Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Kwa mtu makini, Hata Nyerere mwenyewe alikipata kitabu chako (kwani kilitoka zaidi ya miaka miwili kabla kufariki kwake, na ninavyomjua Nyerere alivyokuwa msomi wa vitabu laazima atakuwa amekisoma) Lakini hakuthubutu kuandika kupinga maandiko hayo.Kwani aljua ni lazima atulie na kufanya utafiti kidogo kabla kujibu au alikubaliana na kilichomo ndanimwe.

Unaamini vipi kuwa alikisoma? Au kwa vile alikuwa msomi basi kila kitabu kilichompitia unadhani alikisoma? Haujui msomi anachagua kipi kitamsaidia na kipi hakina tija kwake. Halafu unaditiki kusema kuwa "hakuthubutu" kuandika kupinga kilichoandikwa! Nitajie kuna vitabu vingapi alivyoandika Mwalimu kiasi cha kuamini kuwa hata cha Mohamed Said asingechelea kukiandikia?

Nafikiri inakupasa wakti mwingine ufikirie nje ya box.

Usichukulie maneno ya wanasiasa kuwa Tz ni nchi ya amani na utulivu wakti watu ni waoga na wanafiki ingawa kiukweli kuna dhulma kubwa na unyanyasaji wa hali ya juu.

Kumbuka usitegemee kupanda mchicha ukavuna maharage.

Na kila wakti tunasema penye dhulma na pasipo na haki basi hakuna amani wala upendo bali kuna uwoga. Hiyo ndio Tz.

Soma mnakasha vizuri utagundua hilo. Kinachovunwa sasa na zile mbegu zilizopandwa tokea mlipopata uhuro miaka 50 iliyopita. sasa kazi kwenu kwani kuna mwimbaji mmoja wa Raggae akiitwa Robert Nesta Marley (maarufu kama Bob Marley) alimba katika one of his song
You can fool some people sometime But you can't fool all the people all the time.

Cha ajabu kipi Tanzania kuwa na dhulma. Unataka kutuambia kuwa huko uliko hakuna dhulma? Huko wananchi wako huru kukemea dhulma na udhalimu wanaotendewa na watawala wao? Tunachokataa ni kudai kuwa Tanzania kuna institutionalised dhulma dhidi ya kikundi fulani inayotokana na mtazamo wa kidini. Dhulma ipo lakini si hiyo mnaotaka kutuaminisha.

Na hayo maneno unayodai ni ya Bob Marley, yalisemwa kwanza na Abraham Lincoln.

Skillionare,

Umesema maneno ya busara kabisa.
Sisi Waislam kwa umoja wetu tumepita nchi nzima kuwaelimisha Waislam hatari inayokabili nchi yetu kutokana na mfumokristo.

Tunaisubiri serikali itupe jibu.

Mohamed


Hapa ndipo ulipojivua gamba. Mnawafahamisha ili iwaje? Na hiyo hatari ni ipi?

Katika moja ya nchi za nje nilipangiwa mnakasha mimi bila ya kujua kumbe wale host wa ule mnakasha ni "staunch Catholics" hili ni kundi la wasomi na mabingwa katika historia ya Tanzania. Mnakasha jioni baada ya L 'Asr. Mimi hili na lile sina wala siwajui kama hawa ni Catholics mie nimewachukulia kuwa ni "scholars" wa African history."


Ala! Sikujua hili. Kuwa mkatoliki hawezi kuwa scholar wa historia ya kiafrika hata kama nae ni muafrika. Kumbe ndio maana Nyerere anawaudhi! Anayeweza kuzungumza ukweli kuhusu historia yetu ni muislamu peke yake!

Nimeanza na Mnazi Mmoja Sheikh Suleiman Takadir kapanda jukwaa anapiga fatha inasomwa surat fatha kisha dua na watu wote wamesimama mikono wamenyanyua wanaitikia "Amin."

Kisha Nyerere anatambulishwa na kuombwa kuhutubia...

Wazungu kimya...ukumbi utadhani umemwagiwa maji...nawaambia hizo ndizo "Muslim symbols" katika kupigania uhuru wa Tanganyika na zipo nyingi.


Na alipoenda unyakyusani, wakina Mwakangale waliposalimia jamii kwa kusema "ugonile" nayo ni Nyakyusa symbols katika kupigania uhuru wa Tanganyika?
Unataka kweli kutuaminisha kuwa katika jopo la unaowaita wasomi (ambalo lina utata maana sifa hiyo uliishawanyang'anya na kuwabakizia ya ukatoliki) walishangaa kusikia kuwa katika sehemu iliyojaa waislamu, dua ikatangulia kusomwa? Bila shaka waliduwaa kukuona unachukua kitu kama hicho kuwa ni ishara wa pivotal role ambayo uislamu ulibeba katika kupigania uhuru wa nchi yetu.

Abdu anamjulisha kwa mdogo wake Ally, kwa mama yake Bi Mluguru,Bi Mluguru na Bi Mugaya mama yake Nyerere wanakuwa mashoga wakubwa, Abdu anampeleka Nyerere kwa Dossa, Rupia...Abdu anamfikisha Nyerere kwenye madras ya Sheikh Hassan bin Amir Mtaa wa Udoe, Idd Faiz na nduguye Idd Tosiri wanamchukua ndani ya basi la Bagamoyo hadi kwa Sheikh Mohamed Ramia...wanamwakikishia kuwa wapo pamoja nae kwa kheri na shari.


Hawa ni sehemu ya watu aliokutana nao. Hao ndio uliowaona lakini kuna wakina John (Rupia),Joseph Kasella Bantu, Patrick Kunambi, Joseph Kimalando, Kirilo Japhet. Unasahau mchango mkubwa alioutoa Oscar Kambona, ambaye alikuwa Katibu wa kwanza wa kudumu ambae mshahara wake ulitokana na ada za wanachama aliowaingiza TANU. Unapuuzia mchango wa wakina Munanka na Bomani. Mnadai kuwa ndugu zenu walisahauliwa, mbona wakina Kambona tulifikia hatua ya kuwaimbia nyimbo za kuwatukana wakati wa mchakamchaka? Wakati wote huo ndugu zenu wakiachiwa kufanya biashara na kujilimbikizia utajiri katika nchi ambapo wengine hata kufuga kuku ilikuwa nongwa! Huyo Oscar alikuwa Muislamu? Huyo Kasella Bantu alikuwa muislamu?

