Hii ndio historia ya familia ya Sykes

Hii ndio historia ya familia ya Sykes

HII NDIO HISTORIA YA FAMILIA YA SYKES.

Historia hii inaanzia kwa MZEE SYKES MBUWANE KLEIST. Huyu ndiye baba yake KLEIST SYKES.

MZEE SYKES MBUWANE KLEIST ni nani?
Sykes Mbuwane ni mamluki wa KIZULU aliyechukuliwa yeye na vijana wenzake wa kizulu kutoka kijiji cha LIKUNYI MSUMBIJI.

Walifikaje Tanganyika?
Kipindi cha UTAWALA wa kikoloni wa kijerumani chini ya HERMANN VON WISSMAN aliwachukuwa kwa meli ya kivita kama askari mamluki mpaka Pangani Tanga, Tanganyika kuja kupigana na ABUSHIRI BIN SALIM AL HARITH NA MTWA MKWAWA WA IRINGA.

KLEIST SYKES ALIZALIWA WAPI?

KLEIST SYKES alizaliwa mwaka 1894, Pangani Tanga kwa baba yake SYKES MBUWANE KLEIST na MAMA yake ni Mnyatulu, baada ya baba yake kufariki Kleist Sykes baadae alikuja Dar es salaam.

MAISHA YA KLEIST SYKES BAADA YA KUJA DAR.

KLEIST SYKES alimuoa Bi MLUGURU BINT MUSSA, na alibahatika kupata watoto watatu wa kiume.

(1) ABDULWAHEED KLEIST SYKES. (1924__1968).

(2) ALLY KLEIST SYKES. (1926__2013).

(3) ABBAS KLEIST SYKES. (1929__2021).

Kama inavyoonekana katika Picha namba (1). Waliosimama kutoka kulia ni Abdulwaheed Kleist Sykes, na Ally Kleist Sykes. Aliyekaa kutoka kulia ni Abbas Kleist Sykes na Baba yao mzazi Mzee Kleist Sykes.

Picha hii ilipigwa 1942, kipindi Abdulwaheed Kleist Sykes alipokuja kumuaga baba yake akitokea LOWER KABETE KENYA mafunzoni kabla ya kwenda BURMA kama Askari wa KAR BURMA INFANTRY. Na picha namba 2, ni MZEE ALLY KLEIST SYKES kipindi cha uhai wake.

Vile vile MZEE KLEIST SYKES ALIKUWA NA WAJUKUU.
Wafuatao ni baadhi ya wajukuu wake:

(1) EBRAHIM (EBBY) ABDULWAHEED KLEIST SYKES. 1952__2015). Kama anavyoonekana katika picha namba 3. Huyu ndiye Baba yake mzazi DULL SYKES msanii wa bongofleva.

(2) MUSSA ABBAS KLEIST SYKES.

(3) KLEIST ABDULWAHEED SYKES. Alifariki 22 novemba 2017.

(4) ABRAHAM ALLY KLEIST SYKES.

ASANTENI:

View attachment 2657367View attachment 2657369View attachment 2657370

Aisee
 
Anhaa kumbe wewe ndiye unaefaidika.
Wewe unapata faida ya kuuza vitabu na hayo madili.

ila sisi jamii ya watanzania hautusaidii chochote,unatupotezea tu muda. Usitake kutuektia hapa eti hizo historia zina umuhimu sana kwetu ili utuuzie hivyo vitabu..Wewe ni kama dalali au tapeli fulan.
Afro...
Ikiwa unaona naandika vitabu na makala zisizo na manufaa kwako ucha kuzisoma usipoteze muda wako.
Lakini isemee nafsi yako kwani mimi napendwa na wengi katika ukumbi huu.

Mimi ni mwandishi sihusiki na uuzajiji wa vitabu.
Na uandishi ni usomi si biashara.

Sijui ni nini kimekughadhibisha hadi unanitolea matusi.
Jamii ya Tanzania wananufaika na kalamu yangu.

Nimehusishwa katika uandishi wa kitabu cha maisha ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ("Nyerere Biograph.")
 
Afro...
Ikiwa unaona naandika vitabu na makala zisizo na manufaa kwako ucha kuzisoma usipoteze muda wako.

Lakini isemee nafsi yako kwani mimi napendwa na wengi katika ukumbi huu.

Mimi ni mwandishi sihusiki na uuzajiji wa vitabu.

Na uandishi ni usomi si biashara.

Sijui ni nini kimekughadhibisha hadi unanitolea matusi.

Jamii ya Tanzania wananufaika na kalamu yangu.

