Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
- Thread starter
-
- #121
Stux...Watu wenyewe wote anaowatetea Nyerere aliwapa kazi wao na watoto wao. Mohamed Said sijui alikuwa anataka Nyerere awabebe wazee wa Mohamed Said awabebe mgongoni??
Huihui...Hivyo siyo vitabu ni mkusanyiko wa maandishi ya kiislamu tu. Endelea kufanganya hao wanaokupa nauli ya kwenda Cambridge.
Mama...Ndo maana tunasema kitabu chako ni cha kuhusu uislamu na sio TANU wala historia ya nchi hii.
Che...Nasoma tu
Smart...Ahsante kwa historia...
Naomba wale Wajuzi wa historia mnielimishe kidogo ilikuwa Watu wa DSM walimuomba Julius Nyerere awasaidie katika mapambano ya kudai Uhuru
Mzee Mohamed Said na Wakili Pascal Mayalla karibuni tafadhali
Mlale Unono 😃
Huna uwezo wa kusahihisha historia kwa kuwa uko intoxicated na islamologyStux...
Haya hayahusiani na kazi.
Nimesahihisha historia iliyokuwa na makosa.
Hui...Huna uwezo wa kusahihisha historia kwa kuwa uko intoxicated na islamology
Hui...
Nimeisahihisha historia ya uhuru wa Tanganyika na kitabu kipo toka 1998.
Kiko toleo la nne tunakwenda toleo la tano.
Vitabu nilivyovisahihisha vyote vimekufa vimechapwa toleo la kwanza basi.
View attachment 2700056
Huihui...Mtu mmoja tu uliyekamia kuandika maisha yake hawezi kuwa historia ya Tanzania.
Je ulishafanya tafiti kwanini ilibidi Adbul Sykes ampishe Nyerere?Huihui...
Hakika ni maisha ya historia ya mtu mmoja lakini kupiia maisha yake utasoma maisha ya watu wengi waliokuja kuwa watu maarufu katika historia ya Tanzania.
Kuna picha katika kitabu cha Abdul Sykes na ni picha ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika imepigwa katika miaka ya 1930.
Aliyesimama wa kwanza mstari wa nyuma kushoto ni Maalim Mohamed Matar mwalimu wa Qur'an katika shule ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.
Maalim Matar ni kielekezo cha mateso katika jela za utesaji na Zanzibar baada ya mapinduzi.
Katika picha hiyo utaona majina ya Ali Mwinyi Tambwe Secretary wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Kleist Sykes muasisi wa jumuiya hiyo 1933 na mwanae Abdul Sykes.
Ali Mwinyi ni muhimu sana katika historia ya uhuru wa Tanganyika na mapinduzi ya Zanzibar.
Siku nilipozungumza na Ali Mwinyi aliniambia kuwa Abdul Sykes ni mdogo sana kwake na alinieleza mengi kuhusu African Association.
1953 mwanzoni Abdul Sykes sasa kijana na Ally Mwinyi Tambwe walikwenda Nansio, Ukerewe nyumbani kwa Hamza Mwapachu kujadili suala la uchaguzi wa mwaka wa TAA uliokuwa unafanyika mwezi April.
Abdul Sykes alikuwa TAA Act. President na Secretary.
Mazungumzo yao hao watu watatu ilikuwa Abdul kumpisha Julius Nyerere katika nafasi ya rais wa TAA na mwaka unaofata 1954 TANU iundwe na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru.
Nadhani hadi hapo umesoma kidogo historia ambayo hukuwa unaijua na maarifa yako yameongezeka.
Huihui...Je ulishafanya tafiti kwanini ilibidi Adbul Sykes ampishe Nyerere?
Lakini Mzee Saidi.Huihui...
Kuna sababu kubwa mbili kwa nini Abdul Sykes ilikuwa lazima akae pembeni.
Sababu ya kwanza ilikuwa dini.
Mchakato wa kumtafuta kiongozi wa TAA kisha iundwe TANU ulianza 1951 baada ya viongozi wa TAA kupewa uhamisho kutoka Dar es Salaam kwenda majimboni.
Dr. Vedasto Kyaruzi aliyekuwa President wa TAA aliondokewa Dar-es-Salaam kwenda Kingoluwira Prison kisha Nzega.
Hamza Mwapachu akapelekwa Nansio, Ukerewe.
Sababu ni kushiriki kwao katika Mapendekezo ya Katiba ambamo walidai uchaguzi katika wajumbe wa LEGCO na baada ya miaka 13 Waingereza waondoke watoe uhuru kwa Tanganyika.
Gavana Edward Francis Twining alighadhibishwa na haya mapendekezo ya TAA ndiyo akaamua sasa kuidhoofisha TAA kwa kuhamisha viongozi wake Dar-es-Salaam kuwapeleka mbali.
Abdul Sykes sasa akawa TAA Act. President na Secretary.
