Nyenza mc Stanza
Naendelea na ufundi wa daraja, ili niepushe bundi linalotaka faraja.../
Stress hua gundi katikati ya mapaja, kama ndoto haziungi ubani hauna haja.../
Kukosa mipango ni ugonjwa wa hatari, utagonga milango kumuona daktari.../
Utaomba michango kukusanya daftari, kisa hakuna jambo ulilofanya tayari.../
Kukosa ujuzi ndio kutofika haraka, kukosa kurunzi ndio giza linavyotaka.../
Leo fanya maamuzi ya kisasa, maamuzi ya juzi tayari yaliisha chacha.../
Maswali mengi unayojiuliza, kwanini nuka yako iitwe yai viza.../
Hata wenzako walishawahi umizwa, huu ndo muda wako wa kutenda miujiza.../
Kitoe nje unachokifanya chumbani, kama kina alama ya kushika usukani.../
Vyote vyenye maana vilianzia kichwani, ndoto zako ni pana zisiishie kinywani.../
Fanya yote ila hili tafadhali, kwasiku usikose muda wa kutafakari.../
Wala usichoke kua unawaza mbali, usiogope jambo kama halina hatari.../
Usiwaafiki wanaofanya kitapeli, muwa wa usaliti ndio huzamishaga meli.../
Fanya kile na hiki hata kama vitafeli, ghafla ukifariki uwe ushafanya kweli.../
Uungwana daima uleta ndio, walishazama waliopima matamanio.../
Endapo kama utaniazima masikio, utaanza kufanya dhima za mafanikio.../
Pweza mwenye mikia ya mitaa, anayependwa na wanaoichukia sanaa.../
Anavyovieleza sisi tunapitia haswaa, sisi tuliopotezwa anatuwashia taa.../
Ni harabu kuwa fundi wa sarufi, vina vyenye adabu kwenye kundi la salute.../
Fanya kwasababu kesho huikuti, upo leo kwasababu ndo maana leo hufi.../
Mimi na nyie hakutakalika tena, madini yangu mie yanapita njia njema.../
Yanini mtumie rap kupindisha mema, maana ni mimi tu naye andika vyema.../
Nyenza bwana tumesha kua mzee, huko kupangiana jua usituletee.../
Hasara ya ujana kujichetua aisee, utataka busara ukishakua mzee.../
Beat na kinanda hua na mzuka wake, ndo maana natamba mchaga na duka lake.../
Pamoja na kwamba nayokupa ni machache, ila elewa kwamba hautajuta nifate.../
Unakwenda nje ya nchi kusaka ajira, au unakwenda tu kufata mazingira.../
Ukirudi ndani ya nchi mambo yako bila bila, ulotuacha ndani ya nchi tushazidaka ngawira.../
Bahati mbaya ndo pacha wa samahani japo kwa wengine bahati mbaya ni kejeli, sio mbaya kuweka ukweli kwenye utani ila ni mbaya ka utaleta utani kwenye ukweli.../
Dharau ndio panga yenye nongwa, chumvi ya kidonda chake haipaswi hata kuonjwa.../
Wangapi washakupanga halafu wakakuponda, umesahahu uongo wa mganga ndio nafuu ya ugonjwa.../
Vina vyenye perfume haununui, au unataka vina vyenye pumu uwe haupumui.../
Mkwepa majukumu daima hakui, mbishi hua mgumu hadi kujua hajui.../
Kipi kinaisibu hii hip hop culture, wagonjwa mpo wengi leo nawatibu cancer.../
Mnaojinasibu nyie ni freestyle masta, nadhani majibu tayari mmeshapata.../
Wengi wao hakuna kuumiza kichwa, ndo mana wanajiuliza navyo chanika.../
Vile nahimiza hii culture kuandika, nasikilizwa na wote bila kuacha rika.../
Mitaa yako wanajua we ni king, ila fikra yako tunajua we ni thing.../
Kile ambacho unajua ni ushindi, ukifumbia macho itakua ni upimbi.../
Achana na ishu za kuiga, tobo limeonekana lete kitu kuziba.../
Rap ya jana inakitu ma nigga, leo kila siku nyama kusifia kila figure.../
Vina vyao vyote vina utandu, nawaoiga chenga wote kupitia kanzu.../
Usipende niokote ukijua si chakwangu, sipendi popote kwakua nina kwangu.../
Uswazi ndo kuna mambo ya kusutwa, mademu wako shazi wanadata na sofa za kufa.../
Iko wazi we huwezi kunigusa, siwe uwe radhi useme mama nakufa.../
Nyie makaka mcheze mbali, vina vitawakata tuwacheze mwali.../
Kutoka kwa mtata overdose kali, lei tupo na papa vichwa vya habari.../