Hii hapa mikoa 12 inayoendesha uchumi wa nchi, inamiliki na kushikilia asilimia 70% ya uchumi wa Tanzania

Hii hapa mikoa 12 inayoendesha uchumi wa nchi, inamiliki na kushikilia asilimia 70% ya uchumi wa Tanzania

Kazi ya Mwl ni kelewesha. Tiririka mpaka nikuelewe.
GDP=C+I+G+Net Exports where by
Gross Domestic Product=Pato la Shughuli zote za uzalishaji, uwekezaji na matumizi ndani ya Mkoa husika zikithamanishwa Kwa hela.

C=Consumption,Jumla ya manunuzi/matumizi yote ndani ya Mkoa ya watu, Serikali, taasisi nk

I=Investments, Uwekezaji wa private au Serikali

G=Government Spending/Expenditures,Jumla ya Matumizi ya Serikali Kwa mwaka husika kwenye miradi na Huduma za jamii.

Net Exports (Exports less Imports) kinachobakia ndio kinajumlishwa kama pato na inaweza kuwa positive or negative.

Kiufupi Sasa hiyo 8.8T ya Arusha ndio Kila uzalishaji au service industry kama Utalii nk vilivyozalishwa ndani ya Mkoa Kwa mwaka husika ndio vina thamani hiyo.

Sasa kwenye hiyo serikali imechukua chake Kwa njia ya Kodi ,tozo nk Sasa unaweza Kuta Sasa kwenye kutoa let taarifa za Mapato ukakuta Arusha imechangia Mapato mengi lbda ya TRA sababu ni kwamba Kuna Baadhi ya sekta ziko taxable zaidi au Kwa nature yake Zina attract Kodi mfano Utalii ,lakini kuna Baadhi ya sekta Sina Kodi kiduchu au Hazina mfano Uzalishaji wa Kilimo,mambo hayo ndio huleta utofauti wa Wingi wa Kodi baina ya Mkoa na Mkoa.
 
Nahisi Kagera "inaonewa". Mkoa mzuri kama huu usingepaswa kutajwa miongoni mwa mikoa masikini. Nipo kwenye gari naelekea Ngara mjini nikitokea Rulenge. Mkoa ni mzuri sana.
1. Hali ya hewa nzuri!
2. Milima ya kuvutia
3. Ardhi yenye rutuba. Uoto wake na mazao ya migomba unathibitsha hilo.

Sioni sababu ya Kagera kutokuwa "tajiri"
Mkuu nina mpango nije nioe binti wa kihangaza huko ngara
 
Ukiulizwa jibu vizuri sitaki kukuvunjia heshima kuna baadhi ya watu humu JF uwa nawaheshimu na wewe ukiwemo
Ndio imezidiwa Kwa Pato la Mkoa maana Dom Wana 6T vs 6.7T ya Tabora ila tukija kwenye swala Zima la wapi Kuna concentration ya GDP utakuja Dodoma Mjini ndio imeendelea kushinda Tabora ambayo uchumi wake (GDP) umesambaa na pengine una uwiano kutoka Wilaya Moja Hadi nyingi eg Tofauti ya Nzega,Igunga sio kubwa sana na Tabora mjini.

Lakini Kwa Dodoma,GDP yake haina uwiano baina ya Wilaya yaani hapo Mjini ndio Kila kitu huko Kongww ,Bahi sijui Vijiji gani ni hovyo tuu.
 
Mbeya inabeba uchumi wa mikoa minne...Rukwa,katavi,Songwe etc .
Takwimu sometimes zinadanganya
 
Uwekezaji wa Miundombinu ya Barabara una mchango mkubwa kwenye Uchumi na kuondoa umaskini na sio huo mwingine wa SGR.

