Hii ndiyo sababu ya mimi kutokuwa na huruma na Ndugu

Hii ndiyo sababu ya mimi kutokuwa na huruma na Ndugu

We Kuna kitu unakuTafuta sio bure, yaan unamuhukumu mama yako kisa umepata heka 50 na kiajira , huo upumbv ulisomea kbsa maana sio kwa kiwango Hiko,

Mama ni mama acha ujinga mpe pesa hata za kuzidi stupid wew [emoji57][emoji57][emoji57]
 
Nakumbuka kusoma story kama hii siku za Nyuma wakati UN inafanya kazi Arusha pale AICC ambapo wafanyakazi walipata hela nyingi.
Kama ni tofauti, saidia mama yako halafu, nakushauri kwa dhati kabisa, wasaidie na hao ndugu zako Kama unauwezo wape mitaji midogo midogo kwa masharti kuwa umewakopesha hata kama rohoni unajua umewapa.
Kuwakopesha ni ili waiangalie vizuri. Hii itasaidia kutoa funzo kwenye familia na hizo dharau hazitatokea tena kwa mwingine Ndugu zako ni ndugu zako tu,
Watu hesema; mtoto akijisaidia kwenye mkono wako, hauukati badala yake unauosha na maisha yanaendelea
 
Mkuu,Kuambiwa ukweli sio masimango.Mama alikuwa na uchungu na ilikuwana lazima akwambia maneno yatakayokurudisha kwenye reli hata kama yanaumiza.Unafikiri alifurahia kwamba huna kazi na umesoma.Huyu mleta mada anaoneka ni mtu mwenye roho mbaya ila sasa nafsi inamsuta inabidi ajipe moyo.

Katika maisha yalipita si Ndwele watu wana ganga yajayo.Kama unao uwezo wa kuwapa msaada wape ila usifikiri kwamba watakulipa fadhila na wala usifikri kwamba wangukutendea vyema ungewajali.

Pia hata hao watu baki waliokusaidia naona hata huna time now.So Face IT an BE GOOD.

DO GOOD FOR YOUR OWN GOOD
Kama ni Mimi mama ningepiga chini
 
Pole kwa magumu uliyoyapitia,
Ila katika Dunia hii,"no body owes you anything"
Sio lazima watu wakupe msaada,wakikupa,Sawa,ukinyimwa,songa mbele.
Kitu nilichojifunza,bahati mbaya kwa kuchelewa ni kwamba kwenye haya maisha,mtu wa pekee atakaekuja kukuokoa,ni wewe mwenyewe tu,
Ndugu ni binadamu tu,huwa tunakeleka wanaposhindwa kutusaidia kwa sababu tunaweka matumaini makubwa sana kwao kwa vile tumezaliwa tumbo moja,ni baba,ni mama,tunasahau hizo zote ni lebel tu,they are just Human beings.
Nimekuelewa vizuri Sana mkuu
 
Baba yangu alifariki wakati nikiwa Mtoto mchanga hivyo nililelewa na Mama tu naye hakuwa na uwezo hivyo nilisomeshwa na wasamaria wema. Mtu pekee Aliyekuwa na uwezo wa kiuchumi ni dada aliyeolewa na yeye hakutaka mazoea kabisa.

Kwa jinsi maisha yalivyokuwa magumu, nilipofika Chuo nikawa natumia boom(mkopo wa elimu ya juu) kumtunza mama. Imagine mtu nilikuwa nalipwa laki tano na kumi na kupaswa niitumie kwa miezi miwili lakini nilikuwa najibana kwa kadiri iwezekanavyo nitumie mama Kati ya elfu 60 na 100,000.

Nilipomaliza chuo nikarudi nyumbani, hakuna ajira na sina mtaji wa biashara au kilimo, nikawa nashinda ndani kwa mawazo au siku nikibahatisha kibarua Cha zege au kumsafishia mtu shamba naifanya kwa nidhamu, napata hela ya bundle la muendelezo wa kusaka ajira.

Ajabu ya karne; Mama mzazi alianza kunisimangia chakula na kunilaumu kuwa nilitumia vibaya mkopo wa Chuo nilikuwa nawapa makahaba wa mjini na kwamba ningekuwa na akili ningetambua kuwa mimi ni Mtoto yatima na ningetunza akiba ili nimalizapo chuo nifungue kioski!