Leo hii mnazunguka mkilaani mnachokiita mfumo kristo wakati nchi yenu toka ipate uhuru imekuwa ikibebwa na nchi za Nordic ambako asilimia 90 ya watu wake ni wakristu! Mnalalamika kuwa kodi zenu zinafaidia makanisa wakati mkisahau kuwa mnatulaumu kwa kuhodhi ajira na utajiri ambayo inatufanya kuwa wachangiaji wakubwa wa kodi katika nchi hii, kwa hiyo ni kodi ya wamisheni ndiyo tunayoizungumzia hapa!

Ndipo sasa nikatiwa katika ma "journals" na nikatiwa katika mradi wa Dictionary of African Biographies (DAB), Oxford University Press New York wakishirikiana na Harvard. Hii ni kwa sababu nilikuja na kitu kipya katika duru za kisomi.


Hapa una exaggerate tena. Mradi wa DAB uliokuwa chini ya W.E.B. Du Bois Institu ulikuwa na dhamira wa kukusanya maandiko mengi iwezekanavyo inayohusu waafrika, na "article" ilikuwa mojawapo na si kwa sababu uliandika kitu kipya katika duru ya usomi. Hauwezi kuandika historia ya ujerumani bila kugusa Mein Kampf. Kwa kufanya hivi hakutamaanisha kuwa unakubaliana na vyote vilivyoandikwa mle !

Hivi kweli tumefika mahali pa kudai kuenziwa kwa sababu Mwalimu aliwahi kulala kwenu, au mama yake alikuwa shoga na mama yenu, au mjomba wenu alimpakiza kwenye baiskeli n.k. Wengi tu walifanya yote hayo na zaidi na fadhila waliyopewa ni nchi yao kupata uhuru. Kwa wengi wao, hiyo ilikuwa thawabu tosha!

Amandla.....

 
quote_icon.png
By Mohamed Said
Katika moja ya nchi za nje nilipangiwa mnakasha mimi bila ya kujua kumbe wale host wa ule mnakasha ni "staunch Catholics" hili ni kundi la wasomi na mabingwa katika historia ya Tanzania. Mnakasha jioni baada ya L 'Asr. Mimi hili na lile sina wala siwajui kama hawa ni Catholics mie nimewachukulia kuwa ni "scholars" wa African history."
Fundi Mchundo hapo juu kweli ulisoma katikati ya mistari. Udini umemjaa MS kama yale magunia ya lumbesa ya mkaa!
 
aksanteni wadau itapendeza kuwepo na mijadala moto moto kama kaa huu kwenye mambo kama uchumi na bishara kuhusu GDP, Uwekezaji, Kilimo Kwanza, Muda wa elimu Tanzania,Life epectancy ya taznaia na factor zake, etc
 
aksanteni wadau itapendeza kuwepo na mijadala moto moto kama kaa huu kwenye mambo kama uchumi na bishara kuhusu GDP, Uwekezaji, Kilimo Kwanza, Muda wa elimu Tanzania,Life epectancy ya taznaia na factor zake, etc
Mkuu, niliwahi kuwaambia wadau kuhusiana na hii historia iliyo sahauliwa, na hata watu waliojitolea katika harakati za kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika, nikasema kwamba kama bwana Mohammed Said yeye anaelelzea wakaazi wa Kariakoo na vitongoji vyake, basi na mwingine atufahamishe wanaharakati wengine kutoka maeneo tofauti na Gerezani.

Uko mikoani kama vile Mwanza, Shinyanga, Musoma, Kagera, Lindi, Mtwara. Sumbawanga, sidhani kote uko kutakosekana hao mashujaa, ambao leo hawatajwi.

Lakini kwa bahati ghafi watu wamakurupuka na kuanza kuzozana pasipo na sababu za maana. Bwana Mohammed Said haawezi yeye kuelezea kwa kina wale walioshiriki kugombea uhuru wanaotoka mikoa ya mbali, sasa basi aje mwingine aelezee wazee wetu wengine kutoka mikoa mingine, haijalishi ni dini au kabila gani, tunachotaka watu watajwe kwa marefu na mapana yao.
 
Mkuu, niliwahi kuwaambia wadau kuhusiana na hii historia iliyo sahauliwa, na hata watu waliojitolea katika harakati za kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika, nikasema kwamba kama bwana Mohammed Said yeye anaelelzea wakaazi wa Kariakoo na vitongoji vyake, basi na mwingine atufahamishe wanaharakati wengine kutoka maeneo tofauti na Gerezani.

Uko mikoani kama vile Mwanza, Shinyanga, Musoma, Kagera, Lindi, Mtwara. Sumbawanga, sidhani kote uko kutakosekana hao mashujaa, ambao leo hawatajwi.

Lakini kwa bahati ghafi watu wamakurupuka na kuanza kuzozana pasipo na sababu za maana. Bwana Mohammed Said haawezi yeye kuelezea kwa kina wale walioshiriki kugombea uhuru wanaotoka mikoa ya mbali, sasa basi aje mwingine aelezee wazee wetu wengine kutoka mikoa mingine, haijalishi ni dini au kabila gani, tunachotaka watu watajwe kwa marefu na mapana yao.
Mkuu nadhani kinachogomba hapa ni matumizi ya lugha halafu alichokiandika Mohammed Said ni kitabu ambacho huwezi kubadilisha yaliyoandikwa kwa kutoa habari nyingine iliyo sawia na hii kutoka bara au mikoani.

Na sii kweli kwamba MS hafahamu historia na mchango wa wazee wengine wa bara anawajua vizuri isipokuwa alikuwa na lengo ktk uandishi wake na hoja yake na ndio sababu anakosolewa hivyo kuifanya historia ya Uhuru wa Tanganyika kama alivyoandika kuwa na mapungufu kibao. Binafsi nimemuuliza kuhusu Cecil Matola na akashindwa hata kuelewa kama alikuwa mwenyekiti na rais wa kwanza wa TAA hadi alipokufa mwaka 1931 sasa sielewi ka a anafanya makusudi au kweli alikuwa hajui. na kama alikuwa hajui basi bila shaka historia yake haijakamilika..

