Hip Hop Diss Tracks: Dizasta Vina amjibu Rapcha

Hip Hop Diss Tracks: Dizasta Vina amjibu Rapcha

Nioneshe verse gani hapa imekosa vina

Dizasta Vina
Hatia iii Lyrics
Ah...
Nakusalimu mwafrika...nakusalimu habari gani.../
Nikaribishe tuketi...niseme yaliyo ndani.../
Sahau kuhusu hadithi za kale...za upendo wako.../
Nataka leo tukae...tuijadili kesho yako.../
Kutoka kupiga ramli...na kutii mizimu.../
Umeanza kufata amri...za TV na simu.../
Na ubaya ni kwamba...umeanza kuikacha sanaa.../
Na kufata siasa...ambayo inakulaza na njaa.../
Na kila unachokiona...unataka kubeba.../
Vichache vimekushinda...na unapanga kuongeza.../
Juzuu,Katekisimu mpaka Novena.../
Sio zako...zako zilikuwa ni kutamba ngojera.../
Umezubaa...majirani wameanza kufika kwako.../
Na unaamini kuwa...watakubebea shida zako.../
Kwa sababu ya ujinga,umezidi umasikini.../
Unamjengea jirani...kwako unachimba unabaki chini.../
Zamani...ulikuwa una sembe ya kusaza.../
Uliabudu kazi...ukaliweka jembe kwenye shamba.../
Ghafla ukauza panga...ukapamba jembe kwenye kabati.../
Ukanunua kioo ujirembe...ili uende na wakati.../
Ume...chagua urembo na umetupa werevu.../
Umeuza mifugo...unafuga kucha na ndevu.../
Familia iwe...mwafrika uzame mitini.../
Au uombe msaada..wakati unakufa na fasheni mwilini.../
Mwafrika..una mzigo mkubwa wa madeni.../
Hauna mali ..ardhi yako ni 'future ya wageni.../
Unalala ndani...kungoja hisani ya wenye nguvu.../
Nyumba iko wazi..wewe uko ibadani unaabudu.../
Ujasili ni kujimudu...mwafrika haujui hili.../
Umejaliwa nguvu...na unashindwa kuzihimili.../
Unavamia diplomasia..unatunga hotuba.../
Na hakuna mwenye hisia...kuwa upo nyuma ya muda.../
Ah..
unapoteza stadi za maisha.../
Kwa elimu ya magharibi...ikuweke ofisini suti kubwa..
ukumbatie dawati la nyazifa.../
Huku unauwa..nguvu kazi ya taifa.../
Umepitiliza nyumbani...hauna vituo.../
Umekuwa mtumwa wa sera zao,kiasi kwamba hauna 'future..
hauna dira,hauna lugha hauna nguo.../
Milango ya fahamu..imefungwa na ufunguo.../
Umepewa karatasi...ukaita jina pesa.../
Ukasubiri ikuletee furaha..ikakutesa.../
ukauza umoja...ukauza amani ukauza utu.../
Ukawashusha mashujaa wako..ukamwinua Yesu wa kizungu.../
Una kucha ndefu ..kushika chungu matusi.../
Hauwezi kuandika history..haumudu herufi.../
Ume-bleech nywele,mdomo mwekundu umebusu baruti.../
Nikuite nani...mwafrika mzungu au mzungu mweusi.../
Ah..
Unadanganywa...rangi yako sio nzuri.../
Ili utafute pesa...ukawaungishe vipuri.../
Ume-switch kutoka Mama Afrika...mpaka drama Queen.../
Una nunua TV...uone Afrika ikizama chini...!/
Mwafrika..umeshakosa mipango.../
Unajua kuchonga ngenga..badala ya kuchonga vinyago.../
Unaacha wanyama Mikumi,Serengeti unasafiri.. unaenda kushangaa ghorofa Chicago.../
Unarudi..unajikuta Mmarekani eti real nigga...!/
Mbona haulili bili nigga...?/
Jasiri..haiachi asili real nigga.../
Kamwe usijiite G nigga.../
Hauwezi kuwa warrior../
Unajua majina ya wasanii..kishinda historia.../
Unasahu mapishi..hauendi jikoni.../
Unakufa na ngoma mwilini...cheni shingoni.../
Kwa heshima na taadhima...unautunza Msaafu.../
Unatupa kitenge..kisha unafunga hijabu.../
Na ubaya ni kwamba...bado haujajua sababu.../
Unapewa Zaburi..utafakari mwenyewe wakichukua dhahabu.../
Ufeli majibu...uishie kubuni.../
Ushindane nani msafi...aende mbinguni.../
Mhanga wewe...rudi uzipitie kanuni.../
Umeshikishwa kitabu...wenzio wakushikie uchumi.../
Mwafrika...hii haikuingii nikichana.../
Unanuka sana...kiasi hauvutii kama Jana.../
Kiburi moyoni..haisikii unapokanywa.../
Unatia aibu..kiukweli sijivunii kuwa mwana.../
na bado unaamini..shahada ya shule ni zana.../
Haujui...ukitaka ule ni shamba.../
Unafunga ubongo...unafungua mikono ili wakupe msaada.../
umesahau kuwa...vya bure gharama.../
Mchezo wako...sheria zao utashindwa.../
Ukiishi porini..kama haiwindi..utawindwa.../
Inasikitisha..wenzako wanaigiza ili waishi...ila we unaishi kwa kuigiza sio...?/
umekuwa dekio..umekubali kuwa soko la pombe
na sigara.../
Soko la risasi bunduki na mabomu...
Soko la madawa ya kulevya..yanauwa waafrika wenzio.../
Soko LA dini zao..soko la picha za uchi .../
Soko la vitukukuziba sauti.../
Soko la sera unevu..na mifumo gombanishi...
Magonjwa batiri..unanunua dawa kwa kuhisi sio...?/
Umezagaa visingizio.../
Haujui akiba..ndio maana unashangaa salio.../
Umegeuzwa kifaa cha majaribio.../
imeandikwa..asiyeandaa silaha ataandaa mapambio.../
Mwafrika...
Nakupa nahau kalili.../
Afrika inakufa..mwafrika unadharau dalili.../
Unasahau wito..unafata mkumbo kwa dau batili.../
Unakumbuka kila kitu..na unasahau asili.../
Yote tisa, lets agree hapa, (na hapa ukibisha utakuwa mbishi)
Ni kweli rapcha kamfanya dizasta atrend
Saivi Tribulation ina views 24k kwa masaa 5...Dizasta hajawahi kuwa na hiyo traffic
 
