Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Mzee Said pamoja na ujuzi wote wa maneno na historia kuna kitu kimoja kiko wazi kuhusiana na hizi 'kazi' zake - amezikariri. Amekariri masimulizi ya utotoni na hata alivyozidi kupata ufahamu zaidi ndivyo hivyo hivyo alivyozidi kuzikariri. Hivyo anachotuelezea ni kile ambacho amekariri kwa kusimuliwa au kujisomea n.k Na hivyo anakirudia na ukiangalia kwa juu juu unaweza kweli kuwa impressed. Tatizo linakuja nipale unapozama chini na kuanza kufuatilia 'kujua'. Kuna tofauti kubwa kati ya kujua na kukariri.

Wapo wanafunzi ambao wanakaririshwa Table na hivyo ukimuambia akuambie table ya 12 anaweza akaiimba yote au 'tebo' ya sita akaiimba yote. Lakini mwanafunzi huyo anaweza asijue kuzidisha kwani ukianzia na table ya 13 au kwenda juu atapata shida au ukianza kuchanganya table na kujumlisha anaweza kushindwa. Lakini mwenye kujua kuzidisha anaweza kujua namna ya kuzidisha namba mbalimbali kwa urahisi kabisa na kwa haraka kuliko hata anayetumia kalamu. Kwa mfano, mtu anajua namba yoyote ukizidisha kwa namba yenye 10, 100, 1000 n.k basi unaongeza tu hiyo idadi ya sifuri na jibu linapatikana.

Kwenye historia au utafiti wa aina kama hii ni hivyo hivyo. Mtu anaweza kukariri matukio muhimu au watu muhimu walifanya nini na ni kile tu ambacho amekaririshwa ndicho pekee anaamini anakijua. Ukijaribu kumtoa tu kwenye kukariri anachanganyikiwa kabisa. Ni sawa na kumuweka swala mbele ya taa ya gari usiku akapigwa macho!

Maswali mengi anayoulizwa Bw. Said na watu wengi tangu kuanza kwa mjadala huu yanahitaji kujua siyo kukariri tu. Kwa mfano, Bw. Said anaweza kusema kuwa "tofauti kati ya Nyerere na Waislamu imeanza baada ya ile congress ya 1963". Sasa hicho ni cha kukariri. Ukitaka kumtoa jaribu kumuonesha kuwa walikuwepo Waislamu kabla ambao walikuwa wanamchukia Nyerere tangu siku ya kwanza ametambulishwa kwao na walimchukia si kwa sababu aliwadhulumu Wailslamu au aliwatendea jambo lolote baya - bali kwa sababu ya Ukatoliki wake. Ukimleta Said kwa hilo anapata shida kwa sababu ni kama kumlazimisha kujua.

Utaona maswali yote anayulizwa majibu yake ni ya kukariri.

SWALI: Kwanini kwa miaka karibu ishirini ambayo ulikuwa unafanyia hii historia 'yako' utafiti hukupata nafasi hata ya kuandika barua kwa Mwalimu Nyerere?

JIBU: Prof. Haroub Othman alishangazwa sana akamwendea Nyerere...

SWALI: Kwanini hadi leo hujawahi kumuuliza au hata kujaribu kwenda kuonana na Mama Maria Nyerere na kumhoji kuhusu Sykes na mtazamo wa Nyerere kuhusu Waislamu wakati akiwa madarakani?

JIBU: Maria Nyerere alikuwa anafahamiana sana na Binti Sudi, Binti Zubeda ambaye alikuwa akiishi mkabala na kwa Bw. Selemani ambaye nje ya nyumba yake tulikuwa tunacheza kombolela!

SWALI: Kwanini kama kweli ulikuwa unataka kuandika historia ya mashujaa 'waliosahauliwa' katika historia hukuwagusa wale ambao hawakuwa Waislamu au wale waliokuwa nje ya Dar?

JIBU: Kama na nyie mna wazee wenu nendeni mkaandike habari zao, miye nimeandika habari za wazee wangu na hiyo ndiyo historia yote ya TAnganyika!

SWALI: Je ni mahali gani ambapo wazee walioshiriki kupigania uhuru walipofanya hivyo kwa sababu ya Uislamu wao na kuwa waliongozwa na imani yao na siyo uzalendo wao kwa Tanganyika na kutaka uhuru uwanufaishe watu wote?

JIBU: Katika kampeni zote zilisomwa dua na Nyerere alikuwa anainamisha kichwa chini ili isomwe Al Fatha na wakati mwingine zilitolewa dua hadi wakatoka machozi!

Sasa mtu ambaye is untrained anaweza kuamini kabisa kuwa Bw. Said anajibu maswali lakini for any objective and trained mind anaweza kuona kuwa maswali hawezi kujibu kwa sababu yatamuondoa kwenye kukariri. Matokeo yake ni kuwa mtazungushana hapo hapo kwenye kukariri hadi mchoke kwa sababu alichokariri yeye ndio ukweli na chochote ambacho kitamfanya afikirie nje ya huko kukariri kutaaribu kabisa. Na ukifikiria sana utaona ni kweli. Wakati mwingine kujiuliza kuhusu kule unachoamini kunaweza kabisa kukusababisha ubadilishe mtazamo wako na kupindua kabisa maisha yako.