Nimehusishwa katika uandishi wa kitabu cha maisha ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ("Nyerere Biograph.")
Unaongea maneno mengi ila hauoneshi faida ya unachokifanya kwenye jamii.
Au kupendwa na watu ndio faida?
 
Jabulani,
Umepata kuwasikia akina Manning, Humplink, Taylor, Frisch, Schneider, Lee kwa kuwataja wacgache?
Maalim, nimewahi kuwasikia wawili kati ya hao uliowataja, naona tatizo halikuwa jina bali asili ya hao akina Sykes, Nyerere alimtenga pia Kambona kwa kuwa na asili ya Malawi.

Ni kama wafuasi wa Castro walivyomtenga Che Guevara kwenye madaraka baada ya mapinduzi kwa kuwa alikuwa ana asili ya Argentina
 
Afro...
Mimi ndiye nilyeieleza historia ya ukoo wa Sykes kwa kuandika kitabu cha maisha yao Tanganyika kwa kutumia nyaraka zao zinazokwenda nyuma kuanzia miaka ya mwanzoni karne ya ishirini.

Hizi nyaraka zipo na wamenimefungulia nikazisoma zote.

Hizi ni nyaraka za Kleist Sykes Mbuwane alizotumia kuandika kitabu cha maisha yake.

Kwa simulizi alizopokea kwa wazee wake ambao ndiyo mamluki wenyewe walioingia Tanganyika wakiongozana na Hermann von Wissmann historia ya ukoo wao inaanza na Chaka alipoanza vita kutokea Kwa Bulawayo mwaka 1828 akiteka majirani zake.

Katika kukimbia vita hivi Ukoo wa Sykes wakahamia Kwa Likunyi, Imhambane ambayo sasa ni Mozambique.

Hapo ndipo walipochukuliwa na Wissmann kuja kuwasaidia Wajerumani kuituliza Germany Ostafrika.

Wazulu waliwashinda Bushiri bin Salim Al Harith na rafiki yake Mtwa Abdallah Mkwawa.

Yapo mengi vipi ukoo huu ukaja kuwa mashuhuri hata wakaasisi African Association 1929, Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) 1933 na TANU 1954.

Sasa hakika historia hii ilikuwa haijulikani na zilifanyika juhudi kubwa kuwafuta katika historia ya kuasisi African Association na TANU na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.
Eti kwa nini hilo jina lao la ukoo sio la kibantu, Sykes
 
Eti kwa nini hilo jina lao la ukoo sio la kibantu, Sykes
Wanaogopa kutumia jina la ukoo Mbuwane wataonekana sio wazawa, ila itoshe tu kusema kwamba tuwatambue kama waswahili, ambao ni mchanganyiko wa makabila na mataifa mbalimbali
 
Unaongea maneno mengi ila hauoneshi faida ya unachokifanya kwenye jamii.
Au kupendwa na watu ndio faida?
Afro...
Labda tungefahamiana kwanza.
Ila nashangaa nakuona kama umechukizwa na mimi.

Kitu gani kimekukasirisha katika maandishi yangu?
Mimi siongei ila naandika na wakati mwingine kufanya mihadhara katika vyuo vikuu ninapoalikwa:

PUBLICATIONS/RESEARCH PAPERS/ARTICLES

The Life and Times of Abdulwahid Sykes 1924 –1968 The Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press London, 1998 translated into Kiswahili as Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes 1924-1968 Historia Iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza, Phoenix Publishers, Nairobi, 2002.

The Torch on Kilimanjaro, Oxford University Press, Nairobi, 2006

Contributing author for an African anthology: The Mermaid of Msambweni and Other Stories, Oxford University Press 2007, Nairobi.

Contributing author Dictionary of African Biography (DAB), Oxford University Press 2011, New York.
Uamuzi wa Busara, Abantu Publications 2008, Dar es Salaam.

Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No. 1, Ibn Hazm Media Centre, 2018, Dar es Salaam.
Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No.2, Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam

Dar es Salaam na Wazalendo Wake Mashujaa Katika Kupigani Uhuru wa Tanganyika Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaaam

Watu Mashuhuri Katika Kuulingania Uislam Tanzania, Sheikh Ilunga, Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam
Dola, Kanisa na Tatizo la Udini Tanzania, Ibn Hazm Media Centre, 2018, Dar es Salaam

The School Trip to Zanzibar, Africa Proper Education Network 2020, Dar es Salaam
Rajabu Ibrahim Kirama, Jemadari wa Vita Kuwa Jemadari wa Uislam, Readit, 2020, Dar es Salaam

In Praise of Ancestors (1987) Africa Events (London).
Abdulwahid Sykes: Founder of Political Movement (1988) Africa Events (London).

