Hebu tuitazame ZESCO ya Zambia na TANESCO ya Tanzania kisha tujiulize what went wrong

Tanzania mambo inayoweza kuyafanya kwa ufanisi na yakakamilika kwa Asilimia 💯 ni

1.Ngono.
2.Ulevi
3.Uongo
4.Chuki
5.Wizi
6.Ufisadi


Haya mambo mtanzania atafanya kwa ukamilifu kabisa pasipo shaka lakini si mambo ya maendeleo ya Taifa
NAKAZIA 📌🔨

Watanzania wamelaanika.
 
Makamba kaacha legacy ya kununua software India kwa billion sabini
 
Tunduma watu wanao pata umeme wa Zesco hawajawahi kukatiwa umeme kwa miaka mingi. Hawajuikitu kinaitwa Ratiba ya Upungufu wala ukarabati wa mitambo.
Siasa ya kweli ni hii wanayoifanya Zambia
FaizaFoxy njoo tuharibie uzi wetu
Ataleta udini na upwani...
 
Tofauti ya Zambia na Tanzania ni kwamba Zambia walishaachana na chama cha kimapinduzi, wakapita katika development tofauti na tz tumeng'ang'ania chama chenye sera za karne ya 19, ambazo kwa zaidi ya nusu karne zimeprove failure.
 
ZESCO haiendeshwi na wazawa, shirika limebinafsishwa kitambo tu
 
Unaizungumzia Zesco hiyo iliochukuliwa na Wachina au Zesco nyingine?
 
Tatizo ni kuaminishwa kwamba sisi ni masikini, na sisi tunapokea hivyo kuanzia kwa wasimamizi hadi kwa mwananchi wa kawaida, kibaya zaidi umasikini huu unaopandikizwa vichwani mwetu unabeba fikra na akili zote za kufikiria kufanya jambo jipya hasa kwa wasimamizi wetu tuliowapa dhamana.
Ebu tufikiri kidogo: kwa nini daktari mara nyingi hawezi kumwambia mgonjwa kwamba wewe utakufa tu hata kama anaona dalili hizo? Hiyo ni moja, mbili hakuna nia ya dhati ya mtu kuweza kujiuliza kwa nini miaka yote iwe shida hiyohiyo bado unajiita nina wataalamu wazuri.
Mfano tumekuwa watu wa kubadili majina tu Lakini maana ni ileile.Nyoka ni nyoka tu, kifutu ,chatu,swira,cobra Lakini ni nyoka tu.
Sasa fikiria huko nyuma tuliyopitia escrow,richmond, dowans,iptl n.k.
Jiulize kidogo tu hivi huo umeme wa tanzania tuna tatizo gani mpaka kushindikana kiasi hiki?
Je hakuna mtu au watu wanaofahamu kitaalamu mambo haya?
Kiongozi anakabidhiwa ofisi anaambiwa tatizo ni letu site anakaa miezi saba bado liko palepale Lakini yeye kapata chake,anakwenda ofisi nyingine eti mgeni anafundishwa na yule aliyetolewa kwa kushindwa , unatarajia kipya?
Tunahitaji kutoa akili zetu nje ya box.
 
Unapofanya uongo unakuwa unataka kumfurahisha nani na Ili iweje?

Ukiacha miradi ya size ya kati Kuna msululu wa miradi mikubwa ya umeme ambayo itaanza utekelezwaji wake baada ya bwawa kukamilika.

Mfano miradi ya maji mto Ruhudji,
Unaposena sena Serikali Haina Mpango wowote wa vyanzo vinginevyo una maanisha nini?

Yaani Kwa nini unadanganya na Ili iwaje? Kwamba hujui baada ya bwawa kukamilika pesa zitaelwkezwa kwenye kujenga vyanzo vingine vya umeme ambavyo vimeanishwa kama ifuatavyo?

Mto Ruhudji mw 358
Mto Rumakali mw 222
Mto Vikonge mw 321
Mto malagarasi mw 49.5
Mto Kakono mw 87.8
Gas Asilimia Mtwara mw 300
Gas Asilimia Kinyerezi III mw 450
Gas Asilimia Mkuranga& Tegeta 150 mw
Umeme jua 150mw Shinyanga

Hapo sijataja miradi ya joto Ardhi yenye mw 200 .Acheni upotoshaji usio na msingi.
 
Kujua wewe na hao unaowatetea mna upungufu wa akili ni kuendelea kupanga kuwa na vyanzo vya umeme unaotokana na maji, wakati tatizo lililopo sasa la umeme linatokana na mabadiliko ya tabia nchi UHABA WA MVUA sasa unaendeleaje kuweka vyanzo vingine kutoka kwenye tatizo hilo hilo??? makaa ya mawe yaliyopo yamewekwa hapa yafanye nini?? upepo...nk
 
Wewe utakuwa ni mbumbumbu,hoja Yako uliyojenga hapo umetolea mfano Zesco ambao 80% ni vyanzo vya maji Sasa sijui unaongea nini.

Pili vyanzo vya Umeme vikiwa vingi ,hakuna tena upungufu utatokea Kwa sababu umeme utakuwa mwingi kuliko matumizi.

Mwisho kwenye Mpango umeona ni vyanzo vya maji pekee au umekurupuka kwa kukosa hoja baada kuumbuliwa? Kima wewe
 
Kwenye umeme hatuwawezi Zambia. Wako mbali mno. Mwaka jana ndo walikuwa na mgawo ambao waliulaani sana.. mgawo wa masaa 6 kwa siku 🤣🤣🤣. Kuwalaumu Makamba na Maharage ni kupoteza muda. Ishu ya umeme ina historia ndefu sana ya upigaji. Tangu 1994 ni upigaji tu kwenye umeme. Hela zinatumika kulipa mafisadi badala ya kufanyia maendeleo. ZESCO hawana mambo mengi ya kifisadi.
 
Kwanza ni ni ujinga wetu kuacha makaa ya mawe kuzalisha umeme. Nchi za magharibi wanavunja mioyo nchi changa wasiendeleze mkaa kuzalisha umeme eti kuhifadhi mazingira. Wenyewe wametumia makaa kuzalisha umeme kwa miaka mingi bila kujali mazingira na hadi sasa uchina hawamsikilizi mtu wanazalisha umeme kiasi kikubwa kwa mkaa.
Mkaa ni mali ila kwa ujinga na ukasuku tunaacha kuutumia kuzalisha umeme kwa kua eti wazungu wanapiga kelele kuhusu mazingira. Sisi hatujaharibu mazingira yetu kwa kiwango cha eti tuache matumizi ya mkaa kuzalisha umeme.
Mkiongozwa na aina ya watu wenye fikira kama kina januari na maharage aliyekua tanesco lazima waamini na kufuata chochote wanasema wazungu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…