Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
- Thread starter
-
- #41
Lugoda...Kwahyo unaona huyo shekh wako alikua sahihi kuleta mada za maslah ya waislamu kwenye harakati za uhuru wa taifa lenye dini nyingi?
Lugoda...Kwahyo mzee dhumuni lako ni nini? Yani tufanyaje ili wazee wako nao waheshmike? Mana kama nyuz za kuwahusu ni nyingi ila binafsi sijawahi ona ushauri wako ili watambulike kitaifa. Samahani kama nimekosea.
Sasa utahoji vipi hali ya Waislamu wakati Tanzania ni ya Waafrika na sio ya Waislamu au wakristu. Maswala ya dini ni ya kijinga sanaNelson,
Unazungumzia kitu usichokifahamu.
Hakuna wazee katika TANU waliofukuzwa kwa ukabila na udini.
Ila kuna kisa cha Sheikh Suleiman Takadir aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU.
Sheikh Takadir alifukuzwa TANU kwa kuhoji hali ya baadae ya Waislam katika Tanganyika huru.
Hii ni moja ya historia nyeti sana ya TANU.
Nimekieleza kisa hiki kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
Salamu Mzee wangu ningependa kumfaham zaidi huyu Mzee wetu Ali Migeyo, mana nilipata kusoma elimu yangu ya sekondari bukoba mjini miaka ya 1994 na kuna mtaa ulikua unaitwa Migeyo Street karibu na soko kuu Mohamed SaidDon,
Kitabu cha Abdul Sykes kina historia yote ya wazalendo waliohusika na siasa za kupigania uhuru wa Tanganyika.
Mwanzo tu wa kitabu katika utangulizi nimeweka kwa muhtasari wazalendo niliokutananao katika Nyaraka za Sykes ambao hawamo katika historia ya TANU.
Ndani ya kitabu nimeeleza historia ya Ali Migeyo wa Kamachumu, Salum Mpunga, Sharifa bint Mzee na Yusuf Chembera wa Lindi, Bilal Waikela, Zarula bint Abdulrahman, Nyange bint Chande wa Tabora, Yusuf Olotu, Mama bint Mwalimu, Amin Kinabo, Halima Selengia, Lucy Lameck wa Moshi, Haruna Iddi Taratibu na Yusuf Suleiman wa Dodoma.
Uislam huwezi kuukwepa katika historia ya uhuru wa Tanganyika kama vile huwezi kukwepa kutaja Wakikuyu katika kupigania uhuru wa Kenya.
AHMED ADAM – MNUBI
Tukio dogo la kiburi
Askari mmoja mpita njia
aliingia katika ubishi na kijana mmoja
Hassan Masudi Vuni.
askari huyo alimpiga Vuni kwa kumuonea.
Msepele alitamka kwamba tukio kama hilo kamwe lisingeweza kutokea Dar es Salaam kwa sababu Mwafrika mmoja jina lake Julius Nyerere
Mwafrika huyu aliyekuwa akijulikana kwa jina la Nyerere
Mohamed Ali alimweleza Nyerere kwamba ukoloni ulikuwa bughudha
Mohamed Ali alikuwa na umri wa miaka 45.
Alikuwa hana elimu kama elimu
Zanzibar ilikuwa ndiyo kitovu cha elimu ya Kiislamu Afrika ya Mashariki
kijana Mohamed Ali alisoma kwa Sheikh Mohamed L’Khamus
Hawa walikuwa ndiyo aina ya watu walioanzisha na kuongoza harakati za kumaliza utawala wa kikoloni.
Hawakuwa wajuzi wa lugha ya Kiingereza
kama walivyokuwa baadhi ya Waafrika wengine waliyopata elimu ya Kimagharibi.
Mohamed Ali na akawa mwanachama
na kuanza kufanya kampeni kwa nguvu kwa ajili ya TANU
awafahamishe watu kuwa Nyerere yupo njiani kuja Jimbo la Kusini.
Nyerere aliwahakikishia wasikilizaji wake kuwa kulikuwa na uwezekano mku
mwalimu mmoja wa shule, Abdulrahman Muhibu
Katika hali yake ya ulevi alimpigia kelele Nyerere akamwita muongo.
aliona wazo la mwalimu wa shule Mwafrika kama yeye kuwaongoza watu hadi uhuru upatikane ni jambo lisilowezekana.
