Mcheza Viduku
JF-Expert Member
- Jun 24, 2020
- 1,111
- 2,754
Mzee wangu alikuwa dereva kampuni ya sigara tawi la Tabora alikuwa anaendesha gari aina ya Canter tani 3 na robo na walikuwa wanasafiri watatu.....yeye dereva, keshia na mlinzi mwenye bunduki, kabla haujaanzishwa huu mfumo wa kutokutembea na hela cash......
Anatusimulia kuwa kuna siku walikuwa na zaidi ya Tsh 600 baada ya mauzo wanatoka Urambo kurudi Tabora mjini mlinzi akawageuka anawaambia wachague moja.....wagawane zile hela halafu watoroke au awatie shaba azichukue peke yake.
Majibizano yalikuwa marefu na vitisho vingi kutoka kwa yule mlinzi (mi pia namfahamu vizuri alikuwa anakula sana ganja) mkwara wa kwanza chuma kikalia jiwe la moto likapasua anga kwa sauti zito la kibabe.
Sitanii hapa, risasi ya pili inaondoka na mtu....likawa onyo lake
Kadri walivyokuwa wanaendelea kumsihi pale ndio wadudu kichwani kwake waliendelea kumtia wazimu, sekunde chache basdae dude likaunguruma tena risasi ikafumua tairi la mbele, kumbe wakati anafanya yote hayo huku akijiaminisha kuwa wako porini mbali na msaada ile milio miwili ya risasi ikawashitua wanakijiji cha jirani na eneo lile wakaji-organize na kuanza kusogea kikomando.
Huku porini mlinzi akaachia chuma kingine cha tatu ukawa ni mwisho wakamvaa kwa pamoja kipigo kikaanza na muda huo wanakijiji wakafika, wakamkamata pelekwa polisi na mambo memgineyo yakafuatia.....jamaa alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani.
Baada ya miaka miwili yule keshia akajiongeza akaiba Tsh milioni 120......Muhaya yule hakuwa mjanja kama wenzake akaanza matanuzi pale pale mjini, miezi miwili baadae wakamdaka akafungwa miaka mitano.
Mzee wangu alistaafu mwaka 2003, sio kweli kwamba wana maisha mazuri kiviiiiiiiiile.......ni baadhi yao tu, mzee wangu alifanikiwa kununua kiwanja Mwanza kabla ya kustaafu na kujenga nyumba kubwa ya upangishaji na pia kwa kuwa tupo barabara kuu ya kwenda Shinyanga mbele amejenga frame 12 za maduka na nyuma mtaa wa pili kuna frame 6 za maduka.
Mwisho
Anatusimulia kuwa kuna siku walikuwa na zaidi ya Tsh 600 baada ya mauzo wanatoka Urambo kurudi Tabora mjini mlinzi akawageuka anawaambia wachague moja.....wagawane zile hela halafu watoroke au awatie shaba azichukue peke yake.
Majibizano yalikuwa marefu na vitisho vingi kutoka kwa yule mlinzi (mi pia namfahamu vizuri alikuwa anakula sana ganja) mkwara wa kwanza chuma kikalia jiwe la moto likapasua anga kwa sauti zito la kibabe.
Sitanii hapa, risasi ya pili inaondoka na mtu....likawa onyo lake
Kadri walivyokuwa wanaendelea kumsihi pale ndio wadudu kichwani kwake waliendelea kumtia wazimu, sekunde chache basdae dude likaunguruma tena risasi ikafumua tairi la mbele, kumbe wakati anafanya yote hayo huku akijiaminisha kuwa wako porini mbali na msaada ile milio miwili ya risasi ikawashitua wanakijiji cha jirani na eneo lile wakaji-organize na kuanza kusogea kikomando.
Huku porini mlinzi akaachia chuma kingine cha tatu ukawa ni mwisho wakamvaa kwa pamoja kipigo kikaanza na muda huo wanakijiji wakafika, wakamkamata pelekwa polisi na mambo memgineyo yakafuatia.....jamaa alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani.
Baada ya miaka miwili yule keshia akajiongeza akaiba Tsh milioni 120......Muhaya yule hakuwa mjanja kama wenzake akaanza matanuzi pale pale mjini, miezi miwili baadae wakamdaka akafungwa miaka mitano.
Mzee wangu alistaafu mwaka 2003, sio kweli kwamba wana maisha mazuri kiviiiiiiiiile.......ni baadhi yao tu, mzee wangu alifanikiwa kununua kiwanja Mwanza kabla ya kustaafu na kujenga nyumba kubwa ya upangishaji na pia kwa kuwa tupo barabara kuu ya kwenda Shinyanga mbele amejenga frame 12 za maduka na nyuma mtaa wa pili kuna frame 6 za maduka.
Mwisho