Hii ni moja ya picha ambazo Waingereza hawapendi kuziona

Hii ni moja ya picha ambazo Waingereza hawapendi kuziona

Kupokea pesa- kitu kimoja. Kukubali mashariti, tena ya aina gani - kingine.
Amin baada ya kupokea pesa ya Ghaddafi alipeleka Uganda katika Umoja wa Nchi za Kiislamu - nchi yenye asilimia 5-10 Waislamu kati ya wananchi wake...
Waislamu wenzake walilipa gharama kubwa ya damu baada ya kufukuzwa kwa Amin.


Uganda ina around 30% of population as Muslims na sio hio asilimia unayosema
 
Uganda ina around 30% of population as Muslims na sio hio asilimia unayosema
Naomba sanasana tusirudierudie tu mambo bila utafiti.
Waganda walipoulizwa kwenye sensa 2014, ni watu 4,663,204 waliojibu "mimi Mwislamu" kati ya milioni 34,124,155, yaani asilimia 13.7.
soma hapa hati rasmi: www.ubos.org/onlinefiles/uploads/ubos/NPHC/2014%20National%20Census%20Main%20Report.pdf

Sijatafuta data za kabla hivyo siwezi kusema kama ongezeko hili (ambalo ni kubwa, lkn si kubwa sana) ni tokeo la jitihada za Amin, kama ni furaha ya kuzaa kushinda wengine au kama ni tokeo la da'awa (mahubiri).

 
Naomba sanasana tusirudierudie tu mambo bila utafiti.
Waganda walipoulizwa kwenye sensa 2014, ni watu 4,663,204 waliojibu "mimi Mwislamu" kati ya milioni 34,124,155, yaani asilimia 13.7.
soma hapa hati rasmi: www.ubos.org/onlinefiles/uploads/ubos/NPHC/2014%20National%20Census%20Main%20Report.pdf

Sijatafuta data za kabla hivyo siwezi kusema kama ongezeko hili (ambalo ni kubwa, lkn si kubwa sana) ni tokeo la jitihada za Amin, kama ni furaha ya kuzaa kushinda wengine au kama ni tokeo la da'awa (mahubiri).


The muslimpopulation.com ndio source unbiased hasa katika data kama hizi, mambo ya CIA etc au mataifa yenyewe not that reliable. Reliable labda kutoka kwa mufti mkuu wa Uganda

Anyway TheMuslimpopulation.com says Uganda Muslims not less than 30% of whole Ugandans
 
The muslimpopulation.com ndio source unbiased hasa katika data kama hizi, mambo ya CIA etc au mataifa yenyewe not that reliable. Reliable labda kutoka kwa mufti mkuu wa Uganda

Anyway TheMuslimpopulation.com says Uganda Muslims not less than 30% of whole Ugandans
Ndugu Masamila, je unajua kusoma? Nilisema wapi kitu kuhusu CIA?
Nimeleta chanzo chenyewe, taarifa rasmi ya serikali ya Uganda kuhusu sensa ya 2014. Milioni 34 waliulizwa maswali na pale wanaulizwa pia dini (tofauti na TZ). Maana asili ya data ni wananchi wenyewe jinsi wanavyojibu. Na takriban asilimia 14 walijibu "Mwislamu". Je unataka kusema pale Uganda Waislamu wengi sana ni waoga wanaoficha dini yao na kujiita Wakristo?

Halafu kama ungesoma kweli tovuti www.muslimpopulation.com ungeona mawili tofauti:
1. makadirio ya 30+% ni namba ya mufti aliyehisi walikuwa na Waislamu milioni 6 mwaka 2002. (fungua "reference" katika jedwali) Hakuonyesha chanzo yaani wapi alichota idadi hii. Kumbe miaka 18 badaye ni milioni 4 tu wanaojitambulisha kuwa Waislamu katika taifa lililokua. Je hii tofauti ya milioni mbili walikufa bila kuzaa, wamekuwa Wakristo, wamesahau Uislamu wao? Uwezekano mkubwa ni shehe alihisi tu bila uhakika.