Jambo jingine sikuona mahala popote MS akisema wale Wakristu walioshiriki mwanzo katika harakati za Uhuru walikuwa wakiwakilisha Wakristu ama watu wa bara. hii yote kwa pamoja inatupa picha mbaya yenye lengo la kupandikiza chuki baina ya Waislaam na Wakristu kitu ambacho binafsi sioni faida yake. Na hakuna mtu anayepinga mchango wa hawa wazee wetu ktk harakati za Uhuru isipokuwa tunachosema walishiriki kama Watanzania wenye uzalendo na ari ya kujitawala kama walivyokuwa wakristu na wapagan wengine waliojiunga pamoja.

Ni katika fikra hizi za mgawanyiko ambazo pengine ni mavuno na athari za mfumoKristu ndizo zilipelekea watu kuamini NCCR ni chama cha Wachagga, CUF ni chama cha Waislaam na Chadema chama cha Wakristu ktk kutuza fear, kwani kinachotazamwa hapa ni kina nani waasisi wa vyama hivi kuwa ndio sura ya harakati. Haipendezi hata kidogo isipokuwa inaonyesha jinsi tulivyogawanyika kifikra na tulivyo nyuma ktk mapana ya kujenga hoja..
 
Mkuu nadhani kinachogomba hapa ni matumizi ya lugha halafu alichokiandika Mohammed Said ni kitabu ambacho huwezi kubadilisha yaliyoandikwa kwa kutoa habari nyingine iliyo sawia na hii kutoka bara au mikoani.

Na sii kweli kwamba MS hafahamu historia na mchango wa wazee wengine wa bara anawajua vizuri isipokuwa alikuwa na lengo ktk uandishi wake na hoja yake na ndio sababu anakosolewa hivyo kuifanya historia ya Uhuru wa Tanganyika kama alivyoandika kuwa na mapungufu kibao. Binafsi nimemuuliza kuhusu Cecil Matola na akashindwa hata kuelewa kama alikuwa mwenyekiti na rais wa kwanza wa TAA hadi alipokufa mwaka 1931 sasa sielewi ka a anafanya makusudi au kweli alikuwa hajui. na kama alikuwa hajui basi bila shaka historia yake haijakamilika..

Jambo jingine sikuona mahala popote MS akisema wale Wakristu walioshiriki mwanzo katika harakati za Uhuru walikuwa wakiwakilisha Wakristu ama watu wa bara. hii yote kwa pamoja inatupa picha mbaya yenye lengo la kupandikiza chuki baina ya Waislaam na Wakristu kitu ambacho binafsi sioni faida yake. Na hakuna mtu anayepinga mchango wa hawa wazee wetu ktk harakati za Uhuru isipokuwa tunachosema walishiriki kama Watanzania wenye uzalendo na ari ya kujitawala kama walivyokuwa wakristu na wapagan wengine waliojiunga pamoja.

Ni katika fikra hizi za mgawanyiko ambazo pengine ni mavuno na athari za mfumoKristu ndizo zilipelekea watu kuamini NCCR ni chama cha Wachagga, CUF ni chama cha Waislaam na Chadema chama cha Wakristu ktk kutuza fear, kwani kinachotazamwa hapa ni kina nani waasisi wa vyama hivi kuwa ndio sura ya harakati. Haipendezi hata kidogo isipokuwa inaonyesha jinsi tulivyogawanyika kifikra na tulivyo nyuma ktk mapana ya kujenga hoja..

Mkandara,
Inaonekana unamiss point ya mjadala huu. Kuna issue iliyotokea kabla ya Uhuru na baada ya Uhuru. Hoja inayojengwa hapa ni- upotoshwaji wa historia iliyotengenezwa na pro-Nyerere.
Point-Mchango wa Waislamu ktk Uhuru na matokeo baada ya Uhuru. Dhulma iliyofanywa na Nyerere ktk kurudisha maendeleo ya Waislamu baada ya Uhuru.
 
Fundi Mchundo hapo juu kweli ulisoma katikati ya mistari. Udini umemjaa MS kama yale magunia ya lumbesa ya mkaa!

Sweke34,

Ndugu yangu nikuambie kweli. Uislam naupenda wala sijapata kuona aibu kunasibishwa na Uislam na Waislam.

Wala usitaabike katika hilo.

Nimepata kuambiwa, "Mohamed leo kama si huu Uislam weko ungekuwa mbali sana ungekuwa na cheo kikubwa sana nchi hii maana unazo "skills" zinazohitajika sana lakini mh! huo Uislam wako bwana!"

Wamebaki na vyeo vyao nami nimebaki na Uislam wangu kama ulivyoshuhudia na kueleza hapa jamvini.

Wala moyo wangu haujasononeka kuwaona wenye elimu finyu ndiyo walio juu yangu kwa vyeo.
Alhamdulilah.

Mohamed
 
Sweke34,

Ndugu yangu nikuambie kweli. Uislam naupenda wala sijapata kuona aibu kunasibishwa na Uislam na Waislam.

Wala usitaabike katika hilo.

Nimepata kuambiwa, "Mohamed leo kama si huu Uislam weko ungekuwa mbali sana ungekuwa na cheo kikubwa sana nchi hii maana unazo "skills" zinazohitajika sana lakini mh! huo Uislam wako bwana!"

Wamebaki na vyeo vyao nami nimebaki na Uislam wangu kama ulivyoshuhudia na kueleza hapa jamvini.

Wala moyo wangu haujasononeka kuwaona wenye elimu finyu ndiyo walio juu yangu kwa vyeo.
Alhamdulilah.

Mohamed

Ni "skills" gani hizo unazozizungumzia? Labda uwezo wa kuandika hadithi na soga. Hivi kweli ukarani wa Kampuni ya meli unahitaji "Uislamu weko" ili ufanikiwe kikazi?
 
Unaamini vipi kuwa alikisoma? Au kwa vile alikuwa msomi basi kila kitabu kilichompitia unadhani alikisoma? Haujui msomi anachagua kipi kitamsaidia na kipi hakina tija kwake. Halafu unaditiki kusema kuwa "hakuthubutu" kuandika kupinga kilichoandikwa! Nitajie kuna vitabu vingapi alivyoandika Mwalimu kiasi cha kuamini kuwa hata cha Mohamed Said asingechelea kukiandikia?



