Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Mzee, katika orodha uliyoweka hapo ya mawaziri umewataja sita, kama nimekuelewa vizuri, baraza lilikuwa na mawaziri 15. Sasa hapo ungependa iweje?! Wangekuwa wangapi ndo iwe sawa? Unaweza kutuwekea hapa mawaziri 9 waliobaki?
 
Huhitaji yangu lakini ya umma unaitaka sana ndiyo maana upo hapa ukieneza propaganda. Kwa jinsi masimulizi yako yanavyochambuliwa hapa hata mjinga aliyekuwa anapiga makofi sasa atajiuliza akupigie au la. Muhimu ni sisi kukupa ukweli na ukaukubali bila kupenda, hiyo ndiyo Cambridge si kule watu wasikojua maneromango ni wapi.
Fair enough, sasa tuangalie umezitumiaje hizo nyaraka kuandika historia yako Hapo juu umesema Tewa alikuachia hazina, sasa hili neno 'inasemekana' unalipata wapi wakati wewe una hazina? Tewa kafariki, kuna shida gani ukimnukuu hadi utumie neno inasemekana. Ikifika hapo wale mazuzu wanodhani umefanya utafiti wajiulize upi huo wa kusemekana.

Pili, tumeona Tewa alikwenda kuwa balozi bila polisi au jeshi, kwahiyari yake. Kama nia yake ilikuwa kuwaunganisha waislam na alignundua njama hizo,je kwenda china sio usaliti kwa uislam na waislam! yaani tumbo lake lilikuwa bora kuliko masilahi ya umma wa waislam. Huyu ni shujaa au msaliti. Think about that MohamedKwahiyo unatueleza kuwa elimu sasa ndiyo iliyokuwa inaingia uzaramo, lakini unataraji kuwa ingewezekana kupata katibu mkuu au waziri mzaramo.white elephant!
Tunazidi kuona kurasa zilivyojaa neno inasemekana kutoka kwa mtafiti. Huko nyuma uliwahi kusema waislam wanachagua kiongozi, akaja mtu mmoja na kukushawishi kuwa waislam hawachagui viongozi na ukayumba yumba na kukubaliana naye. Hapa unatupa ushahidi kuwa unakubaliana na hoja ya kuchagua viongozi. Kuyumba kwako kunatokana na kujibu maswali ya habari uliyosimuliwa na kukariri, hivi bado kuna mtu anaamini kulikuwa na utafiti hapa!!!! Mohamed, huyu Tewa aliyewaacha waislam na kwenda kuwa balozi ana Taqwa? wapi alipata moral authority ya kuelezea nani awe kiongozi wakati yeye ni msaliti.Kwanza ni uongo unapomtaja Kawawa kama Mzanzibar, pili hukuwahi kutaja baraza la mawaziri mwaka 1962. Tatu umeficha ukweli kuwa kawawa hakuwa waziri tu alikuwa na cheo kikubwa uischotaka kukieleza kwasababu kitaua hoja yako.

Kibaya zaidi unatumia neno serikali nzima halafu unaweka sehemu ya serikali, hakuna kitu kama hicho Mohamed. Unaposema nzima ina maana yote. Kiswahili kinaleta taabu kwasababu ya kutaka kupindisha ukweli.

Mohamed ili kujenga hoja yake ya chuki sasa anawagawa waislam, kuwa wale waliokuwa baraza la mawaziri ni Wazanzibar kutoka kule kule alikopelekwa sheikh Amir. Hakuwahi kumhoji Jumbe au Maswanya nini kilitokea. Anataka tuamini 'inasemekana'.

Tuendelee kuiangalia simulizi hii katika darubini, hatuandiki kitabu hadi hiki kitakapochambulia herufi zote. umma unazidi kuelewa.
Mwananchi wanachapisha makala zako tena!


Kasema, hajasema, alisikika, hajasikika. Hapo mwenyewe unajiona ndio unachambuwa kweli kweli. Tewa alikuwepo? Tewa alishika hizo nyadhifa?

Hilo moja linakutosha maana zingine umemwaga pumba, hivi wewe umewahi kuandika hata insha?
 
Kasema, hajasema, alisikika, hajasikika. Hapo mwenyewe unajiona ndio unachambuwa kweli kweli. Tewa alikuwepo? Tewa alishika hizo nyadhifa?

