Uchaguzi 2020 Hebu tutafakari sera zinavyonadiwa na mgombea wa CCM John Magufuli na yule wa CHADEMA Tundu Lissu

Uchaguzi 2020 Hebu tutafakari sera zinavyonadiwa na mgombea wa CCM John Magufuli na yule wa CHADEMA Tundu Lissu

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Hakuna mashaka yoyote kuwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, mchuano mkali sana wa kinyang'anyiro hicho cha urais utakuwa baina ya vyama viwili ambavyo ni CCM na CHADEMA.

Kwa maana hiyo ni lazima sisi wananchi tufuatilie kwa makini sana, kwa wagombea wa Urais wa vyama hivyo viwili vikuu, pale wanapomwaga sera zao kwa ajili ya uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu.

Kwa bahati nzuri Mimi mwenyewe nilihudhuria na kushuhudia kampeni ya Urais aliyofanya mgombea wa CHADEMA Tundu Lissu hapo jana katika viwanja vya Tanganyika packers Kawe.

Miongoni ya yale aliyoahidi kupitia kwenye ilani ya chama chake cha CHADEMA ni kama haya yafuatayo:-

1.Wafanyakazi wote ambso hawajaongezewa mishahara yao kwa kipindi chote cha miaka 5, ambayo ni kwa mujibu wa sheria atawaongezea na kulipa malimbikizo yote ya miaka 5.

2. Fao la kujitoa kwa watumishi amesema atalirejesha na akasema wazi kuwa siyo sahihi kwa mfanyakazi anayeacha kazi kusubiria akiba yake aliyoweka kwenye mifuko ya kijamii hadi afike miaka 60.

3. Atawalipa wananchi wote walioathirika na ubomoaji wa nyumba zao, mathalani wakazi wa Kimara hadi Kibaha, kwa lengo la kupisha upanuzi wa barabara ya njia 8 na akaendelea kusema kuwa wananchi hao walifanyiwa huo wakati wananchi hao walilifikisha suala lao mahakamani na mahakama hiyo ikawa imetoa "stop order" lakini serikali haikujali zuio hilo la mahakama na ikaendekea na ubabe wake wa kuzibomoa nyumba hizo bila kulipa fidia yoyote.

4. Ameahidi kurejesha utawala wa sheria nchini, ambao kwa Maelezo yake ni kuwa utawala huu, wa serikali ya awamu ya 5 umeamua kuzikanyaga kanyaga.

6. Ameahidi pia iwapo chama chake kitapewa ridhaa na wananchi kwa kushinda uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi oktoba mwaka huu, nchi yetu itakuwa na Katiba mpya inayotokana na Rasimu ya Warioba ambayo wanaccm waliivuruga

7. Amesema kuwa atarekebisha mfumo wa kodi ambao anasema wafanyibiadhara wanatozwa kodi nyingi sana hadi kufikia kodi 16, na akaahidi kuwa atarekebisha mfumo huo wa kodi na kuwa rafiki kwa wafanyibiashara na kumfanya mfanyibiashara alipe kodi moja pekee.

8 Vile vile ameelezea kuwa atawapiga marufuku TRA kuwabambikia kodi kubwa kwa hila, wafanyibiashara wanaodaiwa kuwa wanawasaidia wapinzani, jambo ambalo limewafilisi wafanyibiathara wengi hapa nchini.

9 Pia amesema atarejesha Uhuru wa wananchi kupata habari, badala ya mfumo uliopo kwenye utawala huu, kwa vyombo vya habari vingi kufungiwa na kupigwa faini, kutokana na sheria mpya kandamizi ya maudhui ya habari iliyopitishwa "fasta fasta" na Bunge letu kwa hati ya dharula

10. Kupunguza malipo ya Bodi ya mikopo kwa wanafunzi waliomaliza vyuo vyao, kutoka asilimia 15 kutoka katika mishahara yao hivi sasa hadi asilimia 3

Hayo ni baadhi ya mambo yaliyo kwenye ilani ya Chadema, ambayo sera zake alizinadi kwenye viwanja vya Tanganyika Packers jana.

Hebu tutazame na ilani ya CCM kama alivyoinadi mgombea wake John Magufuli hapo jana, ambapo nilibahatika kuisikiliza hotuba yake kupitia kwenye "video clip" aliyoitoa kule Dodoma

1. Alisema atajenga uwanja mkubwa pale Dodoma katika awamu ijayo baada ya kuona uwanja wa Jamhuri hautoshi kutokana na watu kufulika Jana kuja kusikiliza ufunguzi wa kampeni za CCM.