Takwimu hizo zinaonesha ushahidi huo huko Mikoani ambako Barabara zimeanza kufungua Uchumi
Ni mapema sana ku judge return ya sgr, ipe next 10 years
 
Sawa.
1. Uko wapi?
2. Kwa nini Muhangaza?
3. Kuna ninachoweza kukusaidia?
Nipo mtwara,nimeambiwa wengi wao ni wife material ni wavumilivu wengi wanafanya rejea kwa mabinti wa kazi wanaotoka huko...vipi na wewe unawafahamu kiundani? Nimeamua nipumzike huku pwani unaoa mwanamke ambae mguu mmoja ndani mwingine nje
 
LINDI..........
1000145860.jpg
 
Nipo mtwara,nimeambiwa wengi wao ni wife material ni wavumilivu wengi wanafanya rejea kwa mabinti wa kazi wanaotoka huko...vipi na wewe unawafahamu kiundani? Nimeamua nipumzike huku pwani unaoa mwanamke ambae mguu mmoja ndani mwingine nje
Nitakujibu endapo utanijibu yafuatayo:
1. Wewe ni mwenyeji wa Mtwara au umehamia?
2. Maelezo yako yanaonesha ulishaoa. Mwangaza atakuwa mke wa ngapi? Uliotangulia kuwao/ kumwoa mngali pamoja?
 
Wale Wana list Yao wa Mikoa maskini zaidi,nitakuja nayo hivi punde 😁😁
Unaongelea maendeleo ya wakazi wa eneo husika au unaongelea mali zinazovunwa katika eneo husika?? Mikoa mingi hapo unaiona juu lakini Maisha yao duni kulika Kagera kwa Sababu ya maliasili zilizopo na zinavunwa kwenda Kuleta maendeleo kwingine. Bora ungekuja na mapato ya halmashauri yanayogusa direct shughuli za wananchi ungeeleweka otherwise hizi porojo unajipigia tu
 
Nipo mtwara,nimeambiwa wengi wao ni wife material ni wavumilivu wengi wanafanya rejea kwa mabinti wa kazi wanaotoka huko...vipi na wewe unawafahamu kiundani? Nimeamua nipumzike huku pwani unaoa mwanamke ambae mguu mmoja ndani mwingine nje
1. Siwafahamu sana Wahangaza, lakini nimeshawahi kuishi na baadhi yao kwa muda mfupi. Ni watu wazuri kama ilivyo kwa Jamii kubwa ya Watanzania.

2. Kama unataka kwenda kuoa Ngara, nenda kwa amani. Lakini si lazima umwoe Muangaza. Kuna na makabila mengine pia huko, hata Wasukuma wapo. Lenga kumwoa mtu utakayeamini mtaweza kushare kila kitu katika maisha yenu. Huoi kabila, unamwoa mtu

3. Kikubwa ni wewe kuthibiti mitazamo yako kiusahihi!

Unajua hata raia wa Mataifa ya kigeni, kama Wanigeria na Wakenya wanaamini mabinti wa Kitanzania ndiyo wanawake bora wa kuwaoa? Wanaposema hivyo, wanawamaanisha Wachaga, Wameru, Wasukuma, Wamakonde, Wamwera, Wamasai, Wasambaa, Wahaya, Wahangaza, Waha, Wafipa, Wakurya, n.k.

4. Ingawa watu wa mikoa mingine wanaamini kuwa Waha na Wahangaza ni wife material, wanaume wengi wa Kiha na Kihangaza, hasa wanaoishi jirani na Burundi, hupendelea kuoa mabinti wa Kirundi. Leo nilipomwuliza kijana mmoja wa Kihangaza sababu inayowapelekea baadhi yao kuamua kuwao Warundi alinipa sababu mbili. Ya kwanza ni kwamba wanawake wa Kirundi ni wachapa kazi sana, na ya pili ni mahari wanayotozwa Burundi ni kidogo sana ukilinganisha na ya kwa Wahangaza.

