Historia ya TANU siku zote imeandikwa na makosa

Historia ya TANU siku zote imeandikwa na makosa

Saig...
Mimi nimezaliwa mwaka wa 1952 na baada ya miaka miwili ndiyo TANU ikaunndwa kwa hiyo michakato ya kutafuta uhuru katika siasa za TANU 1954 hadi 1961 mimi nilikuwa mtoto mdogo.

Lakini babu yangu Salum Abdallah yeye alihusika katika siasa za kutafuta uhuru kutoka miaka ya 1929 wakati African Association inaundwa.

Babu yangu aliongoza migomo mikubwa mitatu (General Strike) 1947, 1949 na 1960.
Bau yangu alikuwa mmoja wa waasisi wa TANU Tabora mwaka wa 1954 na pia ni mwasisi wa Tanganyika Railways African Union (TRAU) akiwa Mwenyekiti na Kassanga Tumbo Katibu 1955.

Kwa ajili historia ya uhuru wa Tanganyika kuanzia 1929 imekuwa ikiishi ndani ya familia yangu.

Hivi ndivyo nilivyokuja kuijua historia ya uhuru kushinda watu wengi sana.

View attachment 2577988
Kulia ni Kassnga Tumbo na anefuatia ni Salum Abdallah​
TUlia kalee wajukuu km huna lingine la maana kuichangia nchi hii. Nchi inahitaji kuunganishwa we unataka kuigawa kwa upotoshaji. Vitabu vilivyoandikwa vya historia viko sahihi.
 
TUlia kalee wajukuu km huna lingine la maana kuichangia nchi hii. Nchi inahitaji kuunganishwa we unataka kuigawa kwa upotoshaji. Vitabu vilivyoandikwa vya historia viko sahihi.
Saig...
Tufanye mjadala wa adabu na kuheshimiana.
 
Ed...
Huenda tatizo kwa baadhi yetu ni kukosa kujua somo tunalojadili.

Maswali mengi ninayokutananayo hapa JF ni tofauti sana na mswali ninayoulizwa kwengineko ninakopita kukutana na wanafunzi wa African History.

Umetumia lugha kidogo haipendezi kusema ujinga.

Sikulaumu kwani wewe historia hii na mchango wa Sheikh Suleiman Takadir katika kupigania uhuru wa Tanganyika historia hii umeisikia kwangu.

Umekuja hapa kujadili historia ambayo huijui.

Soma historia hii ya uhuru wa Tanganyika kama nilivyoieleza katika kitabu cha Abdul Sykes utaelewa kwa nini uhuru ulipokuwa unakaribia baada ya Kura Tatu likajitokeza suala la Waislam katika Tanganyika huru.
alipigania uhuru kwaajili ya waislamu au kwaajili ya watanzania. kabla ya kuwa muislamu alipozaliwa si alikua mwafrika mtanzania. Unahisi mwingereza kipindi anatawala alikua anatofutisha waaafrika kisa dini au kisa uafrika wao
 
alipigania uhuru kwaajili ya waislamu au kwaajili ya watanzania. kabla ya kuwa muislamu alipozaliwa si alikua mwafrika mtanzania. Unahisi mwingereza kipindi anatawala alikua anatofutisha waaafrika kisa dini au kisa uafrika wao
Ed..
Kulikuwa na ushirkiano mzuri na wa karibu kati ya Wamishionari na serikali za kikoloni kuanzia Wajerumani hadi kuingia kwa ukoloni wa Waingereza.

Ukisoma maisha ya Kleist Sykes katika kitabu alichohariri John Iliffe, "Modern Tanzanians," (1973) anasema kuwa kabla ya wao kuasisi African Association Waafrika walikuwa wanawakilishwa na Father Gibbons kutoka Minaki Mission.

Hii ni katika miaka ya 1920.

Wamishionari wakawa wanawatahadharisha waumini wao kujiweka mbali na shughuli za siasa.

Hii ndiyo sababu ikawa Waislam kuwa wengi katika uasisi wa AA na ikaendelea hadi katika TANU.

1680778760590.jpeg

Father Gibbons waliosimama wa kwanza kushoto​
 
Nelson...
Kuna kaburi la halaiki wamezikwa mashujaa yapata 67 wa Vita Vya Maji Maji pale Songea na kuna kaburi amezikwa Abdul Rauf Songea Mbano.

Katika hao walionyongwa kuna mwanamke pekee Bi. Khadija Mkomanile.
Hawa walinyongwa na Wajerumani.

Kabla ya kunyongwa alikuja mmeshionari kutoka Peramiho kuwaambis kuwa ikiwa takubali kubatizwa hawatanyongwa.