Hilo moja linakutosha maana zingine umemwaga pumba, hivi wewe umewahi kuandika hata insha?
Haya ndiyo mambo tunayokataa humu ndani...! Nguruvi kamjibu MS kwa hoja. Sasa tabu iko wapi kwako wewe FaizaFoxy kupita hoja za Nguruvi na kuonyesha jinsi kila hoja yake ilivyojaa pumba? Ukifanya hivyo utakuwa umemsaidia Nguruvi , MS na sisi sote humu ndani.
 
Huhitaji yangu lakini ya umma unaitaka sana ndiyo maana upo hapa ukieneza propaganda. Kwa jinsi masimulizi yako yanavyochambuliwa hapa hata mjinga aliyekuwa anapiga makofi sasa atajiuliza akupigie au la. Muhimu ni sisi kukupa ukweli na ukaukubali bila kupenda, hiyo ndiyo Cambridge si kule watu wasikojua maneromango ni wapi.
Fair enough, sasa tuangalie umezitumiaje hizo nyaraka kuandika historia yako Hapo juu umesema Tewa alikuachia hazina, sasa hili neno 'inasemekana' unalipata wapi wakati wewe una hazina? Tewa kafariki, kuna shida gani ukimnukuu hadi utumie neno inasemekana. Ikifika hapo wale mazuzu wanodhani umefanya utafiti wajiulize upi huo wa kusemekana.

Pili, tumeona Tewa alikwenda kuwa balozi bila polisi au jeshi, kwahiyari yake. Kama nia yake ilikuwa kuwaunganisha waislam na alignundua njama hizo,je kwenda china sio usaliti kwa uislam na waislam! yaani tumbo lake lilikuwa bora kuliko masilahi ya umma wa waislam. Huyu ni shujaa au msaliti. Think about that MohamedKwahiyo unatueleza kuwa elimu sasa ndiyo iliyokuwa inaingia uzaramo, lakini unataraji kuwa ingewezekana kupata katibu mkuu au waziri mzaramo.white elephant!
Tunazidi kuona kurasa zilivyojaa neno inasemekana kutoka kwa mtafiti. Huko nyuma uliwahi kusema waislam wanachagua kiongozi, akaja mtu mmoja na kukushawishi kuwa waislam hawachagui viongozi na ukayumba yumba na kukubaliana naye. Hapa unatupa ushahidi kuwa unakubaliana na hoja ya kuchagua viongozi. Kuyumba kwako kunatokana na kujibu maswali ya habari uliyosimuliwa na kukariri, hivi bado kuna mtu anaamini kulikuwa na utafiti hapa!!!! Mohamed, huyu Tewa aliyewaacha waislam na kwenda kuwa balozi ana Taqwa? wapi alipata moral authority ya kuelezea nani awe kiongozi wakati yeye ni msaliti.Kwanza ni uongo unapomtaja Kawawa kama Mzanzibar, pili hukuwahi kutaja baraza la mawaziri mwaka 1962. Tatu umeficha ukweli kuwa kawawa hakuwa waziri tu alikuwa na cheo kikubwa uischotaka kukieleza kwasababu kitaua hoja yako.

Kibaya zaidi unatumia neno serikali nzima halafu unaweka sehemu ya serikali, hakuna kitu kama hicho Mohamed. Unaposema nzima ina maana yote. Kiswahili kinaleta taabu kwasababu ya kutaka kupindisha ukweli.

Mohamed ili kujenga hoja yake ya chuki sasa anawagawa waislam, kuwa wale waliokuwa baraza la mawaziri ni Wazanzibar kutoka kule kule alikopelekwa sheikh Amir. Hakuwahi kumhoji Jumbe au Maswanya nini kilitokea. Anataka tuamini 'inasemekana'.

Tuendelee kuiangalia simulizi hii katika darubini, hatuandiki kitabu hadi hiki kitakapochambulia herufi zote. umma unazidi kuelewa.
Mwananchi wanachapisha makala zako tena!

Nguruvi3,

Inasemekana jamaa keshawasili.

Na hapo nishazungumzanae na kaniambia keshafika.
Nitakapomueleza mtu kuwa jamaa amewasili nitasema, "Inasemakana jamaa keshakuja."

Hivi ndivyo tunavyozungumza watu wa pwani.
Hii ndiyo nama yetu ya kuongea.

Ziangalie hizo "inasemekana" ziko nyingi.

Makala za Mwananchi zimekuumeni sana.
Taarifa zimenifikia.

Makala zile zimeninyanyua hata sikutegemea na zote walichapa.

Nimepewa mradi mzito wa "documentary."
Mengine sina haja ya kujibu.

Mohamed
 
kwenye bold ...hayo ni mambo 'mepesi'.

