Hii hali kwenye biashara siyo ya kawaida

ALPARSLAN

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2024
Posts
467
Reaction score
1,181
Mnamo mwezi wa nane mwishoni nilifungua biashara ya kuuza kuku Wa kukaanga pamoja na viungo vyake.

Wakati nimeanza mauzo yalikuwa hafifu ikawa hata elfu 5 haifiki ya mauzo, ndo nikaja na Uzi wa kuomba ushauri
Wakajitokeza waungwana wakanipa msaada wa mawazo
Miongoni mwao ni dada angu kutoka kigamboni (jina namhifadhi).

Alinipatia msaada mkubwa niliwahi kuelezea kwenye Uzi
Baada ya hapo mambo yakawa mazuri nikawa nauza sana yani kwa siku nakaanga kama awamu 3 nauza wanaisha
Hali imeanza kubadilika wiki 3 zilizopita siuzi, unakuta nauza elfu 3 au sita.

Biashara yote inabaki kesho yake ukisema ni kuku Wa Jana watu hawanunui Sasa hivi mtaji naona unakata maana hakuna nnachoingiza

Nimeenda kwa mganga akanipa dawa za kuchoma na nyingine za kufukia ila wapi Hali inazidi kuwa mbaya

Nachanganyikiwa yani
 
Kwa mganga umeharibu mkuu
 
Ukipoenda kwa mganga ndipo ukafeli zaidi. Mbinu ya kwanza aliyokupa mdada ili work, why usitumir hiyo hiyo? Au umtafute tena?

When watanzania wataachana na imani za kishirikina kwenye mambo yaliyo wazi?
 
Pole jitahidi uwe unaamka usiku saatisa unamuomba Mungu na ujitahidi kutoa sadaka kila unapopata faida .

Hayo ni mambo ya kiroho πŸ§˜β€β™‚οΈ

Sasa njoo tujadili mambo ya kibiashara out put and in put
πŸ‘‡πŸΎ

Hapa tutaanza na bishara yenyewe
Location , purchasing power

Tukimaliza tutajua tatizo nn
 
Mjuu
Mkuu, mungu namuomba yani Toka mambo yabadilike ila ndo hivo yani sijibiwi
 
Mitaa ninayofanya biashara huwa nawahurumia saana wanavyojiangaisha na nguvu za giza! Ndani ya miezi kadhaa ufilisika na kumuuzia mtu frame/ biashara na kutokome! Huyu naye miezi 2 ni mingi, chalii! Tumia mbinu za sheria ya roho wa uzima. Rumi 8: 1-2
Fafanua mbinu hiyo mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…