Bw. Said akitaka kujua anaweza lakini kujua kuna gharama - na gharama yake ni kuwa kwa kadiri mtu anavyopata ukweli ndivyo anavyoitwa kuufuata na wakati mwingine ukweli ni mgumu sana kuukubali. Ni mtu yule ambaye ana ujasiri wa dhamira yake ndiye pekee anaweza akutafuta ukweli, akauchunguzi na kuuhoji na akiona umethibitika atakuwa tayari kuhama kutoka kuliko alikokuweko.

Ndiyo Yesu alisema mojawapo ya misemo ya kifalsafa ya hali ya juu - 'MTAIFAHAMU KWELI NAYO KWELI ITAWAWEKA HURU" Yoh. 8:32 Ukweli unafungua, unawapa watu sababu ya matumaini, unatuliza moyo na unamuinua mtu kutoka katika hali ya kutokujua. UKWELI wa historia yetu haupatikani katika kitabu cha Bw. Said nayeyote ambaye anasoma ataona kuwa hafunguki! Ila anajikuta anasukumizwa kwenye kifungo cha hatari sana kwenye gereza ambalo nje limeandikwa 'UDINI'. Na huyo anaweza kuanza kujikuta anatumikia hii itikadi ya chuki na atafunguliwa tu pale ambapo yeye mwenyewe atakuwa na ujasiri wa kuhoji anachoambiwa, kuuliza maswali sahihi na akiona majibu hayaji kuunda nadharia za kuelezea kwanini majibu hayaji.

Maswali ambayo yameulizwa ambayo karibu yanafikia 50 sasa hayawezi kujibiwa na Bw. Said kwa sababu yanahusiana na kutafuta ukweli. Kwa vile lengo lake siyo kutafuta ukweli bali kukaririsha watu kile alichosikia basi ni vigumu kabisa kumfanya akubali kuwa kuna vitu ambavyo kwa kweli angefanya jitihada kuvijua zaidi. Lakini itakuwaje kama angefanya jitihada hiyo na baadaye kujulishwa vitu ambavyo vingevunja vunja vile alivyokariri?

MM,

Mie si wa kwanza kuandika historia ya uhuru wa Tanganyika.
Tewa kabla hajafa aliniachia hazina hiyo hapo chini:

Amir, Hassan Sheikh, (Mufti) "Daawat Islamiyya" unpublished paper,1962.

Tewa, S Tewa, "Probe Into the History ofIslam in Tanzania" (unpublished manuscript).

Unadhani kwako wewe kuna mkweli kwetu sisi kumshinda Sheikh Hassan bin Amir?

Nyaraka hizo zipo katika maktaba nyingi Marekani na Ulaya kwa hisani yangu.

Mohamed

 
MM,

Mie si wa kwanza kuandika historia ya uhuru wa Tanganyika.
Tewa kabla hajafa aliniachia hazina hiyo hapo chini:

Amir, Hassan Sheikh, (Mufti) "Daawat Islamiyya" unpublished paper,1962.

Tewa, S Tewa, "Probe Into the History ofIslam in Tanzania" (unpublished manuscript).

Unadhani kwako wewe kuna mkweli kwetu sisi kumshinda Sheikh Hassan bin Amir?

Nyaraka hizo zipo katika maktaba nyingi Marekani na Ulaya kwa hisani yangu.

Mohamed


maswali yote ambayo tunakuuliza hapa na hao waliandika hizo nyaraka wataulizwa. Hatuangalii majina mzee Said tunaangalia substance. Wapo watu wana majina makubwa tu na vitu vingine wameandika ni vya kushangaza japo yawezekana walikuwa na nia nzuri tu.
 
Jibu hoja Mohamed watu hawana interest na tambo wala majigambo, usomi wako unatakiwa ujidhihiri si kukimbia maswali na kujificha katika kichaka cha andika vitabu, hilo ni jibu lisilo na usomi hata kidogo na sasa tutalitumia JF kama kibwagizo.

Tumekupiga shule umekiri mambo 13 mazito. Nakutajia machache
Umekiri kuwa mgogoro wa Mwembechai hakuna mali ya mkristo iliyohujumiwa ikiwa ni pamoja na makanisa
Umekiri kuwa Rupia ni mmoja wa wazee wako hata kama si mwaislam kama unavyotaka iwe.
Umekiri kuwa hujafanya utafiti kuhusu TANU, vinginevyo usingeshindwa kujua nani walikuwepo kamati kuu
Umekiri kuwa Platan na Sykes walikuwa mamluki waliokuja kumsaidia mkoloni na kushambulia waislam na si wazalendo kama unavyodai
n.k

Endelea kuwajibu watu wa gogo vivu, JF is something different my brother. Sasa ulimwengu unajua jinsi gani tamthilia zako zilivyo na tenzi murua.
Mwananchi anachpaisha tena makala zako?