Google inaleta video nyingi sana za mohamed said lakini siyo huyu...! labda ustaadhi mwenyewe atusaidie nadhani anaweza aka nazo kwenye hazina yake.

Sweke34,

Kama uko Dar es Salaam pita msikiti wowote Kariakoo wanakuwa na sehemu wanauza vitabu na DVD utapata DVD zangu hii ndiyo njia nyepesi maana ya "google" inakuwia tabu kidogo.

Nikipata link nitakurushia Insha Allah.

Mohamed
 
MM,

Hivi wewe huoni vibaya kuwa kila siku unapiga fidla ya pili?
Niandike tena "paper" we uje nyuma yangu.

Nitoa kwenye kitabu wewe uje nyuma yangu.
Wewe huoni haya?

Unadhani una uwezo wa kupambana na mimi kwa njia hiyo?
Pumzika.

Tafuta mambo mepesi.
Hapa ndipo kikomo cha usomi wako?

Mohamed
Bwana Mohamed ni jinsi kichwa cha habari chenyewe kilivyo ndiyo maana hali kwenye mjadala huu iko hivi. huwezi amini mimi kwenye zile makala zako kwenye ile thread yako nimechangia mara moja tuu, kwani kama siziamini makala zile sina budi kuandika za kwangu. Lakini Hapa umekosolewa kwa makala zile ndiyo maana kuna wanaomuunga mkono aliyekukosoa na wapo wanaompinga. Wakosoaji (Critics) hawana ulazima wa kuandika vitabu ili wafikie viwango vya kuitwa wakosoaji. Wakosoaji ni wakosoaji na si waandikaji, kwani waandikaji nao ni waandikaji na si wakosoaji.

Wewe kwa majisifu yako kwamba unaingiliana sana na watu wa Magharibi bila shaka unaelewa kwamba si kila anayekaribishwa ulaya ni mtu anayefaa. Mashoga wa Uganda walikaribishwa kwa mbwembwe, vifijo na nderemo walipokwenda Marikani kuelezea jinsi wanavyo "kandamizwa" nchini kwao. Vipi mashoga hao wakikwambia "kama huamini sisi tuna haki nenda kaullize ulaya ambako tumeshatoa mihadhara zaidi ya 50 kwenye vyuo vikuu mbali mbali vya huko". Kwa mtazamo wako Ushoga ni kitu halali kwa sababu tu mashoga hao wa Uganda walikwenda ulaya na marikani kutoa mihadhara kwenye vyuo vikuu vya nchi hizo?

Mimi sikosoi bali namuunga mkono aliyekukosoa wewe na ukosoaji wake ni kitu kipya wala haigi maandishi yako bali ameandika ya kwake kwa tafakuri inayotokana na udhaifu wa kwenye maandishi yako. Mag3 ni Critic.
 

Nguruvi3,

Inasemekana jamaa keshawasili.

Na hapo nishazungumzanae na kaniambia keshafika.
Nitakapomueleza mtu kuwa jamaa amewasili nitasema, "Inasemakana jamaa keshakuja."

Hivi ndivyo tunavyozungumza watu wa pwani.
Hii ndiyo nama yetu ya kuongea.

Ziangalie hizo "inasemekana" ziko nyingi.

Makala za Mwananchi zimekuumeni sana.
Taarifa zimenifikia.

Makala zile zimeninyanyua hata sikutegemea na zote walichapa.

Nimepewa mradi mzito wa "documentary."
Mengine sina haja ya kujibu.

Mohamed


Tena kuna kijana wetu wa Lumumba pale ni mkali kweli wa "ma video" na ametoka Canada baada ya kwenda kuchukuwa ujuzi zaidi, atakuwa msaada mkubwa sana wa kutayarisha "documentary" ntakupa namba zake kwa pm. Unamjuwa sana tu.
 
Kumbuka kuwa hilo ni vazi pia la mapadri na hizo hijab pia huvaa ma nun. Zisikustuwe sana.

Yaani kwa ukigeugeu wewe ni balaa!! Yaani leo Kanzu na Hijabu unayaona ni mavazi tu ya kawaida, wakati huko nyuma mavazi hayo hayo uliyahusisha na Uislamu!!??i

Pia unapenda sana kurekebisha mabandiko ya wenzio lakini na wewe hujanusurika kukosea. Ukisema "hizo hijab pia huvaa ma nun" unamaanisha kwamba ma nun (watawa?) ndiyo huvaliwa na Hijab. Ungeaandika "hizo hijab pia huvaliwa na ma nun" ni ushauri tu ndugu yangu kwamba ukirusha mawe kwenye nyumba ya mwenzio wakati ya kwako ni ya kioo, JIANDAE!!
 