Kwa hiyo, kama unataka kumwoa Muhangaza wewe fanya hivyo, lakini usitarajie mwujiza katika ndoa yako. Mwanamke haolewe akiwa "amekamilika", ni kazi ya mwanaume "kukamilisha".

Ndoa bora ni matokeo ya "uwekezaji" bora.
 
Ni sahihi kabisa lakini hao watu walishaachana na masuala ya takwimu za NBS kwa maana hata wanaozijadili wamejikita katika kuongelea umasikini kwa kuangalia GDP ambayo hata hawajui inatafutwa namna gani na inachangiwa na nini na kuacha nini. Wengine wanajadili kwa kuongozwa na ukabila.

Kuna kitu wengi hawakielewi kuhusu kutengwa kwa makusudi kwa huo mkoa na ukiwa mfuatiliaji kwa kina utalijua hili. Achana na masuala ya kupelekewa meli inayobeba mizigo ambayo serikali haijui inazalishwaje kwa maana sehemu zingine utasikia Serikali imepeleka pembejeo za kilimo kwa wakulima lakini hutasikia kitu cha namna hiyo kwa mkulima wa eneo hilo.

Juzi bungeni kuna mbunge wa huko aliongelea masuala ya NIDA na uhamiaji na akaomba serikali ipeleke maafisa wanaofahamu kwa undani kuhusu hayo maeneo na wale ambao ni eneo geni kwao basi wawe informed na trained ipasavyo kuhusu hilo eneo. Ukiliangalia hili kwa macho ya juu utaona halina maana kwamba mbona maeneo mengine wanaenda tu lakini kwa upande wa mfanyabiashara au mwekezaji ataelewa ni kwanini huyo mbunge aliomba hilo. Nillilima huko miaka kadhaa najua ni kipi wanakumbana nacho sababu nilikumbana nacho mimi nikiwa nimepokelewa vyema na wenyeji.

Ni wazalishaji hodari wa Kahawa lakini jiulize serikali inaweka nini zaidi ya hapa juzi kuja na habari za kupunguza kodi sijui 15 na wakati huo huo unamzuia mtu asiuze kahawa yake sehemu nyingine ambako anapata bei kubwa zaidi kuliko anayoipata hata baada ya kuondoa hizo kodi 15. Ukiuza kwa aliyekuja kutoka nje ya nchi unaambiwa umeuza magendo wakati huo huo yapo maeneo mnunuzi kutoka kenya anaingia mpaka shambani ndani ndani huko bila shida yoyote. Je, hiyo GDP itapandishwaje?

Nilipata mashamba huko maeneo ya Karagwe kama unaenda eneo wanaita chabalisa na mpaka sasa niliyatelekeza yapata miaka 6 na kurudi kwetu kufanya mambo mengine. Sababu ya kuyaacha ni kile kinachoendelea kimya kimya kuhusu hilo eneo. Hivyo hali ya huko naijua vyema hasa katika suala zima la uzalishaji. Achana na ngonjera za mitandaoni sijui wenyeji hawapendi wageni, sijui hawapendi kazi ngumu na blaa blaa nyingi na hizo takwimu za NBS ambazo mtu anayepata mahitaji yake ya chakula cha kila siku kutoka shambani kwake moja kwa moja huku akihitajika kununua vitu vichache sana ambavyo hapati shambani anahesabiwa sawa na yule anayefanya spending ya kila kitu kwa kununua tena kila siku.

Ukiuliza kuhusu viwanda vya samaki vilivyokuwepo utakachojibiwa utaelewa. Kuna kiwanda cha kinaprocess kuuza kahawa ya kopo ya TANICA kama ilivyo AfriCafe. Ukiuliza kuhusu mikakakati ya serikali kukiwezesha zaidi ili kiprocess kwa wingi kahawa inayozalishwa huko utabaki unashangaa.

