Hii style nimeiona kwa wengi mjini

Hii style nimeiona kwa wengi mjini

Nilifanya huu upuuzi. Nilihamia sehemu nje ya mji wanaita Bunju, nikapanga kwa 200,000, na nyumba ni nzuri tu kule ushuani.

Balaaa ni kwenye gharama za uendeshaji maisha huko nje ya mji. Mafuta tu ya gari ni 300,000 kwa mwezi hiyo ni minimum yanaweza kuzidi.

Hapo bado purukushani zingine..... Sasa nikaona si heri kuendelea kuishi huko huko katikati ya mji..... Maana gharama hazikwepeki. Ila unachoweza fanya ni kubudget matumizi yako vema basi.
Kupanga nyumna pembeni ya Mjii ni Upuuzi sana kama mishe mishe zako ni town yani Bora iwe umejenga hukoo mzee...!!

Sent from my SM-G611K using JamiiForums mobile app
 
nitajenga ila kitu kujinyima kuishi vizuri ili nijenge hapana kwa kweli siwezi
Una familia au upo singo? Unasomesha? Ugumu ni pale ambapo ada zinakutana na kodi ya kupanga, hapo ndo huwa akili inakukaa sawa. Hiyo kujenga kwa kujinyima huwa inakuja tu automatic na sio kwa kupenda hasa pale unapoona maji yameshazidi unga
Lakini pia inategemeana na kipato chako, kuna wengine wanaweza kujenga mwanzo mwisho bila kujinyima huku wamepanga na mambo mengine yanaendelea kama kawaida
 
ki ukweli hata mimi nikipata hela uwezi kunishawishi nikakae pembezoni mwa mji yaani nikateseke chumba cha elfu 40, sijui nikaangaike kujenga kanyumba akaeleweki polini uko.

big No izi hela namtafutia nan sasa mimi nitapanga apartment nzuri mjini uko nitajenga taratibu nikiwa mzee pembezoni mwa mji.

Duniani hatujaletwa kuteseka jamaani.
Mawazo yako yanaishia hapo...acha uendelee hivyo hivyo na tuajira twa bank maana ndo hua tuna mabishoo
 
Ni wachache sana wanaojenga wakiwaa wanahela kamili mkononi ,Wengi wetu tumeunga unga na kujinyima ndo maana leo tunaitwa baba mwenye nyumba .Mkuu kufa kupo ila ukifa si tunawatoto watarithi .Hivi hujisikii hasra kumpa laki saba ana milioni mtu km kodi huwazi .Pia uhuru unao kua nao kwako hata ukitoka na taulo ama watoto wanacheza kwao.
Ni kweli Mkuu miaka 10 iliyopita nilinunua kiwanja mil 20 salasala wakati huo kulikuwa shamba kidogo kwa sasa bila mil 80 mpaka 100 hupati kiwanja maeneo hayo.

Mdogomdogo kwa kujibana nimemaliza mjengo. Watoto wanacheza na wanapanda juu mara chini. Maisha safi kabisa. Nimemaliza mjengo huo baada ya miaka 9. No pain no gain. Kama unawaza kufa huwezi kufanya chochote cha maana duniani.
 
Ndugu mleta uzi. Upo sahihi but napenda uniruhusu kuwasilisha maoni yangu kama ifuatavyo.
Mtazamo wa maisha ni jambo very tricky sana usipokuwa makini na maamuzi yako unapoamua kufanya mabadiliko ya maisha.

Kuishi kwa unafuu ni jambo moja zuri ila kwa upande mwingine si jambo lenye faida sana ukitazama in the long run.

Hebu watazame kama wahindi wenzetu mathalani..... Wanaishi maeneo gani?! Umeaona bunju, umewaona tegeta umewaona Chanika.....?!

Wanaishi upanga, kwenye flats na apartment na nyumba za national housing. Na ndio wanampunga kutishinda sisi tunaojiita wajanja......

Siri moja kuhusu maisha, ukitaka unafuu wa chini ya tabaka lako (comfort zone) basi jiandae kushuka daraja.

