Hili suala la nembo kwa jezi mpya ya Yanga ipoje?

vibertz

JF-Expert Member
Joined
Mar 15, 2022
Posts
2,474
Reaction score
4,726
Ninaipongeza klabu ya Yanga kwa kuendelea kufanya vizuri kwenye ku design jezi. Jana zimezinduliwa jezi za kiwango haswa mpaka mashabiki wa Simba wakizitamani. Lakini moja ya jambo ambalo kwangu ni tata ni ishu ya logo ya main sponsor wa mashindano ya Caf inter club ambaye ni total energies.

Ukiangalia logo ambayo Yanga wameiweka kwenye jezi mpya haina rangi halisi ya logo ya Tota energies kwenye nyekundu wameiweka zambarau hivi, kwa waliofanikiwa kuiona jezi live mnaweza kuliweka sawa hili pengine picha ya jezi imenipotosha kukawa na rangi sahihi ya main sponsor.

Kama ikiwa ni kweli ipo hivyo kama ilivyokuwa kwenye picha je hakutakuwa na shida yoyote? Viongozi wa Yanga waliomba ufafanuzi huko CAF na kuonekana hakuna shida? Isije jitihada zote zinazofanyika kwaajili ya michuano ya shirikisho ikaja kukwamishwa na jambo dogo la logo kwa kukwepa wekundu.

 
Yanga hawana legal counsel, yani ni club inayojiendesha kienyeji hawaelewi kuwa Total wanaweza kuwaburuza kizimbani na kuwalipa mabilioni ya hela kwa kuchezea logo yao.

Unafikiri Total anatoa kiasi gani kwa CAF halafu wapuuzi fulani wachezee tu brand ya kimataifa kwa utopolo wao?
 
Ujuaji mwingi kumbe huna unalo jua, umeiona hio jezi? Yanga ni hawajasoma terms za mashindano? total energies wana rangi ngapi kwenye logo yao?
 
Mmetafuta sababu za kukosoa jezi mmekosa mmetafta logo ilimradi tu mpate ahueni
 
PUNGUZA UJUAJI MZEE...

PUNGUZA UJUAJI

TAFITI KWANZA NDO USEME JAMBO.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…