Hili la kufungwa barabara limekaaje? Kwa namna hali ilivyokuwa leo kwenye usafiri maeneo ya Posta na Kivukoni mpaka ifike hiyo tarehe 30 tutakuwa hoi

Hili la kufungwa barabara limekaaje? Kwa namna hali ilivyokuwa leo kwenye usafiri maeneo ya Posta na Kivukoni mpaka ifike hiyo tarehe 30 tutakuwa hoi

Mkuu hufungwa kwa muda tu, pale msafara wa viongozi wanapotaka kupita, na ni kwa wale wenye vyombo vya moto na baiskeli tu, kwa watembea kwa miguu huruhusiwa kuendelea na shughuli zao kama kawaida, baada ya msafara kupita na askari wa usalama barabarani kujiridhisha kuwa hakuna ratiba nyingine ya msafara wa viongozi basi barabara hufunguliwa mara moja kuendelea na shughuli za kiuchumi, nimeona kwa macho yangu hapa Keko mataa, msafara unapita Nyerere road kutoka Nyerere Air port na kupita barabara ya kati ya mwendokasi kuelekea IKUL.U haupiti juu ya (fly over) daraja.
Kwahio barabara hazitafungwa siku nzima?
 
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam imetangaza kuwa Barabara tisa Jijini Dar es Salaam, zimefungwa kwa siku sita kuanzia leo Januari 25 hadi Januari 30, 2025 ili kupisha misafara ya viongozi wanaokuja kutoka nchi mbalimbali kuhudhuria mkutano wa Nishati Afrika.

Taarifa ya Polisi iliyotolewa leo Jumamosi Januari 25,2025 na Kamanda Kanda Maalumu ya Polisi Dar es Salaam, Jumanne Muliro, imesema Mkutano huo utakaofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Januari 27 hadi Januari 28, 2025, unatarajiwa kuhudhuriwa na zaidi ya marais 25 na mawaziri 60 kutoka nchi mbalimbali za Afrika ambapo pia bajaji na bodaboba hazitaruhusiwa kuingia katikati ya Jiji katika kipindi chote ambacho mkutano huo utakuwa ukifanyika.

Barabara zitakazofungwa ni pamoja na Barabara ya Nyerere kutokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwenda katikati ya Jiji, Barabara ya Sokoine, Kivukoni na Lithuli kuanzia taa za Gerezani kwenda Hoteli ya Johari Rotana, Hyatt Regency hadi Ikulu; Barabara ya Ohio kutokea Kivukoni kwenda Hoteli ya Serena na Barabara ya Ghana kutokea barabara ya Ohio kwenda Hoteli ya Onomo

Zingine ni Barabara ya Bibi Titi kutokea makutano ya barabara za Ohio na Ally Hassan Mwinyi kwenda Hoteli ya Crowne; Barabara ya Azikiwe kwenda Hoteli ya Four Points, Hoteli ya Golden Tulip City Center na Hoteli ya Holiday Inn; Barabara ya Morogoro kutokea Sokoine kwenda Hoteli ya Tiffany No. 1; Barabara ya Makunganya kutokea Azikiwe kwenda Hoteli ya Tiffany No. 2 na Barabara ya Garden kutokea barabara ya Lithuli kwenda Hoteli ya Southern Sun pamoja na Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa JNICC.
Dipresheni hama huo mkoa.
 
Mkuu hufungwa kwa muda tu, pale msafara wa viongozi wanapotaka kupita, na ni kwa wale wenye vyombo vya moto na baiskeli tu, kwa watembea kwa miguu huruhusiwa kuendelea na shughuli zao kama kawaida, baada ya msafara kupita na askari wa usalama barabarani kujiridhisha kuwa hakuna ratiba nyingine ya msafara wa viongozi basi barabara hufunguliwa mara moja kuendelea na shughuli za kiuchumi, nimeona kwa macho yangu hapa Keko mataa, msafara unapita Nyerere road kutoka Nyerere Air port na kupita barabara ya kati ya mwendokasi kuelekea IKUL.U haupiti juu ya (fly over) daraja.
Hiyo ya hivyo naifaham, hii ya kuwatoa maafisa usafirishaji kwenye maeneo yao ya kazi ni mateso kwetu wasafiri.
 
Wala sishangai kwa waafrika kukurupuka bila maandalizi
Mwingine nae kabeba vifagio kwenda kufagia barabara

Wao walipokuja UK na kupakiwa kwenye mabasi hawakuona traffic zilikuwa zinaenda tu kila mahali?
Yaani siku zote hizo kweli No hurry in Africa

"Black people are not complete human beings because they don't have a good brain to govern the society as White people. They are still under the process of becoming the complete human beings."

Pieter W. Botha, a former President of South Africa during the Apartheid era.
 
Fyi
 

Attachments

  • IMG-20250126-WA0024.jpg
    IMG-20250126-WA0024.jpg
    174.8 KB · Views: 1
Wamekurupuka hawakufanya tathimini ni barabara zipi zifungwe. Mbona ni rahisi kupanga road pattern kwa misafara ya viongozi hao? Hizo siku itakuwa kero kubwa wa wakazi wa jiji la dar, wavumilie tu hakuna namna
Tupe wewe pattern zako
 
Back
Top Bottom