Hii nchi haina usawa: Mbunge miaka mitano, mafao zaidi ya Tshs. 200M, mwalimu miaka 32 kazini, mafao Tshs. 70M, miezi sita hajalipwa

Hii nchi haina usawa: Mbunge miaka mitano, mafao zaidi ya Tshs. 200M, mwalimu miaka 32 kazini, mafao Tshs. 70M, miezi sita hajalipwa

Siku tukilinganisha mambo mengine na nchi zingine usikimbie


Kwa nini nikimbie? Kwa hiyo ulitaka Mwalimu na Mbunge wawe na kipato sawa? Ni wapi hilo linafanyika labda?
 
Kwahiyo bila bunge kwahiyo bunge likifutwa zitakuwa zinapitishwa na nani ?
Mkuu.

Bunge likifutwa hapo inamaanisha aliyelifuta ndiye anakua inchaji. Kwa nchi yetu Rais ana uwezo huo.

So yeye ndiye atapitisha.
 
Mkuu Mimi huwa mnanikosea hapo tu ukiachana na CCM tatizo siyo chama sisi ndo tupo hivyo kama waafrika mi nipo tayari kuona kiongozi yoyote akae madarakani najua ni yale yale yataendelea. Swala kuu ni kutengeneza FIKRA ya huyu mwafrika achana kabisa na mambo za CCM CDM futa.
 
Hilo GENGE LA WAHUNI hata siku moja haliwezi kuona tofauti hii kubwa sana kati ya mapato ya Wabunge wa Bunge FAKE na madaktari, walimu, manesi n.k. Hakuna haki hata chembe.


Hii nchi haina usawa. Hii nchi haijapata kiongozi wa kuleta usawa ingalau kwa nusu tu miongoni mwa wananchi.

Tumesikia wimbo huu wa kinafiki kuwa, Rais John Pombe Magufuli ni Rais na kiongozi wa wanyonge, wananchi wa hali ya chini.

Si kweli, no uongo na ni propaganda za kisiasa tu kwa ajili ya wapambe na wanafiki wachache wanaomzunguka huku uhalisia wa mambo ukiwa tofauti.

Mfano wa kuthibitisha hili ni huu;

Bunge limevunjwa juzi tarehe 16/6/2020. Hawa wabunge lililovunjwa juzi wameingia kazini mwaka 2015. Wamefanya kazi yao miaka mitano (5) tu toka mwaka 2015 hadi mwaka huu 2020.

Inasemekana mafao ya kiinua mgongo kwa miaka mitano tu kila mmoja ni zaidi ya Tshs. 250,000,000.

Na inasemekana wakati Rais Magufuli (eti Rais wa wanyonge) anahutubia ndani hiyo juzi kulivunja bunge hilo, tayari mzigo wa fedha wa kila mbunge ulishaingia kwenye Bank Account yake.

Hebu tazama upande wa pili wa wanyonge halisi kinachotokea.

Huko Sengerema (na naamini kwingine kote Tanzania nzima), yupo mwalimu aliyefanya kazi miaka 32 (1988 - 2020) kwa taabu na shida nyingi. Amestaafu tangu mwezi Januari, 2020. Baada ya kukokotolewa kwa mafao yake ya mkupuo atapata kama Tshs. 75,000,0000 hivi.

Kinacholeta shida ni kuwa, tangu huyu mwalimu masikini astaafu kwa mujibu wa sheria mwezi january hadi Juni hii mwaka huu, 2020 (miezi 6 sasa) bado anasotea mafao yake haya kidogo, hajalipwa.

Sasa swali la kujiuliza ni hili;

Kati ya wabunge hawa ambao bunge linavunjwa leo huku mafao yao yakiwa yaneshalipwa jana na huyu mwalimu ambaye kastaafu miezi sita (6) iliyopita na bado hajalipwa vijisenti vyake vya mafao, ni nani hasa mnyonge?

Na huu usawa katika nchi hii uko wapi? Iweje mbunge aliyefanya kazi miaka mitano tu alipwe mafao ya kiinua mgongo kikubwa hivyo kwa takribani mara tano ya mwalimu ama nesi ama daktari aliyefanya kazi kwa miaka 35?