Heshima kwako Nguruvi3.

Mkuu wangu haya maswali sitegemei kama Sheikh Mohamed Said atayajibu kwasababu ajenda yake ya kutugawa waTanzania kwa misingi ya Imani itakufa kifo cha mende.Ni vyema mjadala ukafungwa kwakuwa MS hana majibu ingawa anajisifia maandiko yake yapo Marekani na ulaya ajabu anashindwa kujibu nondo za uhakika hapa JF.Kwa maneno rahisi JF ni kiboko wapo magreat thinker uwezi leta upupu ukashangiliwa kama bi harusi.



Mohamed majibu ya namna hii ayalingani na mtu anayetoa mhadhara ulaya na marekani. Kusema sijui au hapana hakumaanishi chochote zaidi ya kujenga ueledi.

Labda nikukumbushe tuhuma, nimeangalia kabrasha langu zipo 45 kubwa na 32 madogo. Kwa kumsaidia Joka kuu na sisi sote naorodhesha zifuatazo na utupe majibu.

1. Uliwahi kumhoji marhumu Kawawa jinsi Nyerere alivyotumia udini kuwaondoa waislam katika uongozi wa TANU na serikali.

2. Umewahi kumuuliza mzee Mwinyi kuhusu tuhuma za wizi wa funguo za madroo alizoongea na Malima wakati huo akiwa Ikulu.

3. Umeshawahi kumhoji mama Maria kuhusu kitoweo alichokuwa anapelekewa na mzee Kiyate, yeye ana kauli gani kwa jambo hili jema.

4. Umewahi kumhoji Salim Ahmed Salim au Butiku kuhusu kukataa kwao kupokea picha za wazee wako.

5. Umewahi kumhoji Tewa kwanini alikubali kuwa balozi nchini China huku akijua kuwa zilikuwa njama za kudhoofisha EAMWS

6.Umewahi kumhoji padre Sivlon kuhusu aliyoandika katika kitabu chake na anasemaje katika kuyathibitisha.

7. Uliwahi kumhoji Platan kuhusu ugomvi wa AMNUT na nini kilikuwa chanzo halisi(walikuwa wanatofautiana nini)

8. Umewahi kuuliza wizara ya elimu namba za mitihani zilianza kutumika lini

9. Umewahi kumhoji mkuu au makamu mkuu wa UDSM kwanini ma lecturer wakikristo hawataki kitabu chako kitumike

10. Umeahi kumhoji Rupia kuhusu tuhuma za Nyerere kuwa mdini na alikuwa na maoni gani

11. Uliwahi kumhoji marhum Bibi Titi Mohamed kwanini aliwekwa ndani, mwaka gani na aliwekwa pamoja na akina nani

12. Uliwahi kumhoji Munaka Bhoke juu ya kiasi gani alikusanya ili kujenga chuo kikuu cha Dar es Salaam

13. Uliwahi kumhoji sheikh Himid Jongo kwanini baada ya kadhia ya mwembechai alikabidhiwa msikiti na serikali ile ile unayoituhumu

14. Umeahi kumhoji Adam Nasibu kuhusu ushiriki wake katika kuanzisha BAKWATA

Ukishayajibu haya tunaweza kuendelea kidogo kidogo.

Ukumbi wako
 
kwenye bold ...hayo ni mambo 'mepesi'.

Google inaleta video nyingi sana za mohamed said lakini siyo huyu...! labda ustaadhi mwenyewe atusaidie nadhani anaweza aka nazo kwenye hazina yake.

Sweke34 unamtoa rangi mwalimu wa spelling hahahah aibu!
 
Sweke3,

Ni "publish" siyo "public."

Maana ya usemi huu ni kuwa kama hutoandika hutokuwepo.

Katika minakasha hiyo wote hapo wajuzi wana vitabu na "papers" lukuki.
Maswali wanayouliza si kama haya yenu.

Mohamed

hili laweza kuwak kweli kabisa kwa sababu wanakuuliza the wrong questions..!
 
