Hayati Magufuli huwezi kusahaulika kwa miaka mingi sana kwa Meli kubwa Ziwa Victoria

Hayati Magufuli huwezi kusahaulika kwa miaka mingi sana kwa Meli kubwa Ziwa Victoria

Mwaka 1996 wakati ajali kubwa ikitokea Ziwa Victoria mimi nilikuwa Ukraine nikiwa nimemaliza mwaka wa kwanza wa lugha nikijitayarisha kuingia mwaka wa masomo. Nakumbuka namna sisi watanzania tulivyoanzisha mjadala juu ya ajali hiyo iliyoua ndugu na jamaa zetu wengi.

Mwaka huu itatimia miaka 27 tangu msiba ule utokee. Huwa tunalo tatizo la kutoa takwimu halisi za vifo haswa kwa malengo ya kisiasa yenye nia ya kujaribu kupunguza hasira za walengwa wa moja kwa moja wa ajali (victims). Ni hulka iliyoendelea kuwepo kwa muda mrefu. Ukisika wamekufa watu 10,000 basi tambua ni zaidi ya 30,000 wamepoteza maisha.

Sina uhakika kama hayati JPM alipoteza ndugu zake wa karibu katika msiba ule mzito. Lakini kwa maamuzi ya kutoangalia watasema nini wale wakosoaji wa kila jambo akaamua kwa ushujaa kuanza kujenga meli kubwa ili itumike katika Ziwa Victoria. Ni maamuzi ya kijasiri sana na ya kizalendo.

Kuwa tayari huku mtaani watu walalamike vyuma vimekaza lakini serikali yake ikiwa inafanya kazi yenye kuacha kitu chenye kuonekana maishani mwetu (tangible).

Serikali ya JPM licha ya lawama na upungufu wa hapa na pale lakini iliweza kwa kiasi kikubwa kupambana kuacha vitu vyenye kuonekana na vyenye kuweza kupigiwa hesabu vimenunuliwa kwa pesa kiasi gani.

Manunuzi ya ndege mpya na ukarabati wa viwanja kadhaa, ujenzi wa daraja la Busisi na haya ya hapa Dar, na mambo mengi yenye kuonekana na hivyo kuchangia katika mzunguko wa pesa kiuchumi na kuinua kiwango cha maisha cha watu hao hao.

Vilio vya wote waliofiwa na ndugu zao pale ziwani tarehe 21 May 1996 angalau vimefutwa machozi na uwepo wa Meli yenye kuweza kubeba watu 2700 na tani 400 za bidhaa mbalimbali.

Wale watoto waliokuwa yatima kwa sababu ya ajali ile katili, angalau wanacho chombo cha kusafiria wakiwa na amani moyoni.

Wale wajane walioishi miaka 27 wakiwaombea misa maalum wenza wao kila siku makanisani wanacho chombo cha kusafiria chenye kulingana na uzito wa kodi wanayolipa kila wanaponunua chochote mahali popote.

JPM kwa hii meli ya Ziwa Victoria mimi kama mtu mwenye asili ya kanda ya ziwa nitakuenzi daima. Ulale mahali pema peponi.
Sukuma gang mna taabu sana, hakuna raisi atakayesahaulika ila huyo Jiwe atakumbukwa pia kwa ubishi wa kupingana na wataalam wa mambo ya afya huku aking'ang'ania malimao na vitunguu saumu kama tiba ya COVID-19 kitu kilichosababisha yeye kuwa raisi wa kwanza kufia madarakani tena kwa uzembe wake mwenyewe na pia atakumbukwa kwa ukatili uliokithiri.
Hiyo meli kama mengine yaliyofanywa na maraisi wengine hakuna hata raisi mmoja aliyetoa pesa zake za mfukoni bali ni pesa za kodi za wananchi, ni mara mia hata kuisifu kampuni iliyounda hiyo meli(japo nao hawakufanya bure,walilipwa kwa kazi hiyo), Jiwe alikuwa mwehu ila alifanikiwa ku-brainwash mazuzu ambao hadi leo wanamuona ni mungu mtu na hata madhila aliyowasababishia watu hatafuta namna ya kuya-justify.
 