Mungu siyo Shetani, baada ya miaka miwili ya ukosoefu wa ajira, nikapata kazi nzuri Sana kwenye moja ya taasisi za Kimataifa, nimeanza kusahau yale maisha magumu. Nimewekeza katika ardhi, nimenunua ekari 50, nimenunua viwanja viwili Arusha mjini na kimoja Kibaha. Kwa Sasa nawaza kununua power tiller(KUBOTA) ili inisaidie kwenye kilimo ambacho nitakianza mwakani rasmi.

Sasa nikikumbuka vituko vya mama, na Ndugu kuwatumia hela napata taswira ya yale maneno yale masimango. Naghairisha.

Yule dada Aliyekuwa na uwezo wa kunisomesha akagoma, Benki imewafilisi, wakaachana na mumewe. Amebaki kunipigia simu eti "nilikuwa nakusalimu" wakati kipindi nipo down hakuwahi kunipigia na nikimpigia hapokei simu, nikimpigia kwa number ngeni akishafahamu Ni mimi, anakata.

Maisha ya hapa Duniani ni fumbo
Anyway ndiyo changamoto na mitihani ya maisha , ili nafsi yako iwe huru wasaidie unavyo weza tu ila kaa nao mbali, mengine mwachie MUNGU!!!
 
Sidhani kama kuna mama anaweza msimangia mwanae chakula, toto hata kama tukutu namna gani atamfichia msos wakat mzee analeta nongwa
 
Nimeelewa kwanini wenzetu wazungu hawaendekezi huu undugu undugu ,kila mtu apambane na life lake , undugu undugu ni unafiki tu. Hasa hizi ngozi nyeusi zilizolaaniwa
 
Kama ungekuwa unaamini ktk Mungu ningekushauri usamehe na anza kuwasaidia. Mungu ananjia nyingi. Huenda kama usingepitishwa kwenye moto na ndg zako, ungebweteka na usingesoma kwa bidii.
 
Baba yangu alifariki wakati nikiwa Mtoto mchanga hivyo nililelewa na Mama tu naye hakuwa na uwezo hivyo nilisomeshwa na wasamaria wema. Mtu pekee Aliyekuwa na uwezo wa kiuchumi ni dada aliyeolewa na yeye hakutaka mazoea kabisa.

Kwa jinsi maisha yalivyokuwa magumu, nilipofika Chuo nikawa natumia boom(mkopo wa elimu ya juu) kumtunza mama. Imagine mtu nilikuwa nalipwa laki tano na kumi na kupaswa niitumie kwa miezi miwili lakini nilikuwa najibana kwa kadiri iwezekanavyo nitumie mama Kati ya elfu 60 na 100,000.

Nilipomaliza chuo nikarudi nyumbani, hakuna ajira na sina mtaji wa biashara au kilimo, nikawa nashinda ndani kwa mawazo au siku nikibahatisha kibarua Cha zege au kumsafishia mtu shamba naifanya kwa nidhamu, napata hela ya bundle la muendelezo wa kusaka ajira.

Ajabu ya karne; Mama mzazi alianza kunisimangia chakula na kunilaumu kuwa nilitumia vibaya mkopo wa Chuo nilikuwa nawapa makahaba wa mjini na kwamba ningekuwa na akili ningetambua kuwa mimi ni Mtoto yatima na ningetunza akiba ili nimalizapo chuo nifungue kioski!

Mungu siyo Shetani, baada ya miaka miwili ya ukosoefu wa ajira, nikapata kazi nzuri Sana kwenye moja ya taasisi za Kimataifa, nimeanza kusahau yale maisha magumu. Nimewekeza katika ardhi, nimenunua ekari 50, nimenunua viwanja viwili Arusha mjini na kimoja Kibaha. Kwa Sasa nawaza kununua power tiller(KUBOTA) ili inisaidie kwenye kilimo ambacho nitakianza mwakani rasmi.

Sasa nikikumbuka vituko vya mama, na Ndugu kuwatumia hela napata taswira ya yale maneno yale masimango. Naghairisha.

