Hii hali inanipa upweke sana nimejitahidi kuikwepa lakini wapi

Hii hali inanipa upweke sana nimejitahidi kuikwepa lakini wapi

Mke fulani hivi mcheshi
Umekaa zako busy na issue zako anatoka huko na ka 👙 anaanza kukatika with no reason🤣

Akupigishe story za hapa na pale akupe umbea wa mashost zake
Akusaidie kukaribisha wageni nyumba isiwe boring
Some how interested,issue nampataje na ninamtambuaje?
 
Mke fulani hivi mcheshi
Umekaa zako busy na issue zako anatoka huko na ka 👙 anaanza kukatika with no reason🤣

Akupigishe story za hapa na pale akupe umbea wa mashost zake
Akusaidie kukaribisha wageni nyumba isiwe boring
Na propose uwe wewe😊😊😊
 
labda hajaona ule uzi 😛😛

ah mshenga wa hiari
Shida jamaa ana vigezo kama vya Oxford Scholarship! With his personality he needs to find a less strict funny girl. Ili akutoe kwenye ‘boring’ life that you’ve. But umesema pia hupendi kelele sa sijui itakuwaje. Muone Psychologist akusaidie.
 
Shida jamaa ana vigezo kama vya Oxford Scholarship! With his personality he needs to find a less strict funny girl. Ili akutoe kwenye ‘boring’ life that you’ve. But umesema pia hupendi kelele sa sijui itakuwaje. Muone Psychologist akusaidie.
Dah!😛,I second you kweli napenda awe mchangamfu with some comedies ,hayo makabila nimetaja nimeishi nao na wameshiriki kuniumiza hata pasipo na hatia kiasi na waogopa,but nothing more
 
Katika maisha yangu yote sijawahi kuwa na marafiki,na sipendi kabisa masuala ya marafiki,hata nikipata tatizo sina rafiki wa kumwambia mtu pekee ninayeweza kumwambia ni mama tu.

Lakini pia si mtu mwepesi wakueleza hisia ama changamoto zangu kirahisi hata kwa mama,huwa namueleza nikiona kabisa hii inaniendea kombo.

Nikikaa na kundi la vijana wenzangu huwa nakuwa msikilizaji tu tena kwa muda flani tu kisha naondoka zangu.

Napenda kujitenga sana na ninaweza kukaa Siku nzima peke yangu bila taabu yoyote ile,nikitumia muda huo kufanya kazi zangu Za kiofisi au nikifanya coding ama kufanya simulation za sakiti mbalimbali kama nipo nje ya majukumu ya kitabibu.

Nikiona mtu anaanza kunizoea huwa namkwepa haraka sana maana sipendi mazoea na watu.

Sehemu ninayoishi wapangaji wenzangu inaweza pita miezi 2 hatuja onana.

Sipendi kabisa kwenda katika matukio ya sherehe na hata ikiwa ni lazima huwa nakuwa mtu wakujitenga sana maana Mara nyingi huwa siambatani na mtu kabisa.

Sipendi kupiga piga picha hovyo kabisa. Napenda sana familia hapo ndio nadhani ni marafiki pekee naweza kudumu não japo sina família.

Japo kuna wakati huwa nakuwa mpweke mno hasa nisipokuwa na na kazi ya kufanya ,hivyo huwa najitahidi kuhakikisha nakuwa na kazi Ya kufanya kila Siku.

Mimi napambana kivyangu na mambo yangu sipendi kumshirikisha mtu kabisa ,ila huwa nakuwa na hisia yakumshirikisha mke tu lakini sina.

Ninaamini kwamba kuwa na marafiki na kujichanganya sana na watu ni njia rahisi ya mimi kujiletee matatizo.

Nafikiria kuoa ili kuepukana na hali hii nadhani itanisaidia.
Ukizeeka utakuwa mchawi
 
Tafuta mtu aliyebobea katika maswala ya kisaikologia uongee nae. Angalia Adam alivyokuwa peke yake, Mungu akamuona mpweke akampa mwenzake. Wewe ni nani uishi kivyako?
 
Mkuu nina utaratibu wakutembelea watoto yatima kila baada ya miezi 3 japo kuna wakati naenda kwa mwaka mara moja,nina makundi ya whatssap huwa natoa michango kwenye matatizo ama furava,nina dispensary natenga kiasi kuhudumia wanaohitaji matibabu lakini hawanafedha kila mwezi hii haitoshi?
Mkuu hakuna mtu ambaye kaumbwa awe pekeake pekeake tuu,kila mmoja anahitaji watu wa kuzunghmza nao,kutaniana na kucheka nao kila siku.

ukijaribu kuikimbia hii nature ndio utaangukia kwenye depression,stress,upweke,na kujiona uko bored na maisha.

ULaya watu wanaishi kipweke sana ndio maana wanasaiokolojia wanafanya kazi vizuri kwa sababu wateja wanao wa kutosha.

Na wateja hawa wanapatikana kupitia life style yao ya kuishi kivyaovyao,mtu katoka kazini,kajifungia ndani kabisa kutoka mpaka kesho,wengine hudhani kwamba kuwa hivi ndio ugenious ama sifa,wanajiumiza wenyewe.

Unahitaji muda fulani kukaa peke yako,lakini hiyo haina maana unahitaji muda wooote uwe peke yako.

Unahitaji muda fulani kulala,hiyo haina maana unahitaji muda wote ili ulale tuu.

Unahitaji muda fulani ili ule,hiyo naina maana unahitaji muda wote ili ule tuuu.

Unahitaji muda fulani kuongea na watu,hiyo haina maana kwamba unahitaji muda wooote kuongea na watu.