Meli imejengwa kwa pesa za watanzania kazi akiifanya mama. Yeye hakuifikia hata 10% ya ujenzi acheni upoyoyo
Si Samia wala Jiwe waliojenga ile meli, meli imejengwa(imeundwa) na kampuni ya nje kwa malipo ya fedha za walipa kodi.
Mwandawazimu/Mwendakuzimu aliharibu sana mazuzu mpaka pesa za kodi za wananchi waliona ya kwamba ni fedha zake binafsi, yaani kwamba fedha zilizokuwa hazina ilikuwa kama ni personal account yake.
 
Hakuna rais wa TZ mwenye mikono misafi kabisa. Nyerere miaka ile alifanya unyama pia.

Pale wizara ya mambo ya ndani kule nyuma karibu na ukuta unaopakana na YMCA, kulikuwa na nyumba ya mabati yenye rangi nyekundu, uliza waliokuwepo miaka ile mle ndani palikuwa ni maalum kwa shughuli zipi.
Hiyo si justification ya lile zimwi Jiwe kuwa katili kwa kiwango kile, bora lilikufa mapema otherwise lingesababisha madhara makubwa zaidi.
 
Nchi hii ni maskini kwa sababu mimi na wewe tunapiga mdomo tu bila hata ya kujitoa kupambana na huo umaskini. Pesa ya China ni sehemu ndogo sana kulinganisha na inayotumika kumalizia treni ya SGR, ni sehemu ndogo sana kulinganisha na ujenzi wa hiyo meli ya Ziwani.

JPM anastahili heshima kwa uthubutu wake, mengineyo ni siasa nyepesi tu.
Jiwe alikuwa mpigaji haijawahi kutokea
 
Ni rahisi kuropoka maneno ukiwa nyuma ya keyboard mbali kabisa na shida za usafiri za watu wa kanda ya ziwa,

Unajua idadi kamili ya waliokufa siku ile pale ziwani wakati meli ilipozama?.
Heee!!sasa kufa kwa watu miaka 27 iliyopita inahusiana vipi na hii meli?kwani si kulikuwa na mv.serengeti na mv.victoria?ziwa victoria hakuna shida ya usafiri kiasi hicho na toka kumekuwa na usafiri wa mabus kwenda bk meli tena imekuwa sio kipaumbele!!kuna miaka kama 2 hakukuwa na usafiri wa meli kati ya mza na bk lakini wakati victoria inafanyiwa matengenezo makubwa na haikuleta athari kubwa!!nenda ziwa tanganyika huko ndio utaona shida ya usafiri.
 
Sukuma gang mna taabu sana, hakuna raisi atakayesahaulika ila huyo Jiwe atakumbukwa pia kwa ubishi wa kupingana na wataalam wa mambo ya afya huku aking'ang'ania malimao na vitunguu saumu kama tiba ya COVID-19 kitu kilichosababisha yeye kuwa raisi wa kwanza kufia madarakani tena kwa uzembe wake mwenyewe na pia atakumbukwa kwa ukatili uliokithiri.
Hiyo meli kama mengine yaliyofanywa na maraisi wengine hakuna hata raisi mmoja aliyetoa pesa zake za mfukoni bali ni pesa za kodi za wananchi, ni mara mia hata kuisifu kampuni iliyounda hiyo meli(japo nao hawakufanya bure,walilipwa kwa kazi hiyo), Jiwe alikuwa mwehu ila alifanikiwa ku-brainwash mazuzu ambao hadi leo wanamuona ni mungu mtu na hata madhila aliyowasababishia watu hatafuta namna ya kuya-justify.
Tatizo sio kutoa pesa zake mfukoni, tatizo ni kupambana mpaka miradi ikamilike. Tatizo ni uthubutu wake binafsi anapotaka jambo lake litimie. Uwezo wa kuamua kuwa Dodoma itakuwa ndio makao makuu na ikawa hivyo, uwezo wa kutatua matatizo ya kirasimu yanayochukua miaka na miaka pasipo kujali watanionaje.