Mfano, umeona kulipa 350,000 ni mzigo na ingawa umeweza kumudu basi wewe unaanza kuishi early retirement wakati haupo katika huo umri wa kuretire. Hayo ni mawazo anatakiwa kuwa nayo mzee wa miaka 85+ ambaye anahitaji utulivu wa kuishi miaka iliyosalia kwa kupumzika na kucheza na wajukuu.....

Kijana wa miaka 20 hadi 70+ unasemaje kuwa unakwenda kujenga nje ya mji kutafuta unafuu wa maisha...... C'amon?!

Nikwambie tu, maisha yanataka katika kila stage unayo graduate au kufika basi usichukulie ndio hitimisho, bali hiyo ni stepping stone ya the following phase ya maisha.... Tena ushukuru umefika hapo kuna mtu akiona wewe unalipa laki tatu na nusu ya kodi anakuona mharibifu sana wa pesa. Sababu yeye ameshajilimit kuwa hatopanga nyumba zaidi ya kodi ya 30,000 kwa mwezi. Huyu mtu unamuonaje hivi?!

Ipo hivi, pesa ndio maana inaitwa "Currency" kutokana na neno CURRENT ambalo humaanisha mkondo. Ukitaka pesa sharti maisha yako yawe na value pesa itakufuata. Kama ninachosema ni uongo tazama uhalisia hivi ukiwa na maisha ya kubana bajeti kesho ukafa ndugu wakagombania muounga wako unakuwa umeacomplish nini kwa mfano?!

Unajua kuna mtu unamfuata unamwambia brother naomba unazime 500,000 chap hapo jibu lake ni okay nikutumie kwenye namba gani?! Unajisikiaje kuongea na mtu wa hivi?!
Mwingine hata elfu 20 tu ataingia kwenye wallet atatoa chap atakupatia.

Mimi as a business person nitavutiwa sana kuongea na mtu anaendesha gari ya wastani 2000, anaishi nyumba ya kupanga hata kama ni 200,000 au 350,000, https://jamii.app/JFUserGuide the price what matters upo comfortable na unaishi kwa nafasi nzuri. Ana budget nzuri na haogopi kufikiria chanzo kipya cha mapato kila baada ya miezi kadhaa. Hii itanipa picha kuwa huyu mtu ana discipline ya pesa na anajiamini na yupo positive financially.

Vijana wengi wa bongo atatoka kodi ya chumba kimoja, ataenda chumba na sebule, akishatiana mimba na mwenzake wakapata tutoto tuwili watakodi kanyumba ka vyumba vitatu then wataanza ujenzi wa nyumba nje ya mji then wakishamaliza wanahamia story imeisha wanajiona ni wazee wameshamaliza maisha, watu wa namna hii huwa hata kuongea nao naona kero maana wanajiona safari ya maisha wameifika na wanasubiria wajukuu na uzee ufike wadedi picha liishe.

Hivi mnaona wenzetu rangi nyeupe wanavyofanya?! Wakati sisi goal yetu na accomplishment kubwa na ya mwisho ya average Tanzanian youth ni kuoa, kupata watoto, kujenga nyumba yenye fremu mbele ya fensi huko nje ya mji, kununua gari, kuwa na shamba mlandizi au chanika la kulima viazi gunia mbili, na kuokota maembe kiroba kimoja kisha kuendelea kuishi tukisubiria uzee utuvae huku tukisomesha watoto kwa hela za pension na kujiuguza magonjwa kama kisukari na pressure sababu ya stress za retirement era,..... Tazama wenzetu race nyingine wanafanyaje huo umri?!

Average white race person goal yake kubwa ni kuishi standard ya maisha itakayompa privilege ya kubakia kuwa superior race no matter what it costs. Amini nakwambia hakuna kitu kama gharama katika haya maisha ila kuna choice za gharama gani unataka maisha yako yawe evaluated.

Unataka kuishi maisha ya free from everything?! Yaani mtu anakwambia anajenga ili kukwepa kulipa bili za makazi kama kodi?! Seriously?! Nani alikwambia kuishi katikati ya mji huku unalipa kodi ni sumu ya kufeli maisha....?!