Cha ajabu kipi Tanzania kuwa na dhulma. Unataka kutuambia kuwa huko uliko hakuna dhulma? Huko wananchi wako huru kukemea dhulma na udhalimu wanaotendewa na watawala wao? Tunachokataa ni kudai kuwa Tanzania kuna institutionalised dhulma dhidi ya kikundi fulani inayotokana na mtazamo wa kidini. Dhulma ipo lakini si hiyo mnaotaka kutuaminisha.

Na hayo maneno unayodai ni ya Bob Marley, yalisemwa kwanza na Abraham Lincoln.



Hapa ndipo ulipojivua gamba. Mnawafahamisha ili iwaje? Na hiyo hatari ni ipi?



Ala! Sikujua hili. Kuwa mkatoliki hawezi kuwa scholar wa historia ya kiafrika hata kama nae ni muafrika. Kumbe ndio maana Nyerere anawaudhi! Anayeweza kuzungumza ukweli kuhusu historia yetu ni muislamu peke yake!



Na alipoenda unyakyusani, wakina Mwakangale waliposalimia jamii kwa kusema "ugonile" nayo ni Nyakyusa symbols katika kupigania uhuru wa Tanganyika?
Unataka kweli kutuaminisha kuwa katika jopo la unaowaita wasomi (ambalo lina utata maana sifa hiyo uliishawanyang'anya na kuwabakizia ya ukatoliki) walishangaa kusikia kuwa katika sehemu iliyojaa waislamu, dua ikatangulia kusomwa? Bila shaka waliduwaa kukuona unachukua kitu kama hicho kuwa ni ishara wa pivotal role ambayo uislamu ulibeba katika kupigania uhuru wa nchi yetu.



Hawa ni sehemu ya watu aliokutana nao. Hao ndio uliowaona lakini kuna wakina John (Rupia),Joseph Kasella Bantu, Patrick Kunambi, Joseph Kimalando, Kirilo Japhet. Unasahau mchango mkubwa alioutoa Oscar Kambona, ambaye alikuwa Katibu wa kwanza wa kudumu ambae mshahara wake ulitokana na ada za wanachama aliowaingiza TANU. Unapuuzia mchango wa wakina Munanka na Bomani. Mnadai kuwa ndugu zenu walisahauliwa, mbona wakina Kambona tulifikia hatua ya kuwaimbia nyimbo za kuwatukana wakati wa mchakamchaka? Wakati wote huo ndugu zenu wakiachiwa kufanya biashara na kujilimbikizia utajiri katika nchi ambapo wengine hata kufuga kuku ilikuwa nongwa! Huyo Oscar alikuwa Muislamu? Huyo Kasella Bantu alikuwa muislamu?

Leo hii mnazunguka mkilaani mnachokiita mfumo kristo wakati nchi yenu toka ipate uhuru imekuwa ikibebwa na nchi za Nordic ambako asilimia 90 ya watu wake ni wakristu! Mnalalamika kuwa kodi zenu zinafaidia makanisa wakati mkisahau kuwa mnatulaumu kwa kuhodhi ajira na utajiri ambayo inatufanya kuwa wachangiaji wakubwa wa kodi katika nchi hii, kwa hiyo ni kodi ya wamisheni ndiyo tunayoizungumzia hapa!



Hapa una exaggerate tena. Mradi wa DAB uliokuwa chini ya W.E.B. Du Bois Institu ulikuwa na dhamira wa kukusanya maandiko mengi iwezekanavyo inayohusu waafrika, na "article" ilikuwa mojawapo na si kwa sababu uliandika kitu kipya katika duru ya usomi. Hauwezi kuandika historia ya ujerumani bila kugusa Mein Kampf. Kwa kufanya hivi hakutamaanisha kuwa unakubaliana na vyote vilivyoandikwa mle !

Hivi kweli tumefika mahali pa kudai kuenziwa kwa sababu Mwalimu aliwahi kulala kwenu, au mama yake alikuwa shoga na mama yenu, au mjomba wenu alimpakiza kwenye baiskeli n.k. Wengi tu walifanya yote hayo na zaidi na fadhila waliyopewa ni nchi yao kupata uhuru. Kwa wengi wao, hiyo ilikuwa thawabu tosha!

Amandla.....

[/B][/B][/B][/B][/B]

Fundi Utumbo,

Umeingia na ghadhabu.

Kwanza Oscar Kambona hakuwa katibu wa kwanza. Katibu wa kwanza ni Zuberi Mtemvu. Nafasi hiyo ilipata vilevile kushikwa na Idd Faizi Mafongo aliyekuwa mweka hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika hii hata Kambona hajafika ofisi ya TANU, New Street.

Haya najua ni makosa ya kawaida sana maana hivi ndivyo ilivyo katika historia rasmi. Historia nzima imeandikwa Idd Faiz hayumo lakini yeye ndiye aliyeanzisha TANU Press Mtaa wa Mchikichi palipokuwa panachapwa "Sauti ya TANU." Idd Faiz ndiye aliyekuwa mwekafedha za TANU safari ya Nyerere UNO 1955.

Hayo mengine ulosema ya fadhila inasikitisha kuwa kwa watu wanaosikia haya kwa mara ya kwanza huwa wanaumia wanahisi kama masimango lakini soma ukiwa umetulia utaona ni maelezo ya moyo wa wazalendo ulivyokuwa wakati wa uhuru na kwangu mimi ni historia ya wazee wangu na naieleza kwa mtazamo huo wala sina nia mbaya ya kutusi.

Pitia maelezo yangu kwa umakini hilo bila shaka utaliona. Wazee wetu walikirimiana na kuadhimishana sana na hayo ndiyo yalikuwa maisha yao.

Siku nilipomfanyia Dossa Aziz mahojiano kanieleza mengi kuhusu baba yangu nk. nk. Titi Mohamed naye ni hivyo hivyo. baba yangu ananiambia yeye kajuana na Nyerere nyumbani kwa Abdu Sykes Mtaa wa Stanley nk. nk.

Mzee Abdallah mhudumu ofisi ya Abdu Sykes Kariakoo Market ananihadithia akimuona Nyerere ofisini kwa Abdu Sykes akisoma gazeti la "Tanganyika Standard" nk. nk.

