Kwa hii comment wewe ni muislam wa kuzaliwa na hujawahi kuwa mkristo.Unafanya dhambi kubwa na kumkosea Muumba wako unapompa Yesu binadamu kama Wewe hadhi ya Mungu.
Yani unamuabudu binadamu mwenzio
Yesu alikuwa Nabii kama manabii wengine, na hakuwahi kusema yeye ni Mungu
Kina Paulo na Waroma ndio waliochakachua na kuanza kumuabudu Kama Mungu.
Shirki mbaya sana.
Uislam umeanza na Adam, kwahyo Kabla yake hakukuwa na wanadamuKabla ya ukirsto na uislamu watu walizaliwa wakiwa dini gani? Mahusiano yetu na Mungu ndio jambo la msingi sana kuliko dini zetu, tunashika, tunatii na kupenda sana dini zetu na madhebu yetu kuliko kumpenda na kumtii Mwenyezi Mungu.
Nabii Issa ni njia mojawapo ya kweli na uzima maana alihubiri uislam, hata Muhammad pia ni njia ya kweli na uzima.Hapana, jibu lako linahitaji uzi mwingine zaidi ili uelimike kuhusu siri ya ukuu wa jina la Yesu kimamlaka.
Mungu mwenyewe kapendezwa tu kumpatia mamlaka hayo Yesu.
Sawa na Bakhressa alivyokaimisha majukumu yake ya kibiashara kwa mwanaye wa kiume kuyasimamia na kuyaongoza haimaanishi mwanaye Bakhressa ni mkubwa zaidi kuliko Bakhressa mwenyewe.
Pia unapaswa uelewe Yesu alikuja katika mwili kuonesha njia ya uzima wa milele jinsi Binadamu tunavyopaswa kuishi kiimani na kimatendo, na alitusisitizia Binadamu kuwa tunao uwezo kuishi maisha mema kitabia na kufanya makuu kuliko yeye Yesu aliyoyafanya hapa duniani.
YESU JINA LIPITALO MAJINA YOTE KIMAMLAKA.
WAFILIPI 2:9-11.
[9]Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
[10]ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;
[11]na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.
YESU NDIYE NJIA YA UKWELI NA UZIMA WA MILELE.
YOHANA 14:6.
[6]Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
Kitabu Quran hakuna shaka ndani yake, ni muujiza thabiti unaojitosheleza.hebu tuthibitishie kuwa kitabu hicho ni cha kweli. na sisi tutakuthibitishia kuwa chetu ni cha kweli. sisi tunaamini chako ni cha uongo hivyo hatuna hata sababu yakukiamini kilichomo ndani yake.
Huyu asikusumbue,hao jamaa ni attention seeker hapa anapima upepo.Ushagongwa muhuri wa ukristu huo muhuri haufutiki hata ufanye nini
Hebu sema ukweli umesilim lini?True story: Tea time,
Nilizaliwa katika ukristo na kukulia kwenye ukristo.
Mwaka Jana nilihamia Tanga kikazi, mtaa niliokuwa Ninaishi ulikuwa una waislam tupu. nyumba nliyokuwa Ninaishi ilikuwa jirani na msikiti, Kila siku pale msikitini walikuwa wanaimba aya za Quran Usiku kucha. Sijui kwanini lakini Ile sauti ilikuwa ni nzuri sana masikioni na ilinifanya nikawa najisikia amani sana nilalapo.
Mwaka huu mwezi fulan nikiwa nimelala, nikaota ndoto ya ajabu iliyonifaonya nisilimu wiki hiyo.
Ndoto yenyewe ilikuwa hivi:
Niliota Mimi na kaka yangu wa Arusha tukitembea maeneo ya mtaani kwetu hapo Tanga. Tukakutana na kundi kubwa la watu wa Kila aina matajiri kwa masikini wakiingia katika ule msikiti jirani.
Pamoja na tofauti zao za kiuchumi lakini wote waliingia ndani katika ule msikiti na kuwa kama kitu kimoja. Hakukuwa na madaraja mule ndani, hakukuwa na mabenchi ila wote waliingia kama watoto wadogo wakijisalimisha kwa Muumba wao. Ni kama vile pesa,vyeo,umaarufu waliviacha nje ya msikiti.
Nikapita jirani nikasikia ndani Quran inasomwa na wote wakistaajabu maajabu ya hiki kitabu kilichoandikwa Karne nyingi zilizopita.
Nikapita kwa pembeni nikielekea zangu nyumbani, ila kwa nje nkakutana na mtu akawa ananialika tuingie kuswali, nikakataa kwa visingizio vingi kama vile Nawahi sehemu,sijui kuswali,siku nyingine nk. Nk.
Lakini yule mtu akanisisitiza na kuniambia kuwa nikiingia Mungu atanitoa gizani na kuniweka kwenye njia ya haki.