Huyu mtetezi wa wanyonge (Bwana Magufuli) anatetea wanyonge na unyonge upi hasa?

Mimi nasema Tanzania haina kiongozi Rais mtetezi wa wanyonge. Haijapata na hakuna kizuri wala kiongozi mzuri atakayetokana na CCM ili kubadilisha hali hii na kuleta tofauti na usawa.
 
Hii nchi haina usawa. Hii nchi haijapata kiongozi wa kuleta usawa ingalau kwa nusu tu miongoni mwa wananchi.

Tumesikia wimbo huu wa kinafiki kuwa, Rais John Pombe Magufuli ni Rais na kiongozi wa wanyonge, wananchi wa hali ya chini.

Si kweli, no uongo na ni propaganda za kisiasa tu kwa ajili ya wapambe na wanafiki wachache wanaomzunguka huku uhalisia wa mambo ukiwa tofauti.

Mfano wa kuthibitisha hili ni huu;

Bunge limevunjwa juzi tarehe 16/6/2020. Hawa wabunge lililovunjwa juzi wameingia kazini mwaka 2015. Wamefanya kazi yao miaka mitano (5) tu toka mwaka 2015 hadi mwaka huu 2020.

Inasemekana mafao ya kiinua mgongo kwa miaka mitano tu kila mmoja ni zaidi ya Tshs. 250,000,000.

Na inasemekana wakati Rais Magufuli (eti Rais wa wanyonge) anahutubia ndani hiyo juzi kulivunja bunge hilo, tayari mzigo wa fedha wa kila mbunge ulishaingia kwenye Bank Account yake.

Hebu tazama upande wa pili wa wanyonge halisi kinachotokea.

Huko Sengerema (na naamini kwingine kote Tanzania nzima), yupo mwalimu aliyefanya kazi miaka 32 (1988 - 2020) kwa taabu na shida nyingi. Amestaafu tangu mwezi Januari, 2020. Baada ya kukokotolewa kwa mafao yake ya mkupuo atapata kama Tshs. 75,000,0000 hivi.

Kinacholeta shida ni kuwa, tangu huyu mwalimu masikini astaafu kwa mujibu wa sheria mwezi january hadi Juni hii mwaka huu, 2020 (miezi 6 sasa) bado anasotea mafao yake haya kidogo, hajalipwa.

Sasa swali la kujiuliza ni hili;

Kati ya wabunge hawa ambao bunge linavunjwa leo huku mafao yao yakiwa yaneshalipwa jana na huyu mwalimu ambaye kastaafu miezi sita (6) iliyopita na bado hajalipwa vijisenti vyake vya mafao, ni nani hasa mnyonge?

Na huu usawa katika nchi hii uko wapi? Iweje mbunge aliyefanya kazi miaka mitano tu alipwe mafao ya kiinua mgongo kikubwa hivyo kwa takribani mara tano ya mwalimu ama nesi ama daktari aliyefanya kazi kwa miaka 35?

Huyu mtetezi wa wanyonge (Bwana Magufuli) anatetea wanyonge na unyonge upi hasa?

Mimi nasema Tanzania haina kiongozi Rais mtetezi wa wanyonge. Haijapata na hakuna kizuri wala kiongozi mzuri atakayetokana na CCM ili kubadilisha hali hii na kuleta tofauti na usawa.
NDIOMAANA SIPOTEZI MUDA KUWAPIGIA KURA CCM
 
Kwa taarifa yenu zile hela anazogawa barabarani na kwenye makanisa ya katoliki ni michango ya wastaafu kutoka psssf. Mfuko upo hoi.

Mlivyo wanafiki, wazushi na wachonganishi, eti: "Magufuli uchangia makanisa ya Kikatoliki!!" Mara ngapi tumeshuhudia akichangia ujenzi wa Misikiti Nchini, juzi hapa kachangia ujenzi wa Msikiti pale Chato - wakati mwingine mjifunze kubakiza akiba ya maneno.