Utaona kwamba maisha ni mkusanyiko wa mambo madogo madogo ambayo utayafanya kila siku.

MUda huu utautumia kula,muda huu utautumia kulala,muda huu utautumia kuwa peke yako,muda huu utautumia kuongea na kukutana na watu.

Hayo ndio maisha,sasa utakapoamua kuyatafsiri maisha kwa kutumia jambo moja ukalifanya kwa muda mrefu jambo hilo basi lazima utajihisi tofauti.

Mfano ukaamua kwamba maisha yako wewe muda wote uwe peke yako,basi hapo utajiharibis mwenyewe maana hakuna unayemtesa na utajipunja kwani afya yako ya akili inahitaji watu wengine na mambo mengine ili uenjoy ile ladha ya maisha.

HApo mtaani tafuta kijiwe chenye heshima wanachoongea mambo ya maana japo kwa uchache kisha jiunge nao.

Au kama unaona kwamba mtaa huo umeshachelewa kujichanganya na ukahisi kwamba ukijichanganya na watu basi utawapa majungu ya kusema kwamba kiko wapi mbona alijifanya anakaa peke yake sasa anajichanganya? Basi hama mtaa tafuta mtaa mwingine ambao utakuwa rahisi kuanza maisha ya kujichanyanya na watu wengine.

Ndio maana watu wa uswahilini hawana stress wala upweke maana wanajichanganya na watu,wanajifunza mambo mbalimbali wanashirikiana vitu mbalimbali na hatimae maisha yanakuwa mazuri tu.

Ila ukiishi kiulayaulaya basi jua upweke utakuandama sana mkuu,na jambo hilo ni jepesi,usitafute mwanasaikolojia bila kutibu chanzo cha tatizo.

Ni sawa na mtu anayelala bila neti(mfano) akiumwa malaria anatafuta dokta anatibiwa then anarudi kulala bila neti anaumwa tena hivo hivo.

Mbona watu wengine hawahitaji wanasaikolojia wanaishi maisha yao vyema tu hawana mashaka yoyote ?

BAdili mfumo wako wa maisha,usijione special saana kwamba watu wengine hawana akili ya kuchanganyika na wewe hapana,unahitaji sana kuchanganyika na watu na bado una mambo mengi sana ya kujifunza na wengine.

Usitafute mchawi,mchawi ni life style yako haina afya.

NA watu aina yako husumbuliwa sana na kukosa usingizi maana muda wote huwa wako ndani,hawapati mwanga wa kutosha machoni,na hiyo inaleta tatizo la kutokulala mapema na kupata usingizi wa kutosha.

Tiba ya haya yote ni kujichanyanya na watu,sahau kuhusu introvert na maujinga mengine,just focus on what make and gives you peace.
 
Katika maisha yangu yote sijawahi kuwa na marafiki,na sipendi kabisa masuala ya marafiki,hata nikipata tatizo sina rafiki wa kumwambia mtu pekee ninayeweza kumwambia ni mama tu.

Lakini pia si mtu mwepesi wakueleza hisia ama changamoto zangu kirahisi hata kwa mama,huwa namueleza nikiona kabisa hii inaniendea kombo.

Nikikaa na kundi la vijana wenzangu huwa nakuwa msikilizaji tu tena kwa muda flani tu kisha naondoka zangu.

Napenda kujitenga sana na ninaweza kukaa Siku nzima peke yangu bila taabu yoyote ile,nikitumia muda huo kufanya kazi zangu Za kiofisi au nikifanya coding ama kufanya simulation za sakiti mbalimbali kama nipo nje ya majukumu ya kitabibu.

Nikiona mtu anaanza kunizoea huwa namkwepa haraka sana maana sipendi mazoea na watu.

Sehemu ninayoishi wapangaji wenzangu inaweza pita miezi 2 hatuja onana.

Sipendi kabisa kwenda katika matukio ya sherehe na hata ikiwa ni lazima huwa nakuwa mtu wakujitenga sana maana Mara nyingi huwa siambatani na mtu kabisa.

Sipendi kupiga piga picha hovyo kabisa. Napenda sana familia hapo ndio nadhani ni marafiki pekee naweza kudumu não japo sina família.

Japo kuna wakati huwa nakuwa mpweke mno hasa nisipokuwa na na kazi ya kufanya ,hivyo huwa najitahidi kuhakikisha nakuwa na kazi Ya kufanya kila Siku.

Mimi napambana kivyangu na mambo yangu sipendi kumshirikisha mtu kabisa ,ila huwa nakuwa na hisia yakumshirikisha mke tu lakini sina.

Ninaamini kwamba kuwa na marafiki na kujichanganya sana na watu ni njia rahisi ya mimi kujiletee matatizo.

Nafikiria kuoa ili kuepukana na hali hii nadhani itanisaidia.
Bora kumbe tupo wengi nilijua ni mimi tu ndo naishi maisha ya namna hii
 
Sema watu wa dizaini kama yako Huwa ni Hatari sana nawaogopa mno nyie hamshindwi hata kupiga matukio ya hatari msijulikane sababu watu kuwahisi ni wapole na mna hasira sana
 
Ndugu nakutana nao kwenye vikao tuu mara chache sana,mama mwenyewe naweza maliza hata miezi sita sijaonana nae na kwa bahati mbaya zaidi mimi nilizaliwa peke yangu kwa baba na wawili kwa mama nasikubahatika kulelewa na wazazi.
Mimi nililelewa na Bibi na babu,siko hivyo,ni kama alivyoshauri jamaa wewe utakuwa melancholy!
 
Back
Top Bottom