Hebu tusemezane: Ulianza kazi mwaka gani na mshahara wako wa kwanza ulikuwa kiasi gani?

Shikamoo babu 😎
 
hapo sawa mzee,

sema its unpredictable
 
Hahaha watu tunatoka mbaliii nimemaliza chuo sina A wala Z nikapata deal la ubaunsa bar moja maarufu ile bar ilikuwa karibu na home so mwenye bar alikuwa rafiki yangu sana akanipa cheo cha ubaunsa na kuangalia usalama wa bar yake....alinipa kishikaji tu coz hata nyama za ubaunsa sikuwa nazo kwa mwezi nikawa nakula 150000, bia 3 kwa siku na chakula cha jioni coz nilikuwa naingia 1 usiku mpaka saa 7 usiku[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16] anyway bia nilikuwa nazibadilisha navuta mpunga
 
Mzee alishakuniambia...sikuhizi Bora mishahara inaeleweka...anasema anashangaa unapata mshahara unaweza kununua hata tv au redio...anasema mshahara wake...alikuwa akipata a
Hawezi hata kununua redio...
Huo ndio uhalisia wa miaka iyo
 
Nimejikuta nawaza tu....

Binafsi ajira yangu ya kwanza ilikua mwaka 2000, na mshahara wangu ulikua 115,000Tsh.

Nakumbuka nilikua nimemzidi babayangu mshahara na alishangaa sana.
Hii ilikuwa noti ndefu sana kwa wakati huo. Mimi mwaka 2006 nilianza na mshahara wa Tsh 117,000/=. Nakumbuka nilienda kuitoa kwenye ATM za NMB Clocktower kisha nikapitia Jogoo House kujipongeza. Nafika Jogoo House na jamaa yangu tukakaa meza moja na jimama fulani lililoonekana lina mpunga mrefu.. yule mama akaongea kwa dharau "leo Jogoo House imejaa kutokana na hivi viwalimu vimepokea vimishahara vyao vinakuja kusumbua, angalia chini ya meza utaona mifuko ya plastic wamebeba vitu baada ya kupitia soko kuu"..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…