Hayati Magufuli pamoja na kuwa hatunae, Malawi wameandika kitabu kuenzi kazi zake

Kwanza kitabu kimeshiba kurasa,hii ndiyo tofauti ya utafiti wa Ki-Professor na Waandishi Kanjanja!
 
Yaani ukitafuta hayo majina kwenye professional writers huwezi mkuta hata mmoja. Hamna hata mmoja kati ya majina hayo aliyewahi ku publish paper yoyote kwenye majarida ya kitaalam.
Magufuli alikuwa mtaalam wa chemistry PhD alichapisha chochote kwenye jalada gani?
 
Mkuu umeona lakini kitabu kilivyoshiba kurasa.Siyo kile kipeperushi cha akina Kibanda!
 
Magufuli hana faida kwa hili taifa,wewe ni mwehu!
Weka mchango wa Mzee wako kwa taifa alafu tulinganishe na Magufuli!
 
Yaani ukitafuta hayo majina kwenye professional writers huwezi mkuta hata mmoja. Hamna hata mmoja kati ya majina hayo aliyewahi ku publish paper yoyote kwenye majarida ya kitaalam.
Nape Nnauye anawaamini kwerikweri,ujinga sana
 
Kiletwe mara moja tukisome
 
Nawe jamaa nawe! Kwa hiyo kati ya huyo Mnyasaland na sisi wabongo nani ameteswa sana na wasiojulikana? Hicho kitabu kimegusia ni kwa nini Lissu alipigwa risasi ktk utawala wa huyo mtu wako?
Kitanda usichikilalia hujui kunguni wake. Over.
Hili jukwaa siku hizi wameingia na watu ambao ni below average IQ.

Mtu kutungiwa kitabu au kutotungiwa, hakumfanyi mtu huyo aonekani ni mzuri sana, anafaa sana au ni mbaya sana na hafai kabisa.

Rais Magufuli alikuwa Rais wa Tanzania na Watanzania. Hao ndio wanoujua ubaya na uzuri.wa Magufuli.

Magufuli hakuwa Rais wa Malawi, Cuba au bara la Afrika. Mambo yote aliyoyafanya Magufuli hayakuvuka mipaka ya Ta zania. Kwa kiasi kidogo utawala wake uliigusa Kenya kwa mabaya, maana aliangamiza vifaranga wa kuku, na kuwapora ng'ombe wafugaji wa Kenya.

Nyerere ndiye Rais pekee ambaye alifanya mengi nje ya Tanzania, hasa katika kupigania uhuru wa Mataifa ya Afrika.

Ni uwendawazimu wa hali ya juu Mtanzania aliyeishi kwenye utawala wa Magufuli kusubiria Mmalawi akuambie kama Magufuli alikuwa kiongozi mbaya au mzuri.

Ni sawa wewe uwe unaishi na Baba yako Ushirombo, halafu unasubiria mtoto wa Nachingwea akuambie kama baba yako ni mtu mzuri au mbaya!!

Ubaya na uzuri wa uongozi wa Magufuli unafamika zaidi na Watanzania kuliko mtu mwingine yeyote. Wakati mtanzania ameuishi utawala wa Magufuli, wengine wanasimliwa tu.
 
Hicho ndicho pekee alichofanikiwa kukifanya Polepole alipokuwa Malawi. Sahizi anaandaa kingine toka Cuba. Rais akimwondoe polepole Cuba, ampeleke Afganstan ili tupate kitabu kingine toke huko.
 
Ni ujinga kuendelea kushupaza shingo kumpondea JPM

Tulionya kwamba, JPM hakuwa kiongozi mwenye kugusa maisha ya watanzania tu, bali Africa na Dunia pia!

Na hiyo inawahusu watu wenye akili kubwa tu, wapumbavu endeleeni kumshambulia maana hamjui Na hamtajua dunia inakoelekea!

Dunia inapobadirika, kunahitaji watu pia wanaokubali kubadirika na kisha kuendana na mabadiriko ya Dunia hasa linapokuja suala la uchumi wa kimafia

Dunia ya sasa inawahitaji watu kama kina hayati Magufuli kuiongoza! Zaidi ya hapo kila mtu ataandamana kwa sababu akili ya viongozi wasio na maono wao kuona kwao ni kudogo kunakoishia kwenye kuongeza kodi na ushuru badala ya uchumi wa kimafia
 
Ingawa umejificha sana kwenye kumuelezea Magufuli kati ya ubaya na uzuri wake,

Ila elewa tu kwamba, Kumbe Magufuli sifa zake za uongozi hazikuishia nchini peke yake, zilivuka mipaka na hata kuwatuza wasomi wa nchi mbalimbali na wameamua kuandika kitabu kuonyesha jinsi Magufuli alivyokuwa kiongozi shupavu
 
Ni kitabu cha Slowslow hicho anajificha kwenye msitu wa shamba la karanga huko Ubalozini.
 
Magufuli alikuwa mtaalam wa chemistry PhD alichapisha chochote kwenye jalada gani?

Sasa wewe unamlinganisha mtu aliyefikia ngazi ya urais na hao wenzio, waandishi wa habari wa kipindi cha kati. Unachekesha sana wewe.
 
Sasa wewe unamlinganisha mtu aliyefikia ngazi ya urais na hao wenzio, waandishi wa habari wa kipindi cha kati. Unachekesha sana wewe.
Mm sijamzungumzia magufuli kama raisi. Nimemzungumzia kama mtaalam wa chemistry. Kwani ukiwa raisi utaalam unapotea?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…