Its okay to own a piece of land ila huwa nashangaa mtu anakimbiaje maisha ya kupambana for the luxury of the comfort zone?! Comfort zone ndipo watu hujitengenezea hell ya uzeeni. Hivi hawa wazee wote wanaodedi kwa pressure, kisukari, msongo wa mawazo, wengi si huwa wana majumba yao ya kuishi, shida huwa ni nini unadhani?!

Ni financial freedom hakuna. Mtanzania average anapoanza kupata access ya kutoka katoka tabaka la chini kuingia la kati anaanza upuuzi huu wa kuishi maisha ya kizee na hatimae kurudi nyuma badala ya kukaza zaidi na kubadili mbinu ilikuwa 100% tabaka la kati yaani tabaka six figures income every month na kurudi chini kwenye tabaka la three to two figures a month.

Walipo wahindi ndio na sisi tunatakiwa kuwapo. Wahindi sasa hivi ni sehemu ya kabila la kitanzania maana wapo waliozaliwa hapa. Why tusiwaige njia zao na sisi tusione shida kwenda kupanga pale upanga kwenye apartments tunaishi maisha ya popo huko vingunguti.

Ukienda nje ya mji barabara mbovu, gari zinaumia, mafuta uhitaji utaongezeka , gharama za vipuli vya gari na services vitakuhusu, plus unaenda kukaa nje ya mji utatakiwa kurejea home mapema sababu ya umbali, pia ni ngumu kuwa karibu na wazee wa connection kupeana connection.....

Nadhani hili hebu tulitazamie upya..... Kila kitu kitawezekana ndani ya muda na sisi tukiwa watu wa kujiongeza na changamoto zetu......
 
Kupata kiwanja cha kujenga nyumba hasa katika prime area ni changamoto kubwa kwa sisi tunao safiri kuelekea uchumi wa kati. Unakuta pango la mwezi unapokaa ni 350, 000, ukipiga hesabu kwa miaka miwili unaona ni kheri ujenge ya kwako.

Umepata kiwanja kwa milioni 20. Bahati nzuri ulikua na akiba ya milioni 5, benki wakakupa milioni 20 mkopo. Rafiki zangu wengi walichofanya ni kujenga nyumba ya kujistiri nyuma ya kiwanja. Ina basic needs tu na kuhamia.

Mbele ya kiwanja anaweka banda la kuku hawa wa kienyeji na matuta manne ya mchicha. Hapo amepiga mahesabu ya kurudisha mkopo. Watoto wakilalamika wamechoka kula mchicha wanapozwa na kuku. Maharage ndiyo kubadilisha menu.
Wengi tumefanya hivo na sasa tunaona heri kwa kias flani. Nihiv watuwengi wameshindwa kujenga mjini sababu ya kuwa na matamanio makubwa zaid ya uwezo wao.
 
Una familia au upo singo? Unasomesha? Ugumu ni pale ambapo ada zinakutana na kodi ya kupanga, hapo ndo huwa akili inakukaa sawa. Hiyo kujenga kwa kujinyima huwa inakuja tu automatic na sio kwa kupenda hasa pale unapoona maji yameshazidi unga
Lakini pia inategemeana na kipato chako, kuna wengine wanaweza kujenga mwanzo mwisho bila kujinyima huku wamepanga na mambo mengine yanaendelea kama kawaida
Hivi kodi na ada huwa zinatokea ghafla tu bila taarifa?!

Katika vitu huwa naelewa mtu anambie amepata mgonjwa ghafla na amezidiwa gharama...... Ila sio eti ada au kodi?!

Hivi mfano hapa unajua kabisa mwezi wa kumi na mbili kodi inaisha na huu ni mwezi February, utakaa tu usubirie ufike uanze kulia.... Au utaanza kuandaa mazingira huo muda ukifika mpunga uwe tayari mkononi?!

Nadhani ni swala la wewe unayachukuliaje maisha......
 
Kupata kiwanja cha kujenga nyumba hasa katika prime area ni changamoto kubwa kwa sisi tunao safiri kuelekea uchumi wa kati. Unakuta pango la mwezi unapokaa ni 350, 000, ukipiga hesabu kwa miaka miwili unaona ni kheri ujenge ya kwako.

Umepata kiwanja kwa milioni 20. Bahati nzuri ulikua na akiba ya milioni 5, benki wakakupa milioni 20 mkopo. Rafiki zangu wengi walichofanya ni kujenga nyumba ya kujistiri nyuma ya kiwanja. Ina basic needs tu na kuhamia.

Mbele ya kiwanja anaweka banda la kuku hawa wa kienyeji na matuta manne ya mchicha. Hapo amepiga mahesabu ya kurudisha mkopo. Watoto wakilalamika wamechoka kula mchicha wanapozwa na kuku. Maharage ndiyo kubadilisha menu.
Maisha ya kigoroko sana haya
 
Ndugu mleta uzi. Upo sahihi but napenda uniruhusu kuwasilisha maoni yangu kama ifuatavyo.
Mtazamo wa maisha ni jambo very tricky sana usipokuwa makini na maamuzi yako unapoamua kufanya mabadiliko ya maisha.

Kuishi kwa unafuu ni jambo moja zuri ila kwa upande mwingine si jambo lenye faida sana ukitazama in the long run.

Hebu watazame kama wahindi wenzetu mathalani..... Wanaishi maeneo gani?! Umeaona bunju, umewaona tegeta umewaona Chanika.....?!

Wanaishi upanga, kwenye flats na apartment na nyumba za national housing. Na ndio wanampunga kutishinda sisi tunaojiita wajanja......

Siri moja kuhusu maisha, ukitaka unafuu wa chini ya tabaka lako (comfort zone) basi jiandae kushuka daraja.

Mfano, umeona kulipa 350,000 ni mzigo na ingawa umeweza kumudu basi wewe unaanza kuishi early retirement wakati haupo katika huo umri wa kuretire. Hayo ni mawazo anatakiwa kuwa nayo mzee wa miaka 85+ ambaye anahitaji utulivu wa kuishi miaka iliyosalia kwa kupumzika na kucheza na wajukuu.....

Kijana wa miaka 20 hadi 70+ unasemaje kuwa unakwenda kujenga nje ya mji kutafuta unafuu wa maisha...... C'amon?!

Nikwambie tu, maisha yanataka katika kila stage unayo graduate au kufika basi usichukulie ndio hitimisho, bali hiyo ni stepping stone ya the following phase ya maisha.... Tena ushukuru umefika hapo kuna mtu akiona wewe unalipa laki tatu na nusu ya kodi anakuona mharibifu sana wa pesa. Sababu yeye ameshajilimit kuwa hatopanga nyumba zaidi ya kodi ya 30,000 kwa mwezi. Huyu mtu unamuonaje hivi?!

Ipo hivi, pesa ndio maana inaitwa "Currency" kutokana na neno CURRENT ambalo humaanisha mkondo. Ukitaka pesa sharti maisha yako yawe na value pesa itakufuata. Kama ninachosema ni uongo tazama uhalisia hivi ukiwa na maisha ya kubana bajeti kesho ukafa ndugu wakagombania muounga wako unakuwa umeacomplish nini kwa mfano?!

Unajua kuna mtu unamfuata unamwambia brother naomba unazime 500,000 chap hapo jibu lake ni okay nikutumie kwenye namba gani?! Unajisikiaje kuongea na mtu wa hivi?!
Mwingine hata elfu 20 tu ataingia kwenye wallet atatoa chap atakupatia.

Mimi as a business person nitavutiwa sana kuongea na mtu anaendesha gari ya wastani 2000, anaishi nyumba ya kupanga hata kama ni 200,000 au 350,000, **** the price what matters upo comfortable na unaishi kwa nafasi nzuri. Ana budget nzuri na haogopi kufikiria chanzo kipya cha mapato kila baada ya miezi kadhaa. Hii itanipa picha kuwa huyu mtu ana discipline ya pesa na anajiamini na yupo positive financially.

Vijana wengi wa bongo atatoka kodi ya chumba kimoja, ataenda chumba na sebule, akishatiana mimba na mwenzake wakapata tutoto tuwili watakodi kanyumba ka vyumba vitatu then wataanza ujenzi wa nyumba nje ya mji then wakishamaliza wanahamia story imeisha wanajiona ni wazee wameshamaliza maisha, watu wa namna hii huwa hata kuongea nao naona kero maana wanajiona safari ya maisha wameifika na wanasubiria wajukuu na uzee ufike wadedi picha liishe.

Hivi mnaona wenzetu rangi nyeupe wanavyofanya?! Wakati sisi goal yetu na accomplishment kubwa na ya mwisho ya average Tanzanian youth ni kuoa, kupata watoto, kujenga nyumba yenye fremu mbele ya fensi huko nje ya mji, kununua gari, kuwa na shamba mlandizi au chanika la kulima viazi gunia mbili, na kuokota maembe kiroba kimoja kisha kuendelea kuishi tukisubiria uzee utuvae huku tukisomesha watoto kwa hela za pension na kujiuguza magonjwa kama kisukari na pressure sababu ya stress za retirement era,..... Tazama wenzetu race nyingine wanafanyaje huo umri?!

Average white race person goal yake kubwa ni kuishi standard ya maisha itakayompa privilege ya kubakia kuwa superior race no matter what it costs. Amini nakwambia hakuna kitu kama gharama katika haya maisha ila kuna choice za gharama gani unataka maisha yako yawe evaluated.

Unataka kuishi maisha ya free from everything?! Yaani mtu anakwambia anajenga ili kukwepa kulipa bili za makazi kama kodi?! Seriously?! Nani alikwambia kuishi katikati ya mji huku unalipa kodi ni sumu ya kufeli maisha....?!

Its okay to own a piece of land ila huwa nashangaa mtu anakimbiaje maisha ya kupambana for the luxury of the comfort zone?! Comfort zone ndipo watu hujitengenezea hell ya uzeeni. Hivi hawa wazee wote wanaodedi kwa pressure, kisukari, msongo wa mawazo, wengi si huwa wana majumba yao ya kuishi, shida huwa ni nini unadhani?!

Ni financial freedom hakuna. Mtanzania average anapoanza kupata access ya kutoka katoka tabaka la chini kuingia la kati anaanza upuuzi huu wa kuishi maisha ya kizee na hatimae kurudi nyuma badala ya kukaza zaidi na kubadili mbinu ilikuwa 100% tabaka la kati yaani tabaka six figures income every month na kurudi chini kwenye tabaka la three to two figures a month.

Walipo wahindi ndio na sisi tunatakiwa kuwapo. Wahindi sasa hivi ni sehemu ya kabila la kitanzania maana wapo waliozaliwa hapa. Why tusiwaige njia zao na sisi tusione shida kwenda kupanga pale upanga kwenye apartments tunaishi maisha ya popo huko vingunguti.

Ukienda nje ya mji barabara mbovu, gari zinaumia, mafuta uhitaji utaongezeka , gharama za vipuli vya gari na services vitakuhusu, plus unaenda kukaa nje ya mji utatakiwa kurejea home mapema sababu ya umbali, pia ni ngumu kuwa karibu na wazee wa connection kupeana connection.....

Nadhani hili hebu tulitazamie upya..... Kila kitu kitawezekana ndani ya muda na sisi tukiwa watu wa kujiongeza na changamoto zetu......
utopolo utakuja kulia vby
 
ki ukweli hata mimi nikipata hela uwezi kunishawishi nikakae pembezoni mwa mji yaani nikateseke chumba cha elfu 40, sijui nikaangaike kujenga kanyumba akaeleweki polini uko.

big No izi hela namtafutia nan sasa mimi nitapanga apartment nzuri mjini uko nitajenga taratibu nikiwa mzee pembezoni mwa mji.

Duniani hatujaletwa kuteseka jamaani.
Nimecheka sana hii post yako. Ila mkuu jaribu kufikiria familia yako kiujumla,unaweza kuanguka ghafla mke hana kazi na watt wanasoma shule za private. Nani atawalipia ada na kodi ya nyumba ulopanga katkat ya mji?

