Hii ndio hali ya Bumbuli ambayo Mbunge wake ni Waziri wa Mambo ya nje ya Nchi

Hii ndio hali ya Bumbuli ambayo Mbunge wake ni Waziri wa Mambo ya nje ya Nchi

Hawa ni watu wachache sana, lakini viongozi wao wamejua jinsi ya kutumia raslimali zao kuu, hasa mbili: Almas na ng'ombe vizuri sana.
Kubwa zaidi, hawana uvumilivu hata kidogo na ufisadi.

Hata sisi, pamoja na wingi wetu huu, raslimali tulizo nazo zingeweza kutusukuma mbele zaidi na kwa haraka, lakini tunakwazwa sana na CCM. Kazi kubwa wanayoifahamu siku hizi hawa watu ni kupeana ulaji tu, na kupewa "kamba ndefu" ili wale kwa urefu wa kamba zao. Hebu tazama teuzi zinavyofanywa siku hizi, hakuna cha 'merit' wala nini, sifa kubwa ni kuwa "chawa" au unategemewa kufaidisha hao wanaokuteuwa ili waendelee kukaa madarakani; akina Makonda ni mfano mzuri hapa.

Botswana hawana mchezo na elimu yao, kama tunavyofanya sisi hapa. Watu wanamaliza kidato cha nne, utadhani ndiyo kwanza wamemaliza shule za primari! Chuo kikuu, sitaki hata kulinganisha.

Mambo ni hivyo hivyo hata Namibia. Si uliwahi kusikia kisa cha Balozi wetu aliyeteuliwa kwenda kutuwakilisha huko; balozi aliyemshangaza hata Rais wao kapelekwa kufanya kazi gani huko!
Ni ipi sababu ya hayo yote mkuu, hapa kwetu wananchi tunasema ni viongozi wanafuja pesa, huko kwao kima cha chini au cha juu wanacholipwa viongozi wao ni kiasi gani??

Maana hapa kwetu ukiritimba unaanzia kwenye mishahara ya viongozi na kusahau kada muhimu.
 
Kuanzia kazungula, pandamatenga, ngwasha, nata, francis town, palapye, mahalapye, Gaborone, A3 ni super road, kwakweli, Namibia kupitia katima mulilo boda, ni super. Na ni landlocked countries. Sijui tumelogwa wapi Watanzania. Dah inauma sana.

Namibia siyo landlocked, ina ufukwe wa atlantic, nimeshaogelea Swakopmund bahari ya Atlantic ila maji yake baridi sana siyo kama kwetu …
 
Umeeleza vizuri. Lakini kwa nini kila kitu cha maendeleo katika wilaya au halmashaurI tusubiri fedha/uamuzi kutoka serikali kuu/hazina. Kama ni hivyo kwa nini tuna wakuu wa wilaya na ma-ded. Na mchango wa wananchi utaonekana wapi. Tusilaumu Waziri Makamba. Inawezekana tatizo ni kubwa kuliko uwezo wake hata kama ana nia nzuri. Tutafute chanzo cha tatizo hilo badala ya kulaumu/kushutumu watu.
Watu wakiambiwa mikoa ifanye kazi kama majimbo wanakua mbogo
Huu mfumo tulio-nao ni mbovu sana na ni ngumu kuleta maendeleo
 
Nikijaaliwa ni moja ya nchi ya kutembelewa mkuu, inasifiwa sana kwa amani na maendeleo bila rushwa
Yes mkuu,ukiwa na private car ni safi zaidi,unaweza tembelea na familia au marafiki,ingilia Botswana thr kazungula OSBP,lala pale Kasane na ujionee tembo/swala/warthog mitaani (relax wana corridors zao na elewa in Botswana animals ana right of the way),next drive to Nata ,kata kulia pale nenda Maun,geuza drive to Francis Town lala pale,then to GABS thr palapye na off course ingia SA thr Mafeking then to joberg,radiation nyumbani kupitia Zimbabwe na malawi (kasumulu border),good luck...andaa kama 4000usd kwa budget ya 4 pax
 
Mara baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge Mheshimiwa January Makamba aliweka utaratibu wa wana Bumbuli kutoa kero zao

View attachment 2972079

Lakini pamoja na kero hizo kutumwa hali ndio kama mnavyoona .

View attachment 2972080

Jambo la Muhimu ambalo hupaswi kusahau ni kwamba , January Makamba alipita bila kupingwa
Kwanza jimbo hilo waliunda kina makamba tu ili kutokea ubunge. Hana muda kushughulikia jimbo maana saa zote ni mipango ya upigaji na kutaka kuja kua rais.
 
Ni ipi sababu ya hayo yote mkuu, hapa kwetu wananchi tunasema ni viongozi wanafuja pesa, huko kwao kima cha chini au cha juu wanacholipwa viongozi wao ni kiasi gani??

