Hii tabia imekuwa sugu; mtu anaamua tu aje Dar kukusalimia na afikie kwako

Mkuu nimestikika kwa kusikia hicho ulicho kiwaza! Huenda umewaza Kwa kutumia makalio! Kabisa ndg Yako katoka Kijijini umuache stend na unaamua kuzima na simu kabisa? Kumbuka hao ndo watakuzika wataomboleza kifo chako hao ndo watapalilia kabuli lako! Hao ndio watakulelea Watoto wako. Elewa ndg atabaki kuwa ndg tu kama hutaki ndg Yako kumsaidia na yupo stendi nani amsaidie ? Hata kama maisha ni magumu kiasi mwambie ukweli akae siku chache mrudishe sio kumtelekeza wengine Bado tunajitafta yamkini tunakula na watu Baki ambao hata si ndg zetu na tumetengeneza undugu. Naishi na kijana alikuja kutafta maisha huku baada kuishi nae Kwa mwaka mmoja nikaamua nimuajiri wazazi wake wakaniokba niende nae wakanifamu

Nilipokelewa Vizuri
Nikachinjiwa mbuzi
Nikapewa debe3 mpunga Ulo kobolewa!
Jogoo la kuku
Michembe debe1

Kwann ndg yangu nimtelekeze? Siwezi

Nina wasiwasi na jinsia Yak😵va.
 
Nimeishi Dar Hadi kuanza Maisha .Dar kigumu,wengi wanaishi Maisha feki..Anakuja mtu kutoka Dar hata samaki wa baharini hajabeba mkoa uliopo unampokea airport siku ya kuondoka unamchukulia na ndoo ya samaki na sehemu za burudani unampeleka unalipa bills Kwa sababu ni mshikaji..Siku wewe ukifika Dar unampigia akupokee ukifika airport anakupitisha Ile pstation ya puma umuwekee mafuta,sehemu za starehe bill anakusukumia mgeni,visingizio kibao,then anakuulizia unafikia hoteli gani...
Mbaya zaidi ukute anafahamu mambo yako siyo poa hata airport hatokei atakwambia Yuko site mapinga...😁
 
Mtanii nakuja kwako week ijayoo, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
YESU KRISTO alipokua akiwaambia wanafunzi wake kuhusu dalili za mwisho wa dunia alisema ni binadamu kutokupendana. Ambapo alilisema ili kwenye Mathayo 24 sura ya 10. ""Akisema Ndipo wengi watakapo jikwaa nao watasalitiana na kuchukiana.

Na sura ya 12 akisema."" Na kwasababu ya kuongezeka maasi upendo wa watu hutapoa.Nipende tu kukwambia Mkuu wew hujui kesho hivyo tenda wema nenda zako.Binadamu siku zote hawana shukrani lakini pia ujue unaemuona Leo ni nuksi kwako kesho anaweza kuwa ndio msaada kwako.
 
Kuna makabila hawapendi kwao, atakuwa mmojawapo
 
Binafsi nawaelewa hawa watu wanaokimbia ndugu. Nauzoefu wa kuishi na ndugu nawajua. Ndugu miyeyusho sana wengi ni ndugu lawama na hawana shukran sio mbaya ku keep distance.

Sema mm nimenyimwa tu hiyo roho, atakama nikidhamilia kumkataa mtu akitia huruma tu kidogo nimeingia kingi. Bas nimeamua kufanya tu sehemu yangu na kusaidia pale napoweza kwa ajili tu ya amani ya nafsi yangu.

Ila kiukweli hamna faida yoyote nayopata tena unaweza kuta wewe unaye saidia ndo unajina baya huko kijijn kuliko asiye saidia kabisa. Yaan basi tu kwasababu roho ya ukauzu sina ngoja n bak hivi mjinga machoni pao maana kulazimisha tabia ambayo huna ni kujiadhibu
 
Mimi walienda kusema nafuja sana pesa badala ya kuwasomesha watoto wao. Mtu kazaa watoto 13 anataka nimsomeshee... Mimi nina 3 tu. Bado wanaenda kusema nakuaje na watoto wachache ... Mwanaume gani. Mke amenikalia kichwani anarudi jioni kama mwanamke. Wanataka wife awafulie nguo zao. Na wanakuwa wakali akirudi awapatie chakula n.k sina hamu na ndugu kabisa.

Mmoja tumekaa naye mwaka mmoja amekuja nimsomeshe diploma. Akirudi toka chuo anaangalia TV mpaka saa 4 akipewa kazi basi za home siku yupo asaidie... Anasema anateswa sana hawezi soma. Nikasubiri likizo. Akaenda kwao kusalimi. Nikamwambia atafute chuo aendelee kusoma huko nitamlipia ada.

Alilia sana anataka arudi Dar. Nlimwambia huku wifi yako atakutesa hutapata muda wa kusoma. Akabembeleza sana nilimkatalia coz alishanipakaza sana kijijini na kumchafua sana wife. Na mtu mwenyewe ni ndugu wa mbali kabisa..
 
