HipHop Fans: Ni underground rapper yupi ambaye anafanya vizuri kuliko baadhi ya mainstreams rappers?

HipHop Fans: Ni underground rapper yupi ambaye anafanya vizuri kuliko baadhi ya mainstreams rappers?

Boshoo Ninja anaflow tamu ila mistari ya kawaida sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Skuizi wauswazi wanaji mix nyuma hawataki kubaki, dada anajiongeza anajisogeza kwa fataki.../

Utaskia naitwa cindy home masaki, kumbe ni mwasiti wa keko magulumbasi.../

Ni wavivu wezi wanajua ku act, nacho wasifu hua hawaaribu kwenye scripts.../

Hali ni tight ila mmh tunaoumia ni sisi, maskini tutakufa na ukimwi uwanja wa fisi.../

Demu wako anaku-cheat na unajua, huna kitu sa ukiwa na wivu si atakuua.../

Una ishu sasa ndo maana unashindwa kuamua, ndo maana unakumbuka ile michezo alivyo kusisimua.../
 
Mi ndo

Mi niko ndani we ni mlinzi, ingia kwenye gemu we ni mshindani mi ni mshindi/

Ukiniona sizi usinichukulie kipimbi, wakati kitaani master naheshimika kama dingi/

Mi ni mfanya kazi we ni kazi nakufanya, hazichaniki maana hauna hadhi ya kuchana/


Tahadhari changa rambi rambi na dhamana, yakua ukaishi kwenye kambi za lawama/

Kule siskiki sishawishiki, kusaliti we ni mwanafunzi mi ndo shule ya muziki/

We ni mume mbona mke halidhiki, unajiita mcee na bado uko nje ya msingi/

Mi kibaka we ndo shingo ya kabali, mi ndo driver we ndo konda au tingo kwenye gari/

We kapuku mi na' bingo la mistari, ogelea kote dizasta ndio kingo za bahari/

Mi ndo tungo shazi nazisuka kama jamvi, we ndo pusha zungusha mi ndo mzuka kwenye nyasi/

Najua ku rythms ma mcee wanajua nini, vilio kila masta navyotua kwenye scene/

Nina mama bora,mama nuru,mama funzo, we ni mtumwa kwenye soko niko huru kwenye tungo/

Tukirudi class we ni good mi ni better, mulize kingo kitaani mi ni babuu we ni sheta/

Wauza sura wana ghani tu majina, wao majini kama kabula mi ndo shetani la vina/

Mi nimenuna bwege cheka na hii vocal, beat tope na dizasta mi ndo mega mining volvo

Mi ndo folder, mi ndo hoja, mi ndo mada kwenye somo kwenye jeshi mi ni mjeda

Mi ndo muosha naogesha midundo, niite dizasta wananiita profesa tungo
 
Salamu kwa kishkwambi, niko kambi na mangi huku hatubakishi nyagi.../

Nakumbuka wakati na balehe, nili wehuka nikawekwa kambi na wazee.../

Nipo kambi ya mieleka, we mdogo wangu we si upo kambi ya umiseta.../

Kambi ya majungu tunateta, hujui kuchana tunabeba mic tunasepa.../

Mwanajeshi unakitambi baki kambi, sisi tusongee ugali we kula tambi.../

Tuache twende vitani tukaue, we kaa kitandani usijisumbue.../

Kua naheshima dogo, na hivi nilivyo mfupi nala kama natokea kambi ya wakongo.../

Staki shobo kwaiyo acha kushoboka, unaongea sana kama mdomo wako umetoboka.../
 
Conversation ya shaolin senetor na dizasta

Shaoilini kacheza kama baunsa anayechukua pesa ya viingilio kwa ajili ya show ambayo inatumbuizwa ukimbini. Wakati dizasta kacheza kama tozi ambaye anafosi kuingia ndani na hana pesa ya kiingilio

Shauli seneta X dizasta

[Shaolin]
Panga mstari hapa mpaka kule, tiketi mkononi maana hakuna wakuzama bure//

Over 18 hichi sio kiwanja cha shule, kuweni makini hii ni kazi inayotufanya tule//

Oya tozi unaenda wapi hauna hela, na unaona foleni rudi nyuma upange tela//

[Dizasta]
We boya usiniguse unanichafua, ntalipaje hela wakati boss wako ananijua//

[Shaolin]
We bishoo acha masihara na kazi, au unataka mpaka tuanze shikana mashati//

[Dizasta]
Yeah jinsi mwili wako unakulaghai, na icho kifua mkate men dawa yake chai// eeh

[Shaoulin]
Tambua kua niko hapa kama mlinzi, na hii nayo ni kazi kwaiyo nacho hitaji shilingi//

[Dizasta]
Nini kazi? Kazi yenyewe ni ubaunsa, haufiki hata nusu ya mshahara wa kaunta//

[Shaolin]
Acha wenge wewe ni mtoto wa mama, kama hauna hela uza buti ili uweze kuzama//