Fundi Mchundo,

Tusivutane kwa hili la Zuberi Mtemvu mimi kanihadithia mwenyewe kuwa yeye aliacha kazi Community Development Department kwa kushauriwa na Nyerere ili ashike nafasi ya ukatibu. Hata hivyo inawezekana pia kuwa pakawa na kugongana kwa kumbukumbu kama tujuavyo TANU wenyewe walipoandika historia yao mengi waliyaacha. Hebu soma hii:
"TANU ilinufaika sana kwa siasa za wastaniza Nyerere, umakini wake na kipaji chake cha kuzungumza. Vilevile harakati kwa ujumla zilinufaika kwa ujasiri waMtemvu na Ally. Wao walitenda mambo kwa ujasiri zaidi. Hawakushughulishwa sana na nadharia katikamaamuzi yao ya siasa. Ilikuwa katika kipindi hiki cha kuijengea TANU misingiimara ya uongozi ndipo Nyerere alimshauri Mtemvu aache kazi serikalini ajiriwena TANU. Mtemvu alikubali ushauri ule na akaacha kazi. Mtemvu akawa katibu wakwanza wa TANU. Mtemvu na Mhando walijukanakama ëwakomunistií na serikali, lakini wao wenyewe hawakuhughulishwa na jinahilo. Hivi ndivyo ilivyokuwa Zuberi Mwinshehe Manga Mtemvu alivyokuja kuwammoja wa viongozi wa juu katika TANU. Tutaona hapo baadaye kisa cha Mtemvukutupana mkono na Nyerere na TANU. Katika siku za mwanzonafasi ya katibu mwenezi ilikuwa ikishikwa na viongozi mbali mbali baina yaMtemvu Denis Phombeah, Oscar Kambona, Iddi Faizi Mafongo na Stephen Mhando.Mtemvu akiwa katibu mwenezi alikuwa na kazi ngumu ya kuwashawishi na kuwashirikishawatu kujiunga na kusajili matawi ya TANU."

Kuna wazalendo umewataja ambao nami nakubaliana na wewe kabisa kuwa historia ya TANU haiwezi kukamilika bila ya kuwataja.

Mimi kama wewe ningependa sana mchango wao ukaelezwa ili waadhimishwe na nimeshauri na kutoa changamoto hapa ukumbini lakini naona hili jambo watu hawana uwezonalo.

Publisher mmoja baada ya kusoma kitabu changu aliniomba niandike short biographies za watu kama Bhoke Munanka, Chief Patrick Kunambi nk. nk. lakini mimi nilimshauri atafute mwandishi mwengine.

Hatujachelewa kazi hii ni muhimu na lazima Insha Allah ifanyike.

Sasa hili la dini. Sisi watu wa pwani Uislam umo hadi katika utamaduni wetu na kwa kuwa TANU iliasisiwa na Waislam hili halikuweza kuepukika.

Ndiyo maana mikutano ya mwanzo ilikuwa ikianza kwa kupigwa "fatha." TANU ikikwama kwenye jambo wanafanya "tawasul" na wakati mwingine wanafunga "saum."

Ndiyo maana Sheikh Hassan bin Amir akiuza kadi za TANU msikitini.

Ndiyo maana Baraza la Wazee wa TANU lilitawaliwa na Waislam.

Huu ndiyo ukweli wa historia ya TANU na ndiyo maana kitabu changu kikavutia wengi kwa kuwa ilikuja na kitu kipya ambacho kilikuwa hakifahamiki kwa wengi.

Nimeweka uzi hapa kuwa katika kongamano moja nilipewa onyo kabla kuwa nisiutukuze Uislam na mie nilopoanza "presentation" yangu nilifungua na "Surat Fatha" nikawaambia Wazungu wale kuwa hii ndiyo dua iliyokuwa ikisomwa kabla ya mikutano ya TANU Mnazi Mmoja kisha Nyerere ndiyo anakaribishwa na Sheikh Suleiman Takadir.

Nakumbuka swali moja waliloniuliza ni kuwa Wakristo walikuwa wapi wakati huo?

Jibu langu nalikumbuka hadi leo: "you find out it will make very interesting topic for reaserch..."


Mohamed

Unakosea tena. Zuberi Mtemvu alikuja baadae, Katibu wa kwanza alikuwa Denis Phombeah ambae alikuwa Meneja wa ukumbi wa Arnatoglou. Zuberi alikuja baadae kama alivyokuja Oscar. Oscar Kambona alikuwa wa kwanza aliyekuwa mwajiriwa full-time. Denis Phombeah alikuwa mnyasa na mkristu kama alivyokuwa Oscar, ndiyo maana unapata ugumu kutambua nafasi yake.

