Hii nchi haina usawa: Mbunge miaka mitano, mafao zaidi ya Tshs. 200M, mwalimu miaka 32 kazini, mafao Tshs. 70M, miezi sita hajalipwa

Hii nchi haina usawa: Mbunge miaka mitano, mafao zaidi ya Tshs. 200M, mwalimu miaka 32 kazini, mafao Tshs. 70M, miezi sita hajalipwa

Hii nchi haina usawa. Hii nchi haijapata kiongozi wa kuleta usawa ingalau kwa nusu tu miongoni mwa wananchi.

Tumesikia wimbo huu wa kinafiki kuwa, Rais John Pombe Magufuli ni Rais na kiongozi wa wanyonge, wananchi wa hali ya chini.

Si kweli, no uongo na ni propaganda za kisiasa tu kwa ajili ya wapambe na wanafiki wachache wanaomzunguka huku uhalisia wa mambo ukiwa tofauti.

Mfano wa kuthibitisha hili ni huu;

Bunge limevunjwa juzi tarehe 16/6/2020. Hawa wabunge lililovunjwa juzi wameingia kazini mwaka 2015. Wamefanya kazi yao miaka mitano (5) tu toka mwaka 2015 hadi mwaka huu 2020.

Inasemekana mafao ya kiinua mgongo kwa miaka mitano tu kila mmoja ni zaidi ya Tshs. 250,000,000.

Na inasemekana wakati Rais Magufuli (eti Rais wa wanyonge) anahutubia ndani hiyo juzi kulivunja bunge hilo, tayari mzigo wa fedha wa kila mbunge ulishaingia kwenye Bank Account yake.

Hebu tazama upande wa pili wa wanyonge halisi kinachotokea.

Huko Sengerema (na naamini kwingine kote Tanzania nzima), yupo mwalimu aliyefanya kazi miaka 32 (1988 - 2020) kwa taabu na shida nyingi. Amestaafu tangu mwezi Januari, 2020. Baada ya kukokotolewa kwa mafao yake ya mkupuo atapata kama Tshs. 75,000,0000 hivi.

Kinacholeta shida ni kuwa, tangu huyu mwalimu masikini astaafu kwa mujibu wa sheria mwezi january hadi Juni hii mwaka huu, 2020 (miezi 6 sasa) bado anasotea mafao yake haya kidogo, hajalipwa.

Sasa swali la kujiuliza ni hili;

Kati ya wabunge hawa ambao bunge linavunjwa leo huku mafao yao yakiwa yaneshalipwa jana na huyu mwalimu ambaye kastaafu miezi sita (6) iliyopita na bado hajalipwa vijisenti vyake vya mafao, ni nani hasa mnyonge?

Na huu usawa katika nchi hii uko wapi? Iweje mbunge aliyefanya kazi miaka mitano tu alipwe mafao ya kiinua mgongo kikubwa hivyo kwa takribani mara tano ya mwalimu ama nesi ama daktari aliyefanya kazi kwa miaka 35?

Huyu mtetezi wa wanyonge (Bwana Magufuli) anatetea wanyonge na unyonge upi hasa?

Mimi nasema Tanzania haina kiongozi Rais mtetezi wa wanyonge. Haijapata na hakuna kizuri wala kiongozi mzuri atakayetokana na CCM ili kubadilisha hali hii na kuleta tofauti na usawa.
Dhana ya "Rais wa wanyonge" ina maana nyingi. Kwa namna wanavyolitumia hawa wenzetu inaonekana wanamaanisha Rais anayetengeneza taifa la watu wanyonge ili awatawale wakiwa katika hali hiyo ya unyonge.
 
Maneno ya Ndugai alipopokea mic kutoka kwa Rais mliyasikia? Akaanza kusema "nimetumwa na wabunge kukwambia Mhe. Rais kuhusu utaratibu...kuhusu utaratibu" huku anacheka cheka... Wabunge nao wanashangilia... halafu akasema "nimeambiwa imeshapita..."

That was beyond reprehensible.

The last thing out of your mouth mbele ya Watanzania milioni 60 wasio na viinua mgongo, pensheni, ajira, savings account, bima, mitaji, nothing, kwenye kufunga bunge ni kuongelea maslahi yenu binafsi, kupigia chapuo mabilioni yenu? Ubinadamu gani huo?

Tena unajifanya kama bado hazijatoka au zinaweza kukwama vile, ili ujipigie kampeni ya kurudi kwenye U-Spika kwamba we ndo ulizipigania wakati unajua zimeshalipwa kwenye benki zenu!

Bado hatuna watu wanaojua ku balance maslahi yao na ya Umma.
 
Ndg yangu mtoa post! Nimeisoma post yako kidogo tu nikajua unakoelekea! Jibu la hoja yako ni dogo tu " Acha kazi hizo unazofanya zenye ujira mdogo" sheria yetu ipo wazi inaruhusu tu na wewe kuzamia humo mjengoni! Vinginevyo utaendelea kushangaa na kulalamika!
 
