo tu bila hata ya kujitoa kupambana na huo umaskini. Pesa ya China ni sehemu ndogo sana kulinganisha na inayotumika kumalizia treni ya SGR, ni sehemu ndogo sana kulinganisha na ujenzi wa hiyo meli ya Ziwani.

JPM anastahili heshima kwa uthubutu wake, mengineyo ni siasa nyepesi tu.
 
Weka tija ya hizo ndege hapa. Unaweza kuweka ni kiasi gani hadi sasa zimeingiza kama faida? Mbona ziko grounded muda mrefu?
Masuala ya muda kuwa grounded, ni mchakato mkuu kuziendesha, haziendeshwi kwa porojo za humu ndani JF.
 
Nchi hii ni maskini kwa sababu mimi na wewe tunapiga mdomo tu bila hata ya kujitoa kupambana na huo umaskini. Pesa ya China ni sehemu ndogo sana kulinganisha na inayotumika kumalizia treni ya SGR, ni sehemu ndogo sana kulinganisha na ujenzi wa hiyo meli ya Ziwani.

JPM anastahili heshima kwa uthubutu wake, mengineyo ni siasa nyepesi tu.

Kwani wale tuliokuwa tunawatuhumu kabla ya Magufuli kuwa ni wezi, waliiba hela zote, na hakuna mradi wowote walifanya?
 
Back
Top Bottom