On July 7, 1954, T.A.A. had its Annual General Meeting in Dar-es-Salaam. On this occasion Julius Nyerere and his friends took a historic decision. Regardless of registration difficulties, they announced the transformation of T.A.A. into the Tanganyika African National Union, the first African political organization in their country’s history.
Nyerere was unanimously elected president, though he lay it down that both he and the members of the National Executive should be subject to re-election by the Annual Delegates conference. The National Executive was to meet quarterly, but in view of communications difficulties, there was to be an Executive Center Committee, Consisting of the president and nine members, all residing in Dar-es-salaam. Denis Phombeah was elected its first secretary; it was to meet weekly and have full responsibility ‘in the event of an emergency’.

Baraza la TANU halikutawaliwa na waislamu. Waislamu walikuwa wengi, ndio, lakini haina maana kuwa waliwatawala wasio waislamu. Kama uliwajua wakina Julius Nyerere, Oscar Kambona, John Rupia, Denis Phombea, bila shaka utakiri kuwa hawa hawakuwa watu wa kuburuzwa. Vile vile tofauti na unavyotaka kutupotosha, hao waislamu hawakuwa bloc bali waligawanyika katika makundi. Wako pengine ambao walitanguliza uislamu wao lakini wengi zaidi walitanguliza utanganyika na ndio maana hoja za wakina Nyerere ziliweza kukubaliwa na kufanyiwa kazi.

Ukweli ni kuwa pamoja na wakina Barubaru kutaka kupunguza sumu ya hoja yako bado ukweli unabaki kuwa unaongozwa na chuki dhidi ya wakristu, haswa wakatoliki na ajenda yako ni kuamsha simanzi ya waislamu wawachukie. Kwako wewe haijalishi mchango wa mtu, cha muhimu ni dini yake. Hakuna mtu anayepinga mchango wa hao unaowaenzi katika taifa letu lakini tunaachpinga ni kuwafanya kuwa walikuwa peke yao na wengine wasio wa dini yako walikuwa wapambe tu! Hauwezi leo kuandika historia ya mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi Afrika ya Kusini bila kuwataja wakina Ruth First, Nadine Gordimer na wengine wengi ambao walikuwa weupe walikuwa tayari kuweka maisha yao rehani kudai haki kwa ajili ya mtu mweusi. Kwa vile tu muingereza aliyetutawala alikuwa dini moja na Oscar haiondoi na haibadilishi mchango wake katika mapambano dhidi ya utawala ule.

Unakotaka kutupeleka ni kubaya na ndio maana hatutakukubalia utuburuze huko maana hatuna ankal Doha wa kukimbilia mambo yakiharibika.

Amandla.......
 
Heshima kwako Nguruvi3.

Mkuu wangu haya maswali sitegemei kama Sheikh Mohamed Said atayajibu kwasababu ajenda yake ya kutugawa waTanzania kwa misingi ya Imani itakufa kifo cha mende.Ni vyema mjadala ukafungwa kwakuwa MS hana majibu ingawa anajisifia maandiko yake yapo Marekani na ulaya ajabu anashindwa kujibu nondo za uhakika hapa JF.Kwa maneno rahisi JF ni kiboko wapo magreat thinker uwezi leta upupu ukashangiliwa kama bi harusi.


Ngongo,

Huwezi kuwa "great" kwa kutamani.
Huwezi kuwa "great" kwa kuuliza maswali ya vichekesho.

Unakuwa "great" kwa kuonyesha uwezo wako katika hicho unachokisemea.
Na hakuna njia ya mkato.

Lazima kuuendea u "great" uandike kwa uchache "paper" moja mbili watu wakusome.
Ikiwa uloandika yana maana utaona unaalikwa katika makongamano na mikutano...

Hatua inayofuatia unaandika kitabu...

Tuishie hapa nadhani ushaipata picha...
Huwezi kuwa "great" JF.

Na kuwa "great" ni kitu kinaweza kikakuchukua umri wako wote.

Mohamed
 
Unakosea tena. Zuberi Mtemvu alikuja baadae, Katibu wa kwanza alikuwa Denis Phombeah ambae alikuwa Meneja wa ukumbi wa Arnatoglou. Zuberi alikuja baadae kama alivyokuja Oscar. Oscar Kambona alikuwa wa kwanza aliyekuwa mwajiriwa full-time. Denis Phombeah alikuwa mnyasa na mkristu kama alivyokuwa Oscar, ndiyo maana unapata ugumu kutambua nafasi yake.