Shariff Attas anasema mimi nikila na Nyerere chakula cha mchana kila siku nk. nk. wakiona fahari kuwa katika historia ya Nyerere.
Haya yote ni katika miaka ya mwanzoni 1950.

Habari hizi ndizo zinazofanya kitabu changu kipendeze kuliko kitabu chochote kilichopata kuandikwa kuhusu historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Umesema mengi siwezi kuyajibu yote maana mengine nimeyaandika katika kitabu changu...Kasella Bantu, John Rupia, Oscar Kambona, Chifu Kunambi inahitaji kusoma faharasha (index) utapata habari zao.

Mohamed
 
Historia iko hivi kwa uchache:
-Rais wa kwanza wa TANU ni JKN.
-Waziri Mkuu wa kwanza wa Tanganyika ni JKN.
-Rais wa kwanza wa Tanganyika JKN.
-Rais wa kwanza wa JMT ni JKN.
- Mwenyekiti wa kwanza wa CCM ni JKN.
Yakibadilika haya, historia ya NCHI hii itaandikwa UPYA. Tutaingiza humo na wazee wetu, DINI zetu na mifumo yetu. Vinginevyo, hadithi hadithi, uongo njoo, utamu kolea viendelee.
 
Barubaru;2772234]Sasa kutokana na historia hiyo kumeweka wazi na kumtaja Nyerere moja kwa moja naye kama kutokana na kutajwa kule kulikuwa kuna lugha za kuongezewa au kupunguziwa jambo dhidi yake na kwa sie tunavyomjua alivyokuwa anapenda kutukuzwa ( nakumbuka alipenda kusema kuwa zidumu fikra za mwenyekiti wa CCM hata zikiwa pumba)basi lazima angetia neno hapo.
lakini kwa kuwa alikaa kimya hata kwenye hotba zake hajagusia kupinga basi pasi na shaka yoyote kilichoandikwa kitakuwa kimesahaulika na hivyo ni budu kiongezewe kwenye historia yenu.Sioni kwa nini watu wanakuwa wabishi wa kuelewa na kusikiliza darsa mwanzo mpaka mwisho kabla kuleta masuala yenye muelekeo na muono
Ahal yangu Baru baru naona umenasa katika mtego wa Mohamed.
Niwaombe wanajamvi kurejea yafuatayo ili waelewe nini watu wanasimamia.
1. Kuna watu wanasoma makala za Mohamed kwa mara ya kwanza(jambo zuri kujisomea na kujifunza) na kuna wanaodurusu makala hizo kwa miaka mingi iliyopita

2. Kuna watu wanasoma wakiongozwa na imani kuwa Mohamed ni mjuvi kuliko wengine na hawa ndio wanaotishika wakisikia amekwenda ulaya na Marekani. Bahati mbaya woga wao umefikia mahali wanadhani kumwambia Mohamed 'si kweli' ni dhabi kubwa na ni kuukataa uislam.

3. Kuna watu wanasoma katikati ya mistari na kuleta fikra kwa kile wanachokisoma. Hawa ndio Mohamed asiowataka katika mnakasha.

Kwanini watu wanahoji makala za Mohamed
1. Mohamed anajaribu kutumia kalamu kuhadaa umma kuwa anaeleza historia ya Tanganyika. Ukweli ni kuwa anacho chake moyoni.

2. Kile anachokiita historia si historia ni masimulizi anayoyaweka katika hali ya kumpa majibu ya kile anachodhani na kuamini.

3. Mohamed anasema amefanya utafiti, lakini utafiti hauongozwi na hisia au chuki. Utafiti ni kitu kinachojidhiri hata kama kinamhukumu baba yako.

4. Mohamed ameficha ukweli wa mambo ambayo yanakinzana na hoja aliyokusudia, hapo anapotosha ukweli kwa makusudi.

Nikupe dondoo za chuki za Mohamed.
Kumfanya Nyerere kama chanzo cha matatizo na kukwepa ukweli kuwa ni wazee wake ndio chanzo kama ni kweli anachodhani ni uonevu wa Nyerere. Haiingii akilini mtu mmoja ashinde wenyeji wake 170 ndani ya baraza la wazee na asilimia 98 ndani ya kamati kuu.

Kuchonganisha watanganyika kwa kutumia dini. Anachuki na hufanya kila jitihada neno la kanisa au katoliki litokee hata pasipo na uhusiano.
Mfano .........mabucha ya nguruwe owned by christiantraders. Kwamba wauza nguruwe ni wakristo na kushambuliwa kwao ni kwasababu ya imani yao. Mohamed anasema .....christian lecturers at UDSM. Kwamba waliokataa kutumia kitabu chake ni wahadhiri wa kikristo kana kwamba chuo kikuu cha Dar ni mali ya kanisa.
Anaendelea..... muslim attacked christian property after 70 years. Hakueleza miaka 70 kuanzia lini maana nchi yetu ina maiaka 50. Lakini kibaya zaidi ni kukwepa ukweli kuwa hakuna kanisa lilioshambuliwa. na mifano mingine 101 n.k

Mfano wa Upotoshaji ni pale anaposema vurugu za mabucha ya nguruwe ni kutokana na umasikini wa Kigoma, Mtwara, Tabora na Kilwa.

Ukisoma masimulizi ya Mohamed kwa uangalifu hutachelea kusema Nyerere ni genius, hakuwa na sababu zozote za maana za kumjibu Mohamed hata kwa bahati mbaya.

Tunachokikataa si historia ya wazee wake wa Gerezani, lakini asiseme ni historia ya Tanganyika maana ushahidi wa kuwa si ya Tanganyika anao Sykes.

Tunachokataa ni hila za Mohamed za kupanda mbegu chafu za chuki za kidini akiwa amejificha nyuma ya taasisi ya siri isiyojulikana.
Tunachokataa ni kuwadanganya watu waamini kuwa wameonewa hata kama watashinda wakiwa wamelala kwenye mikeka.
Tunachokataa ni uchonganishi wa wananchi kuwa Kilwa ni masikini zaidi ya Singida kwa sababu ya dini yao.
Tunachokataa ni kuzua takwimu asizoweza kuzitetea ili mradi tu akidhi kiu yake ya kuleta vurugu.
Tunachokataa ni kuwagawa watanganyika ili washindwe kuyakabili matatizo yao kwa pamoja kwa maneno ya udanganyifu na upotofu.

