Hekima, busara na nidhamu ya chakula (Table Manners) mbele ya kadamnasi ya wageni

Hekima, busara na nidhamu ya chakula (Table Manners) mbele ya kadamnasi ya wageni

kula chakula uku mtu anaongea ni tabia mbaya....kula uku unaangalia wenzako machoni....au kutafuna uku Domo liko wazi Kama nguruwe iyo ni tabia mbaya
Mkuu, kwa hiyo kwa maoni yako mambo ambayo ni kinyume na TABLE MANNERS ndio haya pekee?...
 
Tatizo kubwa kwa jamii za kiafrika ni kutokuwa wawazi na unafiki uliopiitiliza
unaona aibu ni Jambo gani utakuwa huru kufanya mbele ya kadamnasi?
Mkuu, unaweza kutoa hewa chafu mbele ya idadi kubwa ya wageni? Bado nitazidi kusisitiza;

Hekima, busara na nidhamu ya chakula (Table Manners) mbele ya kadamnasi ya wageni.
 
Kaka mkubwa, what do TABLE MENNERS honestly mean to you?...


Sikia bwana mdogo; Katika sherehe moja ya mashamshamu ya sherehe ni msosi, na kulingana na kauli yako ni kwamba msosi huo ulipikwa kwa ajili ya ninyi mliohudhuria sasa kama chakula kilikuwepo na kuna watu ambao walikuwa hawajashiba na taarifa ikatolewa kwamba yule aliyekuwa bado hajashiba na akaongeze chakula shida hapo iko wapi?? au ulitaka chakula kitupwe??--- labda kama hao jamaa walienda kujipakulia bila kuambiwa hapo ndipo ingekuwa ni tatizo (bad manners).
 
MADA YA LEO: NI MUHIMU SANA MTU KUWA NA NIDHAMU YA KULA KWA STAHA MBELE YA WATU (KADAMNASI)

Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums. Mimi mdogo wenu (Last Born) Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty.

Sio kila muda tunapaswa kusoma na kujadili makala zinazohusiana na masuala ya cold war, jeshi na ujasusi wa KGB, CIA na Mossad. Ngoja leo tujadili kidogo changamoto za maisha katika jamii tunamoishi. Kila siku tukikaa kujadili masuala ya wazungu ni nani atazungumzia ustaarabu wetu?

Ndugu zangu wa Tanzania;

Miezi kadhaa iliyopita nilipata kuhudhuria sherehe moja ya harusi ya mtoto wa kike wa ndugu yangu wa karibu sana iliyofanyika katika ukumbi fulani maarufu sana kule mkoani Arusha. Kusema ukweli wa Mungu harusi ile ilifana sana. Ndugu, jamaa na marafiki sote tulijumuika tukala na kufurahi kwa pamoja.

Tulipiga story mbalimbali pamoja na kukumbushana mambo ya zamani kwa maana ilikuwa ni fursa pia ya kuonana na watu ambao hatukuweza kuonana kwa muda mrefu sana. Sasa kama inavyofahamika na wengi kwamba sherehe huwa ni ratiba mahususi na ratiba ile huwa ina vipengele vingi ndani yake ikiwa ni pamoja na kuwapokea maharusi, kutambulishana, kwenda kuchukua chakula pamoja na utoaji wa zawadi.

Hapa kwenye uchukuaji wa chakula ndio mada kuu ya mjadala kwa siku ya leo. Muda wa chakula ulipowadia ndugu mshereheshaji (MC) aliwaita maharusi kwanza, kisha wakafuata wazazi wa pande zote mbili na kumalizia na sisi akina Infantry Soldier (Kwa maana mimi kudandia sherehe ni kama ulimi na mate hahahaaaaaa I am joking....!!!!!!)

Bwana harusi alikuwa ni mtoto wa kiongozi fulani huko na yeye binafsi alikuwa anafanya kazi katika NGO moja kubwa tu huku Dar, hivyo ile sherehe ilikuwa ni ya budget kubwa kiasi. Hakika chakula kile kilikuwa ni kitamu sana sana tena saaaaana.

Kila mtu alikula na kufurahi lakini cha ajabu MC yule yule akatangaza kwa mara kadhaa kwamba ndugu wageni waalikwa mabibi na mabwana, CHAKULA BADO KIMEBAKI KINGI TU KWA ANAYETAKA KUONGEZA RUKSAAA hahahaaaaaa hapa ndio kasheshe ilipokuwapo. Amini usiamini, hakuna aliyethubutu hata kusimama kwenda kuongeza msosi isipokuwa jamaa fulani 3 ambao ni rafiki wa bwana harusi.

Kile kitendo walikifanya wao lakini aibu niliiona mimi. Inakuwaje mtu mzima na ndevu zake anashindwa kuizuia tamaa ya muda mfupi na kuamua kujidhalilisha namna ile mbele ya kadamnsi?