Jibu hoja na maswali, majibu mepesi ya majigambo yasiyo na kitu yanaondoa hata kale ka credibility kadogo kaliko baki.

Nguruvi3,

Mimi nitake "credibility" kwako wewe?
hao watu wa gogo vivu ndiyo ndugu zangu mimi.

Mohamed
 
maswali yote ambayo tunakuuliza hapa na hao waliandika hizo nyaraka wataulizwa. Hatuangalii majina mzee Said tunaangalia substance. Wapo watu wana majina makubwa tu na vitu vingine wameandika ni vya kushangaza japo yawezekana walikuwa na nia nzuri tu.

MM,

"Publish or perish!"
Hujapata kusikia msemo huu?

Tendelee na darsa:

"Mara baada ya ujumbe wa EAMWS kurudi kutokaziara yake, Nyerere alifanya mabadiliko katika baraza la mawaziri na Tewa SaidTewa, Mwenyekiti wa EAMWS upande wa Tanzania akajikuta nje ya serikali. Nyerereakamteua Tewa balozi wa Tanzania katika Jamuhuri ya Watu wa China. MweziJanuari, 1965 Tewa alikwenda China kuanza kazi yake mpya. Inasemekana uteuzi wawa Tewa kwenda China ulisababishwa na juhudi zake za kutaka kuwaunganishaWaislam kuwa kitu kimoja chini ya jumuiya moja yenye nguvu. Wakati ule ilemipango iliyopitishwa na mkutano wa Waislam mwaka 1962 ilikuwa ikitekelezwavyema, shule zilikuwa zimejengwa Ilala, Kigogo na Kurasini, Dar es Salaam;shule zilikuwa zimejengwa Ruvu na Maneromango. Shule hii ya Maneromango ilikuwana umuhimu wa pekee kwa sababu hii ndiyo ilikuwa shule ya kwanza ya Waislamkujengwa Uzaramo. Shule za upili zilikuwa zikijengwa Dar es Salaam, Kinondonina Moshi, Kibohehe. EAMWS ilikuwa vilevile imetiliana mkataba wa makubaliano naserikali ya Misri kuipa scholarship thelathini na tano kila mwaka kwa wanafunziwa Kiislam kusoma Misri. EAMWS ilikuwa imejenga shule, misikiti, shule zaufundi na hosteli kwa ajili ya wanafunzi katika sehemu nyingi za Afrika yaMashariki. Kwa hakika EAMWS ilikuwa ikifanya mambo ya maendeleo kwa Waislam. UgandaTanzaniaKenyaShule77728Misikiti675329Shuleza Ufundi3--Hosteli1--Chanzo: Utafiti Baada ya Tewa kuondoka Bibi Titi Mohamedakachaguliwa kuwa makamu mwenyekiti wa tawi la EAMWS la Tanzania ili kuongezanguvu makao makuu kwa kuwa mwenyekiti hakuwepo. Kutokuwepo kwa Tewa nchinikulileta ombwe ambalo ilibidi lijazwe. Ghafla palizuka uvumi kuwa SheikhAbdallah Chaurembo alikuwa achukue uongozi wa EAMWS. Inasemekana nia yakeilikuwa ni kwanza kupata urais wa EAMWS na kisha achaguliwe kuwa Mufti waTanzania. [1]Uvumi huu ulidumu kwa karibu mwaka mzima hadi pale Tewa aliporudi kutoka Pekingbaada ya kujiuzulu ubalozi kuja kugombea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1965. AliporudiTewa alihojiwa na waandishi wa habari kuhusu uvumi ule na yeye jibu lakelilikuwa kuwa Muislam yeyote mwenye sifa ya maadili mema ana haki ya kugombeanafasi yoyote katika uongozi wa EAMWS. Neno alilolitumia Tewa katika kumuelezamtu ambaye angeweza kuwaongoza Waislam lilikuwa takwa, neno zito la Kiarabu kuelezamtu mcha-mungu.Nikuanzia katika matukio haya ndipo tunawezasasa kuanza kuchunguza jinsi Nyerere akiitumia serikali ilivyoanza kuuhujumuumoja wa Waislam kwa kutumia njama, hujuma za dhahiri na za kificho, magendo nakueneza uongo dhidi ya uongozi wa EAMWS, ambao ulionekana ni tishio kwa utawalawake. Wakati ule serikali nzima ilikuwa mikononi mwa Wakristo. UkiwatoaWazanzibari walioikuwa katika serikali ya muungano A.M. Maalim, Waziri waBiashara na Viwanda; Aboud Jumbe, Waziri Nchi; A.M. Babu, Waziri wa Ardhi,Makazi na Maji; Hasnu Makame, Waziri wa Habari na Utalii; Rashid Kawawa ambaealikuwa mtu wa karibu sana na Nyerere,waziri Muislam katika baraza la mawaziri kumi na tano alikuwa Said AliMaswanya, Waziri wa Mambo ya Ndani. Hali kama hii ya Wakristo kushika nyadhifatakriban zote za serikali ilikuja vipi? Jibu la swali hili linapatikana katikahistoria ya Tanganyika wakati wamisionari wa kwanza walipowasili nchini kujaëkulistaarabisha bara jeusií na halikadhalika katika historia ya TANU."
 