Options zipo zaidi ya hizo mbili..ila Unajua kabisa hatuwez kulinganisha storytelling na hizi zingine. lets compare apples with apples.
Afu Fid Q sio kwamba zote ni majigambo
Mfano Roho huwezi kusema ni Majigambo ila sio story per se.

Hapa umeamua tu kujikata kichwa.
Sasa unarap kuhusu mapenzi unataka ujigambe kwa kipi?

Unashindwa hata kuzingatia muktadha?

Mimi nazungumzia aina ya rap yake jinsi ilivyo yani role yake, sijasema kila ngoma au hana ngoma ambayo ka rap nje ya hapo

Kuanzia Augost 13, Hip Hop, I'm professional kuja chini huko asilimia 85 ka rap majigambo

Na usini quote vibaya ukafananisha majigambo yake na hawa rappers wanaosifia mademu na pesa

Majigambo ya Fid Q yapo kwenye category ya MC, nadhani unaelewa utofauti kati ya Mc na rapper japo wote kwenge ku delivery wana rap
 
Yote tisa, lets agree hapa, (na hapa ukibisha utakuwa mbishi)
Ni kweli rapcha kamfanya dizasta atrend
Saivi Tribulation ina views 24k kwa masaa 5...Dizasta hajawahi kuwa na hiyo traffic
Hata Dizasta kamsaisia Rapcha kutrend

Unafikiri kabla ya hizi diss huyo Rapcha alikuwa anafikisha hizi numbers kwa muda mfupi kama anavyopata kwenye hizi diss?
 