Earle Seaton aliyekuwa mshauri wa TAA katika mambo udhamini wa Tanganyika chini ya Waingereza akashauri kuwa TAA badala ya kupoteza nguvu kupambana na London wafungue mawasiliano moja kwa moja na UNO, New York kudai uhuru.
Abdul na Hamza Mwapachu wakaamua haraka atafutwe kiongozi iundwe TANU lakini kiongozi huyo lazima awe Mkristo.
Sababu ni kuwa haikutaka kuwepo na picha kuwa harakati zile ni za Waislam peke yao kwani wao ndiyo walikuwa wengi mstari wa mbele.
Abdul Sykes alianza mazungumzo na Chief David Kidaha Makwaia achukue uongozi wa TAA kisha waunde TANU na Chief Kidaha aongoze mapambano ya kudai uhuru.
Chief Kidaha hakuafiki na hili na zilikuwapo sababu za msingi.
Alipotokea Nyerere mwaka wa 1952 ikawa imepatikana nafasi mpya.
Nyerere kwa sifa zilezile laiti angekuwa Muislam asingepewa uongozi wa TAA.
Iilikuwa fikra ya Hamza Mwapachu kuwa Tanganyika iingie katika kudai uhuru ikiwa na umoja vinginevyo Waingereza wangewashawishi Wakristo kuunda chama kipingane na TANU iliyojaa Waislam.
India iliingia katika kudai uhuru nchi ikiwa imegawanyika kati ya Wahindu na Waislam; na matokeo yake yanafahamika baada ya uhuru kupatikana.
Hii ndiyo sababu kubwa Julius Nyerere akapewa uongozi ili upatikane umoja wa wananchi.
Pili Nyerere kwa wakati ule alikuwa na elimu kubwa na kwa TAA kuongozwa na mtu kama yeye hilo ndilo lililokuwa likitafutwa.
Che...Lakini Mzee Saidi.
Ni kwanini mlimfukuza Mwarabu Zanzibar?
Na mnampigania aje Tanganyika.
Kwanini hamu mpiganii arudi Zanzibar aendeleze Uislamu na Misikiti?
Si Nendeni hapo tu Dubai muka muombe radhi kwa dhuluma mliyomfanyia.
Nyinyi Wazanzibari ndio mliomfukuza Mwarabu kwa risasi. mliwaua hadi Waarabu wasio na hatia. Waliokuwa wanatoka Shambani kwao kulima na kuvuna mazao yao.
Kwa mujibu wa maneno yako, Mzee Saidi Muhammedi.
Sasa unataka sisi Watanganyika tuwasadieje ?
Katu Watanganyika hatujawahi kumdhalilisha Mwarabu.
Kwa namna yotote ile.
Malizeni tofauti zenu na Mwarabu na mumkaribishe tena hapo Zanzibar.
Furaha irudi tena.
Mama...
Mimi sidhuriki na lugha kali wala kutukanwa.
Majibu ya udini ni haya haya ninayoandika siku zote nikisema kuwa kueleza mchango wa Wakikuyu na Mau Mau katika historia ya uhuru wa Kenya si ukabila.
Msome Bildad Kaggia: "Roots of Freedom."
Hivyo hivyo ndivyo ilivyo kwa Waislam katika uhuru wa Tanganyika.
Nitaendelea kueleza historia ya uhuru wa Tanganyika kwa ushahidi na wewe endelea na kuhamaki na kutoa lugha kali kuwa mimi "mjinga," "mpumbavu" na kadhalika.
Naamini kabisa unajua kuwa mtu mjinga hawezi kuwa mwandishi wa vitabu kadhaa na makala zaidi ya 10,000.
Sina chuki na mtu yoyote.
Mabingwa wa historia ya Afrika katika kukieleza kitabu changu hawakupata popote kuzungumza chuki au udini katika book reviews zao.
Zaidi wamenialika kuzungumza kwenye vyuo vyao Marekani na Ulaya.
View attachment 2581771
Zentrum Moderner Orient (ZMO), Berlin
ZMO ni katika taasisi kubwa za utafiti wa historia ulimwenguni na nilialikwa hapo kwa kufanya mhadhara na kuandika paper yoyote niitakayo katika historia ya Afrika.
Paper niliyoandika ni hiyo hapo chini:
TANZANIA: A NATION WITHOUT HEROES
http://www.awaazmagazine.com/index.php/latest-issue/special-features/item/558-tanzania-a-country-without-heroes Awaaz Magazine, Volum...mohamedsaidsalum.blogspot.com
Hili si suala la udini kwa upande wangu.
Kama kuna udini basi ni kwa wale waliofuta historia ya Waislam katika harakati za kudai uhuru wakapachika historia yao.
Hili hulioni.
Dr.
Sina chuki na mtu yeyote.
Historia ya TANU hii ni historia ya wazee wangu kwa hiyo naijua vizuri.
Ninapoona imekosewa ni wajibu wangu kusahihisha.
Hebu sikiliza hotuba hii ya Diamond Jubilee Hall 1985 na soma chini yake uone inavyopishana niliyoeleza mimi kama nilivyosoma katika Nyaraka za Sykes:
Katika hotuba hii Mwalimu anasema ‘’anadhani’’ Abdul Sykes alikuwa Secretary wa TAA.