Mzee Said pamoja na ujuzi wote wa maneno na historia kuna kitu kimoja kiko wazi kuhusiana na hizi 'kazi' zake - amezikariri. Amekariri masimulizi ya utotoni na hata alivyozidi kupata ufahamu zaidi ndivyo hivyo hivyo alivyozidi kuzikariri. Hivyo anachotuelezea ni kile ambacho amekariri kwa kusimuliwa au kujisomea n.k Na hivyo anakirudia na ukiangalia kwa juu juu unaweza kweli kuwa impressed. Tatizo linakuja nipale unapozama chini na kuanza kufuatilia 'kujua'. Kuna tofauti kubwa kati ya kujua na kukariri.

Wapo wanafunzi ambao wanakaririshwa Table na hivyo ukimuambia akuambie table ya 12 anaweza akaiimba yote au 'tebo' ya sita akaiimba yote. Lakini mwanafunzi huyo anaweza asijue kuzidisha kwani ukianzia na table ya 13 au kwenda juu atapata shida au ukianza kuchanganya table na kujumlisha anaweza kushindwa. Lakini mwenye kujua kuzidisha anaweza kujua namna ya kuzidisha namba mbalimbali kwa urahisi kabisa na kwa haraka kuliko hata anayetumia kalamu. Kwa mfano, mtu anajua namba yoyote ukizidisha kwa namba yenye 10, 100, 1000 n.k basi unaongeza tu hiyo idadi ya sifuri na jibu linapatikana.

Kwenye historia au utafiti wa aina kama hii ni hivyo hivyo. Mtu anaweza kukariri matukio muhimu au watu muhimu walifanya nini na ni kile tu ambacho amekaririshwa ndicho pekee anaamini anakijua. Ukijaribu kumtoa tu kwenye kukariri anachanganyikiwa kabisa. Ni sawa na kumuweka swala mbele ya taa ya gari usiku akapigwa macho!

Maswali mengi anayoulizwa Bw. Said na watu wengi tangu kuanza kwa mjadala huu yanahitaji kujua siyo kukariri tu. Kwa mfano, Bw. Said anaweza kusema kuwa "tofauti kati ya Nyerere na Waislamu imeanza baada ya ile congress ya 1963". Sasa hicho ni cha kukariri. Ukitaka kumtoa jaribu kumuonesha kuwa walikuwepo Waislamu kabla ambao walikuwa wanamchukia Nyerere tangu siku ya kwanza ametambulishwa kwao na walimchukia si kwa sababu aliwadhulumu Wailslamu au aliwatendea jambo lolote baya - bali kwa sababu ya Ukatoliki wake. Ukimleta Said kwa hilo anapata shida kwa sababu ni kama kumlazimisha kujua.

Utaona maswali yote anayulizwa majibu yake ni ya kukariri.

SWALI: Kwanini kwa miaka karibu ishirini ambayo ulikuwa unafanyia hii historia 'yako' utafiti hukupata nafasi hata ya kuandika barua kwa Mwalimu Nyerere?

JIBU: Prof. Haroub Othman alishangazwa sana akamwendea Nyerere...

SWALI: Kwanini hadi leo hujawahi kumuuliza au hata kujaribu kwenda kuonana na Mama Maria Nyerere na kumhoji kuhusu Sykes na mtazamo wa Nyerere kuhusu Waislamu wakati akiwa madarakani?

JIBU: Maria Nyerere alikuwa anafahamiana sana na Binti Sudi, Binti Zubeda ambaye alikuwa akiishi mkabala na kwa Bw. Selemani ambaye nje ya nyumba yake tulikuwa tunacheza kombolela!

SWALI: Kwanini kama kweli ulikuwa unataka kuandika historia ya mashujaa 'waliosahauliwa' katika historia hukuwagusa wale ambao hawakuwa Waislamu au wale waliokuwa nje ya Dar?

JIBU: Kama na nyie mna wazee wenu nendeni mkaandike habari zao, miye nimeandika habari za wazee wangu na hiyo ndiyo historia yote ya TAnganyika!

SWALI: Je ni mahali gani ambapo wazee walioshiriki kupigania uhuru walipofanya hivyo kwa sababu ya Uislamu wao na kuwa waliongozwa na imani yao na siyo uzalendo wao kwa Tanganyika na kutaka uhuru uwanufaishe watu wote?

JIBU: Katika kampeni zote zilisomwa dua na Nyerere alikuwa anainamisha kichwa chini ili isomwe Al Fatha na wakati mwingine zilitolewa dua hadi wakatoka machozi!