Alikuwa binadamu na hakusita kutukumbusha juu ya ubinadamu wake kwamba yatupasa kunyenyekea muda wote.
 
Mwaka 1996 wakati ajali kubwa ikitokea Ziwa Victoria mimi nilikuwa Ukraine nikiwa nimemaliza mwaka wa kwanza wa lugha nikijitayarisha kuingia mwaka wa masomo. Nakumbuka namna sisi watanzania tulivyoanzisha mjadala juu ya ajali hiyo iliyoua ndugu na jamaa zetu wengi.

Mwaka huu itatimia miaka 27 tangu msiba ule utokee. Huwa tunalo tatizo la kutoa takwimu halisi za vifo haswa kwa malengo ya kisiasa yenye nia ya kujaribu kupunguza hasira za walengwa wa moja kwa moja wa ajali (victims). Ni hulka iliyoendelea kuwepo kwa muda mrefu. Ukisika wamekufa watu 10,000 basi tambua ni zaidi ya 30,000 wamepoteza maisha.

Sina uhakika kama hayati JPM alipoteza ndugu zake wa karibu katika msiba ule mzito. Lakini kwa maamuzi ya kutoangalia watasema nini wale wakosoaji wa kila jambo akaamua kwa ushujaa kuanza kujenga meli kubwa ili itumike katika Ziwa Victoria. Ni maamuzi ya kijasiri sana na ya kizalendo.

Kuwa tayari huku mtaani watu walalamike vyuma vimekaza lakini serikali yake ikiwa inafanya kazi yenye kuacha kitu chenye kuonekana maishani mwetu (tangible).

Serikali ya JPM licha ya lawama na upungufu wa hapa na pale lakini iliweza kwa kiasi kikubwa kupambana kuacha vitu vyenye kuonekana na vyenye kuweza kupigiwa hesabu vimenunuliwa kwa pesa kiasi gani.

Manunuzi ya ndege mpya na ukarabati wa viwanja kadhaa, ujenzi wa daraja la Busisi na haya ya hapa Dar, na mambo mengi yenye kuonekana na hivyo kuchangia katika mzunguko wa pesa kiuchumi na kuinua kiwango cha maisha cha watu hao hao.

Vilio vya wote waliofiwa na ndugu zao pale ziwani tarehe 21 May 1996 angalau vimefutwa machozi na uwepo wa Meli yenye kuweza kubeba watu 2700 na tani 400 za bidhaa mbalimbali.

Wale watoto waliokuwa yatima kwa sababu ya ajali ile katili, angalau wanacho chombo cha kusafiria wakiwa na amani moyoni.

Wale wajane walioishi miaka 27 wakiwaombea misa maalum wenza wao kila siku makanisani wanacho chombo cha kusafiria chenye kulingana na uzito wa kodi wanayolipa kila wanaponunua chochote mahali popote.

JPM kwa hii meli ya Ziwa Victoria mimi kama mtu mwenye asili ya kanda ya ziwa nitakuenzi daima. Ulale mahali pema peponi.
Hebu tukumbushane na meli ya Bagamoyo. Ilinunuliwaje na inafanya kazi wapi kwa sasa
 
Hebu tukumbushane na meli ya Bagamoyo. Ilinunuliwaje na inafanya kazi wapi kwa sasa
Nenda katafute rekodi za kiserikali. Nimeleta huo uzi kwa heshima ya wengi walioteseka hapo ziwani kwa miaka mingi.

JPM na madhambi yake yote kwa kujenga hiyo meli ameliweka hai jina lake miongoni mwa watu wa kanda ya ziwa.
 
Back
Top Bottom