Maana hapa kwetu ukiritimba unaanzia kwenye mishahara ya viongozi na kusahau kada muhimu.
Mkuu 'Vishu Mtata', binafsi nisingejali hata kidogo hawa waliopo serikalini wanalipwa vizuri sana kama kazi zao wanazozisimamia zinaleta tija kwa taifa.

Tena ningehimiza walipwe vizuri zaidi, na kwa wale wanaokwapua mali za waTanzania hata kunyongwa wanyongwe kama ushahidi usiokuwa na shaka upo.

Botswana na Namibia viongozi wao na hata wafanya kazi wanalipwa vizuri kulingana na hali zao za uchumi. Wanazo taratibu zao zinazoeleweka, siyo hizi za hapa kwetu za tozo na vikokotoo vinavyoibuliwa bila mpangilio maalum.
 
kiongozi makini hujali taifa kwa ujula

hata mwalimu hakusukumiza mandeleo butiama pekee
Na ndo maana leo butiaMa inaendelea kua kijiji ukifka butiama ni km umeenda kijijini kwenu tu utofauti ni lami na taa za barabarani
 
Mara baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge Mheshimiwa January Makamba aliweka utaratibu wa wana Bumbuli kutoa kero zao

View attachment 2972079

Lakini pamoja na kero hizo kutumwa hali ndio kama mnavyoona .

View attachment 2972080

Jambo la Muhimu ambalo hupaswi kusahau ni kwamba , January Makamba alipita bila kupingwa
Uwe unatumia akili, Waziri hamiliki hazina, Wala Baraza la mawaziri halijipelekei miradi majimboni kwao kwa zamu
 
Hyo hali ni ya Nchi nzima maeneo ya vijijini..
 
Lushoto ilitakiwa iwe ni Switzerland 🇨🇭 ya Tanzania,nilibahatika kufika kule last December,Mwenyezi Mungu kawapa super wilaya ila wale wabunge wake 3 ni zeros kabisa,yaani hawawezi kujenga hata ile barabara ya mombo to mlalo,yaani barabara ipo vile vile alivyoiacha mjerumani,ilitakiwa ile pass ilambwe vema,jenga cable cars kutoka kule milimani hadi barabara kuu ya Moshi,jenga virukio vya maparachuti,yaani hizi ni vyanzo vya usd tu,vijana wake wamekua vibarua na maisha yao wamejikatia tamaa
Selfishness ndio hulka yetu !
Tunafikiria kujilimbikizia kwanza !!
Maendeleo baadaye !
 
Watu wakiambiwa mikoa ifanye kazi kama majimbo wanakua mbogo
Huu mfumo tulio-nao ni mbovu sana na ni ngumu kuleta maendeleo
"Majimbo" si ndiyo hayo hapo kwa jirani Kaskazini? Ufisadi na takataka zote zinazofanyika kwenye serikali kuu sasa zinazalishwa kwenye majimbo 47?

Katika kushindwa kwetu kuwajibishana kwenye hiyo serikali, sasa tunakimbilia kudhani itakuwa bora zaidi kuanzisha mfumo ule ule kwenye serikali za majimbo?
Dhana ya namna hii sijawahi kuielewa hata siku moja.
 
"Majimbo" si ndiyo hayo hapo kwa jirani Kaskazini? Ufisadi na takataka zote zinazofanyika kwenye serikali kuu sasa zinazalishwa kwenye majimbo 47?

Katika kushindwa kwetu kuwajibishana kwenye hiyo serikali, sasa tunakimbilia kudhani itakuwa bora zaidi kuanzisha mfumo ule ule kwenye serikali za majimbo?
Dhana ya namna hii sijawahi kuielewa hata siku moja.
Kwanini umetolea mfano kenya na sio u.s.a, canada, china au australia unaakili ndogo sana

Unataka watu wawajibike kivip nawakati mkuu wa mkoa, wa wilaya na mkurugenzi ni wateule wa rais
Hawaka pale kwa ajili ya wananchi bali kwa ajili ya Rais

Ukitaka watu wawajibike wachaguliwe na wananchi
 
Kwanini umetolea mfano kenya na sio u.s.a, canada, china au australia unaakili ndogo sana
Huu mstari umeonyesha ni kiasi gani ulivyo mtupu kichwani, na mara nyingi watu wa aina yako huwa sina simile nao hata kidogo. Hii Tanzania unailinganisha na hizo nchi ulizotaja hapo wewe, au shule uliyonayo haikupi uwezo wa kujuwa umuhimu wa kulinganisha vitu vinavyo fanana?
Hata hivyo, historia ya hizo nchi unaijuwa wewe; unajuwa walikoanzia na kufika hapo walipofika?

Ngoja kwanza nitazame unajiita nani tena..., pumbavu kabisa, sipotezi tena muda na kenge kama wewe.
 
Back
Top Bottom