Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
basi sawaUkijua kujipangia muda wa kufanya kile unachokitaka, mbona ni kawaida tu kaka.
Kweli mkuuKama Mungu hajakuwekea ulinzi wake, hauwezi kusavaivu attack zao hawa wajinga.
Pole sana ndugu, hivi viumbe nasikia huwa vinapenda kucheza na akili zetu. Sasa kama hukushtuka mapema inakula kwako.🤣🤣🤣We Toka lini mbuzi Kavita kafegi ulitaka kuuvaaa mtumbwi wa vibwengo Mshukuru Mungu kujupa akili yakupita njia yako maana ndio ulikua unaondoka hivo iliwainikuta. Iyo miaka ile tunasoma nawai namba shule mwali mwenyew mwananzo mwisho fimbo haambiwi kumbe nimeamka saa tisa nasema saa kumi na mbili nilikutana na jitu ilo mitaa ya shule mzee chini linakwato za ng'ombe aseee nikicheki juu sioni mwisho ilibidi tukatafute mlinzi wapi yupo kumbe nae alikiona weeee tangu siku ile tulilipoti kwa mkuu washule ikatangazwa sikuwai kuwaishule tn ilibidi nikubaliane na viboko🤣
Siku hiyo baada ya mazoezi ya karate, ulivuta bangi kidogo?Niaje waungwana,
Hiki kisa, au tukio lilintokea miaka mingi kidogo. Enzi zile za kwenda kuangalia movie katika vibanda vya video. Sasa siku hiyo nilienda kuangalia video katika banda moja nililokuwa napenda kwenda kuangalia.
Banda hilo lilikuwa maeneo ya Manzese Midizini kwa mama fulan jina kapuni, na mimi home ni maeneo ya Magomeni mikumi jijini Dar es Salaam.
Njia yangu kubwa kutoka home hadi Midizini, ilikuwa kagera kimamba, nakatiza daraja la mbao, napandisha pale Mburahati Mianzini, napasua Makaburi ya Mburahati kwa jongo hadi midizini. Na kurudi i was doing the same thing kwa kufuata njia ile ile niliyokuja nayo.
Ratiba yangu kwa siku ilikuwa ni shule kwanza, nlipotoka shule, nlielekea mazoezini (mpirani), baada ya kutoka mpirani ndo nikawa naenda sasa kujipoza vibandani kumuangalia Dharmendra, Amita Bachan, Rambo, Anord, Bruce Lee nk.
Ratiba yangu ya mwisho baada ya kutoka huko katika banda la video, ilikuwa ni kwenda katika maskani yetu fulan ambayo ni ya uncle wangu kujifunza mchezo wa karate. Uncle ndo alikuwa masta wetu. Hivyo nilijiamini sana kwamba hakuna kitu au mjinga yeyote anaeweza kunifanyia ushen.z.i mbele yangu. Karate na ngumi ni michezo ambayo humfanya mchezaji ajiamini sana, kwamba anaweza kupambana na mtu yoyote, mahali popote na kwa muda wowote.
Basi bwana siku hiyo nimemaliza kumuangalia Dharmendra mida ya usiku, nakumbuka ilikuwa movie fulan inaitwa LOHA. Tukatoka kila mtu akawa anaelekea kwao. Mimi nikawa natambaa mdogo mdogo kuelekea home.
Nilivyofika katika makaburi ya mburahati kwa jongo kama kawaida yangu, nikageuka nyuma kuangalia huku na huko, sikuona mtu ananifuata nikaendelea na safari yangu.
Sasa nimesogea sogea hadi katikati ya makaburi, kwa mbele nikaona kitu kama mbuzi mweupe, lakini kilichonishangaza na kunitia hofu ni kwamba yule mbuzi alikuwa kama vile amekaa kwenye kitu anavuta sigara, nikafikicha macho kama vile siamini ninachokiona.
Nikaendelea kusogea taratibu ili nihakikishe kuwa ninachokiona ni chenyewe au.
Kusogea nikasikia mbuzi anakohoa, ikabidi nigeuke ili nitoke nduki maana niliona pale hata karate zangu haziwezi kunisaidia.
