Hiki ndiyo kituko nlichowahi kukutana nacho makaburini usiku. Sitosahau

Hiki ndiyo kituko nlichowahi kukutana nacho makaburini usiku. Sitosahau

Enzi zangu nilivyokua napenda ujinga ujinga siku moja Nilikua dodoma Area A nikawa naenda kupanda daladala kwaajili ya kuelekea Fourways njiani kuna sehem moja kuna makaburi ilikua ni jion giza limeanza kuingia, wakati nakatiza pale makaburini nyuma yangu nikaona wadada wawili wanatembea haraka kuniwahi ili tuvuke wote

Walivyofika wakawa wanatembea nyuma yangu tukasalimiana wakaniambia bora hata wameniona maana walikua wanaogopa kuvuka makaburini peke yao mi nikawajibu msijali hata mimi nilivyokua hai kama nyie nilikua naogopa sana kupita makaburini

Walikimbia hadi mimi mwenyewe nikaogopa nikaanza kukimbia pia
Hapo hata mimi ningekukimbia nikuache peke yako makaburini kwako 😂😂😂
 
Niaje waungwana,

Hiki kisa, au tukio lilintokea miaka mingi kidogo. Enzi zile za kwenda kuangalia movie katika vibanda vya video. Sasa siku hiyo nilienda kuangalia video katika banda moja nililokuwa napenda kwenda kuangalia.

Banda hilo lilikuwa maeneo ya Manzese Midizini kwa mama fulan jina kapuni, na mimi home ni maeneo ya Magomeni mikumi jijini Dar es salaam.

Njia yangu kubwa kutoka home hadi Midizini, ilikuwa kagera kimamba, nakatiza daraja la mbao, napandisha pale Mburahati Mianzini, napasua Makaburi ya Mburahati kwa jongo hadi midizini. Na kurudi i was doing the same thing kwa kufuata njia ile ile niliyokuja nayo.

Ratiba yangu kwa siku ilikuwa ni shule kwanza, nlipotoka shule, nlielekea mazoezini (mpirani), baada ya kutoka mpirani ndo nikawa naenda sasa kujipoza vibandani kumuangalia Dharmendra, Amita Bachan, Rambo, Anord, Bruce Lee nk.

Ratiba yangu ya mwisho baada ya kutoka huko katika banda la video, ilikuwa ni kwenda katika maskani yetu fulan ambayo ni ya uncle wangu kujifunza mchezo wa karate. Uncle ndo alikuwa masta wetu. Hivyo nilijiamini sana kwamba hakuna kitu au mjinga yeyote anaeweza kunifanyia ushen.z.i mbele yangu. Karate na ngumi ni michezo ambayo humfanya mchezaji ajiamini sana, kwamba anaweza kupambana na mtu yoyote, mahali popote na kwa muda wowote.

Basi bwana siku hiyo nimemaliza kumuangalia Dharmendra mida ya usiku, nakumbuka ilikuwa movie fulan inaitwa LOHA. Tukatoka kila mtu akawa anaelekea kwao. Mimi nikawa natambaa mdogo mdogo kuelekea home.

Nilivyofika katika makaburi ya mburahati kwa jongo kama kawaida yangu, nikageuka nyuma kuangalia huku na huko, sikuona mtu ananifuata nikaendelea na safari yangu.

Sasa nimesogea sogea hadi katikati ya makaburi, kwa mbele nikaona kitu kama mbuzi mweupe, lakini kilichonishangaza na kunitia hofu ni kwamba yule mbuzi alikuwa kama vile amekaa kwenye kitu anavuta sigara, nikafikicha macho kama vile siamini ninachokiona.

Nikaendelea kusogea taratibu ili nihakikishe kuwa ninachokiona ni chenyewe au.

Kusogea nikasikia mbuzi anakohoa, ikabidi nigeuke ili nitoke nduki maana niliona pale hata karate zangu haziwezi kunisaidia.

Sasa wakati nageuka nikaona nyuma yangu kuna kundi la watu wamebeba jeneza wanakuja upande wangu halafu juu ya jeneza kuna mtu kakaa na yeye anavuta fegi, halafu kila jamaa wakipiga hatua, yeye anajamba.