Sasa unarap kuhusu mapenzi unataka ujigambe kwa kipi?

Unashindwa hata kuzingatia muktadha?

Mimi nazungumzia aina ya rap yake jinsi ilivyo yani role yake, sijasema kila ngoma au hana ngoma ambayo ka rap nje ya hapo

Kuanzia Augost 13, Hip Hop, I'm professional kuja chini huko asilimia 85 ka rap majigambo

Na usini quote vibaya ukafananisha majigambo yake na hawa rappers wanaosifia mademu na pesa

Majigambo ya Fid Q yapo kwenye category ya MC, nadhani unaelewa utofauti kati ya Mc na rapper japo wote kwenge ku delivery wana rap
Ngoma kama kiberiti,Mafanikio,Ulimi mbili,sihitaji marafiki,ielewe mitaa,propaganda...nk. nk. zote sio majigambo.
au unamaanisha nini unaposema majigambo? Naona kama majigambo ni box dogo sana unalotaka kumuweka fid.

Anyway...hayo 'majigambo' ya fidq ni level moja na Dizasta?
 
Hata Dizasta kamsaisia Rapcha kutrend

Unafikiri kabla ya hizi diss huyo Rapcha alikuwa anafikisha hizi numbers kwa muda mfupi kama anavyopata kwenye hizi diss?
Tusisahau rapcha ana hitsong lisa.
Unazijua numbers za lisa?
Tusimung'unye mung'unye maneno, Rapcha yupo mainstream na anamsaidia kumleta Dizasta mainstream kupitia hizi diss.
Dizasta aspopita na huu upepo ndo bas tena.
Anatakiwa azichange sana karata zake hapa aende mainstream, ila kwa hizi pigo za ngoma ya dakk 11 ndo anafel
 
Ngoma kama kiberiti,Mafanikio,Ulimi mbili,sihitaji marafiki,ielewe mitaa,propaganda...nk. nk. zote sio majigambo.
au unamaanisha nini unaposema majigambo? Naona kama majigambo ni box dogo sana unalotaka kumuweka fid.

Anyway...hayo 'majigambo' ya fidq ni level moja na Dizasta?
Majigambo ni kujiongelea wewe mwenyewe kwa kujikweza zaidi

Kwenye Rap ipo ya namna mbili

Moja kujikweza kwenye mambo yako yanayokuhusu wewe binafsi mambo ambayo hayaigusi bila jamii (hii inafanywa na marapa)


Mbili kujikweza kwenye mambo ambayo yanamgusa kila mtu ndani ya jamii (hii inafanywa na ma MC)

No sina maana ya kumuweka kwenye eneo dogo Fid Q ila ni pale napojaribu kuonesha utofauti kati yake na Dizasta.

Fid Q pia kwenye kuizungumzia jamii pia ni kitu ambachi anakifanya kwenye kila wimbo ila namna anayotumia ku delivery ni mfumo flani hivi wa majigambo

Swala la level nimelikataa kuliongelea hata kwenye post yako ya juu

Ni kwamba hata ungesema Profesa Jay na Fid Q nani mkali bado nisingetoa jibu

Ila ukiniambia nifanye comparison ya kuangalia katika miaka hii nani katoa nyimbo kali naweza kusema flani katoa kali

Na ndio maana nimekuambia Fid Q wa mwisho ni yule kwenye Sumu
 
Fid Q dot Com huyo ndio alikua Fid,
Acha uongo we baba fid Q dot com Ni ya mwaka gani?????
Hapo n kabla hata hajatoa mwanza mwanza miaka Kama minne mbele... Na hakuna ngoma ya hip-hop hapa bongo itaigusa hiyo ngoma... Kwann utudanganye baadae akaja kutoa Mapini mengine makali Kama sihitaji marafiki, ielewe mitaa, Siri ya mtungi, bongo hip-hop na Sumu... Hizo zote zimetoka 2010+ kwanini useme uongo [emoji28]
 
Majigambo ni kujiongelea wewe mwenyewe kwa kujikweza zaidi

Kwenye Rap ipo ya namna mbili

Moja kujikweza kwenye mambo yako yanayokuhusu wewe binafsi mambo ambayo hayaigusi bila jamii (hii inafanywa na marapa)


Mbili kujikweza kwenye mambo ambayo yanamgusa kila mtu ndani ya jamii (hii inafanywa na ma MC)

No sina maana ya kumuweka kwenye eneo dogo Fid Q ila ni pale napojaribu kuonesha utofauti kati yake na Dizasta.