Nisieleweke vibaya, hata mini uaikitishwa sana nionapo wastaafu wakipigwa danadana, kucheleweshwa mafao yao, wengine kutolipwa kabisa kutokana na visingizio vya kutunga tu na dhuluma za mwajili bahati mbaya Serikali hii hii ambayo tunaiita ni mtetezi mkubwa wa wanyonge inakuwa na kigugumizi cha kuwachukulia hatua kali/wajibisha waajili wakorofi ,wadhulumaji na mafisadi wanao endedha mashirika ya UMMA kama mali ya UKOO!! Mfano ahi TAZARA, wastaafu wameangahikia kiinua mgongo chao miaka nenda rudi bila mafanikio, Wizara ikufikia hatua ya kuwambia wastaafu jqamba hawastahili kulipwa kiinua mgongo, hivi kuna sheria gani hapa kwetu Tanzania ambayo inasema baadhi ya mashirika ya UMMA haya wajibiki kulipa wastaafu kiinua mgongo, inakuwaje Serikali ya Zambia imewajibika kuwalipa wastaafu wa TAZARA upande wa ZAMBIA lakini Serikali yetu tunayo fikiri ni mtetezi mkubwa wa wanyonge haioni umuhimu wa kuiga mfano mzuri wa Zambia wa kuwalipa kiinua mgongo wastaafu wa TAZARA upande wa Tanzania ambao wengi wao walihusika katika ujenzi wa reli, robo ya wastaafu wamekwisha fariki Dunia, inaelekea tatizo la wastaafu wa East Africa Community linataka kujirudia TAZARA.

Kinacho shangaza zaidi katika suala zima la wastaafu wa TAZARA, atakuta wanao fikisha suala hili mahakamani kwa kutumia mawakili, Serikali inakubali kuwalipa kiinua mgongo chao! Hii inamaanisha wale wasio kuwa na uwezo wa kuwalipa mawakili watakosa haki zao, now a million dollar question is: kwa nini Serikali moja inakuwa na double standard linapo kuja suala la kuwalipa wastaafu wa TAZARA mafao yao.
 
Badala ya kutumia pesa nyingi hivyo kuwalipa wagonga meza, ni bora kuwapa wataalamu angalau wafanye tafiti mbali mbali ikiwemo kutafuta chanjo na dawa za magonjwa kama korona...
 
Nitajie nchi iliyo na usawa kati ya Wanasiasa na watu wa kawaida, ...

Usiniulize swali badala yake lieleze jukwaa kwanini unadhani kusiwe na usawa kati yao?

Sera na ilani ya CCM toka mwaka 1961 mpaka 2020 inasemaje kuhusu hili...?
 
Nina dada yangu Mwalimu amestaafu toka mwezi wa sita mwaka 2018. Mpaka leo anafuatilia mafao yake na hajalipwa. Mbaya zaidi kwa sasa anaumwa na hana msaada wowote wa kifedha.

Hapo ndipo ninapowaona wale wafanyakazi wanaoiba na kuchukua rushwa wakiwa kazini ni mashujaa. Kwa nchi hii hali ilipofikia kufanya kazi kwa uaminifu kwa kutegemea utakuja kulipwa mafao ni ujinga wa hali ya juu!!!

Aisee, It's very sad....

Inaumiza sana ndugu yangu. Mungu amsaidie huyo mama kwanza apate afya na alipwe mafao yake haraka...

Na sisi wengine tusichoke kupiga kelele....

Lazima kila tupatapo nafasi tu - shout against this injustice....

Kelele zetu hizi za msaada zinamfikia Mungu na anasikia...

Ukombozi wetu u karibu, msikate tamaa
 
Usiniulize swali badala yake lieleze jukwaa kwanini unadhani kusiwe na usawa kati yao?

Sera na ilani ya CCM toka mwaka 1961 mpaka 2020 inasemaje kuhusu hili...?


Kwani nimekulazimisha kunijibu? Ondoa jazba kama mtoto, ...
 
Back
Top Bottom