Achana na masuala ya kupanua bandari, kujenga barabara ya njia nne mjini ilhali bidhaa zinakotoka hakuna lolote linalofanyika. Watafute wenyeji na walioko kwenye mifumo ya serikali watakufumbua macho. Wewe hujawahi kujiuliza ni kwa nini Mkoa wa Kagera huwa hautajwi sehemu yoyote kila ikitamkwa mipango na mikakati kwenye mikoa ya kanda ya ziwa? Zaidi utasikia ukitajwa pale kunapolipuka magonjwa yanayoanzia nchi jirani na kebehi kadha wa kadha.

Kuna kipindi Rais Samia alifanya ziara huko na kuelezea mikakati kadhaa lakini jiulize ni kwanini katika kutembelea na kuzindua miradi mikubwa ya kiserikali inayotekelezwa Mkoani humo aliishia kutembelea kiwanda cha Kagera Sugar ambacho kila kiongozi akienda huko akiwemo PM wote wanatembelea hapo tu?

Ulishawahi jiuliza ni kwanini vyuo tuite colleges zilizofunguliwa huko miaka utawala wa JK zilifungwa miaka ya utawala wa JPM na mpaka sasa hazijafunguliwa wakati colleges zenye hadhi sawa na hizo zinaendelea kushamiri kwenye mikoa mingine? Kipindi cha JK alianza taratibu jitihada za kufufua fua baadhi ya sekta lakini alivyoondoka zikaanza kurudishwa na kupotezewa.

Uliwahi kujiuliza kwamba ni kwanini hata zikiwa zinasomwa taarifa kuhusu eneo la kanda ya ziwa itatajwa Mwanza, Mara, Geita na utaambiwa imepakana na Kigoma au Simiyu lakini hutasikia Mkoa wa Kagera ukitajwa?

Hao watu wanapambana wao kama wao na ndiyo maana kwa kiasi kikubwa wanatudharau sisi watu tulio katika maeneo mengine ambao tunapata support kubwa sana ya serikali lakini bado tunalia wakati wao wanapambana wenyewe kama wenyewe na wanasonga.
Umelalamika sana mkuu!!🙄🙄
Hivi mkoa wa Kagera hauna wawakilishi kwenye vikao vya maamuzi?
Shirikianeni na wabunge wenu, zalisheni mahindi, maharage na matunda kwa wingi mrudishe heshima yenu.
 
Tanga haiwezi kuishusha Mbeya, tuache ubishi wa mwanza na mbeya, ile ni zone kubwa Kwa Tanzania lile ni lango, utake kutoka mbeya, south, zimland, zambia, tswanaland, malawi, halafu kilimo, mpunga, mahindi, uchimbaji wa dhahabu japo chunya yote imejaa wasukuma ndio wanaofaidi dhahabu ile, kitu pekee cha ajabu ni serikali kutowekeza miundombinu bora, mfano uyole na mafiati panakosaje bypass au hata vivuko vya juu Kwa watembea Kwa miguu, haya cocoa ujue kyela ndio ina bei nzuri kuliko Tanga na Moro japo nao wana kokoa, Kwa kesi ya moro ngoja waanze kuexport karafuu tutawasikilizia mbali sana
Naunga mkono
 
My Take
Mikoa ya Ruvuma, Shinyanga, Mara, Geita na Tabora ni game changer kwenye Uchumi wa Nchi, kutoka kusikojulikana hadi kuwa Mikoa muhimu ni jambo la kupongezwa na kuonesha kwamba kumbe ukifungua Nchi Kwa miundombinu Uchumi unafufuka.
Mnapoambiwa Bashe kaeleweka sana mikoa ya Ruvuma na Mbeya na ile yenye kutegemea kilimo nyie hamuelewi. Ila hapa namba zinajieleza zenyewe. Kifupi kama mvua zingekuwa za kawaida mikoa hiyo mwaka huu wangevunja rekodi.

Bashe mpeni maua yake, nyie wa makelele endeleeni tu lakini unafuu wa maisha ndio jibu.
 
Back
Top Bottom