Live circuit
Senior Member
- Mar 11, 2023
- 124
- 365
🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣Nzuri umeicopy kutoka wapi?
Kama ni Mimi mama ningepiga chiniMkuu,Kuambiwa ukweli sio masimango.Mama alikuwa na uchungu na ilikuwana lazima akwambia maneno yatakayokurudisha kwenye reli hata kama yanaumiza.Unafikiri alifurahia kwamba huna kazi na umesoma.Huyu mleta mada anaoneka ni mtu mwenye roho mbaya ila sasa nafsi inamsuta inabidi ajipe moyo.
Katika maisha yalipita si Ndwele watu wana ganga yajayo.Kama unao uwezo wa kuwapa msaada wape ila usifikiri kwamba watakulipa fadhila na wala usifikri kwamba wangukutendea vyema ungewajali.
Pia hata hao watu baki waliokusaidia naona hata huna time now.So Face IT an BE GOOD.
DO GOOD FOR YOUR OWN GOOD
Usiweke broooHebu weka link hapa tukomeshe hii tabia.
Nimekuelewa vizuri Sana mkuuPole kwa magumu uliyoyapitia,
Ila katika Dunia hii,"no body owes you anything"
Sio lazima watu wakupe msaada,wakikupa,Sawa,ukinyimwa,songa mbele.
Kitu nilichojifunza,bahati mbaya kwa kuchelewa ni kwamba kwenye haya maisha,mtu wa pekee atakaekuja kukuokoa,ni wewe mwenyewe tu,
Ndugu ni binadamu tu,huwa tunakeleka wanaposhindwa kutusaidia kwa sababu tunaweka matumaini makubwa sana kwao kwa vile tumezaliwa tumbo moja,ni baba,ni mama,tunasahau hizo zote ni lebel tu,they are just Human beings.
Anyway ndiyo changamoto na mitihani ya maisha , ili nafsi yako iwe huru wasaidie unavyo weza tu ila kaa nao mbali, mengine mwachie MUNGU!!!Baba yangu alifariki wakati nikiwa Mtoto mchanga hivyo nililelewa na Mama tu naye hakuwa na uwezo hivyo nilisomeshwa na wasamaria wema. Mtu pekee Aliyekuwa na uwezo wa kiuchumi ni dada aliyeolewa na yeye hakutaka mazoea kabisa.
Kwa jinsi maisha yalivyokuwa magumu, nilipofika Chuo nikawa natumia boom(mkopo wa elimu ya juu) kumtunza mama. Imagine mtu nilikuwa nalipwa laki tano na kumi na kupaswa niitumie kwa miezi miwili lakini nilikuwa najibana kwa kadiri iwezekanavyo nitumie mama Kati ya elfu 60 na 100,000.
Nilipomaliza chuo nikarudi nyumbani, hakuna ajira na sina mtaji wa biashara au kilimo, nikawa nashinda ndani kwa mawazo au siku nikibahatisha kibarua Cha zege au kumsafishia mtu shamba naifanya kwa nidhamu, napata hela ya bundle la muendelezo wa kusaka ajira.
Ajabu ya karne; Mama mzazi alianza kunisimangia chakula na kunilaumu kuwa nilitumia vibaya mkopo wa Chuo nilikuwa nawapa makahaba wa mjini na kwamba ningekuwa na akili ningetambua kuwa mimi ni Mtoto yatima na ningetunza akiba ili nimalizapo chuo nifungue kioski!
Mungu siyo Shetani, baada ya miaka miwili ya ukosoefu wa ajira, nikapata kazi nzuri Sana kwenye moja ya taasisi za Kimataifa, nimeanza kusahau yale maisha magumu. Nimewekeza katika ardhi, nimenunua ekari 50, nimenunua viwanja viwili Arusha mjini na kimoja Kibaha. Kwa Sasa nawaza kununua power tiller(KUBOTA) ili inisaidie kwenye kilimo ambacho nitakianza mwakani rasmi.
Sasa nikikumbuka vituko vya mama, na Ndugu kuwatumia hela napata taswira ya yale maneno yale masimango. Naghairisha.
Yule dada Aliyekuwa na uwezo wa kunisomesha akagoma, Benki imewafilisi, wakaachana na mumewe. Amebaki kunipigia simu eti "nilikuwa nakusalimu" wakati kipindi nipo down hakuwahi kunipigia na nikimpigia hapokei simu, nikimpigia kwa number ngeni akishafahamu Ni mimi, anakata.