Sasa mtu ambaye is untrained anaweza kuamini kabisa kuwa Bw. Said anajibu maswali lakini for any objective and trained mind anaweza kuona kuwa maswali hawezi kujibu kwa sababu yatamuondoa kwenye kukariri. Matokeo yake ni kuwa mtazungushana hapo hapo kwenye kukariri hadi mchoke kwa sababu alichokariri yeye ndio ukweli na chochote ambacho kitamfanya afikirie nje ya huko kukariri kutaaribu kabisa. Na ukifikiria sana utaona ni kweli. Wakati mwingine kujiuliza kuhusu kule unachoamini kunaweza kabisa kukusababisha ubadilishe mtazamo wako na kupindua kabisa maisha yako.

Bw. Said akitaka kujua anaweza lakini kujua kuna gharama - na gharama yake ni kuwa kwa kadiri mtu anavyopata ukweli ndivyo anavyoitwa kuufuata na wakati mwingine ukweli ni mgumu sana kuukubali. Ni mtu yule ambaye ana ujasiri wa dhamira yake ndiye pekee anaweza akutafuta ukweli, akauchunguzi na kuuhoji na akiona umethibitika atakuwa tayari kuhama kutoka kuliko alikokuweko.

Ndiyo Yesu alisema mojawapo ya misemo ya kifalsafa ya hali ya juu - 'MTAIFAHAMU KWELI NAYO KWELI ITAWAWEKA HURU" Yoh. 8:32 Ukweli unafungua, unawapa watu sababu ya matumaini, unatuliza moyo na unamuinua mtu kutoka katika hali ya kutokujua. UKWELI wa historia yetu haupatikani katika kitabu cha Bw. Said nayeyote ambaye anasoma ataona kuwa hafunguki! Ila anajikuta anasukumizwa kwenye kifungo cha hatari sana kwenye gereza ambalo nje limeandikwa 'UDINI'. Na huyo anaweza kuanza kujikuta anatumikia hii itikadi ya chuki na atafunguliwa tu pale ambapo yeye mwenyewe atakuwa na ujasiri wa kuhoji anachoambiwa, kuuliza maswali sahihi na akiona majibu hayaji kuunda nadharia za kuelezea kwanini majibu hayaji.

Maswali ambayo yameulizwa ambayo karibu yanafikia 50 sasa hayawezi kujibiwa na Bw. Said kwa sababu yanahusiana na kutafuta ukweli. Kwa vile lengo lake siyo kutafuta ukweli bali kukaririsha watu kile alichosikia basi ni vigumu kabisa kumfanya akubali kuwa kuna vitu ambavyo kwa kweli angefanya jitihada kuvijua zaidi. Lakini itakuwaje kama angefanya jitihada hiyo na baadaye kujulishwa vitu ambavyo vingevunja vunja vile alivyokariri?

Hivi na wewe unajihesabu katika watu "trained na objective"? Labda hiyo "training" yako ni ya kubabia na kupotosha.

Unajaribu sana kuwa mpotoshaji "rather than objective" hata hayo maswali uliyoyapanga na majibu uliyopewa yote unayaweka "out of context".

Unamwambia Mohamed Said akamuulize Maria Nyerere, akamuulize nini? akamuulize kama anamjuwa Mshume Kiyate? akamuulize kama anamjuwa Abdul Wahid Sykes? kama majibu yako ni ndiyo, basi Mohamed Said katowa majibu tosha kwa hilo kuwa anajuwa kuwa anawajuwa na kakuonesha ni vipi anawajuwa, kuna zaidi hapo? au kama wewe una maswali ya kumuuliza maria Nyerere kwanini umtake Mohamed Said akayaulize? kwa nini usiende wewe kuyauliza?

Zingine zote ni pumba, kutaka kujidai unaelewa kumbe huelewi kitu, umeambiwa andika kama unaweza. Kuwa "objective" ni pale tu utapokuja na maandiko yako tofauti na alivyoyasema Mohamed Said, kuwa Mohamed Said hapa ulisema Mshume Kiyate kampa Nyerere chakula, lakini si kweli kwa sababu Maria Nyerere kasema chakula kilikuwa kinatoka kanisani, huko ndio kuwa "objective.

Kuwa "objective" si kupinga unachoambiwa bila kujuwa hata unachokipinga ni nini? "kwanini, kwanini, kwanini..., hizo kwanini ndio unapewa hayo majibu. Sasa wewe kama hukuyapenda si wewe ueleze kuwa Maria Nyerere kasema hivi. Mashujaa wasio Waislaam ni hawa hapa, na ushujaa wao ulikuwa ni huu na huu na huu. Unaambiwa mtu anatoka Dar kwenda Rufiji na kurudi na baiskeli katika harakati, sasa hapo awekwe jina lipi huyo shujaa? wewe kama unaona hilo si kweli si useme, hapana huyo hakufanya hivyo, au kama yupo mwingine umlete nae tumjuwe.

