Hebu sikieni ninavyowaza!!

Hebu sikieni ninavyowaza!!

OK, tafuta mtumishi aliye karibu nawe, mshirikishe. unahitaji tiba kiroho. adui anawezatumia hiyo nafasi kukuumiza zaidi
 
wifi michelle,,,tutakuwa na dinner ya pamoja na mpenzio mpya leo saa 2 jioni,venue ntakujulisha kwa pm,,,barikiwa sana

Asante wifi....ngoja niende saloon kujiweka sawa....nipendeze ning'ae kama sijawahi kuwa heart broken vile.....(sweet 10).......nasubiri hiyo PM wifi yangu...barikiwa sana!
 
Mwenzenu nilivunjwa moyo miaka miwili iliyopita, Tangu moyo ulivyovunjika nimekuwa nikimuomba Mungu aniponye na nina Imani ameniponya kabisa, manake najiona sina kinyongo, wala uchungu na huyo heart breaker, na ninachomshukuru Mungu zaidi nina furaha na Amani, na maisha yanaendelea vizuri.

Pamoja na hivo ninamshukuru Mungu kwa sababu amenisamehe dhambi niliyokuwa nimeitenda, kwa sababu nilijidai ninampenda sana huyo mtu kuliko hata Mungu, nikampa vyote, nafsi, roho na mwili. Wakati mwingine hata muda wa kwenda kuabudu ulipungua kwa kumpa huyo heart breaker muda mwingi zaidi.

Baada ya tukio hilo,niliamua kujipa likizo ya kumpenda mwanaume, yani nikaziba madirisha yote ya kumkaribisha mwanaume moyoni mwangu.
Siwachukii lakini nimejipa likizo kwa muda wa miaka mitano hivi, na sasa huu ni mwaka wa pili, ina maana bado miaka mitatu.

Je uamuzi wangu wa kujipa likizo ni sahihi?
Najiona ninaweza kuendelea na likizo hadi miaka mitatu iliyobakia iishe, je ni kweli au
naidanganya nafsi yangu.

Angalizo Marufuku kunitania Broken Heart!! Umesikia GY, Asprin, TF, Askofu na Teamo T, bila kumsahau Bigirita. Mjukuu mtiifu umesikia!! na wewe St. RR.
Uko sawa coz unajaribu kuyaendesha mawazo yako.soma post iliyoandikwa (Waliomo wanatamani KUTOKA,na walio nje wanatamani KUINGIA
 
Asante wifi....ngoja niende saloon kujiweka sawa....nipendeze ning'ae kama sijawahi kuwa heart broken vile.....(sweet 10).......nasubiri hiyo PM wifi yangu...barikiwa sana!
Atiiiiiiiii unasemaje..........
 
OK, tafuta mtumishi aliye karibu nawe, mshirikishe. unahitaji tiba kiroho. adui anawezatumia hiyo nafasi kukuumiza zaidi

Lakini nadhani wewe ni mtumishi uliyekaribu na mimi zaidi kuliko huyo wa kwenda kumtafuta tena.
Halafu pia huyo heart breaker alikuwa mtumishi piaaaaa!!!

Bora tu unambie hicho ambacho unadhani mtumishi angeniambia.
Unajua, kuna wakati nasema sitakaa nimkubali MLOKOLE!!!!!! Yani nitamkubali mcha MUngu lakini sio mtu anayeitwa
MLOKOLE au anasali kwa WALOKOLE.
Hivi nawaza Vema kweli.
 
Elodii tunaruhusiwa kuifanya chat rum? si sridi imekua klozdi?
 
Sikiliza LD, ninachoelewa mimi ni kuwa ulikuwa mgeni wa mapenzi (First love), kilichotokea si makosa ila ni mafunzo tu.
Kwanza mshukuru Muumba wako kwa yaliyotokea. Pili, acha kujifunga namna hiyo, si lazima uwe na mpenzi wa kushea naye mapenzi kwa sasa. Ila jiachie, kuwa na marafiki wa kike na wa kiume, badilishana mawazo, fanyia kazi na kuchuja ushauri unaopewa. Lakini usijinyime raha hata kidogo, mwenzio hata habari na wewe hana, wewe unaugulia. Songa mbele, usipige makitaim, jipe moyo, ile ilikuwa wrong choice.
Lakini pia usijihakikishie mambo mengine kihivyo miaka hii, ndoa ni baraka kutoka kwa Mwenyezi Mungu ikitokea shukuru.
Ukimpata mwingine, kaa naye kimtindomtindo, habari ya full kumwamini ipotezee kila mtu ana moyo wake.
Cheaters nowadays wako kibaooo... Fuatilia posts za Mkuu Allien kuhusiana na cheaters, utawatambua asubuhi na mapema. Halafu ni wajanja kama nini, ukiwatilia shaka tu kidogo, haooooooooooooooooooooo........ wanakula mtaa!
Kubwa zaidi mtangulize muumba wako kwa kila jambo, utafanikiwa.
 
Back
Top Bottom