HESLB Mikopo kuunganishwa na NIDA, TIN, Passport na kadi za benki

Boss kinachotakiwa ni kulipa Deni dawa ya Deni ni kulipa kama huna ajira umerahisishiwa kabisa lipa laki moja Tu. Tupo kwenye uchumi wakati unashindwa je kulipa laki moja!?
Ya internet unatoa wapi! Lipa Deni Boss maneno haya malizi deni dawa yake ni kulipa Tu!
 
Hao jamaa ni reckless. They have no clue of what’s going on the the ground. Watu hata chakula hawana , private sector zinakufa ila wanaendelea kukomaa . Ndio maana malipo yake wanataka wayafanye kama kodi ya kichwa
 
Hatulipi . Ubaya ubaya
 
Waswahili wanasema dawa ya deni kulipa. Ubaya tu deni hili limekua kama zile microfinance zilizokuwa zinakopesha walimu laki mbili unakuja kudaiwa milioni 5, sisi wanufaika wa huu mkopo tumeshikilia makali wao wameshika mpini hatuna budi na hatuna wa kutusemea, wabunge watoto wao si wanufaika hivyo maumivu yake hawayapati moja kwa moja. Wanufaika wengi wa bodi ni watoto wa masikini.

Hiyo laki moja kwa wakili anaerenew certificate anaimudu niamini. Kwasababu walio na ajira wanakatwa asilimia 15 ya mshahara kwahiyo wengi wanalipa zaidi ya hiyo laki moja na huo mshahara wenyewe tayari ni kipisi.

Na huo utaratibu wa kusitisha riba huwa hawautangazi sijui kwanini. Ila miaka ya nyuma ukienda pale bodi walikua wanatoa hiyo taarifa sasa sijui kama siku hizi wanao huo utaratibu bado.
 
Hao jamaa ni reckless. They have no clue of what’s going on the the ground. Watu hata chakula hawana , private sector zinakufa ila wanaendelea kukomaa . Ndio maana malipo yake wanataka wayafanye kama kodi ya kichwa
Swala hapa ni ubunifu , kila mtu anataka kuonekana mbunifu na anakusanya mapato.
 
Wanafanya makosa kutokutoa hiyo taarifa kuwa kuna fursa ya kuomba kusitisha riba kama mtu anaona hana ajira.

Pili swala la hiyo 15% sio la kimkataba ni la kisheria, kucharge mtu contrary to the contract ni kinyume cha sheria, nadhani ilikua 8% to be fair wangeondoa hiyo 6% na makato yawe 12 basi hata kama ni kinyume cha mkataba.

Kwa mawakili that is totally unfair kwani mkopo sio kipato hivyo kutokulipa ukimsitishia leseni yake meaning atashindwa kufanya kazi ili alipe hilo deni, it does not make sense at all.
 
Zile fomu za mkopo tulizozisaini tukiwa form 6 zinasema kuwa heslib wanaruhusiwa kubadili chochote ndani ya ule mkopo. Nenda kazisome tena.
 
Swala hapa ni ubunifu , kila mtu anataka kuonekana mbunifu na anakusanya mapato.
Pesa zina hitajika sana na zipo kwa wadaiwa sugu tafadhali sana lipa deni vitu kama hospitali na miundombinu inahitaji hizo pesa au mnadhani zitatoka wapi?
Anza kulipa mwezi huu please!
 
Jiulize hawa wote wanaoweka masharti magumu na masimango kibao wao walisomeshwa na nani?? Mtu hana mtoto wala ndugu wala rafiki eti unamueka Bodi ya Mikopo au Taasisi ya Elimu ya Juu unategemea nini? Ataacha kuweka upupu wake??

Kuna watu roho zinawauma sana wanapoona hela zinatengwa kwajili ya Elimu ya Vijana wetu. Utafikiri zinatoka mifukoni mwao au ya familia zao. Roho mbaya sana hawa watu.
 
Kutokujua sheria au misingi ya jambo fulani hauhalalishi mamlaka kutaoa msamaha huu ni uzembe wa wadaiwa. Hamfuatilie kujuwa deni lenu lipo kwenye hali gani!
 
Kama nilivyosema awali kama mtu anarenew certificate it is presumed anafanya kazi. Na wao wanataka anaefanya kazi awalipe pesa yao. Kuna mawakili wanalipwa na deni hawalipi. Ukiacha mawakili wachache ambao ndio wanaanza their struggle story iko tofauti kidogo ni anaamua tu kurenew anaamini huenda atapata walau kumuandikia mtu affidavit au submissions apate hela ya mboga.

All in all ulipaji wa mkopo uko kandamizi na sheria haikua shirikishi. Waliamka asubuhi wakatunga sheria na ambayo waliamua pia ita act retrospective na kusahahu kuwa kuna watu waliosaini mkataba wa kulipa 8% ya take home yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…