Mzee Mwanakijiji, hakuna cha maana wala "objecitivity" katika hayo maswali yako, unajaribu kupotosha ukweli lakini kumbuka, ukweli ni ukweli hauna pa kuupeleka wala kuubadili. Mshume atabaki kuwa Mshume, Abdul Wahid atabaki kuwa Abdul Wahid, Nyerere atabaki kuwa Nyerere.

John Rupia alipotajwa kuwa katowa kiwanja cha kwanza cha chuo kikuu, hujapaona? au ulitaka uambiwe nini zaidi kuhusu yeye?

Pole sana.
 
Jibu hoja Mohamed watu hawana interest na tambo wala majigambo, usomi wako unatakiwa ujidhihiri si kukimbia maswali na kujificha katika kichaka cha andika vitabu, hilo ni jibu lisilo na usomi hata kidogo na sasa tutalitumia JF kama kibwagizo.

Tumekupiga shule umekiri mambo 13 mazito. Nakutajia machache
Umekiri kuwa mgogoro wa Mwembechai hakuna mali ya mkristo iliyohujumiwa ikiwa ni pamoja na makanisa
Umekiri kuwa Rupia ni mmoja wa wazee wako hata kama si mwaislam kama unavyotaka iwe.
Umekiri kuwa hujafanya utafiti kuhusu TANU, vinginevyo usingeshindwa kujua nani walikuwepo kamati kuu
Umekiri kuwa Platan na Sykes walikuwa mamluki waliokuja kumsaidia mkoloni na kushambulia waislam na si wazalendo kama unavyodai
n.k

Endelea kuwajibu watu wa gogo vivu, JF is something different my brother. Sasa ulimwengu unajua jinsi gani tamthilia zako zilivyo na tenzi murua.
Mwananchi anachpaisha tena makala zako?

Jibu hoja na maswali, majibu mepesi ya majigambo yasiyo na kitu yanaondoa hata kale ka credibility kadogo kaliko baki.

Naona umekosa hoja unarukia gogo vivu, kwa kukujuza tu, hapo ndipo barza aliyotokea la azizi wangu, kipenzi cha roho yangu, na hao ndio "orijino", sasa wewe kaa tu upate darsa, maana hoja huna na kuandika kitabu huwezi. Hata "credibility" huna kwani bado unajificha nyuma ya pazia. Ikiwa wewe hata kusema mimi nilifanya karatasi hii na hii na hii huwezi, inabidi ubaki kama mimi kuuliza maswali na kusikiliza darsa, Muache Mohamed Said atupe vina, wewe huna hata mizani wacha vina.
 
Huko kwenye mihadhara yako ya nje ya nchi huwa unawajibu 'public or perish' wanapokuuliza maswali kama ya kwenye huu mnakasha?

Sweke3,

Ni "publish" siyo "public."

Maana ya usemi huu ni kuwa kama hutoandika hutokuwepo.

Katika minakasha hiyo wote hapo wajuzi wana vitabu na "papers" lukuki.
Maswali wanayouliza si kama haya yenu.

Mohamed
 
watu tunaandika kwa haraka humu ndani ...kwa hiyo makosa yanatokea...!hukunielewa nina maana gani?

Nilikuwa sijakuelewa, lakini kama ni makosa ya "haraka" pole sana, jaribu kufanya vyema zaidi. Halafu hilo lilikuwa ni swali kutoka kwa Mohamed Said au ulifanya hara vilevile kuisoma post yake?
 
watu tunaandika kwa haraka humu ndani ...kwa hiyo makosa yanatokea...!hukunielewa nina maana gani?

Usweke34,

Ni kweli lakini sikuwa na hakika na nilitaka uujuwe huu msemo.
Nimekuelewa ndiyo maana nikakujibu.

Unafuatilia darsa?
Usipuuze hudhuria darsa kila siku kuna mengi utajifunza Insha Allah.

Mohamed
 
Sweke3,

Ni "publish" siyo "public."

Maana ya usemi huu ni kuwa kama hutoandika hutokuwepo.

Katika minakasha hiyo wote hapo wajuzi wana vitabu na "papers" lukuki.
Maswali wanayouliza si kama haya yenu.

Mohamed
Ndiyo maana watu wanahoji u 'scholar' wako ....! kwa utu uzima wako na level ya kisomo ambayo 'unayojiweka' nisingetegemea uanze kushabikia spelling au typing errors. Inaelekea kuna kitu ume lack ...probably confidence...ndiyo maana kila unapopata ka mwanya kidogo unajaribu kumshusha mtu ili angalau uonekane uko juu.
Kwenye red....Haingii akilini wajuzi wenye vitabu lukuki na 'papers' wasikuulize masuala tuliyokuuliza na ukashindwa kuyajibu hapa.
Labda ungetuwekea angalau ka video kamoja tuone jinsi unavyo present 'papers' zako!
 