Maisha ya hapa Duniani ni fumbo
HahahahahhahahahBasi hii ni chai ya viungo maana Restless Hustler nilimkuta jukwaa la Ajira anaomba kuelekezwa kujaza Ajira portal Sasa najiuliza huyu hii Ajira hana anatafuta ajira na hizi hekari 50 ameziokota wapi au anaota asubuhi asije kua Bill Lugano kaja kivingine
Yametupata sana hayo Wenzio. Hao wengine wooooote, waache hapo pembeni. Usiwasemeshe. Wakiwa na shida, wasaidie KWA KIASI. Mama usimwache kamwe na usimkumbushe matendo yake kwako. Huwezi jua walimwengu walimwambia nini kuhusu wewe ulipokuwa chuoni. Nunua zawadi nzuri kabisa, mpelekee Mama, mtandike na bima moja ya afya yenye scheme matata kabisa, hakisha anavaa, anakula vizuri. Utabarikiwa sana na Utakuja kunishukuru mbele za Mungu na mataifa.Baba yangu alifariki wakati nikiwa Mtoto mchanga hivyo nililelewa na Mama tu naye hakuwa na uwezo hivyo nilisomeshwa na wasamaria wema. Mtu pekee Aliyekuwa na uwezo wa kiuchumi ni dada aliyeolewa na yeye hakutaka mazoea kabisa.
Kwa jinsi maisha yalivyokuwa magumu, nilipofika Chuo nikawa natumia boom(mkopo wa elimu ya juu) kumtunza mama. Imagine mtu nilikuwa nalipwa laki tano na kumi na kupaswa niitumie kwa miezi miwili lakini nilikuwa najibana kwa kadiri iwezekanavyo nitumie mama Kati ya elfu 60 na 100,000.
Nilipomaliza chuo nikarudi nyumbani, hakuna ajira na sina mtaji wa biashara au kilimo, nikawa nashinda ndani kwa mawazo au siku nikibahatisha kibarua Cha zege au kumsafishia mtu shamba naifanya kwa nidhamu, napata hela ya bundle la muendelezo wa kusaka ajira.
Ajabu ya karne; Mama mzazi alianza kunisimangia chakula na kunilaumu kuwa nilitumia vibaya mkopo wa Chuo nilikuwa nawapa makahaba wa mjini na kwamba ningekuwa na akili ningetambua kuwa mimi ni Mtoto yatima na ningetunza akiba ili nimalizapo chuo nifungue kioski!
Mungu siyo Shetani, baada ya miaka miwili ya ukosoefu wa ajira, nikapata kazi nzuri Sana kwenye moja ya taasisi za Kimataifa, nimeanza kusahau yale maisha magumu. Nimewekeza katika ardhi, nimenunua ekari 50, nimenunua viwanja viwili Arusha mjini na kimoja Kibaha. Kwa Sasa nawaza kununua power tiller(KUBOTA) ili inisaidie kwenye kilimo ambacho nitakianza mwakani rasmi.
Sasa nikikumbuka vituko vya mama, na Ndugu kuwatumia hela napata taswira ya yale maneno yale masimango. Naghairisha.
Yule dada Aliyekuwa na uwezo wa kunisomesha akagoma, Benki imewafilisi, wakaachana na mumewe. Amebaki kunipigia simu eti "nilikuwa nakusalimu" wakati kipindi nipo down hakuwahi kunipigia na nikimpigia hapokei simu, nikimpigia kwa number ngeni akishafahamu Ni mimi, anakata.
Maisha ya hapa Duniani ni fumbo
Umenena vyema mkuu, Hawa wazazi hubadilika kabisaMama kama binadamu mwingine anaweza kufanya makosa .
Sio mama wote wanapenda watoto wao,
Tusikariri,
Wengine walifanya kila jitihada kutoa hiyo mimba Mungu akakataa.
Sasa mama wa hivyo unazani atakupenda?
Wengine wamejikuta wamezaa tu wala hawakupanga kumzaa huyo Mtoto.
Mtoto anakuwa na Roho ya kukataliwa
Watu hili hawalijui....wanatanguliza Hisia tu!Hata mama anaweza tumwA na nduguzo kukuharibia life
Well said....samehe Kaa nae mbaliKIJANA POLE KWA YALIYOKUKUTA. LEO NIMEAMINI KUWA SI KILA MAMA WA KUKUZAA ANAWEZA KUWA MWEMA AU KUKUPENDA KWA DHATI. MAMA WA KUKUZAA ANAWEZA KUKUPENDA KINAFIKI PIA KAMA RAFIKI AU MTU BAKI TU!. NA HAO AKINA MAMA WA AINA HIYO WAPO.
HILO MOSI, PILI KUSAMEHE AU KUTOSAMEHE NI HIYARI YAKO NA ASITOKEE YEYOTE WA KUKULAZIMISHA USAMEHE, HAKULA LAANA YOYOTE KWA WEWE KUTOSAMEHE, ILA BINAFSI KWA UTASHI WANGU NAKUOMBA UMSAMEHE MAMA ILA USIWE NAYE KARIBU TENA KWA KUMUAMBIA MICHONGO YAKO WALA KUISHI NAYE. HUYO DADA YAKO ENDELEA NAYE KIBABE HIVYO HIVYO.
NB: NI HIYARI YAKO KUSAMEHE, SI LAZIMA. WASITOKEE WACHUNGAJI KOKO KUKUTISHA. SI DHAMBI USIPOSAMEHE PIA SI DHAMBI UKISAMEHE. USIKILIZE MOYO WAKO/NAFSI YAKO.