2. Halafu soma tovuti ileile hapa : "According to the National Census 2002 Islam is practiced by 12.1 percent of the population "
Kumbe ni tovuti ambyo si makini kuhusu namba. Maana sehemu moja wanataja asilimia 30+, penginepo wanataja asilimia 12.

Nakushauri utafute vyanzo halisi, usiamini mambo unayokuta kwa sababu unapenda habari fulani, lakini chungulia kwa akili ya ukosoaji. Lakini ni Shauri lako!
 
Ndugu Masamila, je unajua kusoma? Nilisema wapi kitu kuhusu CIA?
Nimeleta chanzo chenyewe, taarifa rasmi ya serikali ya Uganda kuhusu sensa ya 2014. Milioni 34 waliulizwa maswali na pale wanaulizwa pia dini (tofauti na TZ). Maana asili ya data ni wananchi wenyewe jinsi wanavyojibu. Na takriban asilimia 14 walijibu "Mwislamu". Je unataka kusema pale Uganda Waislamu wengi sana ni waoga wanaoficha dini yao na kujiita Wakristo?

Halafu kama ungesoma kweli tovuti www.muslimpopulation.com ungeona mawili tofauti:
1. makadirio ya 30+% ni namba ya mufti aliyehisi walikuwa na Waislamu milioni 6 mwaka 2002. (fungua "reference" katika jedwali) Hakuonyesha chanzo yaani wapi alichota idadi hii. Kumbe miaka 18 badaye ni milioni 4 tu wanaojitambulisha kuwa Waislamu katika taifa lililokua. Je hii tofauti ya milioni mbili walikufa bila kuzaa, wamekuwa Wakristo, wamesahau Uislamu wao? Uwezekano mkubwa ni shehe alihisi tu bila uhakika.

2. Halafu soma tovuti ileile hapa : "According to the National Census 2002 Islam is practiced by 12.1 percent of the population "
Kumbe ni tovuti ambyo si makini kuhusu namba. Maana sehemu moja wanataja asilimia 30+, penginepo wanataja asilimia 12.

Nakushauri utafute vyanzo halisi, usiamini mambo unayokuta kwa sababu unapenda habari fulani, lakini chungulia kwa akili ya ukosoaji. Lakini ni Shauri lako!


Hio website haiendeshwi na waislamu, na ipo website Dada nyingine ni hao hao, jina sikumbuki vizuri. Hawako biased kama Pew au sources kama CIA maana CIA kwenye mambo ya dini sio wa kuwaamini kabisa
 
Kwa kifupi huyu jamaa walimchafua sana, kutaka kagera iwe sehemu ya uganda tu imesababishwa atungiwe historia za kupandikiza chuki dhidi yake,
 
Kwa kifupi huyu jamaa walimchafua sana, kutaka kagera iwe sehemu ya uganda tu imesababishwa atungiwe historia za kupandikiza chuki dhidi yake,
Si zaidi huyu jamaa alikuwa chafu sana, hakuweza kazi yake ya rais akileta kifo kwa wananchi lakhi nyingi na kuharibu nchi yake?
Ushuhuda upo tele kutoka watu wa wakati wake, siyo kutoka historia iliyotungwa baadaye. Swali ni tu kama unataka kujielemisha au kama unapendelea kusikiasikia bila utafiti... na kufurahia picha ya tamasha ambako dikteta anabebwa na watu waliolazimishwa kufanya vile?
 
Hio website haiendeshwi na waislamu, na ipo website Dada nyingine ni hao hao, jina sikumbuki vizuri. Hawako biased kama Pew au sources kama CIA maana CIA kwenye mambo ya dini sio wa kuwaamini kabisa
Si vile jinsi unavyosema. Hii ni tovuti ya Kiislamu kabisa, tena kwa shabaha ya kupigia debe uenezaji wa Uislamu (hakuna ubaya kupigia debe unachopenda) Fungua sehemu za "contact" tayari unapelekwa kwa IQRA foundation Kanada, tawi la Iqra Bangla Desh. Nilibyosema: tafadhali uchungulie, usiamini tu yale unayopenda kusikia.
 
huyu jamaa baada ya kuja kupata historia yake halisi nilimkubali na kumwelewa sana japo wazungu walikuja mchafua. japo nae alikuwa na kasoro zake ka binadamu,
 
Kuna zilizoongezwa chumvi lakini hiyo haiondoi ukweli kuwa jamaa huyu alikuwa mtata.