Nikaona nyuma hakufai bora huku huku nilipotaka kupakimbia. Nikageuka na kuanza kutoka nduki kuelekea kwa mbuzi anaevuta sigara. Ghafla nikaona na mbuzi na yeye anatoka nduki na sigara yake.

Akili ikanijia nikaacha kukimbia ule upande anakimbilia mbuzi, nikaelelea upande wangu.

Breki ya kwanza ikawa Magomeni Mapipa, yani sikumbuki hata mikumi home nilipapita saa ngapi, au kule Mapipa nilifika fikaje fikaje.

Nikarudi nyumbani salama. Toka siku hiyo sikurudi tena kwenda video usiku, na ukawa mwisho wa kuendekeza movie.

Ni nani mwngine ambae ashawahi kukumbana na songombingo la aina hiyo?

Aisee it was scary
Ulikutana namasizimwe mdogo angu🤣🤣
 
Niaje waungwana,

Hiki kisa, au tukio lilintokea miaka mingi kidogo. Enzi zile za kwenda kuangalia movie katika vibanda vya video. Sasa siku hiyo nilienda kuangalia video katika banda moja nililokuwa napenda kwenda kuangalia.

Banda hilo lilikuwa maeneo ya Manzese Midizini kwa mama fulan jina kapuni, na mimi home ni maeneo ya Magomeni mikumi jijini Dar es salaam.

Njia yangu kubwa kutoka home hadi Midizini, ilikuwa kagera kimamba, nakatiza daraja la mbao, napandisha pale Mburahati Mianzini, napasua Makaburi ya Mburahati kwa jongo hadi midizini. Na kurudi i was doing the same thing kwa kufuata njia ile ile niliyokuja nayo.

Ratiba yangu kwa siku ilikuwa ni shule kwanza, nlipotoka shule, nlielekea mazoezini (mpirani), baada ya kutoka mpirani ndo nikawa naenda sasa kujipoza vibandani kumuangalia Dharmendra, Amita Bachan, Rambo, Anord, Bruce Lee nk.

Ratiba yangu ya mwisho baada ya kutoka huko katika banda la video, ilikuwa ni kwenda katika maskani yetu fulan ambayo ni ya uncle wangu kujifunza mchezo wa karate. Uncle ndo alikuwa masta wetu. Hivyo nilijiamini sana kwamba hakuna kitu au mjinga yeyote anaeweza kunifanyia ushen.z.i mbele yangu. Karate na ngumi ni michezo ambayo humfanya mchezaji ajiamini sana, kwamba anaweza kupambana na mtu yoyote, mahali popote na kwa muda wowote.

Basi bwana siku hiyo nimemaliza kumuangalia Dharmendra mida ya usiku, nakumbuka ilikuwa movie fulan inaitwa LOHA. Tukatoka kila mtu akawa anaelekea kwao. Mimi nikawa natambaa mdogo mdogo kuelekea home.

Nilivyofika katika makaburi ya mburahati kwa jongo kama kawaida yangu, nikageuka nyuma kuangalia huku na huko, sikuona mtu ananifuata nikaendelea na safari yangu.

Sasa nimesogea sogea hadi katikati ya makaburi, kwa mbele nikaona kitu kama mbuzi mweupe, lakini kilichonishangaza na kunitia hofu ni kwamba yule mbuzi alikuwa kama vile amekaa kwenye kitu anavuta sigara, nikafikicha macho kama vile siamini ninachokiona.

Nikaendelea kusogea taratibu ili nihakikishe kuwa ninachokiona ni chenyewe au.

Kusogea nikasikia mbuzi anakohoa, ikabidi nigeuke ili nitoke nduki maana niliona pale hata karate zangu haziwezi kunisaidia.

Sasa wakati nageuka nikaona nyuma yangu kuna kundi la watu wamebeba jeneza wanakuja upande wangu halafu juu ya jeneza kuna mtu kakaa na yeye anavuta fegi, halafu kila jamaa wakipiga hatua, yeye anajamba.

Nikaona nyuma hakufai bora huku huku nilipotaka kupakimbia. Nikageuka na kuanza kutoka nduki kuelekea kwa mbuzi anaevuta sigara. Ghafla nikaona na mbuzi na yeye anatoka nduki na sigara yake.

Akili ikanijia nikaacha kukimbia ule upande anakimbilia mbuzi, nikaelelea upande wangu.