Baraza la TANU halikutawaliwa na waislamu. Waislamu walikuwa wengi, ndio, lakini haina maana kuwa waliwatawala wasio waislamu. Kama uliwajua wakina Julius Nyerere, Oscar Kambona, John Rupia, Denis Phombea, bila shaka utakiri kuwa hawa hawakuwa watu wa kuburuzwa. Vile vile tofauti na unavyotaka kutupotosha, hao waislamu hawakuwa bloc bali waligawanyika katika makundi. Wako pengine ambao walitanguliza uislamu wao lakini wengi zaidi walitanguliza utanganyika na ndio maana hoja za wakina Nyerere ziliweza kukubaliwa na kufanyiwa kazi.

Ukweli ni kuwa pamoja na wakina Barubaru kutaka kupunguza sumu ya hoja yako bado ukweli unabaki kuwa unaongozwa na chuki dhidi ya wakristu, haswa wakatoliki na ajenda yako ni kuamsha simanzi ya waislamu wawachukie. Kwako wewe haijalishi mchango wa mtu, cha muhimu ni dini yake. Hakuna mtu anayepinga mchango wa hao unaowaenzi katika taifa letu lakini tunaachpinga ni kuwafanya kuwa walikuwa peke yao na wengine wasio wa dini yako walikuwa wapambe tu! Hauwezi leo kuandika historia ya mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi Afrika ya Kusini bila kuwataja wakina Ruth First, Nadine Gordimer na wengine wengi ambao walikuwa weupe walikuwa tayari kuweka maisha yao rehani kudai haki kwa ajili ya mtu mweusi. Kwa vile tu muingereza aliyetutawala alikuwa dini moja na Oscar haiondoi na haibadilishi mchango wake katika mapambano dhidi ya utawala ule.

Unakotaka kutupeleka ni kubaya na ndio maana hatutakukubalia utuburuze huko maana hatuna ankal Doha wa kukimbilia mambo yakiharibika.

Amandla.......

Fundi Utumbo,

Ungeliandika kitabu ingelikuwa raha kweli kweli maana sasa mie na we sote tungekuwa tunasomwa pamoja.
Vinginevyo...

Mohamed
 

Nguruvi3,Inasemekana jamaa keshawasili. Na hapo nishazungumzanae na kaniambia keshafika.
Nitakapomueleza mtu kuwa jamaa amewasili nitasema, "Inasemakana jamaa keshakuja."
Hivi ndivyo tunavyozungumza watu wa pwani. Hii ndiyo nama yetu ya kuongea.Ziangalie hizo "inasemekana" ziko nyingi
Mohamed
Mimi ni mtu wa pwani pia, usitake kuwadanganya watu. Baada ya kuona aibu sasa unalitafutia neno hilo maana ili likuondoe na aibu ya hisia ambayo imekuchafua. Neno hili halitumiki kama unavyosema na hapa manguli wa kiswahili wanabaki wakicheka sana jinsi mzee mwenzao ulivyopelekwa kona na unavyojiuma uma.

Lakini kama umeleitumia kwa maana unayosema bado linakuumbua sana. Linaonyesha kuwa kazi yako ya uandishi haizingatiii lugha. Mwandishi anatakiwa awasailiane na hadhira yake bila tatizo la mawasiliano. Njia mojawapo ni kutumia lugha inayoeleweka kwa wote, sio lugha ya mitaani. Sasa kama wewe umelitumia kwa ajili ya watu wa kisiju, Nanjilili, Mjasani , Maneromango hajui hadhira unayotaka kuifikia. Kosa la uandishi na ushahidi wa ubabaishaji.

Maswali wanayokuuliza ulaya hawana background. Hawajui kuwa Tewa alikuwa msaliti kwa waislam wao wanajua Tewa kakuachia makabrasha ya maana. Wanakuuliza kuhusu Nyerere na wewe unawamwagia chuki uliyo nayo dhidi yake kama ya babu yako aliyeendesha mgomo.
Maswali ya wana JF huyawezi kwasababu utatudanganya nini kuhusu mwembechai, kariakoo, Nyerere, Rupia, Kawawa, TANU, TAA n.k.

Kama alivyosema mmoja wetu ukitia mkuu JF usitegemee vigelegele na zumari kama kigoli anayechezwa ngoma mkamba kisiju.
Gogovivu mashalah watakubusu mkono uwanunulie gahwa, hawajui kinachoendelea masikini sio JF

Jibu hoja na maswali hatuhitaji bla blah.
 

Fundi Utumbo,

Ungeliandika kitabu ingelikuwa raha kweli kweli maana sasa mie na we sote tungekuwa tunasomwa pamoja.
Vinginevyo...