[Dizasta]
Kama ungejua mi nina pesa ungenipisha tu nipite, naweza kulipa hadi wenzio sita wanilinde//

Kama haujajua mi ni star basi, jua leo mtaani naheshimika ka gadafi//

Acha gari nyumba kwanza mi ni msafi, ungenipisha tu hata kunishika huna hadhi//

Nimetupia shati juu kofia raba kali halafu nina bonge la modo, naenda kwenye party nafika getini baunsa anasema hanijui hata kidogo//

Oya baunsa unazingua, tozi unazingua..Oya baunsa unazingua, nyie matozi mnazingua...Ona baunsa unazingua, hapana tozi unazingua....Oya baunsa unazingua, tozi unazingua

Yap demu wangu amechoka kusimama, sa si bora ukaniruhusa tu nikazama?// Unajibabaisha, eh unanidhalilisha ujaniskia mi ni star kwenye interview jana?

[Shaolin]
Hauna tiketi rudi nyuma, hauna hela halafu toka mbele yangu nisije nikakuonea huruma/

[Dizasta]
Kwanza nina hela kubwa sidhani kama una chenchi, ebu skiza huyo sio tundamani kwenye stage//

[Shaolin]
Elfu kumi haina chenchi ndiyo mtonyo, kama ipo chukua tiketi dogo acha mdomo//

[Dizasta]
Nitamwaga pesa nyingi hadi ujute kunidani, kama zipo basi zikae mbele kama tai//

[Shaolin]
Kuchugulia ni ruksa, panga tofali kama huwezi subiri fungulia mbwa//

[Dizasta]
Excuse me men, fungulia mbwa kivipi wakati nina track na jux mzee//

Foleni nyuma ni michosho, kukanyagana visa vipi kuhusu juma nyoso//

Halafu huko ndani kuna mchongo, lazima niingie sasa huoni nilivyonyuka mtoko//
 
Nyenza ni habari nyingine
Najua wengi ni mashabiki wa wasanii fulani fulani wa mziki pendwa wa hip hop ila leo nataka tuangazie kidogo hawa ma underground hip hop.

Katika tansina ya muziki huu wa hip hop tunaona jinsi gani evolution ilivyobadili ladha ya mziki huu kiasi cha wasanii kuimba nyimbo ambazo hazina lyrical wala critical.

List yangu ni hii hapa na wewe unaweza kuweka yako.

1. Dizasta vina
2. Nala mzalendo
3. Kadgo
4. Boshoo ninja
5. Kinya mistari
6. Shaolin senetor
7. Mbeya boy chuma
8. Hamis mistari
9. Ado gado
10. Nyenza MC

Wapo wengi ila kwasasa nianze na hao halafu chini nitanukuu mistari yao katika baadhi ya nyimbo zao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nala mzalendo
Screenshot_20200520-151547.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mie siku hizi nimeanza kuzeeka aise..

Nashindwa kabisa kukariri line za wanang..

Nakuelewa sana Scars

Ila namkubali Fuvu Toxic..

Kuna interview alifanya dak10 za maangamizi ni zaidi ya laaaanaaaaa
 
Basi tumetofautiana kimaana, mi nilimaanisha wasanii wasiosikika au chipukizi ambao hawana majina makubwa ambayo yanawafanya wasijulikane na wengi kulingana na mziki wanaoufanya
Mkuu scars ..Hip-hop ya kweli iko kwenye Handaki ...so wasanii wote wa tamaduni wote ni underground ... Haijalishi wanajulikana vipi...

One love
 
Mie siku hizi nimeanza kuzeeka aise..

Nashindwa kabisa kukariri line za wanang..

Nakuelewa sana Scars

Ila namkubali Fuvu Toxic..

Kuna interview alifanya dak10 za maangamizi ni zaidi ya laaaanaaaaa
Ndamcheki nione mautundu yake
 
Najua wengi ni mashabiki wa wasanii fulani fulani wa mziki pendwa wa hip hop ila leo nataka tuangazie kidogo hawa ma underground hip hop.

Katika tansina ya muziki huu wa hip hop tunaona jinsi gani evolution ilivyobadili ladha ya mziki huu kiasi cha wasanii kuimba nyimbo ambazo hazina lyrical wala critical.

List yangu ni hii hapa na wewe unaweza kuweka yako.

1. Dizasta vina
2. Nala mzalendo
3. Kadgo
4. Boshoo ninja
5. Kinya mistari
6. Shaolin senetor
7. Mbeya boy chuma
8. Hamis mistari
9. Ado gado
10. Nyenza MC

Wapo wengi ila kwasasa nianze na hao halafu chini nitanukuu mistari yao katika baadhi ya nyimbo zao

Hii list haijatimia bia kuwepo Kado Kitengo, mkulungwa mmoja matata sana kutoka pande za TMK
 
Back
Top Bottom