Hii kasheshe kubwa

Mie naona kula na aina ya vyakula kama mazoea, umezoea mihogo kupikwa hivyo ila mie naona mapishi ama chakula ni ubunifu sijui nisemaje, na ndio maana ukitoka ukienda nchi nyingine utajionea mashkolo mageni, mchele ni ule ule ila mapishi tofauti na wenzio wanakula bila tabu, na ww ukiwapelekea mapishi yako unayoona ni sahihi watakuona wa ajabu kabisa..

Kuna mtu alinikuta nakunywa zangu uji na mkate akanishangaa kichizi, eti anaona ajabu nikamwambia tatizo umekremisha vitu ulivyovikuta, nikamwambia katika jamii yetu ungekuta watu wanakula hivi nawe ungekuwa unakula mtu akinywa chai na mkate ungemshamgaa "ungekuta nyama inaitwa kisamvu na kisamvu ni nyama pia ungeita hivyo hivyo"..

Utatuzi wa suala lako mkuu, jitahidi uingie jikoni umpikie kama mara 2 mara 3 hiv ataona utofauti ama mueleze ukweli japo hii si njia nzuri saana kibinadamu, we ingia jikoni pika.. Km una nafasi shiriki katika mlo wenu wa siku kuanzia kuchagua mnakula nini mpaka upishi wake.. Mie sijui kwanini wanaume wenzangu wengi hawaprndi kushiriki hili jambo.
 
Mvumilie tu..labda ndivyo mapishi ya kwao hua ivyo..utayazoea tu kama ulivyozoea ya mkeo

Vipi anajua kukunyoa ndevu vizuri lakini?
 
Kwani ule ni uchafu Mkuu. Nadhani ni namna alivyokoroga koroga sababu lait ungepata mpishi huo muogo wala usingekuwa na muonekano huo uliouweka hapo.

Hivyo hakuna kitu cha kuliwa halafu kikaitwa uchafu Mkuu.
Huyo atakua anataka kumrudia mkewe hana lolote
 
Kweli mzee,Me ningekuwa naishia kula nje,mke apike chakula kizuri ..msosi ukiwa mzuri utafurahia hayo mapenzi.
 
Ni kweli si kila mwanamke anajua kupika,ila kuna raha yake kama mume unarudi nyumbani unakuta umepikiwa makwasukwasu kama hayo,ntachoka tu
Ila sio mbaya akatafutiwa darasa la kujifunza kupika sababu sidhani kama huyo mdada anapenda kupika hayo makwasu kwasu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…