Hichilema wa Zambia kama Magufuli wa Tanzania

Niwe mkweli sijakuelewa.
Ukiwa na strong currency nini itakukwaza ku export?
 
Msipende kudanganyana watu jamani kwa mambo msiyoyafahamu.

Nipo Ndola Zambia hadi leo hii zaidi ya wapinzani wa HH wa nne wana kesi za uhujumu uchumi na mali zao zimeshataifishwa.
Muongo mkubwa wewe mayu
 
Hechilema ni raisi makini. Unamfananisha na watu wa ajabu ajabu
 
HH ana style ya Magu ila kijanja. Makada wa chama tawala mmojammoja anapewa kesi za uhujumu uchumi huku mali zikitaifishwa. Waliokuwa mawaziri sasa hivi tumbo joto. Kisasi cha HH sio poa. Kama hufuatilii siasa za Zambia unaweza ukamwona ni malaika.
Itakuwa wahujumu uchumi wa kweli sio wa kutengeneza
 
Mambo makubwa mawili anayofanya Rais wa Zambia katika kujenga nchi leo ndiyo aliyokuwa anafanya Magufuli enzi za uhai wake. Leo hii Zambia wanafurahi.


View attachment 2220919
Ungejua kwamba kwacha ya Zambia iko kwenye crisis hata usingeongea..

Hiyo Nchi ime default haiwezi tena kulipa madeni licha ya kuitwa Middle Income kwa hiyo inapangiwa cha kufanya na Bretton Woods Institutions

Hapo wanajaribu kujikwamua tuu ndio maana wanatekeleza maelekezo ya WB/IMF
 
Chief Hangaya ni mtu wa starene na raha raha tu hawezi kuimplement austerity measures ambazo yeye mwenyewe anatakiwa awe mfano kwa kila mwananchi. Serikali enzi ya Magufuli ilipunguza matumizi sana ya Watu kusafiri kwenda nchi za nje bila Sababu maalum na yeye aliionesha mfano kwa kutokusafiri hovyo!! Serikali ipige marufuku kununua samani kutokana nje ambazo zinaweza kupatina na kutengezwa hapa nchini. Viongozi waoneshe mfano kwa kuvaa nguo zinazoshonwa hapa nchini badala ya kwenda kufanya shopping nje kununua suti na magauni hivyo kuwapa ajira Watu wa nje badala ya kutengeneza ajira nchini! Kuna mambo Mengi yanaweza kufanyika kupunguza matumizi yasiyo ya lazimaili mradi viongozi wawe na utashi.
 
"The implications of words such as "strong" and "weak" can mislead people to believe that an appreciating currency is always better for the economy than a depreciating currency, but this is not the case. In fact, there is no simple connection between the strength of a country's currency and the strength of its economy."
 


Hayo ni makosa yaliyofanywa na mtanguliz wake ambaye jamaa anayasahihisha. Ni kwamba Jamaa anabana matumizi yasiyokuwaya lazima, halafu anawekeza kwenye miundombinu. Hiyo ndiyo njia ya serikali kujenga nchi, siyo hii ya kugawana hela hovyo hovyo kwa malipo yasiyokuwa na umuhimu wowote na kudai kuwa unangeza hela kwenye mzunguko. Hela kwenye mzunguka huletwa na shughuli za kiuchumi, hazigawiwiw na serikali kiyenyeji enyeji tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…