Ungekuwa unandika kwa adabu ningekueleza mengi mbayo huyajui.
Lakini kwa kuwa unadhani kuwa unajua basi na twende hivi hivi.
Mm sikubaliani na maelezo yako ya udini mzee wangu na kumsifia mfanyabiashara dhalimu chotara wa kiarabu Abushiri bin Salim na udhalimu wake wa kuuza binadamu wenzie.
 
Mm sikubaliani na maelezo yako ya udini mzee wangu na kumsifia mfanyabiashara dhalimu chotara wa kiarabu Abushiri bin Salim na udhalimu wake wa kuuza binadamu wenzie.
Nelson...
Lakini Abushiri hakufanya biashara hiyo.

Wala Abushiri hakuwa Mwarabu.
Jifunze historia kwanza ndiyo useme.
 
Ndiyo ishatoka na hairudi hiyo, mzee baba alifanya yake na akasepa huyu Moud afanye yake na yeye.
Today,
Kitabu nilichoandika kinasomwa na kipo katika "ategory" ya "Corrective History."

Kitabu changu hiki ndicho kilichoniingiza katika Cambridge Journal of African History.

Kitabu changu hiki ndicho kilichoniingiza katika Dictionary of African Biography (DAB).

Kitabu changu hiki ndicho kilichonipa ufunguo wa kufungua milango ya vyuo vikuu vingi.

Haya yote sikutegemea.

Kitabu changu hiki ndicho kilichosababisha niwe mmoja wa watu walioshiriki katika kueleza historia ya Julius Nyerere wakati wa utafiti wa kitabu chake, "Nyerere Biography,"(2020).

Mnakesha na mimi hapa.
Mnashindwa kuondoka.

Kitabu miaka 25 toka kichapwe Uingereza 1998 bado kinajadiliwa hadi leo.
Kwa nini?
 
Today,
Kwa nini huandiki kwa busara?
Lugha yako si nzuri.

Wewe historia hii umeijua leo.

Katika vyuo vikuu vinavyosomesha African History historia hii wameanza kuisomesha miaka 25 iliyopita.

Katika historia hii hakuna popote penye chuki.

Review tatu ndani ya Cambridge Journal of African History hakuna hata moja iliyoona udini au chuki.

Kitabu kimependwa kwa kuwa kimechangia mengi katika siasa za Afrika kuwa inawezekana ikafutwa historia ya kizazi kizima ikawekwa historia ya kutunga na ikaaminiwa kuwa ni kweli kwa kipindi cha zaidi ya nusu karne.

Hili limevutia sana.

Nakushauri usome historia hii kwanza uielewe ndipo uje hapa kufanya mjadala.
We mzee kila nikisoma mada zako unaelezea wazee wa kiislam. Inamaana wazee wa kikristo hawakuwepo kwenye hizo mambo unazotueleza? Halafu Mara kwa mara unaonyesha chuki za wazi kwa Nyerere, hii ina maana gani kwako?
Ukitaka watu wakuelewe leta historia zisizo na udini. Haiwezekani kila historia unasema imekosewa kisha unaanza kuwaingiza wazee wako wa kiislam. Udini unakufanya uonekane ni mzee wa ovyo sana. Inaonekana hata huko kwenye jamii yako una udini uliopitiliza.

Ukishakuwa mzee inabidi uwe na busara na kuwaunganisha watu sio kuwatenganisha. Umenizidi zaidi ya miaka 40 Ila kwa haya unayoandika kila siku nakuona kama mzee fulani hivi mwenye fikra za kijinga.
 
View attachment 2576842
''Mwalimu Nyerere na Historia'' (1980)
Kitabu cha Prof. G.A. Mhina
Kitabu hiki nimekuwancho kwa miaka mingi sana.

Lakini kwa kuwa ni kitabu cha picha nilikisoma mara moja tu katika miaka ya 1980 na kikabakia Maktaba.

Sikukigusa tena.

Jana nimeona picha za TANU katika mtandao na haraka nikatambua kuwa picha hizi nimepata kuziona katika kitabu hicho hapo juu.

Ndipo nilipokitafuta kitabu hiki na kuanza kukipitia.

Kwa hakika nilistarehe sana na picha nilizozikuta ndani ya kitabu hiki ikawa kama vile naziona picha zile kwa mara ya kwanza.

Katika moja ya picha ambayo ilinivutia kwa kosa nililoliona katika maelezo ya picha hiyo ni hiyo hapo chini:
Maelezo ya picha hii ya waasisi wa TANU ni kuwa hao ni waanzilishi wa TAA.
Vipi linaweza kufanyika kosa kama hili?

Picha hii ya Waasisi wa TANU mwaka wa 1954 ni maarufu sana.
Hili mosi.

Pili hapajakuwapo na picha ya waasisi wa African Association iliyoanzishwa mwaka wa 1929.

Ingawa nimabahatika kupata picha mbili za waasisi wa chama hicho - picha ya Kleist Sykes na picha ya Mzee bin Sudi.

