Uchaguzi 2020 Hii ndio awamu iliyofeli kuliko awamu zote zilizopita

Uchaguzi 2020 Hii ndio awamu iliyofeli kuliko awamu zote zilizopita

Lack of sense? Yaani kisa amedhibiti wala rushwa na wabadhirifu? Kisa anajenga Sgr,Daraja la wami na busisi? Kisa amenunua ndege kwa hela cash Dremliner na midege ya Airbus. Kajenga hospital ,vituo vya afya na zahanati lukuki. Mlitaka raisi gani? Au ndio upungufu wa akili!
Mkuu hii corona itatusaidia kujua hivyo vituo vya afya na zahanati vimejengwa nchi gani.mpaka sasa corona imeshatusaidia kujua kuwa serikali haina pesa,Yale tuliyokuwa tunaambiwa kwamba pesa ipo yalikuwa yanatokana tu na kiburi cha uzima
 
Alitegemea dhana ya kutawala kwa mkono wa chuma,matokeo yake imemuharibia .

Ni mambo ya muda tu,hata kule Sudan Al Bashir hakutegemea kama siku moja angekuwa mfungwa.
 
Ziko sababu lukuki za kuonesha namna awamu hii ilivyofeli

1. Ikumbukwe walipoingia madarakani walituaminisha masuala ya wafanyakazi hewa na wanafunzi hewa wakatuambia na kiasi walichookoa na wakaendelea kutuaminisha awamu zilizopita zilikusanya kidogo embu tuone kuna ukweli.

(A) Awamu iliyopita hawakuchukua vyanzo vyama halmashauri, kwa wa machinga pia hawakuchukua sekta binafsi ndio ilikuwa injini sasa awamu hiii imechukua vyanzo vyote vya halimashauri lakini inaongoza kwa kukopa tena nje ya utaratibu Leo tycoon akitaka hata ajengewe sanamu yake pale chamwino DODOMA hahitaji baraka za bunge

(B) Mahakama kuwa karibu na serikali hasa kwenye kesi zinazokiuka haki rejea kesi ya Godbless Lema kesi ya viongozi wa chadema ama kesi iliyosomwa jana ya Mike Mushi na Melo nyuma ya hizi hukumu kuna mkono shinikizi kupitia mfumo

2. Hii ndio awamu inayooongoza kwa vitendo vya kikandamizaji tena hawajali rejea mauaji ya Kibiti ama kupotea kwa watu mbalimbali yu wapi msaadizi wa Freeman Mbowe ndugu Ben Rabiu Saanane wapi alipo Simoni Kanguye wapi alipo Azori Gwanda haya yote yanaonesha jinsi awamu hii ilivyoshindwa kulinda ustawi wa jamii

3. Kushambuliwa kiongozi wa upinzani mh Tundu Athipas Lissu katikati ya vipindi vya bunge na kuvuliwa ubunge kinyume cha sheria na pia kukosa hata kumnyima stahiki yake ya matibabu

Yote kwa yote hiii ndio awamu imeshindwa kuajiri kwa miaka zaidi ya minne imeshindwa kupunguza tatizo la ajira imepelekea vijana wengi kushiriki betting kwa kikukosa ajira

Mwisho huu ni mwaka wa uchaguzi ni lazima umma tukarejeshe utu uwajibikaji wa umma na demokrasia ishamiri tena kupitia sanduku la kura hiii ndo fimbo ya mnyonge ya kutetea utu wetu

#stayhome
#tunatakatumehuru
[emoji111]️


Sent using Jamii Forums mobile app
Naunga hoja
 
Awamu hii 5, wasomi ajira yao kuu ni kucheza kamali za wachina a. k. a Bonanza. Magufuli Mungu anakuona.
 
sasa shangaa poliice,tume na watanzania wengine wanavyompigania aongeze miaka 5,yaani sometime unashindwa elewa Kama hao watu ni binadamu au wanyama
Hapa wa kulaumiwa ni wazee wa dsm wakiongozwa na Mzee Ganze walikabidhi nchi kwa shetani badala ya MUNGU

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii awamu ya tano imelitia aibu Taifa hili rekodi yetu ya haki za binadamu imevunjiliwa mbali kwa Watanzania kupigwa risasi hadharani na wengine kuuwawa huko Rufiji