Mi nkaondoka lakini nkamuacha kaka angu akiongea na yule mtu. Ndoto ikaishia hapo.
Kaka angu niliokuwa sijawasiliana naye takriban wiki 3 na sikumwambia kuhusu hiyo ndoto,lakini wiki hiyo hiyo nilisikia kuwa kaka angu wa Arusha amesilimu.
Kiukweli nilistaajabu sana na kujiuliza ni nini hiki na maana yake nini?
Baada ya Tafakuri ya mda mrefu niliamua kwenda kwenye huo msikiti labda nitakutana na yule mtu wa ndotoni na hiyo ndiyo ikawa njia iliyonipelekea kurudi kwenye uislam(Kila mtu huzaliwa muislam).
Katika kumtafuta yule mtu Kuna shehe nilimsimulia, akaamua kuchukua jukumu la kunifunza na kunielezea maajabu ya Quran na kiukweli Ile ndoto + maajabu ya Quran ilinifanya nikasilimu.
Bado naendelea kujifunza mengi mapya katika hii Imani ya kweli na haki.
Allahu akbar.
PS: yule mtu Bado sijampata
PS #2: Braza wa Arusha anajua namimi nimesilimu lakini sijamuhadithia kuhusu Ile ndoto.
Hata kama ni kuhubiri dini siyo kihivi aisee...hiyo ilikuwa ni ndoto toka kwa shetani mwenyewe, umepoteza focus na kitu kikubwa sana maishani mwako, kuna siku utakuja kujuta. lakini hata hivyo una nafasi ya kubadilika na umkiri Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi wa maisha yako, uokoke kwasababu dhambi ya kwanza utakayohukumiwa nayo na ndiyo ambayo wanadamu watahukumiwa nayo ni kumkana Yesu Kristo kuwa Mwokozi wako. sikulaumu kwa hali uliyokuwa nayo kwasababu hata wakati unaota ulikuwa gizani, haukuwa tofauti na huko ulikokweda, kuwa mkristo wa dini hauna tofauti na waislam, kwahiyo haujabadili chochote umetoka kwa shetani ukaenda kwa shetani yule yule umebadilisha vyumba tu. ila kuwa Mkristo aliyeokoka (sio wa dini) ni kitu valuable na special, na ndicho kitakachofanya mtu auridhi uzima wa milele. hapo upo safarini kwenda jehanum ya moto wa milele. uamuzi ni wako.
Nimesilimu mwaka huu, hivi karibuniHebu sema ukweli umesilim lini?
Uislam ni nini/ Muislam ni nani?
Asalam alaykum! Nilisilimu lakini baadhi ya members humu wakawa wanapinga na kusema mimi sio muislam bali ni mnafiq. Sasa Leo nataka kujua kutoka kwa wajuvi wa dini ya kiislam definition ya Uislam/Muislam. Huenda ikanisaidia kuwa muislam safi. Na ikiwezekana wanipe sifa ambazo mtu anapaswa...www.jamiiforums.com
Ukristo ni dini ya kipagani, ni dini ya kuabudu jua
Asalam aleykum...twende kwenye mada Kusali jumapili Amri ya Nne inasema kwamba siku ya kuabudu ni ya 7 ni Sabato. Wakatoliki wanaita hii amri ya Tatu kwa sababu waliifuta Amri ya Pili inayokataza mtu kuabudu sanamu. Ambayo bila shaka Wakatoliki wengi hufanya. Wakati wa Masihi Yehowshuwa...www.jamiiforums.com
Mbona kama unateseka sana na Ukristu?
Mkuu, Mimi nimeripoti tu ulimbukeni wa wafuasi wa Dini. Binafsi siwezi kuwa na upuuzi wa namna hiyo.sasa cha ajabu nini kwa koran kutoungua moto? wakati imetengenezwa kiwandani tu kama vitabu vingine, au hata tungesema kuran ina nguvu nyingine ya ziada kwani hiyo inamaanisha ina nguvu ya Mungu? hata shetani ana nguvu, mbona hiyo ni sababu ndogo sana kukufanya upotelee kwenye imani potofu? kwani majini hayawezi kulinda kitabu chochote kile? kuna jirani yangu ni shehe, nakumbuka tangu tukiwwa watoto, yeye nyumba yake ikifika majira fulani lazima iungue moto. kama yanaweza kuanzisha moto, yatashindwaje kuzuia moto usichome kitabu? unajua ninyi mnavyoongea msiongee kana kwamba sisi hatuishi pamoja na ninyi na tunaijua imani na matendo ya dini yenu, tunawajua na tunaijua imani hiyo sana, na tunawaombea kwa Mungu awasaidie mfunguke macho.
Ulimaanisha Mungu au mungu?Hongera kwa mungu kukuonyesha njia ya haki