Tukirejea kwenye picha hiyo ya Waasisi wa TANU kuna kisa kirefu kuhusu picha hiyo iliyowekwa hapo.

Picha hiyo imechezewa kwa kutiwa mkono.

Katika picha yenyewe ya Waasisi wa TANU Ally Sykes, Tewa Said Tewa na Kasella Bantu hawamo.

Hawa walijitoa kwa kjuwa walikuwa ni watumishi wa serikali na sheria ilikuw ainawakataza kujihusisha na siasa.

Ilipokuwa inapigwa picha wao walikaa pembeni.

Angalia picha halisi hapo chini:

Kasella Bantu kapachikwa kati ya Abdul Sykes na Chief Patrick Kunambi.
Kazi hii ilifanywa na Idara ya Picha Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Siku zote kila nikiangalia picha hiyo iliyotiwa mkono hujiuliza kama haja ilikuw akuwaweka waasisi wote wa TANU kwa nini hazikuwekwa pia picha za Ally Sykes na Tewa Said Tewa.

Tuendelee kubakia katika hili suala la picha hii ya Waasisi wa TANU.

Katika kitabu cha maisha ya Julius Nyerere, ''Nyerere Biography,'' kitabu kinaeleza kuwa picha hii ilipigwa na kamera ya Denis Phombeah yeye mwenyewe akiwa mpigaji wa picha hiyo.

Abbas Sykes alikuwapo katika mkutano wa kuasisi TANU lakini hakuwa mjumbe bali kijana mdogo wa kutumwa na kaka yake Abdul Sykes na wajumbe wengine wa mkutano kufanya hiki na kile katika mkutano ule.

Abbas Sykes amenieleza kuwa picha ya Waasisi wa TANU ilipigwa na mpiga picha maarufu Dar es Salaam jina lake Gomez.

Abbas Sykes anaeleza kuwa walimsubiri Gomez ambae studio yake ilikuwa Acacia Avenue kwa muda hakutokea.

Abdul Sykes akamwambia Abbas achukue baiskeli ya TAA amfate wakapishana.

Wakati Abbas Sykes anamfuata Gomez yeye kumbe alikuwa njiani akija New Street kuwapiga picha waasisi wa TANU.
Katika kitabu hiki cha ''Nyerere na Watanzania,'' kuna picha hapo chini ya baiskeli ya kwanza ya TANU.

Bila shaka hii ndiyo baiskeli ya kijana mdogo Abbas Sykes alipanda kumfata mpiga picha Gomez:

View attachment 2576879
Baiskeli ya TANU

View attachment 2576880
Picha niliyopigwa na Gomez 1956
Mwandishi ni huyo kushoto kulia ni ndugu yangu Kapufi Yunge
Ukiangalia picha hii utaona nimeshika kitabu.

Mama anasema nilikuwa situlii kwenye kiti ndipo Gomez akanipa kitabu nishike.

Studio ya Gomez ilikuwapo hadi miaka ya 1980.
Uwongo mtupu ili kujusty fundamentalism yake kwenye Islam religion. Ila mze you are finished, dunia ya kistaarabu UDINI hauna nafasi. Hata uandike ujaze makataba ya Taifa kutetea wazazi wako itabakia ni riwaya tu au rumours. Wewe ni nani ubadili historia ya J K Nyerere?
 
We mzee kila nikisoma mada zako unaelezea wazee wa kiislam. Inamaana wazee wa kikristo hawakuwepo kwenye hizo mambo unazotueleza? Halafu Mara kwa mara unaonyesha chuki za wazi kwa Nyerere, hii ina maana gani kwako?
Ukitaka watu wakuelewe leta historia zisizo na udini. Haiwezekani kila historia unasema imekosewa kisha unaanza kuwaingiza wazee wako wa kiislam. Udini unakufanya uonekane ni mzee wa ovyo sana. Inaonekana hata huko kwenye jamii yako una udini uliopitiliza.

Ukishakuwa mzee inabidi uwe na busara na kuwaunganisha watu sio kuwatenganisha. Umenizidi zaidi ya miaka 40 Ila kwa haya unayoandika kila siku nakuona kama mzee fulani hivi mwenye fikra za kijinga.
Clever...
Ninaposoma mtu kaanza kuandika kwa, ''We mzee...'' najua kaghadhibika.
Lakini nini kinamghadhibisha?

Anasema kuna udini.
Udini kuandika historia ya kweli na kuwataja wahusika wa historia hiyo?

Ndiyo kusema wale walioandika historia ya TANU na kufuta majina ya Waislam katika historia ya kupigania uhuru walifanya hivyo kwa kuogopa udini ikiwa majina ya wazalendo Waislam yatatawala historia ya uhuru?