Cha ajabu zaidi hawana nia ya kuibadili tume ya uchaguzi na wizi wa kura na upendeleo utabakia pale pale
 
Ukandamizaji ni asiri ya mwanadamu inawezekana hata wewe wapo ndugu zako unaowakandamiza kwenye familia yenu. Yawezekana una miaka kadhaa hata wazazi wako huendi kuwasalimia, itazame kasoro yako. Nimeona barabarani mwenye Lori anamdharua wa kosta, na wa kosta anamdharau wa bajaji, wa bajaji anamdharau wa pikipiki wa pikipiki anamdharau mwenda kwa miguu.
 
Ukandamizaji ni asiri ya mwanadamu inawezekana hata wewe wapo ndugu zako unaowakandamiza kwenye familia yenu. Yawezekana una miaka kadhaa hata wazazi wako huendi kuwasalimia, itazame kasoro yako. Nimeona barabarani mwenye Lori anamdharua wa kosta, na wa kosta anamdharau wa bajaji, wa bajaji anamdharau wa pikipiki wa pikipiki anamdharau mwenda kwa miguu.

Binadamu asili yake ni ubinafsi sio ukandamizaji kuna tofauti ya ubinafsi na ukandamizaji


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapa wa kulaumiwa ni wazee wa dsm wakiongozwa na Mzee Ganze walikabidhi nchi kwa shetani badala ya MUNGU

Sent using Jamii Forums mobile app
Mtawalaum sana Ila tatizo si wao,tatizo ni wewe na Mimi,tulio wengi tunadhani Mambo ya nchi hii hayatuhusu so tumeachia kikundi cha watu wasio zidi 1000 na wafuasi wao Kama milioni 9 na ndo waamue kila kitu kinachomhusu watanzania wote milioni 55,
 
Ameanzisha mamiradi yanayoitwa WHITE ELEPHANT; ile SGR na Stiglers Gorge. Hii miradi inakula fedha nyingi, itachukua muda mrefu kukamilika na hawezi kuleta FAIDA hata ikikamilika.

Amehamishia Serikali Dodoma lakini muda wote viongozi wanaongoza wakitokea DSM. Wanakwendaga Dodoma karibu na vikao vya Bunge ili kuwatisha wabunge wa CCM kwenye party caucuss.

Awamu ya 5 imerudisha maendeleo nyuma kwa miaka 50 kama alivyosema Jenerali Ulimwengu. Tulikosea sana mwaka 2015, hasa KIKWETE kwa kumg'ang'ania BENARD MEMBE ndipo tukaangukia kwenye AJALI hii.
 
Hii ni awamu ambayo wapigaji wamefeli sana, wamebaki kutapatapa na kueneza chuki za Kijinga.
Chadema mlimtukana sana Mzee Wa msoga na mpaka mkampa jina Vasco Da Gamma, Na mlisema ndio Rais ovyo kabisa,ushaidi kibao humu, Leo hii mmesahau? Ukiomba upewe unachotaka kubali.
MUNGU amejibu maombi yenu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndio awamu pekee ambayo 1.5 trillion inaibiwa alafu poa tu hakuna maelezo Yani poa tu
 
Ajira imeshuka katika sekta binafsi na kampuni zinakufa
Hilo la mwisho la kuajiri; kazi ya serikali ni kuweka mazingira wezeshi ili sekta binafsi ndio iendeshe uchumi hiyo kutoa ajira na kulipa kodi stahiki. Hivyo cha kuajiri ni kuangalia ajira za zimeongezeka katika sekta binafsi badala ya kuangalia tuu ajira serikalini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali inabambikia wafanyabiashara kesi Leo watu wameondoa mitaji Yao imeshindwa kuiwezesha sekta binafsi Leo tenda utasikia jkt mara magereza hizo ajira zitakuja je kwenye sekta binafsi


Sent using Jamii Forums mobile app
Mara TBA, TEMESA, TANESCO.
Sasa ukiangalia hapo kampuni za ujenzi zinakufa Mana JKT na TBA wanamchukua dili , TEMESA nao wanamchukua dili , umeme ivyoivyo TANESCO wanamchukua dili. Kampuni kibao zinakufa .
Zidumu fikra za awamu ya tano kwa ubunifu didimizi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom