Hii ndiyo sababu ya mimi kutokuwa na huruma na Ndugu

Hii ndiyo sababu ya mimi kutokuwa na huruma na Ndugu

Huu uzi ni feki kabisa...

dogo juzi tu kahitimu chuo 2021

kaanza kutuma maombi ya chuo mpaka 2022 hajapata Job..

hapa kaja na uzi kafukuzwa kazi katengwa na kila mtu mpaka chawa wamemkimbia😅


Halafu anatupanga kirahisi tu eti kanunua shamba heka 50, mara anunue trekta which is not less than 30mil dadek..

dogo hebu mrudishe mkeo shule mjenge familia mkiwa wote na akili mingi

Nimeongelea power tiller wewe unaingelea trekta. Ama kweli, majungu yapo hadi mitandaoni
 
Tatizo waswahili wanajua kusanehewa ni kuanza kupewa hela.
Mimi kuna ndugu zangu wala sina shida nao,tukikutana story tunapiga..ila mazoea sitaki na siwezi wapa hela yangu abadani.
😅😅😅😅
 
Baba yangu alifariki wakati nikiwa Mtoto mchanga hivyo nililelewa na Mama tu naye hakuwa na uwezo Hivyo nilisomeshwa na wasamaria wema. Mtu pekee Aliyekuwa na uwezo wa kiuchumi Ni dada aliyeolewa na yeye hakutaka mazoea kabisa.

Kwa jinsi maisha yalivyokuwa magumu, nilipofika Chuo nikawa natumia boom(mkopo wa elimu ya juu) kumtunza mama. Imagine mtu nilikuwa nalipwa laki tano na kumi na kupaswa niitumie kwa miezi miwili lakini nilikuwa najibana kwa kadiri iwezekanavyo nitumie mama Kati ya elfu 60 na 100,000.

Nilipomaliza chuo nikarudi nyumbani, hakuna ajira na Sina mtaji wa biashara au kilimo, nikawa nashinda ndani kwa mawazo au siku nikibahatisha kibarua Cha zege au kumsafishia mtu shamba naifanya kwa nidhamu, napata hela ya bundle la muendelezo wa kusaka ajira.

Ajabu ya karne; Mama mzazi alianza kunisimangia chakula na kunilaumu kuwa nilitumia vibaya mkopo wa Chuo nilikuwa nawapa makahaba wa mjini na kwamba ningekuwa na akili ningetambua kuwa mimi ni Mtoto yatima na ningetunza akiba ili nimalizapo chuo nifungue kioski!

Mungu siyo Shetani, baada ya miaka miwili ya ukosoefu wa ajira, nikapata kazi nzuri Sana kwenye moja ya taasisi za Kimataifa, nimeanza kusahau yale maisha magumu. Nimewekeza katika ardhi, nimenunua ekari 50, nimenunua viwanja viwili Arusha mjini na kimoja Kibaha. Kwa Sasa nawaza kununua power tiller(KUBOTA) ili inisaidie kwenye kilimo ambacho nitakianza mwakani rasmi.

Sasa nikikumbuka vituko vya mama, na Ndugu kuwatumia hela napata taswira ya yale maneno yale masimango. Naghairisha.

Yule dada Aliyekuwa na uwezo wa kunisomesha akagoma, Benki imewafilisi, wakaachana na mumewe. Amebaki kunipigia simu eti "nilikuwa nakusalimu" wakati kipindi nipo down hakuwahi kunipigia na nikimpigia hapokei simu, nikimpigia kwa number ngeni akishafahamu Ni mimi, anakata.

Maisha ya hapa Duniani ni fumbo
Ushauri wangu mimi hao ndugu zako waache kama walivyo ila Mama yako Mzazi msaidie kwa kila hali hata kama alikulaumu kivipi? Wewe tekeleza wajibu wako kumuangalia Mama yako mzazi kwani umetoka nae mbali sana. Ukikosa kumsaidia mama yako mzazi ujuwe utaharibikia kila kitu chako ulicho kipanga huo ndio ushauri wangu ukiweza ufuate usipo weza uachilie mbali upite zake.
 
Mmmh ndugu Sina hamu Mimi. Nilifirisiwa kwa siku 1. Sikuyaamini macho yangu. Nimesamehe Ila ukaribu noo.
 
Ushauri wangu mimi hao ndugu zako waache kama walivyo ila Mama yako Mzazi msaidie kwa kila hali hata kama alikulaumu kivipi? Wewe tekeleza wajibu wako kumuangalia Mama yako mzazi kwani umetoka nae mbali sana. Ukikosa kumsaidia mama yako mzazi ujuwe utaharibikia kila kitu chako ulicho kipanga huo ndio ushauri wangu ukiweza ufuate usipo weza uachilie mbali upite zake.
Ahsante mkuu
 
Oya skia hapo ushatoboa maisha njoo sasa tule bata maneno ya mama yatimie utapanye pesa mpka zikukome
 
Baba yangu alifariki wakati nikiwa Mtoto mchanga hivyo nililelewa na Mama tu naye hakuwa na uwezo hivyo nilisomeshwa na wasamaria wema. Mtu pekee Aliyekuwa na uwezo wa kiuchumi ni dada aliyeolewa na yeye hakutaka mazoea kabisa.

Kwa jinsi maisha yalivyokuwa magumu, nilipofika Chuo nikawa natumia boom(mkopo wa elimu ya juu) kumtunza mama. Imagine mtu nilikuwa nalipwa laki tano na kumi na kupaswa niitumie kwa miezi miwili lakini nilikuwa najibana kwa kadiri iwezekanavyo nitumie mama Kati ya elfu 60 na 100,000.

Nilipomaliza chuo nikarudi nyumbani, hakuna ajira na sina mtaji wa biashara au kilimo, nikawa nashinda ndani kwa mawazo au siku nikibahatisha kibarua Cha zege au kumsafishia mtu shamba naifanya kwa nidhamu, napata hela ya bundle la muendelezo wa kusaka ajira.

Ajabu ya karne; Mama mzazi alianza kunisimangia chakula na kunilaumu kuwa nilitumia vibaya mkopo wa Chuo nilikuwa nawapa makahaba wa mjini na kwamba ningekuwa na akili ningetambua kuwa mimi ni Mtoto yatima na ningetunza akiba ili nimalizapo chuo nifungue kioski!

Mungu siyo Shetani, baada ya miaka miwili ya ukosoefu wa ajira, nikapata kazi nzuri Sana kwenye moja ya taasisi za Kimataifa, nimeanza kusahau yale maisha magumu. Nimewekeza katika ardhi, nimenunua ekari 50, nimenunua viwanja viwili Arusha mjini na kimoja Kibaha. Kwa Sasa nawaza kununua power tiller(KUBOTA) ili inisaidie kwenye kilimo ambacho nitakianza mwakani rasmi.

Sasa nikikumbuka vituko vya mama, na Ndugu kuwatumia hela napata taswira ya yale maneno yale masimango. Naghairisha.

Yule dada Aliyekuwa na uwezo wa kunisomesha akagoma, Benki imewafilisi, wakaachana na mumewe. Amebaki kunipigia simu eti "nilikuwa nakusalimu" wakati kipindi nipo down hakuwahi kunipigia na nikimpigia hapokei simu, nikimpigia kwa number ngeni akishafahamu Ni mimi, anakata.

Maisha ya hapa Duniani ni fumbo
Kuna kitu hakipo Sawa kwenye hii Hadithi yako maan Hadithi ya kuanzia utotoni haiwezi kuisha Kwa mistari michache ulioiandika,
Otherwise kuna kitu unatuficha.
Pili, Kwa nin unaamini kwamba Dada yako alikuwa na uwezo wa kukusomesha?
Imani uliyokuwa nayo kwamba Dada yako ana uwezo ndo Imani hyo hyo ambayo Mama yako aliamini ulikuwa na Pesa isipokuwa uliitumia kuhonga.
Kama hutaki kuwasaidia ndg Kwa kigezo cha kwamba umetoboa basi wewe kausha,
Maana Kwa maelezo yako hujalazimishwa kuwasaidia Ila unajihisi Tu kwamba Kwa kuwa sasa hv wanakupigia cm basi wanatak msaada,
Hao watu wameishi Maisha Yao Bila hata msaada wako ambao unahisi Una umhimu,
Ikifikia hatua ukaona kwamba Mama yako hafai Basi subili Tu kufundishwa na Ulimwengu,
Yaani mtu (Mama) ambae unakiri kabisa kwamba alihangaika na wew tangu ulipoachwa ukiwa mchanga,
Leo hii Kwa sababu Tu za kununua heka 50 cjui na PT ndo unaona hakufai?
Are you serious?
Mama yako japo simjui naamini ataendelea kuishi hata Bila huo msaada wako,
 
Pole kwa magumu uliyoyapitia,
Ila katika Dunia hii,"no body owes you anything"
Sio lazima watu wakupe msaada,wakikupa,Sawa,ukinyimwa,songa mbele.
Kitu nilichojifunza,bahati mbaya kwa kuchelewa ni kwamba kwenye haya maisha,mtu wa pekee atakaekuja kukuokoa,ni wewe mwenyewe tu,
Ndugu ni binadamu tu,huwa tunakeleka wanaposhindwa kutusaidia kwa sababu tunaweka matumaini makubwa sana kwao kwa vile tumezaliwa tumbo moja,ni baba,ni mama,tunasahau hizo zote ni lebel tu,they are just Human beings.
 
Mama ni mama siku zote, mtunze mama achana na hao wengine
 
Back
Top Bottom