Mwiba Gani huo? AU hawaondoki kurudi kwao?
 
Kuna wakati niliwahi kupokea mtoto wa baba mdogo, yaani hivi, James alizaa watoto 2 Otimbi na Timbilio. Otimbi akamzaa baba yake huyo dogo na Timbilio akamzaa baba yangu mimi.
Huyu dogo alikuwa anawasiliana na dame wake waliyekutana mtandaoni. Kwetu ni mkoa wa mbali, inachukua masaa 18 mwendo wa bus kufika. Dogo akasafiri kufata demu.

Alivyotoka kijijini aliaga anakwenda mjini (ndani ya ule mkoa) kwa baba yangu mimi. Alipofika kwa baba akalala siku 1 akaaga anakuja huku DSM kwenye ishu zake. Baba hakumhoji kivile akamuacha akaondoka. Amezoeleka huwa anakwenda na kuondoka. Dogo aliku amevuka 18 lakini ni below 25, alikua anacheza 22 au 23 hivi.

Alipokuwa njiani, akakumbuka kaka Sean yuko DSM. Akaomba namba yangu kwa mdogo wangu wa tumbo 1, akanipigia, akanieleza kuwa yeye anakuja huku ila ana mambo yake na mwenyeji wake. Mi nikaitikia sawa, ila ukifika jitahidi tuonane.

Siku ya 2 majira ya saa 3 asubuhi ananipigia kuwa kafika ila mwenyeji wake hajatokea stand. Haelewi cha kufanya na hajui anaishije!!!
Mimi niko job mida hiyo, thanks to my daily routines zinaniruhusu kutoka nje ya kituo cha kazi hata kwa siku nzima. My colleague had a car back then, nikamwambia anidrop mahali nilikomwelekeza dogo. Alikosea, akashuka kituo cha nyuma sana ikabidi apande tena gari mpaka akafika.

Nilimpokea ilikua ishafika saa 5, kwa namna alivyokuwa kama si ndugu yako akikusogelea unaweza kumkimbia. Alikua kachafuka sana. Hapo sijamhoji lolote. Nikaongozana naye kuelekea kituo cha daladala. Njiani akaniambia bro nna kiu sana nisaidie maji. Nikamnunulia maji. Hapa nikaanza kupata wasi wasi huyu hana hata 100.
Nikashuka naye kituoni, kabla ya kufika home nikaingia naye mgahawani kwanza. Nilishahisi ana njaa pia..... Nikamuagizia ugali na samaki. Akaniambia bro huu ugali mbona mdogo sana, nikamwita mhudumu nikamwambia alete ugali mwingine. Sikushangaa kula yake.....ukiachilia mbali tabia ya watu wa vijijini kula sana, baba yake anakula sana na hutambulika na sifa hiyo karibia kijiji chote. Hata yale mashidano ya kipuuzi ya kula kula keshafanya wakati huo akiwa janki. Hivyo niliwaza naye huenda karithi. Naye aliniambia "baba ugali kama huu anakula hata sahani 5". Nikasema kweli, ila hajambo mzee, akaitikia hajambo huku akiendelea kukata matonge. Sina kumbukumbu kama niliagiza chochote kwenye vinywaji lakini sikuagiza chakula per se.

Alipomaliza, nikampeleka nyumbani kwangu. Hapakuwa mbali na pale tulipokuwa. Hapo nimefura nna hasira ameshaniharibia ratiba nzima ya siku. Na jioni niandae report ya kazi, ambayo kimsingi sijafanya.
Itaendelea.......
 
Hilo neno ulilomaliza nalo hapo mwisho linadhihirisha wewe ni chocol (shoger)
 
Mliozaliwa kijijini Mna tabu kweli Alhmdullillah familia yangu yote ipo town

Sent from my SM-A047F using JamiiForums mobile app
 
Nimegawa likes kama njugu

Sent from my SM-A047F using JamiiForums mobile app
 
Tusameheni wakuu...

Siku nyingine tukitaka kuja huko Daslaam tutatoa taarifa mapema.

Saint Anne
Huwezi ukawaacha ndugu zako barabarani
Huo ni uchawi😂

Ila sasa watoe tu taarifa mapema ili uandae mapokezi....

Wale ndugu zetu wa karibu zaidi wanaelewa ratiba zetu,,
Ila wengine ambao si wa karibu sana hawajui hata hekaheka za vibarua vya kausha damu Kwa muhindi..
Anachojua yeye ni kukulaumu tu kuwa ulituma mtu aende kumpikea,hukwenda mwenyewe ...ama umempikia chakula hakieleweki,,wakati amekuja ghafla .


Na hapo akikaa atalalamika kuwa haukumsindikiza matembezini kwake.. hajui unavyostruggle vibaruani Kwa muhindi hakuna off🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…