Mohamed

Hatuwezi wote kuwa waandishi. Na si maandishi yote yanastahili kuheshimiwa na/au kukubaliwa. Kitabu kimoja kinachofanana na chako ni Mein Kampf ambamo mwandishi alielezea historia yake na imani yake. Na kama ilivyo kwa kitabu chako, kilikataliwa na kupingwa na wale wanaoutakia mema ulimwengu wetu!

BTW, Salman Rushdie yuko katika maktaba zote ulaya na anaheshimiwa sana katika akademia. Kwa mtazamo wako basi huyu nae kwa vile amesomwa na wengi na ametoa mada katika majukwaa makubwa, anastahili kuenziwa na jamii yetu!

Amandla.....
 
MS

Endelea kutoa darsa, hawa jamaa wanaojiita critics hawana maswali ya maana zaidi ya kashfa.

Kuna watu wengi wanasoma hii historia. Tunaomba uendelee kutupa vitu.
 
Mimi ni mtu wa pwani pia, usitake kuwadanganya watu. Baada ya kuona aibu sasa unalitafutia neno hilo maana ili likuondoe na aibu ya hisia ambayo imekuchafua. Neno hili halitumiki kama unavyosema na hapa manguli wa kiswahili wanabaki wakicheka sana jinsi mzee mwenzao ulivyopelekwa kona na unavyojiuma uma.

Lakini kama umeleitumia kwa maana unayosema bado linakuumbua sana. Linaonyesha kuwa kazi yako ya uandishi haizingatiii lugha. Mwandishi anatakiwa awasailiane na hadhira yake bila tatizo la mawasiliano. Njia mojawapo ni kutumia lugha inayoeleweka kwa wote, sio lugha ya mitaani. Sasa kama wewe umelitumia kwa ajili ya watu wa kisiju, Nanjilili, Mjasani , Maneromango hajui hadhira unayotaka kuifikia. Kosa la uandishi na ushahidi wa ubabaishaji.

Maswali wanayokuuliza ulaya hawana background. Hawajui kuwa Tewa alikuwa msaliti kwa waislam wao wanajua Tewa kakuachia makabrasha ya maana. Wanakuuliza kuhusu Nyerere na wewe unawamwagia chuki uliyo nayo dhidi yake kama ya babu yako aliyeendesha mgomo.
Maswali ya wana JF huyawezi kwasababu utatudanganya nini kuhusu mwembechai, kariakoo, Nyerere, Rupia, Kawawa, TANU, TAA n.k.

Kama alivyosema mmoja wetu ukitia mkuu JF usitegemee vigelegele na zumari kama kigoli anayechezwa ngoma mkamba kisiju.
Gogovivu mashalah watakubusu mkono uwanunulie gahwa, hawajui kinachoendelea masikini sio JF

Jibu hoja na maswali hatuhitaji bla blah.

Du!
Mbona umenzindua sikuwa na khabari kama JF ina hadhi kubwa kiasi hiki ingawa bado hatujatoa "paper" hata moja.

Mie hanitoi mtu humu.
Naiweka katika CV yangu.

Sasa jamaa watanikoma.

Mohamed
 
MS

Endelea kutoa darsa, hawa jamaa wanaojiita critics hawana maswali ya maana zaidi ya kashfa.

Kuna watu wengi wanasoma hii historia. Tunaomba uendelee kutupa vitu.

Mr Right,

Si utani historia hii niloandika imewavuruga sana jamaa zetu.

Mohamed
 

Fundi Utumbo,

Ungeliandika kitabu ingelikuwa raha kweli kweli maana sasa mie na we sote tungekuwa tunasomwa pamoja.
Vinginevyo...

Mohamed

MS,

Wasio upande wako au wasiokubaliana nawe ndio wanapaswa kuandika vitabu au "papers" ili ukubali hoja zao au iwe "raha kweli kweli" lakini wanaokubaliana na wewe au wanatetea hoja hizi za udini hao hilo la kuandika vitabu or papers haliwahusu. Double standards? Au ndio "mfumo mbadala"? Waulize pia hawa wanaotetea hoja zako za "mfumo kristo" "Uovu wa Nyerere" na Historia ya wazee wako, vitabu au "papers" zao ziko wapi?

Ikishindikana basi hii hoja yule anayehoji unachotaka kutuaminisha anaambiwa kuandika kitabu/vitabu/papers itakuwa haina maana na mjadala undelee na maswali yajibiwe.
 
Back
Top Bottom