2 Vile vile aliahidi kuongeza kununua ndege nyingine 5 za abiria katika awamu ijayo kwa madai kuwa ndege zilizopo hivi sasa hazitoshi na nchi yetu ni tajiri kwa hiyo tunao uwezo wa kufanya manunuzi hayo kwa pesa "cash"

3. Aliahidi pia katika awamu ijayo atajenga uwanja wa ndege wa kimataifa hapo msalato kwa kile alichodai kuwa hiyo Dodoma ishakuwa ni mji mkuu, kwa hiyo kunahitajika ndege kubwa za kutua kwenye mji huo

4 Kama kawaida yake pia aliahidi pia ataendelea kujenga miundo mbinu ya barabara za lami zitakazoenea nchi nzima.

Hebu sisi wananchi tutafakari kwa makini ni yupi hapo tumpe kura zetu na aingie Ikulu.

Kila la kheri wananchi na mtumie vyema kura zenu kwa manufaa yenu na vizazi vijavyo.
 
Watanzania tuna njaa, mpaka sasa mgombea mwenye sera bora ni mzee Rungwe, wananchi hawawezi kula ndege,madaraja, flyover au uhuru na demokrasia. Wananchi wanaweza kula wali kuku, CHAUMA oyeee !!!!
images (13).jpeg
 
Uhuru, Haki na Maendeleo ya wananchi.
VS
Ununuzi wa ndege.

Ipi sera nzuri hapo ya kumkwamua mwananchi kutoka kwenye lindi la umasikini?
Kiongozi umeisoma ilani ya Chama Cha Mapinduzi!? Kwanza!?

Pili Hakuna Haki Bila Wajibu... Na Serikali haitengenezi fedha toka Mbinguni.. Ni Kama kuendesha duka tu..lazima unapoanza ujitoe kweli kweli uwekeze upunguze matumizi.

Ukishafanikiwa unaweza Hata kukaa nyumbani na bado ukala. Wakayi issue ya ubungo kimara ilitolewa ufafanuzi kwa mujibu wa mpango kabambe wa jiji wa mwaka 1979..imekwisha prescribe upana ROW ya Barabara hiyo.

Utaratibu wa watu kuvamia na wanasiasa kuwa pressure watumishi kuwamilikisha kwa ajili ya kupata kura ndicho kilichotufikisha hapa. Lakini Kama mpango upo lazima ufuatwe huo ndio utawala wa haki na sheria.

Lissu anatuambia atalipa malimbikizo na fidia kwa watu waliovamia mbona tutakuwa masikini siku tatu, Sio kitu kibaya kupandisha mishahara na kulipa malimbikiz, ila kwa Sasa Ni kwa fedha ipi!?

Kwann tusitengeneze Kwanza hiyo nyingi kwakuwekeza Kama kweli tunataka longevity kwenye hayo mafao!? Au tulipane ikiisha tukae tuangaliane!?

Kwa kipindi hiki nakushauri soma ilani ..achana na maneno ya jukwaani.. kila mtu anataka kuonekana mwema atasema chochote kuvutia.. despite the facts saying otherwise.

Issue ya Ndege Tano iko kwenye mpango wa upanuzi wa Shirika.. nne za abiria na Freight Jet Moja. Kwa ajili ya kusaidia katika usafirishaji wa mizigo.

Uwanja mkubwa Dodoma ni pamoja na kwa matumizi ya dhifa za kitaifa now we have moved Government operations to Dodoma.

Ila sema ni uchaguzi time anything can be said anyhow.!

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Kutokujitambua ni kutaka kumchagua mtu sababu ya sera. Sera nyingi hazitekelezeki la sivyo sasa hivi TZ ingekuwa nchi ya ulimwengu wa kwanza.
 
Watanzania tuna njaa, mpaka sasa mgombea mwenye sera bora ni mzee Rungwe, wananchi hawawezi kula ndege,madaraja, flyover au uhuru na demokrasia. Wananchi wanaweza kula wali kuku, CHAUMA oyeee !!!!
View attachment 1553627
Huyo Rungwe naye anataka tu kupata "airtime"

Hivi tangu lini kula ubwabwa ikawa ndiyo Sera kuu ya chama cha siasa?
 
Huyo wa ccm kesha ona watanzania simbilisi hivyo hata ilani hataki kuipngelea.
 