Sheria ungekuwa unatunga wewe ?
vilaz.a wale watatunga sheria gani ya maana, si bora hizo sheria kukawa na kakikundi kadoogo ka watanzania WATAALAM wakatusaidi kuzitunga hizo sheria.
Bunge la tz uwepo wake hauna tija yoyote...ni bahati mbaya wananchi wa kawaida hatuna namna yoyote ya kupinga hali hiyo...labda kizazi kijacho kitapata "namna" ya kuukataa ujinga huu!!!.
 
Ndg yangu mtoa post! Nimeisoma post yako kidogo tu nikajua unakoelekea! Jibu la hoja yako ni dogo tu " Acha kazi hizo unazofanya zenye ujira mdogo" sheria yetu ipo wazi inaruhusu tu na wewe kuzamia humo mjengoni! Vinginevyo utaendelea kushangaa na kulalamika!
Kwahio akizamia mjengoni yeye matatizo ya mafao kwa walimu wote nchini yataisha?
 
Wengine mafao yetu hayazidi laki Saba lakini mpaka leo hatujapata tunazidi kufuatilia tu .
 
Ndio maana wanatoa rushwa, kulogana, kujipendekeza ili wapate ubunge, na kazi yao kubwa bungeni nikupiga tu makofi na kusema ndio. Ningekuwa Raisi ningeshusha mshahara wa wabunge ka kada nyingine ili wapatikane wazalendo wa kweli wakutunga sera za kimaendeleo kwa nchi.
Inahuzunisha sana Tanzania siasa imesha kuwa the big business, tuombe Mungu huko mbele abadili kila kitu siasa iwe ni kazi ya kujitolea ili kuwasaidia wananchi,. Ni Nyerere peke yake ndio alikuwa mwanasiasa mzalendo Tanzania. Wabunge walikuwa wanasafiri kwa mabasi kwenda bungeni.
 
Hakuna mwanasiasa anayeweza kuleta usawa wa kipato,ni porojo tu.
 
Hii nchi haina usawa. Hii nchi haijapata kiongozi wa kuleta usawa ingalau kwa nusu tu miongoni mwa wananchi.

Tumesikia wimbo huu wa kinafiki kuwa, Rais John Pombe Magufuli ni Rais na kiongozi wa wanyonge, wananchi wa hali ya chini.

Si kweli, no uongo na ni propaganda za kisiasa tu kwa ajili ya wapambe na wanafiki wachache wanaomzunguka huku uhalisia wa mambo ukiwa tofauti.

Mfano wa kuthibitisha hili ni huu;

Bunge limevunjwa juzi tarehe 16/6/2020. Hawa wabunge lililovunjwa juzi wameingia kazini mwaka 2015. Wamefanya kazi yao miaka mitano (5) tu toka mwaka 2015 hadi mwaka huu 2020.

Inasemekana mafao ya kiinua mgongo kwa miaka mitano tu kila mmoja ni zaidi ya Tshs. 250,000,000.

Na inasemekana wakati Rais Magufuli (eti Rais wa wanyonge) anahutubia ndani hiyo juzi kulivunja bunge hilo, tayari mzigo wa fedha wa kila mbunge ulishaingia kwenye Bank Account yake.

Hebu tazama upande wa pili wa wanyonge halisi kinachotokea.

Huko Sengerema (na naamini kwingine kote Tanzania nzima), yupo mwalimu aliyefanya kazi miaka 32 (1988 - 2020) kwa taabu na shida nyingi. Amestaafu tangu mwezi Januari, 2020. Baada ya kukokotolewa kwa mafao yake ya mkupuo atapata kama Tshs. 75,000,0000 hivi.

Kinacholeta shida ni kuwa, tangu huyu mwalimu masikini astaafu kwa mujibu wa sheria mwezi january hadi Juni hii mwaka huu, 2020 (miezi 6 sasa) bado anasotea mafao yake haya kidogo, hajalipwa.

Sasa swali la kujiuliza ni hili;

Kati ya wabunge hawa ambao bunge linavunjwa leo huku mafao yao yakiwa yaneshalipwa jana na huyu mwalimu ambaye kastaafu miezi sita (6) iliyopita na bado hajalipwa vijisenti vyake vya mafao, ni nani hasa mnyonge?

Na huu usawa katika nchi hii uko wapi? Iweje mbunge aliyefanya kazi miaka mitano tu alipwe mafao ya kiinua mgongo kikubwa hivyo kwa takribani mara tano ya mwalimu ama nesi ama daktari aliyefanya kazi kwa miaka 35?

Huyu mtetezi wa wanyonge (Bwana Magufuli) anatetea wanyonge na unyonge upi hasa?

Mimi nasema Tanzania haina kiongozi Rais mtetezi wa wanyonge. Haijapata na hakuna kizuri wala kiongozi mzuri atakayetokana na CCM ili kubadilisha hali hii na kuleta tofauti na usawa.

Vipi kuhusu madiwani wanapata mafao kiasi gani?
Aisee watu wanauana kwenye nafasi za kisiasa
 
Na mfano hai aliekuwa mbunge wa Kilombero kabla ya huyu alieomba kaz ya kupiga deki na kufagia Lumumba, mpk sasa ni marehemu.
uko sahihi kabisa, zile pesa ni DHULUMA hauwezi kufanikiwa maishani.
Wengi wao wakitoswa ubunge hufa masikini!!.
Ogopa sana kudhulumu masikini.
cc Job Ndugai
 
Back
Top Bottom