NB: Kila mtu ana muono wake wa maisha. Nisikupangie namna ya kuishi
 
Ndugu mleta uzi. Upo sahihi but napenda uniruhusu kuwasilisha maoni yangu kama ifuatavyo.
Mtazamo wa maisha ni jambo very tricky sana usipokuwa makini na maamuzi yako unapoamua kufanya mabadiliko ya maisha.

Kuishi kwa unafuu ni jambo moja zuri ila kwa upande mwingine si jambo lenye faida sana ukitazama in the long run.

Hebu watazame kama wahindi wenzetu mathalani..... Wanaishi maeneo gani?! Umeaona bunju, umewaona tegeta umewaona Chanika.....?!

Wanaishi upanga, kwenye flats na apartment na nyumba za national housing. Na ndio wanampunga kutishinda sisi tunaojiita wajanja......

Siri moja kuhusu maisha, ukitaka unafuu wa chini ya tabaka lako (comfort zone) basi jiandae kushuka daraja.

Mfano, umeona kulipa 350,000 ni mzigo na ingawa umeweza kumudu basi wewe unaanza kuishi early retirement wakati haupo katika huo umri wa kuretire. Hayo ni mawazo anatakiwa kuwa nayo mzee wa miaka 85+ ambaye anahitaji utulivu wa kuishi miaka iliyosalia kwa kupumzika na kucheza na wajukuu.....

Kijana wa miaka 20 hadi 70+ unasemaje kuwa unakwenda kujenga nje ya mji kutafuta unafuu wa maisha...... C'amon?!

Nikwambie tu, maisha yanataka katika kila stage unayo graduate au kufika basi usichukulie ndio hitimisho, bali hiyo ni stepping stone ya the following phase ya maisha.... Tena ushukuru umefika hapo kuna mtu akiona wewe unalipa laki tatu na nusu ya kodi anakuona mharibifu sana wa pesa. Sababu yeye ameshajilimit kuwa hatopanga nyumba zaidi ya kodi ya 30,000 kwa mwezi. Huyu mtu unamuonaje hivi?!

Ipo hivi, pesa ndio maana inaitwa "Currency" kutokana na neno CURRENT ambalo humaanisha mkondo. Ukitaka pesa sharti maisha yako yawe na value pesa itakufuata. Kama ninachosema ni uongo tazama uhalisia hivi ukiwa na maisha ya kubana bajeti kesho ukafa ndugu wakagombania muounga wako unakuwa umeacomplish nini kwa mfano?!

Unajua kuna mtu unamfuata unamwambia brother naomba unazime 500,000 chap hapo jibu lake ni okay nikutumie kwenye namba gani?! Unajisikiaje kuongea na mtu wa hivi?!
Mwingine hata elfu 20 tu ataingia kwenye wallet atatoa chap atakupatia.

Mimi as a business person nitavutiwa sana kuongea na mtu anaendesha gari ya wastani 2000, anaishi nyumba ya kupanga hata kama ni 200,000 au 350,000, **** the price what matters upo comfortable na unaishi kwa nafasi nzuri. Ana budget nzuri na haogopi kufikiria chanzo kipya cha mapato kila baada ya miezi kadhaa. Hii itanipa picha kuwa huyu mtu ana discipline ya pesa na anajiamini na yupo positive financially.

Vijana wengi wa bongo atatoka kodi ya chumba kimoja, ataenda chumba na sebule, akishatiana mimba na mwenzake wakapata tutoto tuwili watakodi kanyumba ka vyumba vitatu then wataanza ujenzi wa nyumba nje ya mji then wakishamaliza wanahamia story imeisha wanajiona ni wazee wameshamaliza maisha, watu wa namna hii huwa hata kuongea nao naona kero maana wanajiona safari ya maisha wameifika na wanasubiria wajukuu na uzee ufike wadedi picha liishe.