Ipo interview yake mwenyewe anaelezea jinsi atakavyoipiga Israel..sasa mwenyewe waweza kupata picha alikuwa Mtu wa aina gani.
Hao wazungu unyama waliotutendea hata angewapiga poa tu
 
huyu jamaa baada ya kuja kupata historia yake halisi nilimkubali na kumwelewa sana japo wazungu walikuja mchafua. japo nae alikuwa na kasoro zake ka binadamu,
Kosa lake ni kukubali ile ndege iliyotekwa itue kwake..kumbuka hata gadafi aligoma kuipa hifadhi. Hapo wazungu wakaona huyu hafai inabidi atoke maana alishaanza mishe na mataifa mengine waivamie kabisa israel. Na ndo maana hata baadae historia yake wakaiongezea chumvi. Inngawa haitoi ukweli kuwa nae alikuwa kichaa kabisa. Yeye na nyerere walikiwa na mawazo tofauti ndo ugomvi ulipoanzia. Sababu hata mchonga nae alikuwa puppet kwa jamaa hao
 
Kosa lake ni kukubali ile ndege iliyotekwa itue kwake..kumbuka hata gadafi aligoma kuipa hifadhi. Hapo wazungu wakaona huyu hafai inabidi atoke maana alishaanza mishe na mataifa mengine waivamie kabisa israel. Na ndo maana hata baadae historia yake wakaiongezea chumvi. Inngawa haitoi ukweli kuwa nae alikuwa kichaa kabisa. Yeye na nyerere walikiwa na mawazo tofauti ndo ugomvi ulipoanzia. Sababu hata mchonga nae alikuwa puppet kwa jamaa hao
Hupendi kusikia Waganda wenyeje walisemaje juu yake wakati ule na jinsi wanavyosema leo? Maana walimchukia, walisikitika uharibifu wa nchi yao, mauaji na mateso?

(halafu: unaamini kweli mtu yeyote alihofia Amin angeweza kufanya chochote kuhusu Israeli?? Kumwua huyu Mama mzee mgonjwa aliyelazwa hospitalini Kampala wakati wa stori ya ndege ilikuwa kilele cha uwezo wake - pamoja na kutupa raia zake mtoni ili waliwe na mamba. Hakuna aliyefikiri huyu alikuwa na uwezo wowote nje ya kuharibu nchi yake)
 
huyu jamaa baada ya kuja kupata historia yake halisi nilimkubali na kumwelewa sana japo wazungu walikuja mchafua. japo nae alikuwa na kasoro zake ka binadamu,
Kumbe wengine hapa wanapenda kujadili "wazungu waliomchafua".

Kwa hiyo Waganda waliosema huyu alikuwa mhuni, mjinga, mnyama kwa uso wa kibinadamu, muuaji, mbakaji, mporaji, mharibifu wa nchi yao - hawastahili kusikiwa? (tena wale waliomkosoa wakati Waingereza bado walimbebeleza?)

Jamani, roho ya kitoto gani hapa? Je hao "Wazungu" ni muhimu zaidi kuliko wahanga wake?
 
Kumbe wengine hapa wanapenda kujadili "wazungu waliomchafua".

Kwa hiyo Waganda waliosema huyu alikuwa mhuni, mjinga, mnyama kwa uso wa kibinadamu, muuaji, mbakaji, mporaji, mharibifu wa nchi yao - hawastahili kusikiwa? (tena wale waliomkosoa wakati Waingereza bado walimbebeleza?)

Jamani, roho ya kitoto gani hapa? Je hao "Wazungu" ni muhimu zaidi kuliko wahanga wake?
mkuu ka ulisoma vizuri naamini ungekuwa umenielewa,nirudie tena nae alikuwa na kasoro zake na ni ka hayo aliyowafanyia ndugu zake wa nyumbani, na hilo ni kosa ambalo lipo kwa watawala wetu karibu wote. natumai hapo umenielewa baada ya ufafanuzi huo kwa uchache
 
Back
Top Bottom