Nyerere alipomaliza ziara yake ya Jimbo la Kusini, fikra za watu wengi zilibadilika.
Nduku...Salamu Mzee wangu ningependa kumfaham zaidi huyu Mzee wetu Ali Migeyo, mana nilipata kusoma elimu yangu ya sekondari bukoba mjini miaka ya 1994 na kuna mtaa ulikua unaitwa Migeyo Street karibu na soko kuu Mohamed Said
Ed...Sasa utahoji vipi hali ya Waislamu wakati Tanzania ni ya Waafrika na sio ya Waislamu au wakristu. Maswala ya dini ni ya kijinga sana
Mzee said una chuki ya udini.Sababu nishawahi kukusikia mahala unasifia makanisa kugeuzwa stoo na miskiti huko uingereza.Na pia unalaumu baraza la mitihani linafelisha wanafunzi kimakusudi.Nelson,
Hapana sina chuki na mtu yoyote.
Nimeandika kitabu kueleza historia ya kweli ya uhuru.
Sikusukumwa na chuki ila nilitaka historia ya wazee wangu waliopigania uhuru isipotee.
Mzee ana hasira na Nyerere.Leo anataka kudanganya watu eti vijana wa UD wamechezea picha, huyu jamaa anawafanya watu humu wakuda eeh?.
Yaani anadhani kizazi hiki ndicho kile cha "rudi nyumbani nitakuletea pipi" NO!.
Yule shekh alitaka waislamu tu,ndio wawe viongozi wa Tanu.Wakaanzisha makundi ya kidini ndani ya Tanu.Kwahyo unaona huyo shekh wako alikua sahihi kuleta mada za maslah ya waislamu kwenye harakati za uhuru wa taifa lenye dini nyingi?
We mdini sana halafu mpotoshaji sisomagi nyuzi zako, sijui nia ni nini. Wenzako wanakemea udini we unaukoleza je una tofauti na shetani?Kitabu hiki nimekuwancho kwa miaka mingi sana.
Lakini kwa kuwa ni kitabu cha picha nilikisoma mara moja tu katika miaka ya 1980 na kikabakia Maktaba.
Sikukigusa tena.
Jana nimeona picha za TANU katika mtandao na haraka nikatambua kuwa picha hizi nimepata kuziona katika kitabu hicho hapo juu.
Ndipo nilipokitafuta kitabu hiki na kuanza kukipitia.
Kwa hakika nilistarehe sana na picha nilizozikuta ndani ya kitabu hiki ikawa kama vile naziona picha zile kwa mara ya kwanza.
Katika moja ya picha ambayo ilinivutia kwa kosa nililoliona katika maelezo ya picha hiyo ni hiyo hapo chini:
Maelezo ya picha hii ya waasisi wa TANU ni kuwa hao ni waanzilishi wa TAA.
Vipi linaweza kufanyika kosa kama hili?
Picha hii ya Waasisi wa TANU mwaka wa 1954 ni maarufu sana.
Hili mosi.
Pili hapajakuwapo na picha ya waasisi wa African Association iliyoanzishwa mwaka wa 1929.
Ingawa nimabahatika kupata picha mbili za waasisi wa chama hicho - picha ya Kleist Sykes na picha ya Mzee bin Sudi.
Tukirejea kwenye picha hiyo ya Waasisi wa TANU kuna kisa kirefu kuhusu picha hiyo iliyowekwa hapo.
Picha hiyo imechezewa kwa kutiwa mkono.
Katika picha yenyewe ya Waasisi wa TANU Ally Sykes, Tewa Said Tewa na Kasella Bantu hawamo.
Hawa walijitoa kwa kjuwa walikuwa ni watumishi wa serikali na sheria ilikuw ainawakataza kujihusisha na siasa.
Ilipokuwa inapigwa picha wao walikaa pembeni.
Angalia picha halisi hapo chini:
Kasella Bantu kapachikwa kati ya Abdul Sykes na Chief Patrick Kunambi.
Kazi hii ilifanywa na Idara ya Picha Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.