Hivi mnaona wenzetu rangi nyeupe wanavyofanya?! Wakati sisi goal yetu na accomplishment kubwa na ya mwisho ya average Tanzanian youth ni kuoa, kupata watoto, kujenga nyumba yenye fremu mbele ya fensi huko nje ya mji, kununua gari, kuwa na shamba mlandizi au chanika la kulima viazi gunia mbili, na kuokota maembe kiroba kimoja kisha kuendelea kuishi tukisubiria uzee utuvae huku tukisomesha watoto kwa hela za pension na kujiuguza magonjwa kama kisukari na pressure sababu ya stress za retirement era,..... Tazama wenzetu race nyingine wanafanyaje huo umri?!

Average white race person goal yake kubwa ni kuishi standard ya maisha itakayompa privilege ya kubakia kuwa superior race no matter what it costs. Amini nakwambia hakuna kitu kama gharama katika haya maisha ila kuna choice za gharama gani unataka maisha yako yawe evaluated.

Unataka kuishi maisha ya free from everything?! Yaani mtu anakwambia anajenga ili kukwepa kulipa bili za makazi kama kodi?! Seriously?! Nani alikwambia kuishi katikati ya mji huku unalipa kodi ni sumu ya kufeli maisha....?!

Its okay to own a piece of land ila huwa nashangaa mtu anakimbiaje maisha ya kupambana for the luxury of the comfort zone?! Comfort zone ndipo watu hujitengenezea hell ya uzeeni. Hivi hawa wazee wote wanaodedi kwa pressure, kisukari, msongo wa mawazo, wengi si huwa wana majumba yao ya kuishi, shida huwa ni nini unadhani?!

Ni financial freedom hakuna. Mtanzania average anapoanza kupata access ya kutoka katoka tabaka la chini kuingia la kati anaanza upuuzi huu wa kuishi maisha ya kizee na hatimae kurudi nyuma badala ya kukaza zaidi na kubadili mbinu ilikuwa 100% tabaka la kati yaani tabaka six figures income every month na kurudi chini kwenye tabaka la three to two figures a month.

Walipo wahindi ndio na sisi tunatakiwa kuwapo. Wahindi sasa hivi ni sehemu ya kabila la kitanzania maana wapo waliozaliwa hapa. Why tusiwaige njia zao na sisi tusione shida kwenda kupanga pale upanga kwenye apartments tunaishi maisha ya popo huko vingunguti.

Ukienda nje ya mji barabara mbovu, gari zinaumia, mafuta uhitaji utaongezeka , gharama za vipuli vya gari na services vitakuhusu, plus unaenda kukaa nje ya mji utatakiwa kurejea home mapema sababu ya umbali, pia ni ngumu kuwa karibu na wazee wa connection kupeana connection.....

Nadhani hili hebu tulitazamie upya..... Kila kitu kitawezekana ndani ya muda na sisi tukiwa watu wa kujiongeza na changamoto zetu......
Nimekuwlelewa sana lakini unatambua kuwa Afrika tu ndiyo wenye bahati ya kuwa na uwezo wa kununua ardhi na kujenga nyumba ya uwezo wako. Mfano Uingereza ardhi yote ni mali ya Malkia na hata ukinunua nyumba ukizeeka inauzwa ili pesa ikutunze.

Wazungu wanaitegemea serikali kama safe net mambo yakiwa Magumu. Serikali itakupa nyumba, utailipia kwa mwezi lakini huwezi kuiuza, si ya kwako.

Wahindi wana family and friends support kama safe net. Hata biashara zikiharibika wanapeana bidhaa wauze waanze tena. Hii community kwa Waafrika iliharibiwa na Ukoloni.

Si wengi tunaweza biashara, mfano mimi binafsi biashara ninayoitegemea nikiwa mzee ni nyumba za kupangisha. Kuna wastaafu wengi waliishi nyumba za kupanga au nyumba za serikali , sasa hivi wamestaafu ndiyo wanatafuta kiwanja kwa hela ya pension. Sasa hivi ndiyo upate shamba Mlandizi uanze kujenga ukiwa na miaka 70.