Sasa ndio nikajawa na maswaki mengi kuliko majibu kwamba;

Je, unafikiri ni jambo sahihi na busara mtu kukosa Busara na nidhamu ya chakula (Table Manners) mbele ya kadamnasi ya wageni?

USISAHAU
: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

BIASHARA: Ninauza Vitabu Vya Kujifunzia Lugha Ya Kijerumani. Ich komme aus der Stadt Dar Es Salaam und verkaufe diese Deutsch-Lernbücher

MAONI YA MDAU
=======
Siku zote anza kwa kuchukua chakula kiasi ili wote mpate, kisha ongeza chakula kwani wapo ambazo kila kiasi cha mwanzo kimewatosha, hii ndiyo table manner sahihi.
 
Sikia bwana mdogo; Katika sherehe moja ya mashamshamu ya sherehe ni msosi, na kulingana na kauli yako ni kwamba msosi huo ulipikwa kwa ajili ya ninyi mliohudhuria sasa kama chakula kilikuwepo na kuna watu ambao walikuwa hawajashiba na taarifa ikatolewa kwamba yule aliyekuwa bado hajashiba na akaongeze chakula shida hapo iko wapi?? au ulitaka chakula kitupwe??--- labda kama hao jamaa walienda kujipakulia bila kuambiwa hapo ndipo ingekuwa ni tatizo (bad manners).
Aisee umemuelezea vizuri sana huyo bwana mdogo. Unajua tatizo hawa wamezoea kwenda kwenye kipaimara, vijiharusi uchwara na maulid za kiswahili so hawajui chochote kuhusu table manners.
 
Mkiambiwa pombe ziko nyingi mkaongeze huwa hamogopi kuoneka walevi mbwaa! Ila sisi tunapoenda kuongeza misosi mnatuita walafi na warohoo.
 
Mkuu, unaweza kutoa hewa chafu mbele ya idadi kubwa ya wageni? Bado nitazidi kusisitiza;

Hekima, busara na nidhamu ya chakula (Table Manners) mbele ya kadamnasi ya wageni.
Mfano wako wa kutoa hewa chafu ni irrelevant, hayo ni Mambo ya faragha na bado pia tunafeli sana upande huo, juzi tu hapa nimempa lift jamaa flan tumetembea karibu km80 mkojo umembana lakini alishindwa kuniambia nisimamishe chombo ajisaidie, you can imagine Kama kukojoa tu ambapo Kila mtu anafanya hivo mtu anaona aibu kusema utafikiri ni dhambi Fulani

Table manners ni ndihamu tu ya ukiwa mezani haiusiani kabisa na Uhuru wa mtu
 
Sikia bwana mdogo; Katika sherehe moja ya mashamshamu ya sherehe ni msosi, na kulingana na kauli yako ni kwamba msosi huo ulipikwa kwa ajili ya ninyi mliohudhuria sasa kama chakula kilikuwepo na kuna watu ambao walikuwa hawajashiba na taarifa ikatolewa kwamba yule aliyekuwa bado hajashiba na akaongeze chakula shida hapo iko wapi?? au ulitaka chakula kitupwe??--- labda kama hao jamaa walienda kujipakulia bila kuambiwa hapo ndipo ingekuwa ni tatizo (bad manners).
Asante sana watu Wana overate Mambo Hadi kero , imagine mtu yupo radhi alale na njaa ililmradi asionekane kaongeza chakula !!
Na hii ndio sababu tunatengeneza vizazi vya ovyo sana , watu wanapenda kufanya Mambo mengi gizani ili wasikosolewe au kusemwa vibaya ..
Hapo kwenye sherehe Kila mtu alionekana kashiba kumbe Kuna uwezekajo wengine walilala na njaa
 
Asante sana watu Wana overate Mambo Hadi kero , imagine mtu yupo radhi alale na njaa ililmradi asionekane kaongeza chakula !!
Na hii ndio sababu tunatengeneza vizazi vya ovyo sana , watu wanapenda kufanya Mambo mengi gizani ili wasikosolewe au kusemwa vibaya ..
Hapo kwenye sherehe Kila mtu alionekana kashiba kumbe Kuna uwezekajo wengine walilala na njaa
mhhh, ila wee jamaa mawazo yako hata siyapendagi
 
Kama wanavyosema bahati haiji mara mbili
Nikipata hii hiyo fursa
Mimi nitafata maelekezo ya huyu mchungaji wangu Ameen

 
Kuongeza msosi mm huwa naongeza sn tu tatizo moja ukifila kwenye kuku huwa wapakuaji wanalaza hvo wanataka uongeze vitu lkn kuku wanabana
Sijawahi faidi nyama za sherehe, kwanza ni kubwa, likuku likuuubwa kulishika kero, afu nakuwaga nimeshiba nakula kiduchu, kurudi home tumbo empty. Mi naona walevi ndo wanafaidi sherehe.
 
Back
Top Bottom