Fid Q pia kwenye kuizungumzia jamii pia ni kitu ambachi anakifanya kwenye kila wimbo ila namna anayotumia ku delivery ni mfumo flani hivi wa majigambo

Swala la level nimelikataa kuliongelea hata kwenye post yako ya juu

Ni kwamba hata ungesema Profesa Jay na Fid Q nani mkali bado nisingetoa jibu

Ila ukiniambia nifanye comparison ya kuangalia katika miaka hii nani katoa nyimbo kali naweza kusema flani katoa kali

Na ndio maana nimekuambia Fid Q wa mwisho ni yule kwenye Sumu
Wewe sema tu ulimchokea hapo
ila kuna ngoma kali kama mafanikio,kiberiti,imeisha nk.
 
Tusisahau rapcha ana hitsong lisa.
Unazijua numbers za lisa?
Tusimung'unye mung'unye maneno, Rapcha yupo mainstream na anamsaidia kumleta Dizasta mainstream kupitia hizi diss.
Dizasta aspopita na huu upepo ndo bas tena.
Anatakiwa azichange sana karata zake hapa aende mainstream, ila kwa hizi pigo za ngoma ya dakk 11 ndo anafel
Rapcha ana hit song ya Lisa kwanini hana hit song ya nyimbo zingine

Kwanini nyimbo zake zote zisiwe na hit song kama kweli kigezo cha hit song ni ubora na kuwa mainstream sana?

Hit song inaweza ikatokea hata kwa coincidence tu

Mwaka 2017 Darasa alikuwa na hitsong ya maisha na muziki ambayo ilimfunika hadi Diamond ambaye ni msanii wa mainstream kwa muda wote

Yule dada aliyeimba yerusalem unafikiri hana nyimbo zingine?

Ulifatilia Diss ya Mawenge kwa Nikki? Uliona views alizo gain kwa muda mchache tangu aachie ile diss

Kwa hiyo utasema zile numbers alibustiwa na Nikki kutokana na fame yake kwenye mainstream?
 
Wewe sema tu ulimchokea hapo
ila kuna ngoma kali kama mafanikio,kiberiti,imeisha nk.
Yap inaweza ikawa ni hoja kwasababu pengine nilichokuwa nakikubali kutoka kwake sikuwahi kukiona kwenye track zake mpya
 
Dizasta ametoa taarabu DK 11 za nn wakati Dk 2.30 zingetosha tu
 
Hapo n kabla hata hajatoa mwanza mwanza miaka Kama minne mbele
Yes kitambo hicho baba Fid hataki mchezo na jukwaa, ana hasira na Jukwaa balaa kabla hajatoa I am Professional,

dada zako wako wakiniona mtaani utasiki Fid Q/
Fid Q dot Com Mwanza ndio home
 
Hahahahhahaah we jamaa sijui Kama unajua unachokiongea....
Kwahiyo Dizasta Hana hit song ..
Umeiskiliza kanisa? Sister kadata, no body is safe, hatia, siku mbaya na SHAHIDI...

Kwanza n aibu Dizasta kubato na dogo Kama Raptcha ambaye hana punchline hata moja tangu aanze kuchana...
 
nakuhurumia kafifte kako usije laza familia njaa siku 3
Hahhahahah maneno ya nn anzisha Uzi lengo sio hiyo 50k uthibitishe we n mkali hata Simba ya Yanga hutumia mabilioni kushinda NBC tittle yenye hela kiduchu ya kumsajili tu Aziz Ki au Chama... Njo tubato utuoneshe unayoyasema
 
Back
Top Bottom