Islam and Politics in Tanzania (1989) Al Haq International (Karachi)
The Plight of Tanzanian Muslim (1993) Change (Dar es Salaam).

Tanzania - The "Secular" Unsecular State (1995) Change (Dar es Salaam).

The Question of Muslim Stagnation in Education in Tanzania - A Muslim Riddle (Paper presented at the Conference of the Global World of the Swahili Intercultural Dialogue on the Indian Ocean Zanzibar, February 20 - 23, 2003).

Islamic Education and Intellectualism in Eastern Africa ‘Themes from the Pulpit in Tanganyika (Tanzania Mainland) 1800 – 2000’ (Paper presented at International Symposium on Islamic Civilisation in Eastern Africa Kampala, Uganda organised by the Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA), Istanbul and the Islamic University in Uganda, Mbale December 15th – 17th 2003).

Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27th February – 4th March 2004).

Islamic Movement and the Christian Lobby in Tanzania - the Experience of the late Prof. Kighoma Ali Malima (1938 – 1995) (Paper Presented to Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) Sokoine University of Agriculture (SUA) Morogoro 11th April 2004).

Terrorism in East Africa the Tanzanian Experience (Paper Presented at the Conference on Islam, Terrorism and African Development University of Ibadan, Nigeria 8th - 10th February 2006).

Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma bin Khamis (1940 – 1994) and the Pork Riots of 1993. (Paper Presented at the Regional Conference on Islam in Eastern Africa: Islam Encounter with the Challenges of the 21st Century 1st - 3rd August 2006, Kenyatta University, Nairobi.

Muslim Bible Scholars of Tanzania – The Legacy of Sheikh Ahmed Deedat (1918 – 2005) Paper Presented at the International Symposium on Islamic Civilisation in Southern Africa Organised by The Organisation of Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA) The National AWQAF Foundation of South Africa (AWQAF SA 1 – 3 September 2006 University of Johannesburg.

Tanzania: A Nation Without Heroes Seminar Organised by IFRA French Institute for Research in Africa and BIEA British Institute in East Africa 23rd and 24th September 2013 at IFRA Nairobi.

Awards: Several Awards

Visiting Scholar: (2011)
University of Iowa, Iowa City, USA
Northwestern University, Chicago, Illinois, USA
Zentrum Moderner Orient (ZMO), Berlin.

OTHER COUNTRIES VISITED

Zambia, Ethiopia, Great Britain, Swaziland, Msumbiji, Zimbabwe, Zambia, Sudan, Egypt, Saudi Arabia, United Arab Emirates, Oman, Yemen, Uganda, Switzerland, Iran, France, Netherlands, Turkey and Abu Dhabi.
 
Eti kwa nini hilo jina lao la ukoo sio la kibantu, Sykes
Johnny....
Kleist jina lake ni Abdallah jina hili lipo katika kaburi lake.
Schneider Plantan jina lake ni Abdillah.

Mashado Plantan jina lake ni Ramadhani.

Hayo majina ya KIjerumani ni majina ambayo Wajerumani waliwapa na kuwasajili kwa majina hayo walipozaliwa.
Ukoloni una karaha zake.

1686941639915.jpeg

Kaburi la Kleist (Abdallah) Sykes
 
Huo ni unini tuite? Unge heshimu alicho leta mbona ni jambo jema kujua historia.
Mzee...
Kuna watu wamekasirishwa na mimi kusahihisha historia ya uhuru.
Historia ilikuwa inaeleza kuwa TANU iliundwa na Julius Nyerere.

Nilipoandika kitabu cha Abdul Sykes na kueleza kuwa Mwalimu alipokelewa na Abdul Sykes na akaikuta TANU kwa Abdul Sykes hawakupendezewa.

Ikawa historia hii imewaudhi.
 
Wanaogopa kutumia jina la ukoo Mbuwane wataonekana sio wazawa, ila itoshe tu kusema kwamba tuwatambue kama waswahili, ambao ni mchanganyiko wa makabila na mataifa mbalimbali
Jabulani,
Wakati hawa watoto wanazaliwa hapakuwa a siasa za uzawa.

Hawa wote wakijulikana kuwa ni Wazulu kutoka Mozambique na watu waliotoka nje ya Tanganyika walikuwa wengi Tanganyika wengi katika miaka ya 1950s.

Walikuwa kizazi cha pili na cha tatu.

Mimi ni Mmanyema kizazi cha nne babu yangu Mkuu Mwekapopo Samitungo yeye alikuwa kutoka Begian Congo na kaletwa na Wajerumani kama askari.

Mimi ni kizazi cha nne na kipo cha tano katika karne hii ya 21.
 