Dhana ya kukaa kimya aendelee kupotosha bila kumwambia 'wait a minute' hapana. Hapana kwasababu hapa ni JF haonewi mtu wala hahurumiwi mtu. Haogopwi mtu kwa safari zake au kipara chake, kinachoheshimiwa ni hoja zenye mashiko.
Tutachambua neno moja hadi jingine kwa uyakinifu na utilimilifu tukiongozwa na Utanzania na mapenzi ya nchi yetu.
 
Mkandara,
Inaonekana unamiss point ya mjadala huu. Kuna issue iliyotokea kabla ya Uhuru na baada ya Uhuru. Hoja inayojengwa hapa ni- upotoshwaji wa historia iliyotengenezwa na pro-Nyerere.
Point-Mchango wa Waislamu ktk Uhuru na matokeo baada ya Uhuru. Dhulma iliyofanywa na Nyerere ktk kurudisha maendeleo ya Waislamu baada ya Uhuru.
Watu walitumwa na misikiti au Uislamu wao kudai uhuru wa NCHI hii? Mwalimu alitumwa na kanisa kuungana na wazee hawa kudai uhuru? Dhulma gani hasa aliifanya Mwalimu? Aliandika historia ya Nchi hii akawasahau wazee wetu hawa?
 
Watu walitumwa na misikiti au Uislamu wao kudai uhuru wa NCHI hii? Mwalimu alitumwa na kanisa kuungana na wazee hawa kudai uhuru? Dhulma gani hasa aliifanya Mwalimu? Aliandika historia ya Nchi hii akawasahau wazee wetu hawa?

WC,

Nakuomba uwe na subira.

Nimeweka somo sasa tuko 1961 Tanganyika ni nchi huru, Nyerere kakabidhiwa nchi kwa salama sasa tunaingia 1962 Sheikh Hassan bin Amir anahamasisha Waislam katika elimu na unafanyika mkutano wa kwanza wa Waislam (Muslim Congress, 1962).

Ni kisa kizuri cha kusisimua.
Tulia tembea na Sheikh Hassan bin Amir...

Utamjua Nyerere, Kanisa Katoliki na mustakbali mzima wa nchi yetu ilipotoka hadi hapa tulipofika miaka 50 ya uhuru.
Historia hii huwezi kuipata popote duniani ila kwa Mohamed Said.

Hao mabingwa wa African History Northwestern University, Chicago wameisoma kwangu na mimi nimeisoma kwa wanafunzi wa Sheikh Hassan bin Amir.

Alhamdulilah.

Mohamed
 
Ahal yangu Baru baru naona umenasa katika mtego wa Mohamed.
Niwaombe wanajamvi kurejea yafuatayo ili waelewe nini watu wanasimamia.
1. Kuna watu wanasoma makala za Mohamed kwa mara ya kwanza(jambo zuri kujisomea na kujifunza) na kuna wanaodurusu makala hizo kwa miaka mingi iliyopita

2. Kuna watu wanasoma wakiongozwa na imani kuwa Mohamed ni mjuvi kuliko wengine na hawa ndio wanaotishika wakisikia amekwenda ulaya na Marekani. Bahati mbaya woga wao umefikia mahali wanadhani kumwambia Mohamed 'si kweli' ni dhabi kubwa na ni kuukataa uislam.

3. Kuna watu wanasoma katikati ya mistari na kuleta fikra kwa kile wanachokisoma. Hawa ndio Mohamed asiowataka katika mnakasha.

Kwanini watu wanahoji makala za Mohamed
1. Mohamed anajaribu kutumia kalamu kuhadaa umma kuwa anaeleza historia ya Tanganyika. Ukweli ni kuwa anacho chake moyoni.

2. Kile anachokiita historia si historia ni masimulizi anayoyaweka katika hali ya kumpa majibu ya kile anachodhani na kuamini.

3. Mohamed anasema amefanya utafiti, lakini utafiti hauongozwi na hisia au chuki. Utafiti ni kitu kinachojidhiri hata kama kinamhukumu baba yako.

4. Mohamed ameficha ukweli wa mambo ambayo yanakinzana na hoja aliyokusudia, hapo anapotosha ukweli kwa makusudi.

Nikupe dondoo za chuki za Mohamed.
Kumfanya Nyerere kama chanzo cha matatizo na kukwepa ukweli kuwa ni wazee wake ndio chanzo kama ni kweli anachodhani ni uonevu wa Nyerere. Haiingii akilini mtu mmoja ashinde wenyeji wake 170 ndani ya baraza la wazee na asilimia 98 ndani ya kamati kuu.

Kuchonganisha watanganyika kwa kutumia dini. Anachuki na hufanya kila jitihada neno la kanisa au katoliki litokee hata pasipo na uhusiano.
Mfano .........mabucha ya nguruwe owned by christiantraders. Kwamba wauza nguruwe ni wakristo na kushambuliwa kwao ni kwasababu ya imani yao. Mohamed anasema .....christian lecturers at UDSM. Kwamba waliokataa kutumia kitabu chake ni wahadhiri wa kikristo kana kwamba chuo kikuu cha Dar ni mali ya kanisa.
Anaendelea..... muslim attacked christian property after 70 years. Hakueleza miaka 70 kuanzia lini maana nchi yetu ina maiaka 50. Lakini kibaya zaidi ni kukwepa ukweli kuwa hakuna kanisa lilioshambuliwa. na mifano mingine 101 n.k

Mfano wa Upotoshaji ni pale anaposema vurugu za mabucha ya nguruwe ni kutokana na umasikini wa Kigoma, Mtwara, Tabora na Kilwa.

Ukisoma masimulizi ya Mohamed kwa uangalifu hutachelea kusema Nyerere ni genius, hakuwa na sababu zozote za maana za kumjibu Mohamed hata kwa bahati mbaya.

Tunachokikataa si historia ya wazee wake wa Gerezani, lakini asiseme ni historia ya Tanganyika maana ushahidi wa kuwa si ya Tanganyika anao Sykes.