(Katika hotuba iliyoko katika maandishi neno, ''nadhani,'' limeondolewa lakini ukisikiliza audio utalisikia amelitamka).
Mwalimu hana hakika na hili.
Kuanzia mwaka wa 1953 alipokuwa President wa TAA hadi mwaka wa 1985 Mwalimu bado hajui Abdul Sykes alikuwa na nafasi gani katika TAA.
Anasema mambo yalikuwa ‘’yamesinzia.’’
Ukweli ni kuwa TAA kuanzia mwaka wa 1950 uongozi ulipochukuiwa na Dr. Vedasto Kyaruzi kama President na Abdul Sykes Secretary TAA ilifanya mengi kuanzia kuunda TAA Political Subcommittee na kumleta Earle Seaton kama mshauri wa TAA katika masula ya sheria katika mambo ya Mandate Territories, yaani Nchi Chini ya Udhamini kama ilivyopitishwa na UNO.
TAA ilifanya mazungumzo ya siri na Jomo Kenyatta, Nairobi pia mazungumzo na Chief David Kidaha Makwaia kumwingiza TAA achaguliwe President kwa nia ya kuunda TANU mbali na kumwajiri Alexander Tobia kama kama mtumishi wa TAA.
Yapo mengi sana.
Mwalimu anasema kwa muda mfupi kufika April TAA ‘’ikafufuka.’’
Lakini April 1953 ndiyo Mwalimu anaingia madarakani kama President wa TAA Abdul Sykes akiwa Vice President baada ya uchaguzi wa Arnautoglo.
Ikiwa Mwalimu kaifufua TAA ndiyo kusema kaifufua TAA mwezi ule alipochaguliwa kuwa President.
Ukweli ni kuwa yeye alipochukua uongozi wa TAA April 1953 chama kilisinzia.
Mwalimu anaeleza mkutano wa Arnautoglo ambao alichaguliwa kuwa President, ‘’wao,’’ lakini hasemi nafasi hiyo aligombea na nani.
Mwalimu anasema ‘’akaandika,’’ katiba mpya.
Hapakuwa na ‘’uandikaji’’ wa katiba mpya.
Kilichofanyika ni kuwa ilinakiliwa katiba ya Convention People's Party (CPP) ya Kwame Nkrumah wa Ghana na sehemu ya CPP waliweka TANU.
Mwalimu anazungumza mkutano wa Songea na Mbeya mwaka wa 1955.
Safari ya kwanza ya Mwalimu ilikuwa Morogoro akiongozana na Zuberi Mtemvu na walifanya mkutano wa ndani ambao haukuwa na mafanikio.
Hii ilikuwa August, 1955.
Baada ya Morogoro Mwalimu, Ali Mwinyi Tambwe na Rajab Diwani walikwenda Lindi.
Yapo mengi sana.
Mwalimu kaichukua TAA ikiwa ina mipango madhubuti na fedha za kutosha.
Picha: Abdul na Ally Sykes Burma Infantry/Waasisi wa TANU/Baraza la Wazee wa TANU.
Nyioku....First, I state five premises I have extracted from Said’s paper; some are given verbatim, and others are imputed or paraphrased.
A) Authoritarian regimes generally distort national histories.
B) History is made not by one hero, but by a diversity of heroes.
C) Leaders in Africa fear heroes other than themselves.
D) Religion is a primary driver of social change.
E) Islam is a socially progressive religion while Christianity is not.
Second, I state the principal conclusions drawn by Said.
A) Muslims, not Christians, liberated Tanzania from colonial rule.
B) Muslim activists have been written out of the official history.
C) The welfare of the Muslims in Tanzania has been sorely neglected.
D) The religious divide propels the socio-political affairs in Tanzania.
E) Muslims no longer love and respect Nyerere the way they did earlier.
Mzee hapo unaonyesha udini wako, na mnapenda kulialia wakati hamna mipango endelevu kwenye elimu na afya kwa taasisi zenu!
Utahoji vipi hali ya Waislamu katikati tanganyika wakati taifa halina dini. Kufukuzwa walipaswa wangetaka mambo ya Uislamu wangeenda jenga nyumba MakkaNelson,
Unazungumzia kitu usichokifahamu.
Hakuna wazee katika TANU waliofukuzwa kwa ukabila na udini.
Ila kuna kisa cha Sheikh Suleiman Takadir aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU.
Sheikh Takadir alifukuzwa TANU kwa kuhoji hali ya baadae ya Waislam katika Tanganyika huru.
Hii ni moja ya historia nyeti sana ya TANU.
Nimekieleza kisa hiki kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
Edwayne,Utahoji vipi hali ya Waislamu katikati tanganyika wakati taifa halina dini. Kufukuzwa walipaswa wangetaka mambo ya Uislamu wangeenda jenga nyumba Makka
Sent using Jamii Forums mobile app