Tetesi: Hayawi Hayawi, Diamond kumposa Zuchu Ijumaa!

Tetesi: Hayawi Hayawi, Diamond kumposa Zuchu Ijumaa!

Naona umebadili ID ndugu yangu, bahati nzuri umeacha avatar ileile nisingekujua.

Harusi tunayo.
Ndiyo dada, nimeona watu wanajua mimi wa huko.iringa nikaona bora niandike ID ya kabila langu.
Ndoa ni ibada wacha wafanye hiyo ibada Insh Allah.
 
Ni fact tu kwamba, Simba anazaa na kila anaye-date naye.

Sasa iweje kwa Zuchu iwe bila bila hadi now?
Hamna bwana, hiyo sio fact. Amedate na wengi kuliko tunaowafahamu na hawajazaa naye.

Kuzaa ni maamuzi binafsi yakiwemo na makubaliano pia.
 
Mimi nahisi baada ya Zuchu kuwa serious kusema Mondi anaweza kumuoa mwanamke mwingine akiridhia na kuwakazia wasafi kwa kumdhalilisha hivi karibuni, ndio Mondi kaona ataachwa kweli. Wanaume bwana ukizubaa unaweka kwenye uboyfriend na ugirlfriend zone miaka na miaka. Ladies kuwa king'ang'anizi kunalipa si unamuona Chioma wa davido and now Zuchu mume wanao na wanatamba nao lol
 
View attachment 3225842

Hatimaye!
Baada ya sarakasi nyingi, Msanii Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ amekata shauri la kumuoa mpenzi wake ambaye ni msanii ndani ya lebo yake ya muziki (WCB) Zuhura Othman Soud ‘Zuchu’

Uamuzi huo umekuja huku kukiwa na sintofahamu nyingi juu ya mahusiano yao ambapo mwishoni mwa mwaka jana Zuchu alitangaza kwa mara nyingine kuachana kwao japo amekuwa akifanya hivyo mara nyingi na baadaye kurudiana.

Safari hii mambo yamekuwa tofauti kidogo baada ya majuzi kuibuka ugomvi ndani ya kampuni upande wa redio kwa Zuchu kuwashutumu wafanyakazi wa Diamond kumvunjia heshima.

Zuchu ameonekana ‘kukaza’, hajacheka na yeyote akiwemo Diamond mwenyewe na pengine hili limesogeza karibu ndoa yao.

Zuchu ameshinda vita iliyowashinda wengi?…
The mother in law from hell, Mama Diamond amekuwa mwiba mchungu takribani kwa kila mwanamke aliyetoka kimapenzi na Diamond.

Amesemekana kikwazo kikuu kwa Diamond kuoa, hivyo posa hii kwa Zuchu inatuacha njia panda kwamba Mama Dangote kapata kiboko yake? Je posa hii ina baraka za mama yake Diamond?

Ndoa ni kabla ya Ramadhani…
Mwezi uliopita Diamond akiwa na msanii mwenzie Nandy katika mkutano mkuu wa CCM, alionekana akisema atamuoa Zuchu kabla ya Ramadhani ya mwaka huu ambayo inategemewa kuanza mapema mwezi Machi.

Diamond amekuwa akitoa ahadi nyingi hivyo wengi hatukuchukulia tamko lile kwa uzito, nimeshtuka baada ya kupewa taarifa za uhakika kuwa ni kweli na posa hiyo itapelekwa nyumbani kwa Bi Khadija Kopa Ijumaa ya kesho kutwa tarehe 7.

Haya jamani, mambo ndio yako hivyo na hii ni habari endelevu nitakuwa hapa kuwajuza mapema kadiri nitakavyopokea taarifa.

Straight From The Horse’s Mouth,

Nifah.

Viruka njia hawawezi kuona serious. Huyu dada anatafuta drama tu kwenye maisha yake atakuja kuachwa hapa na baba watoto ambaye ana wanawake kila kuna. 😂. Nashukuru sio dada yangu
 
Mimi nahisi baada ya Zuchu kuwa serious kusema Mondi anaweza kumuoa mwanamke mwingine akiridhia na kuwakazia wasafi kwa kumdhalilisha hivi karibuni, ndio Mondi kaona ataachwa kweli. Wanaume bwana ukizubaa unaweka kwenye uboyfriend na ugirlfriend zone miaka na miaka. Ladies kuwa king'ang'anizi kunalipa si unamuona Chioma wa davido and now Zuchu mume wanao na wanatamba nao lol
Chioma hapana, yule ana moyo wa peke yake.
 
