Chouder
JF-Expert Member
- Mar 29, 2023
- 558
- 876
Ni kawaida kujiuliza hivo vijiswali...mtu anapopata kitu huwashangaa wasionacho,mimi nikiwa kwenye gari nawashangaa watembea kwa mguu,nikipata siti kwenye daladala nawashangaa waliosimama,nikila kuku nawashanga waliokula mihogo,nikivaa nguo mpya nashangaa waliovaa kukuu so that is life alienacho anamshanga asiyenacho.Wadau salaam.
Naamua mpo safii kabisa, kwa wenye changamoto basi ni dua zangu Mungu akufanyie wepesi.
Kabla sijaingia katika mahusiano swali langu kichwani lilikua " hivi hawa watu wanaitana wapenzi, nini wanaenjoy na vipi wana feel kufuatana fuatana....!?!?!"
Sikupata jawabu zaidi ya kuona ni kupotezeana time na umakini wa kupambana na maisha.
Muda umeenda huku na huku nimejipata ndani penzi zito. Mind you ni serious relationship nikiwa na utimamu wa akili kama ilivokua awali kabla sijajiingiza huko.
Jinsi nimeishi na kuintertain mapenzi nikajipata narudia swali lilelile lakini katika muktadha wa tofauti kidogo. " Hivi hawa watu wanaoishi Single yani bila mpenzi wanaishi je?!? " Hapa nikasahau kama nilikua naona mapenzi ni upumbavu wa kupotozeana time tu na focus.
Hii issue ya kujiuliza Hivi kundi flani linaishije katika mazingira flani inafanya wakati flani nicheke huku nikitafakari nini hasa huwa sikielewi katika hali zote mbili.
Wadau Imekaaje hii...?