Siku zote kila nikiangalia picha hiyo iliyotiwa mkono hujiuliza kama haja ilikuw akuwaweka waasisi wote wa TANU kwa nini hazikuwekwa pia picha za Ally Sykes na Tewa Said Tewa.
Tuendelee kubakia katika hili suala la picha hii ya Waasisi wa TANU.
Katika kitabu cha maisha ya Julius Nyerere, ''Nyerere Biography,'' kitabu kinaeleza kuwa picha hii ilipigwa na kamera ya Denis Phombeah yeye mwenyewe akiwa mpigaji wa picha hiyo.
Abbas Sykes alikuwapo katika mkutano wa kuasisi TANU lakini hakuwa mjumbe bali kijana mdogo wa kutumwa na kaka yake Abdul Sykes na wajumbe wengine wa mkutano kufanya hiki na kile katika mkutano ule.
Abbas Sykes amenieleza kuwa picha ya Waasisi wa TANU ilipigwa na mpiga picha maarufu Dar es Salaam jina lake Gomez.
Abbas Sykes anaeleza kuwa walimsubiri Gomez ambae studio yake ilikuwa Acacia Avenue kwa muda hakutokea.
Abdul Sykes akamwambia Abbas achukue baiskeli ya TAA amfate wakapishana.
Wakati Abbas Sykes anamfuata Gomez yeye kumbe alikuwa njiani akija New Street kuwapiga picha waasisi wa TANU.
Katika kitabu hiki cha ''Nyerere na Watanzania,'' kuna picha hapo chini ya baiskeli ya kwanza ya TANU.
Bila shaka hii ndiyo baiskeli ya kijana mdogo Abbas Sykes alipanda kumfata mpiga picha Gomez:
View attachment 2576879Ukiangalia picha hii utaona nimeshika kitabu.
Baiskeli ya TANU
View attachment 2576880
Picha niliyopigwa na Gomez 1956
Mwandishi ni huyo kushoto kulia ni ndugu yangu Kapufi Yunge
Mama anasema nilikuwa situlii kwenye kiti ndipo Gomez akanipa kitabu nishike.
Studio ya Gomez ilikuwapo hadi miaka ya 1980.
Historia ya kweli we ulikuwepo kwenye michakato ya kutafuta uhuru?Nelson,
Hapana sina chuki na mtu yoyote.
Nimeandika kitabu kueleza historia ya kweli ya uhuru.
Sikusukumwa na chuki ila nilitaka historia ya wazee wangu waliopigania uhuru isipotee.
Ok subiria upate elimu nzuri ujue kuuenzi ubantu wako na sio uarabu.Nelson. ...
Sawa nasubiri.
Shukran sana Mzee wangu nimepata kujifunza kitu ubarikiwe na uwe na saum njema Mohamed SaidNduku...
HAMZA MWAPACHU NA ALI MIGEYO "WAASISI" WA TANU AMBAO HAWAKUHUDHURIA MKUTANO ULIOASISI TANU
Siku zote nimekuwa nikiungua ndani ya moyo wangu kwa nini Hamza Mwapachu na Ali Migeyo hawajapewa heshima wanayostahili katika kuunda chama Cha TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.
Huu ni mmoja wa misiba ya historia ya TANU.
Lakini pia unaweza ukaniuliza kwani nani kapewa heshima ya kuunda chama Cha TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika hadi leo niwataje Hamza Mwapachu na Ali Migeyo?
Hao wazalendo wengine vipi mbona huwataji ilhali wao ni waasisi wa TANU?
Siku zote mimi nimewahesabu wazalendo hawa wawili, Hamza Mwapachu na Ali Migeyo katika kundi la waasisi wa TANU na kufanya hesabu yangu ya waasisi wa TANU kuwa watu 19 badala ya 17.
Nani Hamza Mwapachu (1913 - 1962)?
Ana mengi sana katika historia ya uhuru wa Tanganyika na historia ya Julius Nyerere.
Hamza Mwapachu ndiye aliyefanya juhudi kubwa sana kuwa TAA iongozwe na vijana na hawa vijana ndiyo waunde TANU na kuongoza harakati za kudai uhuru.
Hamza Mwapachu alikuwa rafiki mkubwa wa Abdul Sykes.