Tunachokataa ni hila za Mohamed za kupanda mbegu chafu za chuki za kidini akiwa amejificha nyuma ya taasisi ya siri isiyojulikana.
Tunachokataa ni kuwadanganya watu waamini kuwa wameonewa hata kama watashinda wakiwa wamelala kwenye mikeka.
Tunachokataa ni uchonganishi wa wananchi kuwa Kilwa ni masikini zaidi ya Singida kwa sababu ya dini yao.
Tunachokataa ni kuzua takwimu asizoweza kuzitetea ili mradi tu akidhi kiu yake ya kuleta vurugu.
Tunachokataa ni kuwagawa watanganyika ili washindwe kuyakabili matatizo yao kwa pamoja kwa maneno ya udanganyifu na upotofu.

Dhana ya kukaa kimya aendelee kupotosha bila kumwambia 'wait a minute' hapana. Hapana kwasababu hapa ni JF haonewi mtu wala hahurumiwi mtu. Haogopwi mtu kwa safari zake au kipara chake, kinachoheshimiwa ni hoja zenye mashiko.
Tutachambua neno moja hadi jingine kwa uyakinifu na utilimilifu tukiongozwa na Utanzania na mapenzi ya nchi yetu.

Nguruvi3,

Umezungumza mengi lakini niko katikati ya darsa ziwezi kulivunja wanafunzi wana "full concentration na mwalimu..."

Nitakujibu moja tu kuhusu mapenzi ya nchi hii.

Wewe (samahani kwa kukunyooshea kidole) na wengine mfano wa wewe hamuwezi kuwa na mapenzi ya nchi hii kupita Said Chamwenyewe aliyeiletea TANU wanachama wake wa mwanzo kutoka Rufiji safari akenda kwa baiskeli wala haombi masurufu na akirudi Dar es Salaam anarudi na hela za kadi alouza anamkabidhi, Idd Faiz Mafongo mweka hazina wa TANU.

Wewe na mfano wa wewe hamuwezi kuwa na mapenzi ya nchi hii kupita Abdulwahid Sykes aliyejitolea kwa hali na mali kuunda TANU na hakuna ajuae marehemu Abdu alitoka kiasi gani kwa TANU katika uhai wake.

Wewe na mfano wako hamuwezi kuwa na mapenzi ya nchi kushinda Dossa Aziz ambae kafa kafilisika, masikini.

Wewe huwezi kuipenda nchi hii kuliko wengi wengi wengi katika wazee wangu ambao wamekufa na kinyongo...nimeshaeleza humu habari za Mshume Kiyate ambae kuna mtu kamkashifu kuwa ni mpeleka kabichi.

Wewe huwezi kuipenda nchi hii kushinda babu yangu Salum Abdallah aliyeweka historia Tanganyika kwa kuongoza mgomo uliodumu siku 82 mwaka 1960...alijitolea kwa mali na hali kuunga mkono harakati za uhuru...akaishia kuwekwa kizuizini...Ali Migeyo...Dharura biti Abdulrahman, Yusuf Ngozi, Tatu biti Mzee, Asha Ngoma, Mama biti Maalim, Yusuf Chembera, Salum Mpunga,Fundi Muhindi, Bilal Rehani Waikela, Sheikh Yusid Badi orodha ni ndefu sana, sana, sana, sana...

Naishia hapa nina darsa linanisubiri Insha Allah.

Mohamed
 
Nguruvi3,

Umezungumza mengi lakini niko katikati ya darsa ziwezi kulivunja wanafunzi wana "full concentration na mwalimu..."

Nitakujibu moja tu kuhusu mapenzi ya nchi hii.

Wewe (samahani kwa kukunyooshea kidole) na wengine mfano wa wewe hamuwezi kuwa na mapenzi ya nchi hii kupita Said Chamwenyewe aliyeiletea TANU wanachama wake wa mwanzo kutoka Rufiji safari akenda kwa baiskeli wala haombi masurufu na akirudi Dar es Salaam anarudi na hela za kadi alouza anamkabidhi, Idd Faiz Mafongo mweka hazina wa TANU.

Wewe na mfano wa wewe hamuwezi kuwa na mapenzi ya nchi hii kupita Abdulwahid Sykes aliyejitolea kwa hali na mali kuunda TANU na hakuna ajuae marehemu Abdu alitoka kiasi gani kwa TANU katika uhai wake.

Wewe na mfano wako hamuwezi kuwa na mapenzi ya nchi kushinda Dossa Aziz ambae kafa kafilisika, masikini.

Wewe huwezi kuipenda nchi hii kuliko wengi wengi wengi katika wazee wangu ambao wamekufa na kinyongo...nimeshaeleza humu habari za Mshume Kiyate ambae kuna mtu kamkashifu kuwa ni mpeleka kabichi.

Wewe huwezi kuipenda nchi hii kushinda babu yangu Salum Abdallah aliyeweka historia Tanganyika kwa kuongoza mgomo uliodumu siku 82 mwaka 1960...alijitolea kwa mali na hali kuunga mkono harakati za uhuru...akaishia kuwekwa kizuizini...Ali Migeyo...Dharura biti Abdulrahman, Yusuf Ngozi, Tatu biti Mzee, Asha Ngoma, Mama biti Maalim, Yusuf Chembera, Salum Mpunga,Fundi Muhindi, Bilal Rehani Waikela, Sheikh Yusid Badi orodha ni ndefu sana, sana, sana, sana...

Naishia hapa nina darsa linanisubiri Insha Allah.

Mohamed

Ahsantum kwa kutujali sisi tunaofuatilia mnakasha huu kwa makini sana. Kwani kila wakti wenzetu wamekuwa ima wanataka wageuze mada au kurejesha nyuma mnakasha kwa kuuliza masuala yasiyo msingi mkuu wa mada husika.

maalim tafadhwal endelea....
 
WC,

Nakuomba uwe na subira.

Nimeweka somo sasa tuko 1961 Tanganyika ni nchi huru, Nyerere kakabidhiwa nchi kwa salama sasa tunaingia 1962 Sheikh Hassan bin Amir anahamasisha Waislam katika elimu na unafanyika mkutano wa kwanza wa Waislam (Muslim Congress, 1962).

Ni kisa kizuri cha kusisimua.
Tulia tembea na Sheikh Hassan bin Amir...

Utamjua Nyerere, Kanisa Katoliki na mustakbali mzima wa nchi yetu ilipotoka hadi hapa tulipofika miaka 50 ya uhuru.
Historia hii huwezi kuipata popote duniani ila kwa Mohamed Said.