Breki ya kwanza ikawa Magomeni Mapipa, yani sikumbuki hata mikumi home nilipapita saa ngapi, au kule Mapipa nilifika fikaje fikaje.

Nikarudi nyumbani salama. Toka siku hiyo sikurudi tena kwenda video usiku, na ukawa mwisho wa kuendekeza movie.

Ni nani mwngine ambae ashawahi kukumbana na songombingo la aina hiyo?

Aisee it was scary
Ulitakiwa utulie kwenye kiba-dachi au juchum seogi, hapo ungeona jinsi wanavyosepa mbio na kukuachia makaburi
 
Hawaniwezi
Ukiona hivyo ujue Mungu yuko upande wako.

Kipindi fulani nilienda Rufiji mwisho kabisa katika kijiji fulani kinaitwa mloka. Kutokana na ubovu wa barabara na mvua ilinyesha nyingi tukafika kule usiku kama saa 6 hivi.

Japo ilikuwa usiku na tuliruhusiwa kulala ndani ya gari, lakini mimi sikutaka kulala ndani ya gari, nikaona bora niende kulala katika gesti ya karibu alafu asubuhi niendelee mpaka kijijini. Gesti ya pale stand ilijaa hivyo nikapata nyingine ya pembeni kidogo na stand.

Nimeoga nikaingia ndani kujipumzisha huku nachungulia chungulia JF kama ilivyo kawaida yetu members. Ilipofika mida ya 7 na nusu nikaanza kuhisi nywele kusisimka, alaf kama vile nahisi nimekaa na watu ila siwaoni. Nikawa siijali ile hali nikahisi labda ni hali ya mchoko tu anbayo imesababisha akili nayo ichoke. Baadae nikaona mlango wangu unafunguliwa, na wakati nilifunga kwa ndani. Ila baada ya kufunguliwa sikuona mtu anaingia. Nikanyanyuka taratibu kuelekea mlangoni ili kuchungulia na kujua ni nani aliefungua mlango ule.

Sikuona mtu nikaufunga, nikarudi kitandani. Ghafla nikaona kitanda changu kishakuwa upande mungine wa dirisha, nikasema msinitanie, nikatoka nje nikaenda kukaa katika kibaraza kilicho karibu na dirisha langu alafu nikachukua sim nikaweka movie ya X (porn) nikaweka kasauti kakubwa kidogo, nikawa naongea mwenyewe nasema kama kuna mtu anataka kuangalia na mimi hii movie ruhusa.

Kumbe wale jamaa wakiwa katika mambo yao huwa hawapendi mambo ya kijinga jinga namna hiyo. Nikasikia bonge la msonyo alafu eneo likawa kimya. Mimi sikurudi ndani wala sikulala. Ilipofika saa 11 alafajir, nikaoga na kuondoka zangu kuelekea kijijini.

Nilipowaeleza wenyeji wangu, wakasema jamaa walikuwa wanakuja kukupima, ila wakagundua kuwa wanaempima mwenyewe ameshavurugwa tayari na maisha. So wakaamua kwenda kumtafuta mnyonge mungine kule katika gest ya stand 😂😂😂
 
Sisi tulikua tunatoka bagamoyo kumzika jirani yetu. Kufika njiani tukakuta pembeni ya barabara kuna fimbo ina kofia. Jamaa mmoja akasema hapa kuna mzee anataka kwenda mjini (Dar) hivyo hii fimbo ni saini ya kuonesha kuwa gari itakayoanza kufika hapa na kuona fimbo na kofia hii isimame kumsubiri huyo mzee aje apande tuende nae.

Dereva wetu alivyosikia vile akataka asimame kumsubiri huyo mzee ambae hata yeye alikuwa hamjui. Sisi tukaanza kupiga kelele kuwa asisimame maana wengine tunachelewa katika shughuli zetu, dereva akatusikia akaendelea.

Kufika mbele kabla ya kufika katika mpaka wa Dar na Bagamoyo gari yetu ikaacha njia, tukaenda kulivamia bonge la mti dereva hapo hapo akakata moto, i mean akafariki.

Haya mambo sio poa
Hayo mambo ya bagamoyo nilikuwa nayasikia ila sikuwa nayaamini hata kidogo. Kumbe kweli yapo.
So sad...
 
OIG (22) (2).jpeg
 
Back
Top Bottom