Hamza Mwapachu alikuwako katika TAA Political Subcommittee iliyoundwa mwaka wa 1950.
Hii ilikuwa kamati ya wataalamu na watu wenye sauti katika siasa za Tanganyika na ndiyo waliotengeneza mapendekezo ya katiba ya Tanganyika yaliyowasilishwa kwa Gavana Edward Francis Twining mwaka wa 1950.
Katika mapendekezo haya yalikuyowasilishwa kwa Waingereza katka mapendekezo yaliyoighadhibisha serikali ilikuwa pendekezo la uchaguzi huru na pendekezo la kuwataka Waingereza kuondoka Tanganyika baada ya miaka 13 kuanzia pale uchaguzi utakapofanyika.
Wajumbe wa kamati hii walikuwa: Dr. Vedasto Kyaruzi, Abdulwahid Sykes, Hamza Mwapachu, Sheikh Hassan bin Ameir, Said Chaurembo, Steven Mhando na John Rupia.
Hamza Mwapachu ndiye aliyempendekeza Julius Nyerere kwa Abdul Sykes kuwa Nyerere atiwe katika nafasi ya uongozi wa juu wa TAA katika uchaguzi wa mwaka wa 1953 na mwaka unaofuatia 1954 TANU iundwe na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.
Ilikuwaje Hamza Mwapachu muasisi wa fikra kama hizi hakuhudhuria uasisi wa chama alichokuwa anakihangaikia kiasisiwe ni kisa ambacho In Shaa Allah tutakisoma katika kumbukumbu za Juma Mwapachu mtoto wa Hamza Mwapachu.
Tuwe na subra.
Ali Migeyo ndiye aliyekuwa akiwasha moto wa ukombozi Kanda ya Ziwa.
Ali Migeyo alikuwa fupa lililokwama kwenye koo la Waingereza.
Siku moja mwaka wa 1953 Ali Migeyo akiwa anahutubia wananchi wa Kamachumu mkutano ulivamiwa na mabomu yakapigwa.
Ali Migemo alikamatwa, akashitakiwa na kufungwa jela ya Butimba, Mwanza.
Wakati viongozi wa TAA walipokutana Dar es Salaam kuunda TANU, Ali Migeyo alikuwa jela anatumikia kifungo chake.
Hii ndiyo sababu hakuweza kuhudhuria mkutano ule.
Kwangu mimi Hamza Mwapachu na Ali Migeyo ni waasisi wa TANU ambao hawakuhudhuria kikao cha kuasisi chama cha TANU.
Mzee kanidanganya mpaka kuhusu vita vya maji maji kua ni jihad ya waislamu na pia anamsifia yule mfanyabiashara chotara wa kiarabu wa pembe za ndovu na watumwa Abushir bin salim kua alikua anatetea masilahi ya wabantu weusi alipopigana na wajerumani ambao walimzuia asifanye biashara haramu ya kuuza binadamu wenzie.Historia ya kweli we ulikuwepo kwenye michakato ya kutafuta uhuru?
Saig...Historia ya kweli we ulikuwepo kwenye michakato ya kutafuta uhuru?
Saig...We mdini sana halafu mpotoshaji sisomagi nyuzi zako, sijui nia ni nini. Wenzako wanakemea udini we unaukoleza je una tofauti na shetani?
Nelson...Mzee kanidanganya mpaka kuhusu vita vya maji maji kua ni jihad ya waislamu na pia anamsifia yule mfanyabiashara chotara wa kiarabu wa pembe za ndovu na watumwa Abushir bin salim kua alikua anatetea masilahi ya wabantu weusi alipopigana na wajerumani ambao walimzuia asifanye biashara haramu ya kuuza binadamu wenzie.
Sijui analipwa na nani kwa uptoshaji na udini na anapata faida gani. Anadanganya vijana hasa wa kiislamu kuhusu historia ya nchi.Mzee kanidanganya mpaka kuhusu vita vya maji maji kua ni jihad ya waislamu na pia anamsifia yule mfanyabiashara chotara wa kiarabu wa pembe za ndovu na watumwa Abushir bin salim kua alikua anatetea masilahi ya wabantu weusi alipopigana na wajerumani ambao walimzuia asifanye biashara haramu ya kuuza binadamu wenzie.