Hao mabingwa wa African History Northwestern University, Chicago wameisoma kwangu na mimi nimeisoma kwa wanafunzi wa Sheikh Hassan bin Amir.

Alhamdulilah.

Mohamed
Mohamed,
Umejibu maswali yangu? Namshukuru Mwalimu aliyeuona UDINI ukiinyemelea Tanganyika huru mapema akaukemea na kuuzima. Hao akina Sheikh Hassan bin Amir wangeruhusiwa kuendelea na mipango yao hiyo tusingekuwa na Tanzania hii ya sasa ambayo hatugawani vyeo, madaraka, ajira, elimu kwa kigezo cha DINI. Tumshukuru Mungu asiye na DINI kuifanya TANZANIA isiwe na DINI pia.
 
Nguruvi3,

Umezungumza mengi lakini niko katikati ya darsa ziwezi kulivunja wanafunzi wana "full concentration na mwalimu..."

Nitakujibu moja tu kuhusu mapenzi ya nchi hii.

Wewe (samahani kwa kukunyooshea kidole) na wengine mfano wa wewe hamuwezi kuwa na mapenzi ya nchi hii kupita Said Chamwenyewe aliyeiletea TANU wanachama wake wa mwanzo kutoka Rufiji safari akenda kwa baiskeli wala haombi masurufu na akirudi Dar es Salaam anarudi na hela za kadi alouza anamkabidhi, Idd Faiz Mafongo mweka hazina wa TANU.

Wewe na mfano wa wewe hamuwezi kuwa na mapenzi ya nchi hii kupita Abdulwahid Sykes aliyejitolea kwa hali na mali kuunda TANU na hakuna ajuae marehemu Abdu alitoka kiasi gani kwa TANU katika uhai wake.

Wewe na mfano wako hamuwezi kuwa na mapenzi ya nchi kushinda Dossa Aziz ambae kafa kafilisika, masikini.

Wewe huwezi kuipenda nchi hii kuliko wengi wengi wengi katika wazee wangu ambao wamekufa na kinyongo...nimeshaeleza humu habari za Mshume Kiyate ambae kuna mtu kamkashifu kuwa ni mpeleka kabichi.

Wewe huwezi kuipenda nchi hii kushinda babu yangu Salum Abdallah aliyeweka historia Tanganyika kwa kuongoza mgomo uliodumu siku 82 mwaka 1960...alijitolea kwa mali na hali kuunga mkono harakati za uhuru...akaishia kuwekwa kizuizini...Ali Migeyo...Dharura biti Abdulrahman, Yusuf Ngozi, Tatu biti Mzee, Asha Ngoma, Mama biti Maalim, Yusuf Chembera, Salum Mpunga,Fundi Muhindi, Bilal Rehani Waikela, Sheikh Yusid Badi orodha ni ndefu sana, sana, sana, sana...

Naishia hapa nina darsa linanisubiri Insha Allah.

Mohamed
Ni kama vile bila hawa uloowataja hapa Tanganyika isingekuwa huru kamwe! Mwalimu alienda mbali zaidi ya uhuru wa Tanganyika. Anatajwa Msumbiji, Zimbabwe, Afrika Kusini, Namibia,...
 
Mohamed,
Umejibu maswali yangu? Namshukuru Mwalimu aliyeuona UDINI ukiinyemelea Tanganyika huru mapema akaukemea na kuuzima. Hao akina Sheikh Hassan bin Amir wangeruhusiwa kuendelea na mipango yao hiyo tusingekuwa na Tanzania hii ya sasa ambayo hatugawani vyeo, madaraka, ajira, elimu kwa kigezo cha DINI. Tumshukuru Mungu asiye na DINI kuifanya TANZANIA isiwe na DINI pia.

WC,

Njia kuu ya kupata elimu mpya ni kuuwacha ubongo uwe wazi kwanza uingize kisha ndiyo unakaa kitako kufanya tafakuri.

Huyo Sheikh Hassan bin Amir ndiye kwa nyie ni kama Polycarp Pengo. Hassan bin Amir alikuwa Mufti wa Tanganyika na Zanzibar na kamuunga mkono Nyerere. Au hujasoma katika nyuzi za nyuma?
Sasa udini uko wapi?

Baraza la Wazee wa TANU chini ya Sheikh Suleiman Takadir kisha Idd Tulio Waislam watupu wamemuunga mkono Nyerere.
Sasa udini uko wapi?

AMNUT Waislam wameikataa.
Sasa udini uko wapi?

Hebu tulia piga goti kwa mwalimu usome hii historia ambayo nyinyi hamuijui.
Wewe huoni kama hii ni nema kwako?

Wenzako wanaitolea tiketi ya ndege na Five Star Hotel wewe hapa kidole chako tu.

Tulia nimalize Muslim Congress 1962 tuje Muslim Congress 1963 uone sasa mambo yalivyobadilika.
Bilali Rehani Waikela muasisi wa TANU Tabora, 1955 katibu wa EAMWS Western Province kidole machoni na Nyerere.

Nini ugomvi wao na hawa kwa pamoja walipigana bega kwa bega kumng'oa Muingereza Tanganyika?
WC vuta subira majibu yote Insha Allah utayapata.

Mohamed
 
Ni kama vile bila hawa uloowataja hapa Tanganyika isingekuwa huru kamwe! Mwalimu alienda mbali zaidi ya uhuru wa Tanganyika. Anatajwa Msumbiji, Zimbabwe, Afrika Kusini, Namibia,...

WC,

Nakuomba jitulize.
Sipendi niache kukujibu ukapate hisia nimekudharau.

Mohamed
 
"In order to appreciate the impending danger we need to agree thatMuslims are a majority[1]
Mohammed,
Hili ndilo tatizo lako kubwa. Unapokuja na statistics za kupikwa na zisizo sahihi matokeo yake ni kwamba hata conclusions zako zote zinakuwa si sahihi.

Jasusi,

Hapana nimesema kwa kile nilichokiona.

Takwimu hizo zinaweza kuwa si sawa na kwa hakika wapi wengi wapi pungufu si kitu muhimu sana.

Jambo la kutushughulisha ni kuwa na jamii ambayo kuna haki sawa.

Mohamed
 
Back
Top Bottom