Anachonadi ccm Ni sawa na baba anayejenga ghorofa huku watoto wake wanakula mlo mmoja wa nyasi,..ghorofa(miundo mbinu) ikiisha baba atakua amebaki mifuko mitupu hapa watoto watakula nyasi wakiwa ghorofani...

Baada ya miaka kadhaa uchumi wa baba utakua mzuri kidogo watoto watatarajia wale,wavae,wasome na kutibiwa vizuri lakini ghorofa litakua limeanza kudhoofu linahitaji matengenezo,..kushtuka watoto wamekua ila dhoofu bin hali na huzuni zisizoisha.

Mimi na watanzania wenzangu naona huruma na huzuni Kali sana kwamiaka mitano MICHUNGU ijayo.Mungu ibariki Tanzania yangu...hii inaitwa mwanakulitafuta mwanakulipata
 
Hana seraa zozote zaidiii amejaaa kiburi na fedhuri , matusi na hasiraaaa. Yaaaaniii hafai ata kugombea udiwaniiiii.
Anawapeleka puta hata mnalazimisha kurudi Mambo ya miaka ya 70
 

Attachments

  • FB_IMG_1598766129859.jpg
    FB_IMG_1598766129859.jpg
    33.4 KB · Views: 1
Anachonadi ccm Ni sawa na baba anayejenga ghorofa huku watoto wake wanakula mlo mmoja wa nyasi,..ghorofa(miundo mbinu) ikiisha baba atakua amebaki mifuko mitupu hapa watoto watakula nyasi wakiwa ghorofani...Baada ya miaka kadhaa uchumi wa baba utakua mzuri kidogo watoto watatarajia wale,wavae,wasome na kutibiwa vizuri lakini ghorofa litakua limeanza kudhoofu linahitaji matengenezo,..kushtuka watoto wamekua ila dhoofu bin hali na huzuni zisizoisha.
Mimi na watanzania wenzangu naona huruma na huzuni Kali sana kwamiaka mitano MICHUNGU ijayo.Mungu ibariki Tanzania yangu...hii inaitwa mwanakulitafuta mwanakulipata
Halafu Baba Mwenye Ghorofa aliyewalisha nyasi anakufa anamanlizia nyasi.. anawaachia grorofa mnaendelaje kula kuku mpaka mnazeeka... No pain No Gain.. iko hivyo toka Beginning of times.

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Kutokujitambua ni kutaka kumchagua mtu sababu ya sera. Sera nyingi hazitekelezeki la sivyo sasa hivi TZ ingekuwa nchi ya ulimwengu wa kwanza.
Ni upuuzi wetu tu sisi ngozi nyeusi.

Unaahidi hiki unafanya kile,ndo maisha ya muafrika.
 
Ujima and ujamaa mentality
Anachonadi ccm Ni sawa na baba anayejenga ghorofa huku watoto wake wanakula mlo mmoja wa nyasi,..ghorofa(miundo mbinu) ikiisha baba atakua amebaki mifuko mitupu hapa watoto watakula nyasi wakiwa ghorofani...Baada ya miaka kadhaa uchumi wa baba utakua mzuri kidogo watoto watatarajia wale,wavae,wasome na kutibiwa vizuri lakini ghorofa litakua limeanza kudhoofu linahitaji matengenezo,..kushtuka watoto wamekua ila dhoofu bin hali na huzuni zisizoisha.
Mimi na watanzania wenzangu naona huruma na huzuni Kali sana kwamiaka mitano MICHUNGU ijayo.Mungu ibariki Tanzania yangu...hii inaitwa mwanakulitafuta mwanakulipata
 
Yaani hi Li jiwe lina akili kama likandarasi linalotapatapa likikuona unakunywa bia linadhanl wewe unatafuta fundi ujenzi! hiyo ilani ya ccm nitahakikisha naipata na kuitunza kwaajili ya kumbukumbu kwa kizazi kijacho kiwasaidie kijifunza kutengeneza BOQ ya kuomba tenda za ujenzi kutoka kwa mamilionea watakaojaliwa muhula wa RAISI TUNDU LISU of ukweli hii ilani ya FISIEMU ndiyo itakuwa ya mwisha kuinadi 2025 sijui kama Lumumba patakuwa na MTU hata bukusaba watakuwa wamerudi kwao kimyakimya..
ILANi ya uchaguzi ya fiFISIEMU imekaa kama BOQ imewasilishwa kwenye bodi ya tender!
 
Back
Top Bottom