Ndiyo maana watu wanahoji u 'scholar' wako ....! kwa utu uzima wako na level ya kisomo ambayo 'unayojiweka' nisingetegemea uanze kushabikia spelling au typing errors. Inaelekea kuna kitu ume lack ...probably confidence...ndiyo maana kila unapopata ka mwanya kidogo unajaribu kumshusha mtu ili angalau uonekane uko juu.
Kwenye red....Haingii akilini wajuzi wenye vitabu lukuki na 'papers' wasikuulize masuala tuliyokuuliza na ukashindwa kuyajibu hapa.
Labda ungetuwekea angalau ka video kamoja tuone jinsi unavyo present 'papers' zako!

Sweke34,

Wala nia yangu haikuwa hivyo.
Nilitaka ujue tu kile nilichokuandikia.

"Lack confidence..."
Hunijui.

Mie nimemwandika Nyerere katika magazeti kuhusu historia ya TANU na dhulma dhidi ya Waislam wakati watu wananon'gona.

Mimi nimemuandikia barua Sokoine wakati wa nguvu kazi kuhusu madras za Waislam vibarazani alipotaka zifungwe.
Nikamwambia huenda huijui Dar es Salaam lakini elimu yetu hapo ndipo inaposomeshwa miaka na miaka.

Nikaandikiwa barua nifike Ofisi ya TANU, Lumumba kwa ufafanuzi.
Nikapeleka jibu kuwa ufafanuzi siuhitaji mie wanahitaji Waislam wenye madras zao mnazotaka zifungiwe.
Kimya hadi leo na hakuna mgambo aliyethubutu hata kuinyooshea madras hata moja kidole hata cha gumba.

Ningekuwa sijiamini nisingeweza kuzungumza katika mihadhara na makongamano...
Nipime vizuri utanifahamu Insha Allah.

Mohamed
 
Ndiyo maana watu wanahoji u 'scholar' wako ....! kwa utu uzima wako na level ya kisomo ambayo 'unayojiweka' nisingetegemea uanze kushabikia spelling au typing errors. Inaelekea kuna kitu ume lack ...probably confidence...ndiyo maana kila unapopata ka mwanya kidogo unajaribu kumshusha mtu ili angalau uonekane uko juu.
Kwenye red....Haingii akilini wajuzi wenye vitabu lukuki na 'papers' wasikuulize masuala tuliyokuuliza na ukashindwa kuyajibu hapa.
Labda ungetuwekea angalau ka video kamoja tuone jinsi unavyo present 'papers' zako!

Unaijuwa google? kama jibu ni ndiyo, itumie.

Si unaona ulipokoselewa kidogo tu sasa hivi umekuja na maandiko marefu na hayana makosa ya "haraka". Imesaidia sana. Hizo ndio faida za darsa.
 
Unaijuwa google? kama jibu ni ndiyo, itumie.

Si unaona ulipokoselewa kidogo tu sasa hivi umekuja na maandiko marefu na hayana makosa ya "haraka". Imesaidia sana. Hizo ndio faida za darsa.
kwenye bold ...hayo ni mambo 'mepesi'.

Google inaleta video nyingi sana za mohamed said lakini siyo huyu...! labda ustaadhi mwenyewe atusaidie nadhani anaweza aka nazo kwenye hazina yake.
 
Nguruvi3,Mimi nitake "credibility" kwako wewe?Mohamed
Huhitaji yangu lakini ya umma unaitaka sana ndiyo maana upo hapa ukieneza propaganda. Kwa jinsi masimulizi yako yanavyochambuliwa hapa hata mjinga aliyekuwa anapiga makofi sasa atajiuliza akupigie au la. Muhimu ni sisi kukupa ukweli na ukaukubali bila kupenda, hiyo ndiyo Cambridge si kule watu wasikojua maneromango ni wapi.
Mohamed Said;2803958]MM,Tewa kabla hajafa aliniachia hazina hiyo hapo chini:
Amir, Hassan Sheikh, (Mufti) "Daawat Islamiyya" unpublished paper,1962.

Tewa, S Tewa, "Probe Into the History ofIslam in Tanzania" (unpublished manuscript).
Unadhani kwako wewe kuna mkweli kwetu sisi kumshinda Sheikh Hassan bin Amir?Nyaraka hizo zipo katika maktaba nyingi Marekani na Ulaya kwa hisani yangu.Mohamed
Fair enough, sasa tuangalie umezitumiaje hizo nyaraka kuandika historia yako
Mohamed Said;2804124MM, . Nyerereakamteua Tewa balozi wa Tanzania katika Jamuhuri ya Watu wa China. MweziJanuari, 1965 Tewa alikwenda China kuanza kazi yake mpya. Inasemekana uteuzi wawa Tewa kwenda China ulisababishwa na juhudi zake za kutaka kuwaunganishaWaislam kuwa kitu kimoja chini ya jumuiya moja yenye nguvu.
Hapo juu umesema Tewa alikuachia hazina, sasa hili neno 'inasemekana' unalipata wapi wakati wewe una hazina? Tewa kafariki, kuna shida gani ukimnukuu hadi utumie neno inasemekana. Ikifika hapo wale mazuzu wanodhani umefanya utafiti wajiulize upi huo wa kusemekana.