Achana na historia hizi zinaweza kutwistiwa ili kufit narrative na malengo ya wanayoisimulia.
Muda tunaoishi ni sasa.
Muda unaomatter ni sasa.
Muda wa kufanya mabadiliko ni sasa.
Afro...
Sijaelewa unakusudia nini.
Sijaona tatizo lolote katika uandishi wangu.

Publishers wanachapa vitabu vyangu na vinasomwa kwingi.
Hakuna publisher aliyerejesha mswada wangu.

1686942703605.png

1686942954756.png

1686943025829.png
 
Mzee...
Kuna watu wamekasirishwa na mimi kusahihisha historia ya uhuru.
Historia ilikuwa inaeleza kuwa TANU iliundwa na Julius Nyerere.

Nilipoandika kitabu cha Abdul Sykes na kueleza kuwa Mwalimu alipokelewa na Abdul Sykes na akaikuta TANU kwa Abdul Sykes hawakupendezewa.

Ikawa historia hii imewaudhi.
Hii kwamba Nyerere alipokelewa na Abdul Sykes na akaikuta TANU, hapa umeamua kutumia kalamu yako vibaya kupindisha ukweli sababu ya chuki zako binafsi dhidi ya Nyerere. Unajipa kazi ngumu ambayo huwezi kubadili ukweli.
 
HII NDIO HISTORIA YA FAMILIA YA SYKES.

Historia hii inaanzia kwa MZEE SYKES MBUWANE KLEIST. Huyu ndiye baba yake KLEIST SYKES.

MZEE SYKES MBUWANE KLEIST ni nani?
Sykes Mbuwane ni mamluki wa KIZULU aliyechukuliwa yeye na vijana wenzake wa kizulu kutoka kijiji cha LIKUNYI MSUMBIJI.

Walifikaje Tanganyika?
Kipindi cha UTAWALA wa kikoloni wa kijerumani chini ya HERMANN VON WISSMAN aliwachukuwa kwa meli ya kivita kama askari mamluki mpaka Pangani Tanga, Tanganyika kuja kupigana na ABUSHIRI BIN SALIM AL HARITH NA MTWA MKWAWA WA IRINGA.

KLEIST SYKES ALIZALIWA WAPI?

KLEIST SYKES alizaliwa mwaka 1894, Pangani Tanga kwa baba yake SYKES MBUWANE KLEIST na MAMA yake ni Mnyatulu, baada ya baba yake kufariki Kleist Sykes baadae alikuja Dar es salaam.

MAISHA YA KLEIST SYKES BAADA YA KUJA DAR.

KLEIST SYKES alimuoa Bi MLUGURU BINT MUSSA, na alibahatika kupata watoto watatu wa kiume.

(1) ABDULWAHEED KLEIST SYKES. (1924__1968).

(2) ALLY KLEIST SYKES. (1926__2013).

(3) ABBAS KLEIST SYKES. (1929__2021).

Kama inavyoonekana katika Picha namba (1). Waliosimama kutoka kulia ni Abdulwaheed Kleist Sykes, na Ally Kleist Sykes. Aliyekaa kutoka kulia ni Abbas Kleist Sykes na Baba yao mzazi Mzee Kleist Sykes.

Picha hii ilipigwa 1942, kipindi Abdulwaheed Kleist Sykes alipokuja kumuaga baba yake akitokea LOWER KABETE KENYA mafunzoni kabla ya kwenda BURMA kama Askari wa KAR BURMA INFANTRY. Na picha namba 2, ni MZEE ALLY KLEIST SYKES kipindi cha uhai wake.

Vile vile MZEE KLEIST SYKES ALIKUWA NA WAJUKUU.
Wafuatao ni baadhi ya wajukuu wake:

(1) EBRAHIM (EBBY) ABDULWAHEED KLEIST SYKES. 1952__2015). Kama anavyoonekana katika picha namba 3. Huyu ndiye Baba yake mzazi DULL SYKES msanii wa bongofleva.

(2) MUSSA ABBAS KLEIST SYKES.

(3) KLEIST ABDULWAHEED SYKES. Alifariki 22 novemba 2017.

(4) ABRAHAM ALLY KLEIST SYKES.

ASANTENI:

View attachment 2657367View attachment 2657369View attachment 2657370
Sidhani kama ilikuwa inawezekana Wajerumani kuchukua askari kutoka koloni la Wareno Msumbiji au babu yako mmanyema kutoka koloni la wabelgiji kuja kuwasaidia kupigana Tanganyika , wakati kwenye hayo makoloni napo kulikuwa na vurugu. Kuna changa la macho unatupiga hapa.
 
Back
Top Bottom