Hii ndio sababu magari yanayosafirisha sigara yana ulinzi mkali tofauti na magari yanayosafirisha pombe

NetMaster

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2022
Posts
1,454
Reaction score
4,925
Gari la sigara ni rahisi kuporwa mzigo wote maana mabox ya sigara ni mepesi, mwizi anaweza akabeba box 1 tu akaenda kuuza bei ya hasara milioni 1 na nusu tofauti na kreti ya bia ni nzito halafu inaweza kuwa elf 40 tu

pakiti ya sigara = sigara 20
bunda moja lina pakiti 10 = sigara 200
box moja kuna bunda 50 = sigara 10,000

mfano bei ya wastani ya sigara moja ni shilingi 200, hivyo thamani ya box moja ni shilingi milioni 2

pick up ndogo tu ikibeba box 50 ni sawa na malori matatu makubwa yanayobeba kreti za bia

scania inaweza kubeba box hadi elf 1, mzigo hapo unasoma bilioni 2.
 
Nahis Aina ya watumiaji was hicho kilevi ndo sababu kuu
 
Sikuwahi kujua hzi hesabu
 
Umeongea ukweli mtupu mkuu, na Sigara zinauzika sio kawaida
 
Pombe watu hawaibi na gari likipata ajali walevi wanaweka kituo hapohapo na kufungua pub bila wahudumu bali ni self service
 
Haijawahi kutokea gari la sigara kupinduka kisha watu wakagawana puff?
 
Ila bia inaingiza mapato makubwa serikalini kuliko sigara. Per company.


Bia 10 ni 15,000tsh.

Ni ngumu kuvuta sigara za tsh15000
Kwa siku moja.
Hapo Kodi ya serikali ni shilingi ngapi maana umetoa mapato ghafi tu ambayo mwenye kampuni anaingiza.....
 
Mara nyingi zinasafirishwa kwa ndege toka production area na kusambazwa kwenye miji midogo. Ili kupunguza risk ya upotevu au ajali
Kumbe sigara ni asset namna hii

Najiuliza kama serikali inahamasisha watu wasivute kwa kulinda afya ya mapafu, inakuwaje inawekeza kwenye utengenezaji sigara?


Bangi inajulikana kabisaa ni tiba lakini serikali kupitia vyombo vyake wanaisagia kunguni mwanzo mwisho. Polisi na wanajeshi kibao wanakula ndumu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…