Ni kheri uwe na kiwanja, hata usipojenga nyumba mafao ya pension yanaweza kuboresha tu mazingira. Wakati huo umekwisha kutengeneza network na majirani.

Hakuna formulae moja ya maisha kumbuka.
 
Hivi kodi na ada huwa zinatokea ghafla tu bila taarifa?!

Katika vitu huwa naelewa mtu anambie amepata mgonjwa ghafla na amezidiwa gharama...... Ila sio eti ada au kodi?!

Hivi mfano hapa unajua kabisa mwezi wa kumi na mbili kodi inaisha na huu ni mwezi February, utakaa tu usubirie ufike uanze kulia.... Au utaanza kuandaa mazingira huo muda ukifika mpunga uwe tayari mkononi?!

Nadhani ni swala la wewe unayachukuliaje maisha......
Nilichomaanisha ni kwamba jinsi majukumu yanavyoongezeka na hela ndo inakua haigawanyiki

Ni kweli ada na kodi sio emergency issues, lakin kwa wenye vipato constant hawana marupurupu wala safari wakati mwingine hizo hela hazitunziki, we haijawahi kukutokea plan yako ikafeli?

ku plan ni swala moja lakini lakini kufikia hilo lengo pia ni ishu nyingine mkuu, ndo mana wale wanaokopesha kwa riba makazini wanakula sana hela zetu na ukifatilia mikopo mingi ni ada na kodi
 
Nyumba kuuuuubwaaa ya nini wakati unalala chumba kimoja? Manyumba ya hivyo waachie mafisadi maana pesa zao ni chafu na hazina uchungu wowote

Jenga nyumba ndogo nzuri. Maana baada ya muda watoto wakikuwa wanaondoka na kukuachia mjumba mkuuubwaaa unaishi wewe na mwenzako.
 
Hiz habar za kujenga nyumba ndog kwanza halaf et tutajenga kubwa baadae mimi nilishayakataa....unajenga kijumba cha kisela af matokea yke unajikuta unazeekea humo...kwanin usijipe muda tu ukiinuka unainuka mzima mzima?

Ndio yale unakuta mstaafu anajengea nyumba pesa ya pensheni. Si sawa sana sema tu ndio maisha. Binafsi naona ni bora nijenge bangaloo pagare complete nipige bati na kuingia nitai finish taratibu mdogo mdog kuliko kujenga kijumba kidogo na kukipiga finishing huku nina mpango wa kujenga nyumba kubwa baadae hapana
binafsi upo kama mimi.
Wakati huo sijaoa nilikuwa nanunua vitu lakshari tu kama godoro na kitanda na vitu vingine,nilipotaka kuoa nikaona vyote havifai nikaingia gharama upya wakati nilikuwa na uwezo wa kununuaa vitu vya kutumia hata baada ya kuoa.

Wakati huo nilijipa matumaoni kuwa aah si nipo peke angu acha tu ntanunua kikubwa baadae nomejifunza kupitia vitu hivyo vya kawaida sitaki kufanya makosa kwemye nyumba.

Nina kaeneo kangu kapo kanfokanfo ya jiji la dar nilichofanya ninatafuta ramani ya nyumba yangu ninayoitaka najua kujenga kwa mkupuo siwezi ila nakomaa nayo hata kama miaka kumi basi nasimamisha kitu ninachokitaka inakuwa poa sana.
 
Nyumba kuuuuubwaaa ya nini wakati unalala chumba kimoja? Manyumba ya hivyo waachie mafisadi maana pesa zao ni chafu na hazina uchungu wowote

Jenga nyumba ndogo nzuri. Maana baada ya muda watoto wakikuwa wanaondoka na kukuachia mjumba mkuuubwaaa unaishi wewe na mwenzako.
Unajenga nyumba yako chumba tatu,sebule,choo,ukumbi,sehemu ya kula n.k poa sana.

Vyumba kumi unajenga kwa ajili ya wageni wanaokuja kukaa kwa muda na kuondoka vyumba vinabaki tupu mwishowe waswahili wakuseme kwamba kuna vyumba hufungui unafuga nyoka
 
Back
Top Bottom