Hivi ina maana Zuchu hadi leo bado hajajipata hadi awe na mawazo kama haya ya kimaskini?
Hujawajua wanawake wewe wako kimkakat zaid hasa ukiwa na pesa angekua amejipata angekua ameshasepa sio kwa manyanyaso anayopitia familia ya mume haimpend haimtaki lakin bado anafosi mkamkat wake utimie
 
Sasa mbona Diamond hajawahi kuweka mahusiano yao wazi kama hao wenzie?
My dear unadhani kuwekwa hadharani ndio kupendwa?sometimes hao maslay queen wanatumika kwa show off tu.....ulisikia alivyokiri kuhusu yule Sarah kamwambie uliwahi kuona anapiga mapicha nae? Na angalia wengi wanaolewa mara nyingi mahusiano ni yale ya chinichini ......
 
Hujawajua wanawake wewe wako kimkakat zaid hasa ukiwa na pesa angekua amejipata angekua ameshasepa sio kwa manyanyaso anayopitia familia ya mume haimpend haimtaki lakin bado anafosi mkamkat wake utimie
Hapo wabongo ndio tunapokwamaga.. unataka familia ya mumeo ikupende ili iwaje?we unaolewa na familia na mumeo?
 
My dear unadhani kuwekwa hadharani ndio kupendwa?sometimes hao maslay queen wanatumika kwa show off tu.....ulisikia alivyokiri kuhusu yule Sarah kamwambie uliwahi kuona anapiga mapicha nae? Na angalia wengi wanaolewa mara nyingi mahusiano ni yale ya chinichini ......
Sara ilikuwa kabla hajaanza muziki mpenzi. Wapo slay queens wa kimyakimya wengi tu amekula lakini nao pia walibaki kimya sio Zuchu kutwa anasema yeye tu ila bwana hajawahi kusema kokote ana mahusiano naye zaidi aliwahi kupost kukana kuhusishwa naye kimapenzi.

Sawa anamuoa lakini hajawahi kutamba naye.
 
Sara ilikuwa kabla hajaanza muziki mpenzi. Wapo slay queens wa kimyakimya wengi tu amekula lakini nao pia walibaki kimya sio Zuchu kutwa anasema yeye tu ila bwana hajawahi kusema kokote ana mahusiano naye zaidi aliwahi kupost kukana kuhusishwa naye kimapenzi.

Sawa anamuoa lakini hajawahi kutamba naye.
Kutamba kunasaidia nini kama hujafanywa madam CEO😂😂?Zuchu kaweza shoga yangu tukubali tukatae ,kweli king'ang'a ila imemlipa
 
Mimi nahisi baada ya Zuchu kuwa serious kusema Mondi anaweza kumuoa mwanamke mwingine akiridhia na kuwakazia wasafi kwa kumdhalilisha hivi karibuni, ndio Mondi kaona ataachwa kweli. Wanaume bwana ukizubaa unaweka kwenye uboyfriend na ugirlfriend zone miaka na miaka. Ladies kuwa king'ang'anizi kunalipa si unamuona Chioma wa davido and now Zuchu mume wanao na wanatamba nao lol
Kwa nini umng'ang'anize mtu akuoe?

Wewe ni mbaya hivyo?

Are you so ugly and undesirable that you have to force someone to marry you?

Does nobody else want you?
 
Kwa nini umng'ang'anize mtu akuoe?

Wewe ni mbaya hivyo?

Are you so ugly and undesirable that you have to force someone to marry you?

Does nobody else want you?
Age imeenda soko langu kwenye dating pool limeshuka, namng'ang'ania anayejitokeza

Kashanizalisha, na wanawake ukishazalishwa wanaume wanaona una carry extra baggage wansku avoid...si unasikia story zao humu...inabidi umng'ang'anie aliyekuzalisha.

Being ugly ugly ama being told you are ugly self esteem being low you know.

Benefits, so long ananipa ninachokitaka, security, resources kwa nini nisimng'ang'anie hata kama hanitaki...

Sio mimi jamani nimeobserve tu'Kiranga be easy on me 😆
 
Age imeenda soko langu kwenye dating pool limeshuka, namng'ang'ania anayejitokeza

Kashanizalisha, na wanawake ukishazalishwa wanaume wanaona una carry extra baggage wansku avoid...si unasikia story zao humu...inabidi umng'ang'anie aliyekuzalisha.

Being ugly ugly ama being told you are ugly self esteem being low you know.

Benefits, so long ananipa ninachokitaka, security, resources kwa nini nisimng'ang'anie hata kama hanitaki...

Sio mimi jamani nimeobserve tu'Kiranga be easy on me 😆
Najua wewe mrembo hapa tunaongea kidhahania tu 😂😂
 
Back
Top Bottom