Umeuliza wazee wa Kikristo hawakuwapo?
Wakristo walikuwapo.

African Association iliasisiwa mwaka wa 1929 na waasisi ni hawa: Cecil Matola (President), Kleist Abdallah Sykes (Secretary), Mzee bin Sudi, Ibrahim Hamisi, Zibe Kidasi, Ali Said Mpima, Suleiman Majisu, Raikes Kusi na Rawson Watts.

Unasema naonyesha chuki za wazi dhidi ya Nyerere.
Tafadhali weka ushahudi wa hizo chuki wasomaji wazione.

Waasisi wa African Association walikuwa tisa kati ya hawa Wakristo walikuwa watatu.

Nina mifano mingi sana ya namna hii.
Ikiwa ujaridhika na mfano huu nifahamishe nikuongeze mingine.

1680982173120.jpeg

Mzee bin Sudi
Muasisi wa African Association (1929) na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika
(Umoja wa Waislam wa Tanganyika) 1933​
 
Clever...
Ninaposoma mtu kaanza kuandika kwa, ''We mzee...'' najua kaghadhibika.
Lakini nini kinamghadhibisha?

Anasema kuna udini.
Udini kuandika historia ya kweli na kuwataja wahusika wa historia hiyo?

Ndiyo kusema wale walioandika historia ya TANU na kufuta majina ya Waislam katika historia ya kupigania uhuru walifanya hivyo kwa kuogopa udini ikiwa majina ya wazalendo Waislam yatatawala historia ya uhuru?

Umeuliza wazee wa Kikristo hawakuwapo?
Wakristo walikuwapo.

African Association iliasisiwa mwaka wa 1929 na waasisi ni hawa: Cecil Matola (President), Kleist Abdallah Sykes (Secretary), Mzee bin Sudi, Ibrahim Hamisi, Zibe Kidasi, Ali Said Mpima, Suleiman Majisu, Raikes Kusi na Rawson Watts.

Unasema naonyesha chuki za wazi dhidi ya Nyerere.
Tafadhali weka ushahudi wa hizo chuki wasomaji wazione.

Waasisi wa African Association walikuwa tisa kati ya hawa Wakristo walikuwa watatu.

Nina mifano mingi sana ya namna hii.
Ikiwa ujaridhika na mfano huu nifahamishe nikuongeze mingine.

View attachment 2581503
Mzee bin Sudi
Muasisi wa African Association (1929) na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika
(Umoja wa Waislam wa Tanganyika) 1933​
Ukitaka vijana tukusome maandiko yako andika historia bila kuchagua zile zenye wazee wako wa kiislamu...nje na hapo tutakupuuza tu.
Mimi ni mkristo ila hata ajitokeze mtu humu kila siku yeye analeta historia ya nchi kwa kuyumbia kwa wakristo nitamuona ni wa ovyo tu na wewe unayependelea upande mmoja.
Ni ushauri tu, andika historia achana na haya unayoandika.
 
Uwongo mtupu ili kujusty fundamentalism yake kwenye Islam religion. Ila mze you are finished, dunia ya kistaarabu UDINI hauna nafasi. Hata uandike ujaze makataba ya Taifa kutetea wazazi wako itabakia ni riwaya tu au rumours. Wewe ni nani ubadili historia ya J K Nyerere?
Huihui,
Mimi si niliyebadili historia ya Julius Nyerere.
historia ya Mwalimu imebadilika kwa utafiti na niliyoyakuta katika Nyaraka za Sykes.

''Mwezi June, makao makuu ya TAA yalitangaza kamati yake ya utendaji: J. K. Nyerere, Rais, Abdulwahid Sykes, Makamu wa Rais; J. P. Kasella Bantu, Katibu Mkuu; Alexander M. Tobias na Waziri Dossa Aziz, Katibu wa muhtasari.

Wajumbe wa kamati: Dr Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said Tewa, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo na Patrick Aoko.''

(Tanganyika Standard 19 June 1953)

Mifano kama hiii iko mingi katika kitabu cha Abdul Sykes na chanzo ni hizo nyaraka.
 
Ukitaka vijana tukusome maandiko yako andika historia bila kuchagua zile zenye wazee wako wa kiislamu...nje na hapo tutakupuuza tu.
Mimi ni mkristo ila hata ajitokeze mtu humu kila siku yeye analeta historia ya nchi kwa kuyumbia kwa wakristo nitamuona ni wa ovyo tu na wewe unayependelea upande mmoja.
Ni ushauri tu, andika historia achana na haya unayoandika.
Clever...
Nani kakuambia kuwa mimi nataka kusomwa na vijana?

Mimi nimeandika kitabu wala sikumlenga yeyote.

Unasema niandike historia.

Kwani hapa wewe unasoma kitu gani?
 
Back
Top Bottom