Pili, tumeona Tewa alikwenda kuwa balozi bila polisi au jeshi, kwahiyari yake. Kama nia yake ilikuwa kuwaunganisha waislam na alignundua njama hizo,je kwenda china sio usaliti kwa uislam na waislam! yaani tumbo lake lilikuwa bora kuliko masilahi ya umma wa waislam. Huyu ni shujaa au msaliti. Think about that Mohamed
ule ilemipango iliyopitishwa na mkutano wa Waislam mwaka 1962 ilikuwa ikitekelezwavyema, shule zilikuwa zimejengwa Ilala, Kigogo na Kurasini, Dar es Salaam;shule zilikuwa zimejengwa Ruvu na Maneromango. Shule hii ya Maneromango ilikuwana umuhimu wa pekee kwa sababu hii ndiyo ilikuwa shule ya kwanza ya Waislamkujengwa Uzaramo
Kwahiyo unatueleza kuwa elimu sasa ndiyo iliyokuwa inaingia uzaramo, lakini unataraji kuwa ingewezekana kupata katibu mkuu au waziri mzaramo.white elephant!
Ghafla palizuka uvumi kuwa SheikhAbdallah Chaurembo alikuwa achukue uongozi wa EAMWS. Inasemekana nia yakeilikuwa ni kwanza kupata urais wa EAMWS na kisha achaguliwe kuwa Mufti waTanzania.
Tunazidi kuona kurasa zilivyojaa neno inasemekana kutoka kwa mtafiti. Huko nyuma uliwahi kusema waislam wanachagua kiongozi, akaja mtu mmoja na kukushawishi kuwa waislam hawachagui viongozi na ukayumba yumba na kukubaliana naye. Hapa unatupa ushahidi kuwa unakubaliana na hoja ya kuchagua viongozi. Kuyumba kwako kunatokana na kujibu maswali ya habari uliyosimuliwa na kukariri, hivi bado kuna mtu anaamini kulikuwa na utafiti hapa!!!!
Neno alilolitumia Tewa katika kumuelezamtu ambaye angeweza kuwaongoza Waislam lilikuwa takwa, neno zito la Kiarabu kuelezamtu mcha-mungu.
Nikuanzia katika matukio haya ndipo tunawezasasa kuanza kuchunguza jinsi Nyerere akiitumia serikali ilivyoanza kuuhujumuumoja wa Waislam kwa kutumia njama, hujuma za dhahiri na za kificho, magendo nakueneza uongo dhidi ya uongozi wa EAMWS, ambao ulionekana ni tishio kwa utawalawake
Mohamed, huyu Tewa aliyewaacha waislam na kwenda kuwa balozi ana Taqwa? wapi alipata moral authority ya kuelezea nani awe kiongozi wakati yeye ni msaliti.
Wakati ule serikali nzima ilikuwa mikononi mwa Wakristo. UkiwatoaWazanzibari walioikuwa katika serikali ya muungano A.M. Maalim, Waziri waBiashara na Viwanda; Aboud Jumbe, Waziri Nchi; A.M. Babu, Waziri wa Ardhi,Makazi na Maji; Hasnu Makame, Waziri wa Habari na Utalii; Rashid Kawawa ambaealikuwa mtu wa karibu sana na Nyerere,waziri Muislam katika baraza la mawaziri kumi na tano alikuwa Said AliMaswanya, Waziri wa Mambo ya Ndani.
Kwanza ni uongo unapomtaja Kawawa kama Mzanzibar, pili hukuwahi kutaja baraza la mawaziri mwaka 1962. Tatu umeficha ukweli kuwa kawawa hakuwa waziri tu alikuwa na cheo kikubwa uischotaka kukieleza kwasababu kitaua hoja yako.

Kibaya zaidi unatumia neno serikali nzima halafu unaweka sehemu ya serikali, hakuna kitu kama hicho Mohamed. Unaposema nzima ina maana yote. Kiswahili kinaleta taabu kwasababu ya kutaka kupindisha ukweli.

Mohamed ili kujenga hoja yake ya chuki sasa anawagawa waislam, kuwa wale waliokuwa baraza la mawaziri ni Wazanzibar kutoka kule kule alikopelekwa sheikh Amir. Hakuwahi kumhoji Jumbe au Maswanya nini kilitokea. Anataka tuamini 'inasemekana'.

Tuendelee kuiangalia simulizi hii katika darubini, hatuandiki kitabu hadi hiki kitakapochambulia herufi zote. umma unazidi kuelewa.
Mwananchi wanachapisha makala zako tena!
 
Toka asubuhi nipo Darsa ngoja nikapate chakula kwanza tarudi baadae kwenye Darsa..

Mujahidi Mohamed Said nimejifunza mengi sana kutoka..

Ingiwa kuna watu povu linawatoka hawapendi unachoandika, lakini ndio hivyo tena huwezi kuzuia mvua..

Endelea kutoa Darsa...
 
Back
Top Bottom