Sasa wakati nageuka nikaona nyuma yangu kuna kundi la watu wamebeba jeneza wanakuja upande wangu halafu juu ya jeneza kuna mtu kakaa na yeye anavuta fegi, halafu kila jamaa wakipiga hatua, yeye anajamba.
Nikaona nyuma hakufai bora huku huku nilipotaka kupakimbia. Nikageuka na kuanza kutoka nduki kuelekea kwa mbuzi anaevuta sigara. Ghafla nikaona na mbuzi na yeye anatoka nduki na sigara yake.
Akili ikanijia nikaacha kukimbia ule upande anakimbilia mbuzi, nikaelelea upande wangu.
Breki ya kwanza ikawa Magomeni Mapipa, yani sikumbuki hata mikumi home nilipapita saa ngapi, au kule Mapipa nilifika fikaje fikaje.
Nikarudi nyumbani salama. Toka siku hiyo sikurudi tena kwenda video usiku, na ukawa mwisho wa kuendekeza movie.
Ni nani mwngine ambae ashawahi kukumbana na songombingo la aina hiyo?
Aisee it was scary
Eti mwendo wa ferari nimecheka mbavu hoi,🤣🤣🤣Pole sana ndugu, hivi viumbe nasikia huwa vinapenda kucheza na akili zetu. Sasa kama hukushtuka mapema inakula kwako.
Mimi nilijiongeza mapema, kwa sababu nilishangaa iweje kibwengo awakimbie vibwengo wenzie, hapo lazima kuna jambo limepangwa dhidi yangu, hivyo mimi nikakunja kulia huku nikiruka makaburi kwa mwendo wa ferari.
Nahisi hata mbuzi mwenyewe alipogeuka hakujua nimepotelea upande gani, aliambulia kuona vumbi tu 😂😂😂
Mbona unashtuka dear mbona makaburi yale ya kinondoni malaya ndio vitanda vyaoMmmmh
Kipindi iko Malaya wakiwa na hofu ya Mungu saivi upwiru unakatiwa paleMbona unashtuka dear mbona makaburi yale ya kinondoni malaya ndio vitanda vyao
🤣🤣Manina nimecheka 😂😂😂 una uhakika ulikuwa huvuti ?
🤣🤣🤣🤣🤣Wacha nicheke tu siku iwe murwaaaaaaaaaNingekuwa mzembe wangeenda kunifanya mishikaki 😂😂😂
Walikuwa wanakuelewa sana. Ndio maana hukuona kitu.....Haya makaburi ya kwa jongo hayana wachawi zaidi ya usiku kujaa waganga wa kienyeji wakiwa na wateja wao mfano mganga wa diamond uwa ndio eneo lake la kuwatibia wasanii na mbuzi wapo wengi sana wamejaa pale makaburini wanazaliana mpaka leo hawana mmiliki kwani wenyeji wana waogopa kuwachukua ,wanadai wamesomewa albadili.
Mimi kipindi cha ujana nimekatiza sana hapo katikati ya makaburi tena muda mbaya saa 8 mpaka saa 9 nikitoka kwenye muziki kurudi nyumbani zaidi nilikua nakutana na waganga wakiwa na wadada au wamama.mji huu watu wanaishi kwa mambo ya ajabu sana.
Sio kukuteka sababu wangehitaji kukufanya vibaya bado ilikua simple tuu,inshu waliona umeshaleta mazoea na viwanja vyaoHiyo ninayokwambia mimi imetokea miaka ya 90. Alafu haya mambo hutokea pale ambapo mtu hukutarajia.
Mimi mwenyewe kama unavyosema, nilikuwa napita sana usiku yani ndio ilikuwa njia yangu ya kila siku. Sasa siku ile nahisi vibwengo walikuwa washachoka kunivumilia kupita pale, wakaamua kutaka kuniteka ndo nikatoka nduki.
Wavutaji watakuwa wanapata raha. Huona dunia ingine kabisa!!
Utandawazi umetawanya maadili haswaaaAsubuhi unakuta condom kibao pemben ya makaburi.