Yule dada Aliyekuwa na uwezo wa kunisomesha akagoma, Benki imewafilisi, wakaachana na mumewe. Amebaki kunipigia simu eti "nilikuwa nakusalimu" wakati kipindi nipo down hakuwahi kunipigia na nikimpigia hapokei simu, nikimpigia kwa number ngeni akishafahamu Ni mimi, anakata.

Maisha ya hapa Duniani ni fumbo
Yametupata sana hayo Wenzio. Hao wengine wooooote, waache hapo pembeni. Usiwasemeshe. Wakiwa na shida, wasaidie KWA KIASI. Mama usimwache kamwe na usimkumbushe matendo yake kwako. Huwezi jua walimwengu walimwambia nini kuhusu wewe ulipokuwa chuoni. Nunua zawadi nzuri kabisa, mpelekee Mama, mtandike na bima moja ya afya yenye scheme matata kabisa, hakisha anavaa, anakula vizuri. Utabarikiwa sana na Utakuja kunishukuru mbele za Mungu na mataifa.
 
Wewe utakuwa na tofauti gani na wao?

Au tu wao walianza wewe unamaliza.

Wasaidie pale unapoona unahitajika msaada wa kibinadamu, siyo kwa sababu wamekutendea mema, la hasha. Kwa sababu ya ubinadamu.

Saidia wengine hata ambao siyo ndugu zako, ambao wapo kama wewe wa enzi zile....


Tizama ridhiki ilipitishwa kwao wakaitumia kama fimbo, imehamishiwa kwako uwe baraka kwa watu wote, Mungu asijute kukupa.
 
Nikisoma nyuzi kama hizi kisha nikumbuke marehemu mama yangu alivyoteseka kutulea, huwa natamani afufuke hata siku moja nimtunze kisha aage dunia tena, maana aliaga dunia kipindi naanza kupata visenti, sikupata fursa ya kumlipa chochote.
Aisei yule ningemsamehe hata kama angenisimanga kivipi, jameni mna bahati nyie ambao mama zenu bado wako hai.
 
Mkuu upo sahihi kwa uamuzi wako
Katika maisha ndugu yako wa kwanza ni mama yako katika hali yoyote ile kama alikukosea ni lazima umsamehe
Hao wengine watajua wenyewe..
 
Mama kama binadamu mwingine anaweza kufanya makosa .

Sio mama wote wanapenda watoto wao,

Tusikariri,

Wengine walifanya kila jitihada kutoa hiyo mimba Mungu akakataa.

Sasa mama wa hivyo unazani atakupenda?

Wengine wamejikuta wamezaa tu wala hawakupanga kumzaa huyo Mtoto.

Mtoto anakuwa na Roho ya kukataliwa
Umenena vyema mkuu, Hawa wazazi hubadilika kabisa
 
KIJANA POLE KWA YALIYOKUKUTA. LEO NIMEAMINI KUWA SI KILA MAMA WA KUKUZAA ANAWEZA KUWA MWEMA AU KUKUPENDA KWA DHATI. MAMA WA KUKUZAA ANAWEZA KUKUPENDA KINAFIKI PIA KAMA RAFIKI AU MTU BAKI TU!. NA HAO AKINA MAMA WA AINA HIYO WAPO.

HILO MOSI, PILI KUSAMEHE AU KUTOSAMEHE NI HIYARI YAKO NA ASITOKEE YEYOTE WA KUKULAZIMISHA USAMEHE, HAKULA LAANA YOYOTE KWA WEWE KUTOSAMEHE, ILA BINAFSI KWA UTASHI WANGU NAKUOMBA UMSAMEHE MAMA ILA USIWE NAYE KARIBU TENA KWA KUMUAMBIA MICHONGO YAKO WALA KUISHI NAYE. HUYO DADA YAKO ENDELEA NAYE KIBABE HIVYO HIVYO.

NB: NI HIYARI YAKO KUSAMEHE, SI LAZIMA. WASITOKEE WACHUNGAJI KOKO KUKUTISHA. SI DHAMBI USIPOSAMEHE PIA SI DHAMBI UKISAMEHE. USIKILIZE MOYO WAKO/NAFSI YAKO.
Well said....samehe Kaa nae mbali
 
Back
Top Bottom